Jaji aliyemhukumu IGP Masengeli kifungo jela apokonywa walinzi; Jaji Mkuu Koome ataka warejeshwe mara moja

Jaji aliyemhukumu IGP Masengeli kifungo jela apokonywa walinzi; Jaji Mkuu Koome ataka warejeshwe mara moja

Ikaria

Member
Joined
Jul 17, 2019
Posts
93
Reaction score
238
Jaji wa Mahakama ya Juu Lawrence Mugambi amepokonywa walinzi wake siku tatu tu baada ya kumhukumu kifungo cha miezi 6 jela Kaimu Inspekta Jenerali Mkuu Gilbert Masengeli, kwa kosa la kudharau mahakama.

Kufuatia kitendo hicho Tume ya Huduma za Mahakama(JSC) ikiongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome imehutubia Wanahabari ikitaka Idara ya Polisi kumrejeshea Jaji Lawrence Mugambi walinzi wake mara moja.

Jaji Lawrence alimhukumu IGP Masengeli Ijumaa iliyopita lakini mpaka sasa IGP hajajisalimisha kwa Mkurugenzi wa Idara ya Magereza kama alivyoagizwa na mahakama. Ikumbukwe mahakama iliongeza kuwa iwapo IGP hatojisalimisha, basi Waziri wa Mambo ya ndani Professor Kithure Kindiki atoe agizo la kukamatwa kwake.

20240916_145810.jpg
20240916_145812.jpg
20240916_145816.jpg
20240916_145818.jpg
 
Democrasia Africa ni maigizo tupu

Nilisoma andiko moja Jana linasema mahakama inayo haki kisheria kutoa hukumu kwa kaimu IGP wa Kenya ila vyombo vinavyohusika na ukamataji na uhifadhi wa waharifu na wizara ya ulinzi na usalama kiujumla havina mamlaka ya kumkamata huyo mkuu kumpeleka gerezani labda aamue kujisalimisha mwenyewe.

Huko ndiko tunaambiwa kuna kiwango kikubwa cha demokrasia, ni miezi kadhaa tu imepita toka mahakama itoe katazo la kupeleka polisi Haiti ila serikali ilipuuza.
 
Kwa Hali ilivyo,Kaimu IGP ,lazima atalamba jela,nakibarua kinakwisha
Vinginevyo awe mkimbizi
 
Yeye ajisalimishe tu! Aanze kutumikia kifungo chake mapema. Akumbuke sheria ni msumeno
 
Jaji wa Mahakama ya Juu Lawrence Mugambi amepokonywa walinzi wake siku tatu tu baada ya kumhukumu kifungo cha miezi 6 jela Kaimu Inspekta Jenerali Mkuu Gilbert Masengeli, kwa kosa la kudharau mahakama.

Kufuatia kitendo hicho Tume ya Huduma za Mahakama(JSC) ikiongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome imehutubia Wanahabari ikitaka Idara ya Polisi kumrejeshea Jaji Lawrence Mugambi walinzi wake mara moja.

Jaji Lawrence alimhukumu IGP Masengeli Ijumaa iliyopita lakini mpaka sasa IGP hajajisalimisha kwa Mkurugenzi wa Idara ya Magereza kama alivyoagizwa na mahakama. Ikumbukwe mahakama iliongeza kuwa iwapo IGP hatojisalimisha, basi Waziri wa Mambo ya ndani Professor Kithure Kindiki atoe agizo la kukamatwa kwake.

View attachment 3097466View attachment 3097469View attachment 3097471View attachment 3097472
No way
How come only the Judiciary need extreme superiority over other pillars of the government? How come the soldiers be willing to protect the judge who disrespected their boss? There are ways to deal with such a higher authority notto show your superiority over other pillars
 
Democrasia Africa ni maigizo tupu

Nilisoma andiko moja Jana linasema mahakama inayo haki kisheria kutoa hukumu kwa kaimu IGP wa Kenya ila vyombo vinavyohusika na ukamataji na uhifadhi wa waharifu na wizara ya ulinzi na usalama kiujumla havina mamlaka ya kumkamata huyo mkuu kumpeleka gerezani labda aamue kujisalimisha mwenyewe.

Huko ndiko tunaambiwa kuna kiwango kikubwa cha demokrasia, ni miezi kadhaa tu imepita toka mahakama itoe katazo la kupeleka polisi Haiti ila serikali ilipuuza.
Katika mihimili mitatu, upi una nguvu? Hii ni vita ya mihimili, kama unashindwa kumheshimu IGP iweje yeye akuheshimu?

Tanzania IGP hawezi shitakiwa kijinai hadi aondolewe hadhi ya kuwa IGP. Hata askari wa cheo cha chini kabisa, hashitakiwi hadi aondolewe hadhi ya kuwa askari.

1. Lazima ashitakiwe kijeshi na kukutwa na hatia
2. Hatia aliyokutwa nayo iwe ni ile inayopelekea afukuzwe kazi na kufikishwa mahakama zakirai
3. Akisha fukuzwa jeshini, ndipo hukabidhiwa kwa mahakama.

IGP siyo mtu mdogo, nilisema tangu mwanzo, huu ni mtego wa kikatiba na ki mhimili. Nani atakubali IGP afikishwe mahakamani kabla ya kumvua madaraka yake?

Judge alichemka na ameingiza nchi kwenye migogoro ya kimhimili kwa kutopambanua hadhi ya IGP
 
Back
Top Bottom