Jafo: Wakurugenzi watakaoshindwa kupata 50% ya mapato hadi Januari wanaweza kuwekwa pembeni

Naiona kodi ya kichwa ikirudi kwa kasi kama enzi za ukoloni, tujiandae kisaikolojia.

Maana uwezo wa kutafuta vyanzo vipya vya mapato bila kugusa wanyonye sidhani kama wanao hao wakurugenzi.
 
Sawa msemaji mdogo wa serikali, but sifahamu hao wawekezaji wapya watatoka wapi kama waliopo kila siku wanalalamika kodi kubwa zisizoendana na kipato cha biashara zao, hivyo wengi kuishia kufunga biashara zao kwa sababu ya kulemewa na mzigo wa kodi unaotokana na presha wanayoipata wakurugenzi kwa sababu ya matamko kama hilo la Waziri Jaffo.
 
Wangoje Januari mbali hivyo, hii ni kuanzia kesho unagongewa geti na Jamaa wanakwambia wanakagua mazingira hujakata fensi faini shilingi elfu 50.

Hao wa juu wanaona raha tu kutamka ila kivumbi ni huku chini.
 
Wangoje Januari mbali hivyo, hii ni kuanzia kesho unagongewa geti na Jamaa wanakwambia wanakagua mazingira hujakata fensi faini shilingi elfu 50.

Hao wa juu wanaona raha tu kutamka ila kivumbi ni huku chini.
Unakumbuka wale askari wa usafi wa Makonda ?
 
Nadhani wewe ndio msemaji mkuu wa kambi hiyo. Usijali kabisa mambo bambam
 
Wakurugenzi mnachuma Malipo ya Dhambi zenu ya kuwafanyia figisu Wapinzania
 
View attachment 1656956

Hayo yamesemwa na Waziri wa Tamisemi Mh Jaffo alipokuwa akiongea mkoani Njombe....
Sasa hao MaDED hizo fedha wanazolazimishwa kukusanya, wananchi watazitoa wapi kama uchumi umedorola? Hawa Mawaziri wasiotumia akili hawapaswi kupewa hadhi hiyo kwani wanabwabwaja tu ili mradi wasikike na bwana mkubwa kuwa nao wapo!!
Kwa mtindo huu mtawafukuza MaDED wengi ili mpate nafasi ya kuwateua ndugu zenu!!
 
Laana ya kushiriki unyama wa uchaguzi imeanza kuwatafuna MA DED
 
Wawatoe tu hawa ndio walioipitisha CCM kwa magumashi bila kusimamia misingi ya kidemokrasia sasa ni zamu yao kuonja joto la jiwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…