Itaje hapa shule ya Msingi ya Serikali inayotoa elimu kwa lugha ya kiingereza (English medium) iliyopo mkoani kwako

Itaje hapa shule ya Msingi ya Serikali inayotoa elimu kwa lugha ya kiingereza (English medium) iliyopo mkoani kwako

~ Tuanzie kwenye ada kwanza ni sh. Ngapi?
Halafu kwa nini hizo shule hazitangazwi ili wapiga kura wa sisiem wajue?

Hizo shule ni za wanasiasa na familia zao?
 
WIZARA ya Elimu, Sayansi na Ufundi imetoa waraka wa elimu kuhusu elimumsingi bila malipo na kutoa orodha ya shule za msingi 11 za Serikali ambazo hazihusiki na utoaji wa elimu bure uliotangazwa na Rais John Magufuli.

Elimumsingi inajumuisha elimu ya awali, ya msingi na sekondari ambayo itaanza Januari mwakani.

Katika Waraka Elimu Namba 6 wa Mwaka 2015 kuhusu utekelezaji wa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari, wizara hiyo imetaja shule hizo kuwa ni Shule ya Msingi Olympio (Dar es Salaam); Shule ya Msingi Diamond (Dar es Salaam); Shule ya Msingi Oysterbay (Dar es Salaam); Shule ya Msingi Iringa (Iringa) na Shule ya Msingi Mkapa (Mbeya).

Nyingine ni Shule ya Msingi Angaza (Mbeya); Shule ya Msingi Nuru (Mbeya); Shule ya Msingi Lupilisi (Ruvuma); Shule ya Msingi Tanga (Tanga); Shule ya Msingi Arusha (Arusha) na Shule ya Msingi Kisimani iliyoko mkoani Arusha.

Wizara hiyo pia imesema waraka huo hauzihusu shule zinazomilikiwa na mashirika ya umma ama taasisi za umma ambazo zinaendeshwa kwa taratibu sawa na shule za binafsi.

Katika waraka huo, wizara hiyo imetoa majukumu yanayotakiwa kufanywa na Wizara hiyo, Tamisemi, wakurugenzi wa manispaa na halmashauri ya wilaya, wakuu wa shule, bodi za shule, wazazi na wananchi.
Ahsante mkuu, Ina maana ndio hizi english medium za serikali tanzania nzima?
 
Ndugu mwandishi kuna error hapo, ya Tanga inaitwa Changa Primary School na siyo Tanga Primary!
 
Habari zenu wanabodi,

Kuna watu wengi hawafahamu kama serikali inazo shule zake za msingi za mitaala ya kiingereza (English medium) kwa gharama nafuu, Tusaidiane kufahamu majina na zilipo kwa kila eneo/mkoa hizi shule. Naanza

1. Olympio - Dar Es Salaam
2. Diamond - Dar Es Salaam
3. Magufuli - Mbeya
4. Mapinduzi - Gangilonga Iringa
5. Mkapa - Mbeya
6. Oysterbay primary school - Dar
7. Nyasa primary school - Kyela, Mbeya
8. Arusha primary school - Arusha
9. Angaza - Mbeya
10. Nuru - Mbeya
11. Iringa primary school - Iringa
12. Lupilisi - Ruvuma
13. Tanga Primary school - Tanga
14. Kisimani - Arusha
15....................................................
16........................................................
17.....................................................
18..........................................................
19.........................................................
20..............................................................


Karibuni wakuuu
siioni shule ya msingi Azimio, Mbeya au ndio hiyo inaitwa magufuli katika post #1
 
~ Tuanzie kwenye ada kwanza ni sh. Ngapi?
Halafu kwa nini hizo shule hazitangazwi ili wapiga kura wa sisiem wajue?

Hizo shule ni za wanasiasa na familia zao?
kama laki tatu hivi ukiachana na michango mingine
 
Ngoja nitie kambi hapa, huu uzi utanifaa. Morogoro hamna shule za namna hii
 
hapana hii magufuli ni mpya, mbeya kuna shule nyingi hivi, why kumependelewa?
sio shule za serikali tu hata shule za ccm ni nyingi Mbeya. kuna watu wameumia mpaka kufika hapa, nakumbuka 2001 wachuuzi wa soko la makunguru walikua wakitwangana na mgambo wa manispaa kila siku kupinga eneo lao kuchukuliwa na manispaa.

walituma wawakilishi Dodoma kumlilia mkapa awasaidie ( sijui kama ni kweli). Mkapa alisimama upande wa manispaa na lile eneo likatwaliwa kimabavu na kujengwa shule ambayo ikapewa jina la Mkapa kama shukrani kwa prezidaa.
 
Kila mkoa au wilaya kungekuwa na shule angalau moja za serikali zinazofundisha kwa kiingereza.
 
sio shule za serikali tu hata shule za ccm ni nyingi Mbeya. kuna watu wameumia mpaka kufika hapa, nakumbuka 2001 wachuuzi wa soko la makunguru walikua wakitwangana na mgambo wa manispaa kila siku kupinga eneo lao kuchukuliwa na manispaa.

walituma wawakilishi Dodoma kumlilia mkapa awasaidie ( sijui kama ni kweli). Mkapa alisimama upande wa manispaa na lile eneo likatwaliwa kimabavu na kujengwa shule ambayo ikapewa jina la Mkapa kama shukrani kwa prezidaa.
Kwa hiyo chief, ndio chanzo cha kujengwa shule zote hizo za msingi kwa mtaala wa kiingereza
 
Habari zenu wanabodi,

Kuna watu wengi hawafahamu kama serikali inazo shule zake za msingi za mitaala ya kiingereza (English medium) kwa gharama nafuu, Tusaidiane kufahamu majina na zilipo kwa kila eneo/mkoa hizi shule. Naanza

1. Olympio - Dar Es Salaam
2. Diamond - Dar Es Salaam
3. Magufuli - Mbeya
4. Mapinduzi - Gangilonga Iringa
5. Mkapa - Mbeya
6. Oysterbay primary school - Dar
7. Nyasa primary school - Kyela, Mbeya
8. Arusha primary school - Arusha
9. Angaza - Mbeya
10. Nuru - Mbeya
11. Iringa primary school - Iringa
12. Lupilisi - Ruvuma
13. Changa Primary school - Tanga
14. Kisimani - Arusha
15. Azimio - Mbeya
16. Nyanza primary school - Mwanza
17. Nyakahoja primary school - Mwanza
18..........................................................
19.........................................................
20..............................................................


Karibuni wakuuu
Changa inamilikiwa na serikali?
 
Screenshot_20200716-153017.png
 
Back
Top Bottom