Uchaguzi 2020 Jaji Kaijage ana nafasi nzuri ya kutengeneza historia na hata kupendekezwa kugombea Tuzo ya Amani ya Nobel

Uchaguzi 2020 Jaji Kaijage ana nafasi nzuri ya kutengeneza historia na hata kupendekezwa kugombea Tuzo ya Amani ya Nobel

Mshana, una maanisha ' Nobel peace prize' ? Kweli? Kwa kipi hasa. Sema unatania ili heshima ulojijegea humu iendelee kutamalaki .
Chaguzi nyingi za Africa huchafuliwa na tume za uchaguzi ..kwasasa hili unaweza kuliona ni jambo dogo sana...lakini katika udogo wake linaweza kupindua historia
 
Shida ni pale unapoona hadi watu wenye akili timamu nao wanasubiri Magufuli kuenguliwa
Mkuu umenifanya nichekee kwa sauti kubwa.

Vijana wa bavicha huwa wanajua kujitoa ufahamu.

Lakini siyo mbaya kujipa matumaini.
 
Andaeni sababu baada ya kushindwa mwezi October. Sio kuota ndoto za alinacha
 
Tuzo ya Amani ya Nobel?
Mzee unaijua hii tuzo vizuri?
Inatolewa kwa mtu aliyesuluhisha Vita au machafuko yaliyokuwepo muda mrefu
Mfano yule Waziri Mkuu wa Ethiopia kwa kumaliza yale machafuko ya waOromo kipindi kile
Hata huyu kaijage akitenda haki atakuwa emesuluhisha machafuko na vita.
 
Bado mapema, lakini so far utendaji wa Tume umeridhisha ukiondoa uhuni uhuni mdogo mdogo uliofanyanywa na wasimamizi wa chaguzi majimboni na kwenye kata!!
 
Bado mapema, lakini so far utendaji wa Tume umeridhisha ukiondoa uhuni uhuni mdogo mdogo uliofanyanywa na wasimamizi wa chaguzi majimboni na kwenye kata!!
Dalili njema...!?
 
Bandiko Zuri Lenye Hamasa Ya Haki Na Amani....

Hongera kwalo!

Nitofautiane Nawe Kidogo;

Tuzo Ya NOBEL si ya mchezomchezo......

Apewaye Ni Lazima Kuwe Na Jambo Kubwa Alilolifanya "KUENDANA" na MAZINGIRA ya nchi.....

Je Tanzania ni nchi yenye migogoro ya umwagaji damu KISIASA KIDINI NA KIKABILA?!!!

Jibu: HATUJAFIKA HUKO na HATUELEKEI KUFIKA HUKO japo tuna sintofahamu za hapa na pale.....

Simuoni Jaji Wetu Kipenzi Kaijage Kufikiriwa kuwavuta wale NGULI,rafiki zetu na WAHISANI wetu NORWAY kumkabidhi TUZO YA NOBELI......

Wote Waliopata Hiyo Tuzo Hapa Afrika, walikuwa na sababu Nzito na Kuntu mno....

Iwe ni Sirleaf...
Iwe ni Sadat....
Iwe Ni Luthuli....
Iwe Ni Mandela.....


Tanzania Ya Amani,
Tanzania Ya Haki,
Siempre Siempre Tanzania.
 
Macho yote yako tume ya uchaguzi chini ya jaji Kaijage mziki huu school mate wangu kihamia asingeuweza kamwe. So far tume inafanya vema. Si vibaya kwa hatua hii kutoa pongezi za awali.

Kuna mambo yanatokea kwa kasi ya ajabu na kwa haraka mno mpaka kuna vitu vinatupita. Ni ukweli usiopingika CCM HAKUKO SHWARI Kuna kila dalili mgombea kasusiwa ama kaachwa yatima wale manguli wa kuisimamia ccm hasa nyakati hizi hawaonekani popote wakikipigania na kukipamba chama.

Kasi ya mgombea wa CHADEMA inaleta taharuki mpya kila hatua anayopiga..na ni taharuki ya hoja zilizojaa sheria...ni wazi kabisa CCM haikujiandaa kabisa na hili waligeuza mazoea yakawa sheria

CCM kumepooza! Huo ndio ukweli mchungu na hata makada wake mitandaoni ni kama wamegeuka majuha na kichekesho kwa hoja zao zilizokosa weledi na mashiko

Jaji Kaijage karahisishiwa kazi nyingi na mgombea wa Chadema ambaye kitaaluma ni mwanasheria nguli...Hivyo basi jaji Kaijage akizisimamia sheria za tume ya uchaguzi kwa weledi (hitaji kubwa la CHADEMA) Bila kujali matokeo yatakuwaje atajitengenezea jina na historia tukuka

Akifanikiwa hilo namuona wazi akitutoa kimasomaso kwenye tuzo za amani za dunia
Mi ninachofurahi Ni kuwa kwa wiki mbili tu lissu ameaza kuondoa uoga uliotamalaki miongoni mwa taasisi za umma na serikali

Mahakama imeanza kujirudi, polisi nao wanalazimika kunyooka, na Sasa tume nao wameanza kunyooka
 
Angalieni presha isije ikawaua. CCM chini ya mhe rais Magufuli, tutashinda kwa kishindo kikubwa sana.

