Itakuaje siku Diamond akiwaomba radhi clouds TV?

dogo hapo ni wale vindakindaki WCB hawezi kukuelewa hata umpe facts gani anakupotezea mda a ah
 
Mwaka mzima hamjapiga hata nyimbo moja ya WCB na jamaa hawajafeli,sasa utasemaje CMG inashikilia WCB .WCB mwanzo ndio ilikuwa in revolve around WCB and Diamond family's,lkn sasa hivi wasanii washaanza kuwa support na kugundua nguvu ya WCB ,hadi sasa kuna interviews za wasanii kibao zimefanyika,wasanii sasa hivi wanafanya mpaka jingo,Ben pol,Jux,Giggy,Young dee,Country boy etc wanahang out na kushirikiana na WCB na sikia mwanzoni CMG walikuwa wanawapiga mikwala (Bado huoni jamaa influence yao inazidi shuka).

MIMI NARUDIA TENA 100% CMG INAENDA KUDROP NA SOCIAL NETWORKS ZITA TAKE OVER NA SYSTEM ITABADILIKA ILI MSANII UWEZE SURVIVE BASI UNATAKIWA UWE MZURI KUTUMIA SOCIAL NETWORKS,kwani social networking sasa hivi zimekuwa kama kilevyi mtu yupo tayari akose kula lkn si bando.Ipo siku nitakukumbusha hii thread.

Ila kwako wewe unaona sawa huu mfumo wa kibepari ambao unawakandamiza wasanii au wewe ni mnufaika au wewe unaona sawa kutengeneza mastaa masikini wenye majina makubwa kwa kigezo cha promo.
 
dogo hapo ni wale vindakindaki WCB hawezi kukuelewa hata umpe facts gani anakupotezea mda a ah
Wewe je ni kindakindaki wa CMG.Unataka nipewe facts wakati wewe mwenyewe,umeshindwa kutoa facts unaleta stori za vijiwe vya kawaha,bring here tangible evidence (reference).kutoka ktk taasisi husika umeshindwa,alafu unataka facts.
 
Hakuna sehemu nimesema CMG inashikiria WCB, bali nimesema inashikiria mziki waTz bado na nikakwambia wasanii wa WCB ni 0.001 ya wasanii wote wa TZ vituo vyao vya habari havijaweza wasaidia wasanii wengine kama ambavyo Salam alikuwa anajinasibu kuwa Diamond kaja kuwa mkombozi wao maana ukifuatilia vituo vya WCB vina revolve around WCB na familia ya Mond.
Mikwara wapi hayo maneno ya mtaani, Diamond ameanza gombana na WCB na anawapiga majungu lakini wao waliendelea piga nyimbo zao mpaka pale ambapo majungu yaligeuka kuwa wazi wazi.
Same applied to Ruby, watu walikuwa wanasema Ruby kagombana na Ruge ila nyimbo zake ziliendelewa pigwa mpaka pale alipoanza kumshambulia bila amfumbo Ruge.
Hata JD nyimbo zake zilipigwa mpaka alipozuia mwenyewe zisipigwe.
Diamond kugombana na ruge ilikuwa ni hype aliyotumia kupandisha vituo vyake status wakati anavizindua maana kwa ku plan matukio hajambo.
Tujipe muda ni maana toka ameondoka CMG haujatimia hata mwaka ngoja tusubiri mwaka upite hata wengine wali survive zaid ya kipindi hiki.
 
Nyie Wa dar ndo mnajua hayo yote sisi huku shy,mbeya tunajua kuna clouds tu hao wachafi Malaya hatuwajui hata
 
Diamond alivyokuwa akihojiwa na Lil Ommy aliliongelea hili,la wasanii kukataa kuhojiwa na WCB ,mwanzo walikuwa wanachomoa.

Mwaka ushaisha huu trending,charts zote zao.Diamond haitaji gombana na Ruge ili apandishe vituo vyake sababu ni yeye master mind wa social networks ambayo ina nguvu kuliko Ruge na anajua kufanya biashara ya mziki,hizi ndizo sifa za Diamond na WCB.Kila chenye mwanzo kina mwisho kulikwa na Radio free,Radio One zote zime drop ,ndio ikaja Clouds nayo ita ddrop na hata hao WCB nao wakizingua wata drop.

Angalia beef zao za kijinga zimemuathiri mpaka Millard Ayo views zimepungua Youtube,wenzake GPL (SUBSCRIBER 1M+) na Dizzim washaanza kumpita.
 
Diamond single moja tu anaifanyia tukio ije kuwa kuipa hype tv na redio yake.
Diamond akihojiwa uwa anasema lolote hata uongo na ukweli ndani. Bahati mbaya tulisikia kutoka upande mmoja tungesikia na kutoka CMG ila ubaya ni kwamba Ruge akigombana na mtu uwa hamwongelei kabisa kabisa kama ni fitina atakuwa anazifanya pasipo kumwongelea.
Unajua muda haudanganyi so ngoja tusubiri huenda mwakani siku kama ye leo tutakuwa kwenye hii thread imefukuliwa tukiongea kuhusu nani kafail na nani kawin. Tuombe uzima
 
Mimi ni mtizamaji wa Wasafi TV nililiona hilo na hata Lili Omy aliliona hilo na ndio maana akamuuliza.Hii industry ina hela tatizo ubabe wa washika dau na kufanya mambo kishikaji,wasanii wanaumia na tukisema iendeshwe kisomi kama mbele,hao ndugu zako wataumia
 
Turudi kwa msanii wake Rich Mavoko anasemaje kuhusu hilo, mbona aliondoka kwa madai ya kunyonywa na mpaka sasa wanavutana mara wapelekane BASATA.
Kiface mwenyewe kwenye interview anadai alikuwa anampa 5000 kwa siku wakati kipindi hicho alikuwa anakuja humu anatutambia kuwa analipwa ela ambayo hata wafanyakazi serikalini wenye vyeo wanaiota.
Aisee kuwaamini hawa watoto ni kazi sana.
 
