Jaji Bomani umenena:CCM waachane na wazo la Serikali 2


Kila jambo na wakati wake,sasa ni wakati wa kubadilisha mfumo wa muungano,kero za muungano 18-21 mpaka leo hii hazijaweza kutatuliwa kwa mfumo wa serikali 2.Pia wewe huoni kuwa zanzibar wameshajiandaa kujitegemea kwa kila kitu?Jee mmesha wahi kuwaeleza wananchi kwa nini mnataka serikali 2 zaidi ya kusema habari za nyerere?muungano uliopo ni maamzui ya watu 2 nyerere na karume tuu haukushirikisha wananchi,sasa ni wakati wa kushirikisha wananchi wote.NYIE MA CCM ya bara mnatumiwa na wanaccm wachache wenye uchu wa madaraka huku bara bila ya nyie kujitambua!!!

Wewe huna elimu hata chembe ya waliyonayo hao wazeee!elimu ya kuwadia ma miss utaiiata elimu nayo?sema hapa sababu zako za kung'ang'angania serikali 2 ni kuone kama una kitu kichwani
 
Jamani wale wenye kumbukumbu vizuri naomba mnikumbushe. Hivi CCM imezaliwa mwaka gani?
Mkuu, kateleza tu hapo ila ni kwamba alimaanisha kujiunga na TANU. Tatizo letu ni kubadilibadili majina ndio maana hata ukimuuliza waziri mkuu Tanzania ilipata uhuru wake mwaka gani, atakujibu tarehe 9 December, 1961!!!!!!!!! Ila mzee Bomani katoa nasaha bora mno kwa chama chake.
 
- Kichwa cha maji huwa kinajisema chenyewe kaka, huyu bomani ni mnafiki asingekuwa angesema enzi za MWalimu, wale wote ambao hawakusema then wanyamaze wamuchaie Kasaka Njelu aseme!1

Le Mutuz

Kamfufue basi Nyerere,sisi tunazungumzia 50yrs to come wewe unaleta habari za 50yrs backward!!!
 
- Wanafiki na besides leo 2014 hatuwezi kuamuliwa maamuzi na watu walioongoza wakati hatujazaliwa man, enough!!

Le Mutuz
Sio kweli mkuu. Kama ndio msimamo wako huu basi Biblia haifai wakati huu.
 
- Kichwa cha maji huwa kinajisema chenyewe kaka, huyu bomani ni mnafiki asingekuwa angesema enzi za MWalimu, wale wote ambao hawakusema then wanyamaze wamuchaie Kasaka Njelu aseme!1

Le Mutuz
Duh! Nilidhani umelelewa kiutu kumbe ndio hivo ulivo, nahisi hata wazazi wako huwaheshimu.
 
Ni wachache mno humo CCM wanaotaka nchi hii iwe na migogoro siku zote. Kwa mfano ZNZ wale waliokuwa wakipinga maridhiano kati ya CUF na CCM mpaka kumlazimisha Rais Karume kuwa mkali ndio hawa hawa wanaotaka kulishana yamini katika kupinga maoni ya wengi katika rasimu hii. Hapa inatakiwa itumike busara ya Rais Kikwete na Shein (kama alivofanya Kikwete na Karume katika kupata maridhiano) katika suala hili kwa manufaa ya nchi yetu.
 
mkuu siasa haina ukongwe kwa sababu hubadilika kulingana na wakati kila jambo na wakati wake mkuu huzi zama siyo zile za kipindi kile acha habari zako kabisa.

Umenena vyema, hizi sio zile 'zama', ndio maana serikali tatu zinahitajika
 

Wewe Le Mutuz, umesahau Baba yako alipokuwa waziri mkuu? Unakumbuka alichokisimamia kuhusu muundo wa Muungano? Kwa nini unawaita wazee wenye fikra pevu wanafiki? Usiwe msahaulifu wa histroria, ungeanza kwa kutoa comment kumhusu Baba yako kwanza.
 

Enzi za Nyerere Zanzibar walikuwa bado hawajavunja Katiba ya JMT na kuunda Katiba yao - ambayo imeongeza utata wa kero za Muungano. Ikumbukwe kuwa ni utawala wa CCM uliokuja baada ya Mwalimu ulioruhusu uvunjivu huo. Kwa hivyo, yale matumaini kidogo yaliyokuwepo kwamba pengine tungeelekea kuwa na serikali moja yametoweka KABISA. Basi katika muktadha kama huu, suluhisho muafaka ni serikali tatu. Mintaarafu hoja hii, huwezi kabisa kuwalaumu vijana wa zamani kuwa ni wanafiki. Badala yake ungewapongeza kwa kuangalia mambo kufuatana na mazingira yaliyopo badala ya kung'ang'ania ukale na 'zidumu fikira za mwenyekiti' ambazo tayari zimekuwa mgando. In fact, hawa vijana wa zamani wana fikira za kiukombozi kuliko vijana wa leo waliopofushwa na fikira za kifisadi! Wanaonufaika na muundo wa serikali mbili ni watawala, period. Kwa mfano, watawala wa kutoka upande wa Zanzibar wanaona watapoteza marupurupu ya serikali ya JMT ikiwa ni pamoja na nyumba za serikali walizogawiwa bure pale Oysterbay. Hawa ni lazima walishane viapo kulinda sera ya serikali mbili. Lakini mwananchi wa kawaida wa Zanzibar hana anachopoteza. Watawala wa upande wa Tanganyika wanahofia muundo wa serikali tatu kupunguza nguvu ya CCM kuendelea kubaki madarakani.
 

