Itachukua Miaka Mingi Kumpata Rais Samia Mwingine Mwenye moyo wa upendo, uvumilivu, Hekima, Busara, Unyenyekevu, Subira, Usikivu na uzalendo

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Ni viongozi wachache Sana wenye moyo Kama alionao Rais mama Samia, Wenye uwezo wa kuvumilia kukosolewa na kila mtu na yeyote, mwenye uwezo wa kumsikiliza kila mtu bila kujari itikadi za kisiasa,mwenye uwezo wa kukaa mezani na yeyote kujadili masuala ya kitaifa,mwenye uwezo wa kusoma maandishi ya kila mtu bila kujali aina ya maandishi na mtu aliyeandika ,mwenye uwezo wa kusikiliza sauti zote bila kujari aina ya sauti na mahali zilikotoka

Ni wachache Sana wenye kifua Cha uongozi na ngozi ya kiuongozi Kama aliyonayo Rais Samia, Mama yetu anatambua mamlaka aliyonayo kikatiba na kisheria namna yalivyo makubwa, Rais Samia Anafahamu nguvu aliyonayo katika ulimi wake na mikononi mwake kupitia kalamu ya maagizo, anafahamu yeye ndiye Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama lakini huwezi ukamsikia akijivunia madaraka na mamlaka hayo aliyonayo kikatiba na kisheria.

Huwezi kumsikia akitoa lugha za vitisho kwa raia wake Wala maneno ya dharau au kuwakatisha Tamaa watu, Ni mama anayezungumza ukweli muda wote,Ni mama na kiongozi anayeongea uhalisia wa kinachoendelea katika serikali yake,Moyo wake umejaa upendo uvumilivu uzalendo unyenyekevu ujasiri Subira hekima na busara. Ni kiongozi anayetoa maneno katika kinywa chake yakiwa hayana ukakasi Wala kutisha au kukatisha Tamaa au kuwagawa watu

Tanzania Ina amani utulivu na upendo miongoni mwa watanzania kwa kuwa Rais Samia amekuwa kiunganishi Cha Taifa na Mfariji wa Taifa, kiongozi wa wote.karuhusu kutamalaki na kushamiri kwa Uhuru,watu wapo huru kuzungumza na kukosoa,watu wapo huru kueleza dukuduku zao bila hofu,hakuna mwenye Hofu Wala wasiwasi katika kutoa na kueleza hisia zao.Hii ndio sababu hata upinzani hauna ushawishi kwa watanzania kwa kuwa watu wanajisemea wenyewe kwa vinywa vyao na serikali yao inawasikiliza na kufanyia kazi maoni yao,hii yote Ni kwa kuwa Rais Samia Ni Msikivu na mvumilivu na kuwafanya watanzania kuwa na amani katika mioyo Yao,Hakuna aliyebeba sumu kinywani Mwake,Watanzania wanazungumza amani na upendo,Subira na uvumilivu, kuvumiliana na kuheshimiana, kupendana na kushirikiana.

Ukitaka ufahamu namna mh Rais mama Samia alivyomvumilivu na mwenye kifua Cha kiuongozi angalia namna ambavyo watanzania wengi wanavyokosa uvumilivu pale wanapokosolewa,unakuta mtu kwenye Ukurasa wake wa kijamii Kama vile Twitter au Facebook hata humu jamii forum akikosolewa kidogo unakuta anapolomosha matusi utafikiri Kuna mishipa ya fahamu imekatika kichwani,au unakuta ana wa block wote wanaomkosoa

Sasa Kama mtu siyo kiongozi na Hana mamlaka yoyote Yale lakini anakosa uvumilivu je Ni vipi atawavumilia watu wanaomkosoa pale Atakapokuwa na madaraka makubwa ya kutoa Amri? Ni vipi atakaa meza moja na mpinzani wake mkuu kutafuta suluhu na kujenga nchi kwa pamoja Kama afanyavyo mama yetu mpendwa mama Samia? Mtu wa namna hii akipewa madaraka makubwa ya kiuongozi Ni lazima atawaumiza wakosoaji wake kwa namna yoyote Ile atakayoona inafaa na itakayomhakikishia usalama masikioni mwake.

Ndio maana nasema kuwa itatuchukua miaka mingi Sana kumpata Rais Samia Mwingine Mwenye moyo Wa upendo uvumilivu Hekima Busara Unyenyekevu Subira Usikivu Na uzalendo , Mwenye uwezo wa kusikiliza sauti zote na kusoma maandishi yote bila kumuumiza mtu zaidi ya kuhubiri HAKI tu katika kinywa chake Msamiati ambao Ni mgumu na mchungu kutoka katika vinywa vya Baadhi ya Viongozi wa kiafrika waliopo Madarakani.

Watanzania Tuendelee kumwamini Rais wetu na Tuendelee kumuunga mkono Mama yetu na Tuhakikishe kuwa Tunamwombea uzima na Afya njema na kuhakikisha kuwa Uchaguzi ujao anapata Nafasi ya Kuendelea kuliongoza Taifa letu na kututumikia watanzania kwa moyo wa uzalendo na upendo Kama alio uonyesha kwa Sasa katika kuijenga nchi yetu na kuipeleka mbele kimaendeleo

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu:0742-676627
 
Hivi hauna Kazi nyingine za kufanya ?

Nb:Sijasoma na sotasoma bandiko lako nimesoma heading tu.
Kwani muda huu bado upo kazini? Au unaingia usiku? Mimi nafanya kazi zangu za kilimo mchana na siyo usiku maana huwezi ukalima na Giza
 
Hawa ni mamluki.
Wanatumiwa kuiconfuse jamii ili isiungane kumpinga mkoloni wa kijani
Watanzania Wana Imani kubwa sana na serikali hii ya CCM chini ya uongozi shupavu wa Mama Samia Suluhu Hassan. Wakoloni tulishawafungashia virago vyao Tangia miaka ya 60 huko na kubaki tukiijenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe
 
YA RABBI MOLA MUWEZA FANYA MAMA YETU KIPENZI HUYU AWE WA KWANZA NA WA MWISHO WA MITHILI YAKE KUJA KUTAWALA NCHI HII. NA IKIKUPENDEZA EWE MOLA LAINISHA NAFSI YAKE AACHIE MADARAKA KABLA HATA YA 2025 KWA HIARI YAKE AENDE KULEA WAJUKUU, AMIN.

Jamaa tafuta hata bustani upande mchicha uuze. Acha kujitoa ufahamu kwa kutarajia uteuzi.
 
We jamaa angalia basi hata kombe la dunia, we kila siku ni nyuzi za mama yako mwisho si atahisi unamtaka!
 
Tangu lini Mnyiha akawa na akili?
 
Mkuu huyu jamaa hajapewa asali tuuu inaonekana kahaidiwa hadi K
Hizo ndizo akili nilizosema kuwa watu aina yako waliokosa adabu hekima busara uvumilivu na malezi ya wazazi hamuwezi kuwa viongozi na Kama mkipewa uongozi itakuwa Ni sawa na kichaa kupewa rungu ambapo ni lazima wote watatwangwa tu vichwani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…