Nimekujibu hili swali ,rudia post zangu utaona.
 
Nimekujibu hili swali ,rudia post zangu utaona.
Trust me hakuna siku kitu kitakuwa juu kikose malalamiko, hata hao WCB ipo siku utasikia mengi ipo siku utasikia Rayvanny hana hiki hana kile alikuwa tu ana brag, unakumbuka wakati ITV iko juu, watu walikuwa wanamlaumu mengi kuwa anawalipa ovyo wafanyakazi wa IPP sema kwakuwa mengi siyo mtu wa mchezo mchezo na social media platforms hazikuwa nyingi ndiyo maana mambo yalikuwa haya trend.
Tuombe uzima WCB waanzishe WASAFI festival wawashirikishe na wasanii wengine wengi then utaanza sikia habari sasa.
 
The Boss haya maugomvi mengine ni upumbavu fulani wa roho mbaya na kupenda kuwa bwana mkubwa daima milele na milele,
Ikiwa leo Korea kasikazini na kusini wanaweka pembeni maugomvi yao kwa zaidi ya miaka sabini sisi kwanini tusijiulize?
 

Unataka kuniambia WCB hawajaitetemesha clouds? Clouds ishajifia mzee Baba! Hao Shilawadu hawana Cha kuongelea maana umbea wote WCB , XXL hawana ngoma kali ya kupiga maana Ngoma zote Kali WCB, Wamebaki akina Kibonde tuu Na Mbwiga
 
We si mzima sasa hao SETUP kudevelop 2 websites ndio kunaifanya WCB iwe sehemu ya CMG,IT gani hiyo uliyosomea wewe sikia,mimi mwenyewe nipo katka IT Industry nime specilize katka Networking (Routing,Switching na Security),nina jamaa zangu ni madeveloper,kwa hiyo huwezi nidanganya.

Hao Set up ni kamapuni kama uonavyoona kampuni za kujenga,sasa kisa jamaa waliojenga jengo la NSSF ,wakija kujenga kwangu ndio inawafanya NSSF kuwa wamiliki wa Nyumba yangu na kwa kuwa wao ndio walio develop WASAFI ni jukumu lao kufanya development na maintance hapo chini wameandika.Ngoja nikuambie katika Programming (nina uhakika hata language moja hujui) kila mtu ana style yake ya kuandika code zake na ndio maana wao ndio waliyoitengeneza na wao ndio wanatakiwa kufanya development na maintanance ya Website yoyote ile walioitengeneza,sababu code zilizotumika ni zao,acha uongo.

Ukitaka umiliki wa kampuni yoyote ile Tanzania taasisi inayohusika ni BRELA,nilikuambia kuna mdau hapa alimwaga data za uhakika 100% kuhusu wamiliki wa EFM,acha stori za kwenye vijiwe vya kahawa.
 
Clouds inapumulia milija sasahivi,zile enzi za kuwakalilisha mashabiki wa muziki kwamba msanii wanaomtaka ndo mkali zimeshapita,wasanii hawana hofu kama zamani tena,WASAFI MEDIA ITAIMALIKA MARADUFU na itakuwa zaidi ya hapa,sasahivi ni TV tu lakni mawingu wamesanda,TV INAYOONGOZA KWA KUTAZAMWA SASAHI NI WASAFI TV,bado radio ikianza kurusha matangazo ndo balaa..Wanachotakiwa WASAFI TV sasahivi nikuwalipa vizuri wasanii wengine kwenye WASAFI FESTIVAL inayoanza soon..Nyakati za kutengeneza wasanii masikini zimepita na zinatakiwa kukemewa na wasinii wenyewe..Nchi kama NIGERIA msanii akitoa nyimbo hata tano tu na akawa msanii mkali unakuta ana mijengo na usafiri wa maana,lakn bongo msanii Anatoa heat 10 lakini bado amepanga ,yote hayo nikwasababu kulipwa LAKI 3 za fiesta..
 
Hahahaha..wabongo bhana..kwahiyo hao wasanii wanategemea tu fiesta,hakuna show nyingine??
 
dogo umapiga sana kelele na kushinda jf kujiona mjuaji...haya baki na ujinga wako ukijipa moyo dogo anatoboa kumbe nyie washika kamera wa dogo na wajibuji mitandaoni mnaektiwa
 
dogo umapiga sana kelele na kushinda jf kujiona mjuaji...haya baki na ujinga wako ukijipa moyo dogo anatoboa kumbe nyie washika kamera wa dogo na wajibuji mitandaoni mnaektiwa
Huna unachokijua kuhusu IT ndio maana unapayuka.Mimi sio mjuaji bali najua ninachokifanya na ndio maana nimekufafanulia ki professional zaidi, kama una hoja za kupinga hiki nilichokiandika kiweke hapa, lkn si kuzusha uongo.Sasa ukitaka kujiona ww mjinga nenda ktk jukwaa la science and tech alafu mtafute programmer yoyote mtag hii comment yako, alafu uone utakavyo chekwa na ujinga wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…