huna lolote zaidi ya ushabiki wa kijinga! dr slaa alisema ataanzisha mchakato wa katiba mpya ndani ya siku 100! katiba ni mali ya wananchi na hatutungi katiba mpya ya mizigo,hivyomagamba waachane na ndoto ya sera yao!
 

Le mutuz salaam,

which is better?? tuwe na serikali moja tu, maana hata hizi mbili does not make sense, Zanzibar iwe dissolved basi

Nyerere ni kama Mbowe leo hii, people never questioned him, akina Kambona, malecela sr, Jumbe, tuntemeke sanga, etc wote waliowahi kujaribu kumuuliza au kuwa na mawazo tofauti hawakuishia pazuri
 


Bange tamuuuu sana!!! by Obama
 
Wanaotetea serikali 2 hawana hoja zaidi ya kutoa kashfa na matusi kwa wazee wa watu.... Kwa miaka 50 muundo huu umeishindwa sio tu kutuondolea kero za muungano bali pia umeshindwa kusukuma maendeleo mbele... CCM Znz ndo wanafiki wakubwa.. Kama wanataka serikali 2 kwanini walibariki mabadiliko mkubwa ya Katiba ya Znz yenye tafsiri ya Kuvunja muungano?


Teteteni kwa hoja sio matusi,, tutaondoaje the so called kero za muungano kwa mfumo wa serikali 2,, ambao umeshindwa kwa miaka 50...? Huku kuhoji eti wakina warioba na boman walikuwa wapi kuhoji kipindi cha Nyerere,,, ni hiyo isiyo na mashiko... Hivi kila alichokiasisi Nyerere kimegeuka kuwa msahafu ambao haufanyiwi marekebisho.... Mbona hamhoji Azimio la Arusha, mbona mnauza viwanda vyetu, mbona mnagawana nyumba za serikali, mbona mnaua elimu yetu, mbona mnazurumu ardhi wananchi, mbona mnawakumbatia mafisadi?

Msimtumie Nyerere kwenye suala la serikali tatu.... Kama mlimwamini msingevunja na kuvuruga misingi ya taifa...

wanaotaka serikali mbili ni wale wale ambao wanataka waendelee kuwepo madarakani kwa kutumia fedha chafu na mfumo mbovu ili waendelee kujinufaisha... Watanzania hamtudanganyi tena,,, dawa ni serikali tatu. Tu...
 
Jamani Zanzibar na Tanganyika zote zife kuwa Tanzania huru kama ilivyo sasa Tanganyika haijatendewa haki kufa peke yake ! ni mwungano gani huo maajabu hayo muyaone viongozi wetu;ukitaka kumuua nyani usimwangalie uso.
 
Wakati ule ni zamani, sasa tunahitaji mabadiliko, nyie wenye fikra mgando msiotaka mabadiliko ndo mnatukwamisha, hao wazee wanaelewa sana tu! wanajua kuwa sasa ni muda mwafaka wa serikali tatu! mabadiliko huwa ni ya taratibu sasa tumefika muda wake!Tunaelewa vizuri sababu zenu! bahati nzuri M/Kiti wenu taifa kashawaambia mjiandae kisaikolojia,badilikeni acheni upuuzi! Na wewe mleta mada unataka kujifananisha na hao wazee, we rudi zako kwenye udaku kule ndo zaizi yako hao ni wataalaam dont try........
 
Kile tunachokiogopa ndio kitatokea kweli. Waasisi wa Taifa letu hawapaswi kutulazimisha nini cha kufanya kwenye mazingira yetu. Nafikiri cha msingi ni kuboresha namna tutakavyo kwenda mbele kama Taifa tena kwa hoja na kuelimishana kuliko vitisho au lugha za kukejeriana. Hatutaweza kuzuia watu watakachoamua kama tukijaribu kulazimisha mambo.
 
Mkuu, umenena vilivo sasa hatutaki kuburuzwa na akili ndogo kuongoza akili kubwa. Azimio la Arusha limesema:- Tumenyonywa kiasi cha kutosha, tumeonewa kiasi cha kutosha na tumenyanyaswa kiasi cha kutosha............... Sasa basi.
 
Jaji Bomani yuko sahihi kabisa. CCM=TANU+AFRO-SHIRAZ vyama ambavyo vimekuwepo tangu miaka ya 1950s. serikali tatu ni chagua la wananchi si la CCM.ni kosa kwa chama kuteka agenda ya katiba na kuifanya yake. Wananchi ndio waamuzi number 1 sio chama chochote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…