TANZIA Jackson Makwetta (Mbunge na Waziri wa zamani) afariki dunia

TANZIA Jackson Makwetta (Mbunge na Waziri wa zamani) afariki dunia

Sumaye alikuwa hampendi huyu mzee kwa sababu mzee makweta alipo kuwa wazri wa kilimo sumaye aliku naibu wake sumaye alishindwa kuiba kutokana na huyu mzee kukaba mpaka penati mambo yaka mgeukia dingi sumaye alipo kuwa pm mzee akaanza kutoswa . Kalale pema peponi mzee
 
hawa ndo wangestahili hata kuzawadiwa v8 kwa utumishi wao badala yake eti Shimbo ndo anapewa v8 ...Mungu amtangulie.amen

umetamka kitu kikubwa sana..wanaohusika wamekisoma!!!!!!!!!!!
 
R.I.P Jackson, tutakukumbuka kwa kuwa msema ukweli daima. Mfano, siku ile unamtambulisha Sumaye bungeni kwa mara ya kwanza kama waziri mkuu.
 
Bila kutafuna maneno Marehemu Kighoma Ali Malima ni waziri wa kwanza wa Elimu TZ aliebadilisha mfumo wa majina kwenda mfumo wa namba ktk mitihani ya sekondari baada ya kugundua ubaguzi na uchujaji wizarani!

Huyu ni Waziri bora kabisa alieiongoza Wizara ya elimu miaka ya 80 na kuleta mageuzi makubwa ktk wahitimu na kusababisha lawama kubwa toka upande wa pili na kumshinikiza Rais Mwinyi kumbadilishia Wizara!

Mmmmh...
 
This is sad. He Jakson Makweta was a rare "brand". I once introduced myself to him and when he wondered who was I? I told him he need not wonder as I new him from when I was a kid and am proud of his services as a senior citizen of this country. We had a good laugh. Unfortunately it was during the time that he was sidelined for the reasons that Mkapa and Sumaye know better.
You mean that he was supposed to be a minister during Mkapa era?
 
Ni aliyekuwa mbunge wa huko Njombe na waziri katika serikali ya awamu ya kwanza na ya pili Mhe. Jackson Makwetta amefariki dunia jioni ya leo.

Alazwe pema peponi

Chanzo: Ndugu wa karibu na marehemu.

Mungu amlaze pema mzee wetu!! Naamini ni pigo kwa watanzania wote.
 
RIP MAKWETA. Waziri bora zaidi wa elimu. Tutakukumbuka daima
 
Mzee huyu alikuwa ni miongoni mwa viongozi wachache wa CCM waliotumikia taifa lao kwa uadilifu na kwa uzalendo wa hali ya juu, akiwa waziri wa serikali kwa miaka 25 mfululizo (1975 - 2000), lakini hakuna mahali alitumia vibaya madaraka yake kwani inasemekana kwamba hata nyumba ya kuishi nje kidogo ya jiji la Dar-es-salaam alijengewa na wanae kabla ya kustaafu na hata hivyo haikukamilika ipasavyo; na katika kipindi karibia chote cha ustaafu wake alikuwa anaishi kwao kijijini;

Lakini kwa vile serikali yetu ya CCM haijali watu kama hawa, msiba wake utaendeshwa kinafiki tu; Misiba yenye kupewa uzito ni ile ya viongozi wasiokuwa wazalendo ambao utashi wao unapimwa kwa utajiri wao; Lakini ipo siku yote haya yatabadilika;

Poleni wafiwa; Mwenyezi mungu amlaze mahali pema peponi Mzee wetu Makweta, Amen;

waupe hadhi kama msiba wa rejia mtema ulivyopewa hadhi!
 
Apumzike kwa amani mzee Makwetta. Hawa wazee waliishi kwa uadilifu kweli kweli walipokuwa katika utendaji!!!!
 
Eti kwetu Njombe, huu ni unafiki mbona mlimnyima ubunge katika uchaguzi wa kura za maoni ndani ya CCM 2010? Mnamkumbuka wakati amekwishatangulia mbele ya Mwenyezi Mungu? Kweli wengi mtakwenda motoni kwa unafiki wenu. R.I.P ya dhati Makweta.

Mbona unatukana? Habari za uchaguzi sio mahali pake hapa, kama ujuavyo,chaguzi zetu ni sarakasi tupu. Nazungumzia kumbukumbu za Marehemu Makweta ambazo hata saa hizi ukienda Njombe zipo na zitaishi. Suala la Elimu linajulikana kwa wengi wenye akili timamu. Kama ni kusimamia maendeleo jimboni kwake na taifa alifanya, sasa unataka tusiseme?
 
RIP Makweta,
Poleni sana wafiwa na Watanzania wote kwa ujmla.
 
Eti kwetu Njombe, huu ni unafiki mbona mlimnyima ubunge katika uchaguzi wa kura za maoni ndani ya CCM 2010? Mnamkumbuka wakati amekwishatangulia mbele ya Mwenyezi Mungu? Kweli wengi mtakwenda motoni kwa unafiki wenu. R.I.P ya dhati Makweta.

Inapendeza kupokezana vijiti ktk uongozi, hata kama una mazuri mengi kama alivyokuwa marehemu, ni muhimu kukaa pembeni na kuona wengine nao wakichangia. Hili la kumpinga ktk uchaguzi halifuti mema yake kwa Wananjombe na taifa kwa ujumla. Kama unaona kuna unafiki basi achana nao,tujifunze mazuri yake na tuyaenzi.
 
Kijijini kwetu tunamkumbuka sana kwa jinsi alivyopigana kiume mpaka tukapata barabara na RTC enzi hizo akiwa mbunge wa njombe ( Ludew,Makete,Wanging`ombe zilikuwa bado kumegwa). Kweli watu wazuri wanakufa yanabaki manung`ayembe yanayotuhangaisha.

Kwa njombe, alipigania elimu sana kupitia NDDT, shule zikafunguliwa kwa wingi. Mungu amekupenda zaidi.

RIP MAKWETA.
kwani sasa si mna madam speaker si na yeye anafanya makubwa tu ndugu yangu
 
Ni kwa sababu alikuwa mbunge kwa muda mrefu na hakutumia uwaziri wake kuiba mali ya umma ili kupeleka miradi ya maendeleo kwa wananchi kwa fedha za ufisadi kama wenzake waliokamata nyadhifa hizo;

Hiyo ndiyo tofauti na Mawaziri wa sasa. Mzee Jackson Makweta alikuwa anafahamu wajibu wake kwa Taifa zima. "A true statesman" Ndiyo maana hakujipendelea au kupendelea jimbo lake pekee kama wanavyofanya viongozi wa sasa tena kwa pesa za kifisadi ambazo ndizo zinasababisha mikataba isiyokuwa na manufaa kwa Taifa. Waziri na mbunge anauza Taifa zima kwa ajili ya jimbo moja! Ni fedheha tupu!
RIP Mzee Makweta.
 
Back
Top Bottom