Hivi wanaoweza kufa kwa pressure ni wepi haswa?

Ni hawa ambao wamezoea ushindi haramu na kutoyaelewa maumivu ya kushindwa katika uchaguzi na sasa GIZA LA KUSHINDWA LIKIWA LIMETANDA MBELE YA NYUSO ZAO?

AU

Wale ambao wanayajua machungu ya kushindwa katika uchaguzi na sasa wanaiona NURU YA USHINDI MBELE YAO na hayupo wa kuizima NURU HIYO?

KWA UPANDE MWINGINE;

Hebu fikiri kuhusu tajiri ambaye hajawahi kuonja taabu za umasikini.

NA

Na upande huu mfikirie masikini anayejua machungu na taabu za umaskini. Leo anapata neema ya kuondolewa taabu na mahangaiko yake...

Ni yupi yuko kwenye position ya kufa kwa pressure kutokana na mabadiliko anayopitia ktk maisha yake?

Obviously ni tajiri anayeingia kwenye umasikini!

Sasa weka akili zako kumkichwa ung'amue fumbo hili...
 
Bandiko Zuri Lenye Hamasa Ya Haki Na Amani....

Hongera kwalo!

Nitofautiane Nawe Kidogo;

Tuzo Ya NOBEL si ya mchezomchezo......

Apewaye Ni Lazima Kuwe Na Jambo Kubwa Alilolifanya "KUENDANA" na MAZINGIRA ya nchi.....

Je Tanzania ni nchi yenye migogoro ya umwagaji damu KISIASA KIDINI NA KIKABILA?!!!

Jibu: HATUJAFIKA HUKO na HATUELEKEI KUFIKA HUKO japo tuna sintofahamu za hapa na pale.....

Simuoni Jaji Wetu Kipenzi Kaijage Kufikiriwa kuwavuta wale NGULI,rafiki zetu na WAHISANI wetu NORWAY kumkabidhi TUZO YA NOBELI......

Wote Waliopata Hiyo Tuzo Hapa Afrika, walikuwa na sababu Nzito na Kuntu mno....

Iwe ni Sirleaf...
Iwe ni Sadat....
Iwe Ni Luthuli....
Iwe Ni Mandela.....


Tanzania Ya Amani,
Tanzania Ya Haki,
Siempre Siempre Tanzania.
[emoji1752][emoji1545][emoji1545][emoji1545]tuzo za Nobel zina madaraja tofauti ...unamkumbuka huyu Mama Wangare Maathai?
PHOTO-Wangari_Maathai-c-Patrick-Wallet.jpg
 
Macho yote yako tume ya uchaguzi chini ya jaji Kaijage mziki huu school mate wangu kihamia asingeuweza kamwe. So far tume inafanya vema. Si vibaya kwa hatua hii kutoa pongezi za awali.

Kuna mambo yanatokea kwa kasi ya ajabu na kwa haraka mno mpaka kuna vitu vinatupita. Ni ukweli usiopingika CCM HAKUKO SHWARI Kuna kila dalili mgombea kasusiwa ama kaachwa yatima wale manguli wa kuisimamia ccm hasa nyakati hizi hawaonekani popote wakikipigania na kukipamba chama.

Kasi ya mgombea wa CHADEMA inaleta taharuki mpya kila hatua anayopiga..na ni taharuki ya hoja zilizojaa sheria...ni wazi kabisa CCM haikujiandaa kabisa na hili waligeuza mazoea yakawa sheria

CCM kumepooza! Huo ndio ukweli mchungu na hata makada wake mitandaoni ni kama wamegeuka majuha na kichekesho kwa hoja zao zilizokosa weledi na mashiko

Jaji Kaijage karahisishiwa kazi nyingi na mgombea wa Chadema ambaye kitaaluma ni mwanasheria nguli...Hivyo basi jaji Kaijage akizisimamia sheria za tume ya uchaguzi kwa weledi (hitaji kubwa la CHADEMA) Bila kujali matokeo yatakuwaje atajitengenezea jina na historia tukuka

Akifanikiwa hilo namuona wazi akitutoa kimasomaso kwenye tuzo za amani za dunia
MSHANA JR, LEO UMEKULA NINI MBONA UNATEMA MADINI SANA. GREAT POST UBARIKIWE.
 
[emoji1752][emoji1545][emoji1545][emoji1545]tuzo za Nobel zina madaraja tofauti ...unamkumbuka huyu Mama Wangare Maathai?
View attachment 1548941

Hakika.....Mama Yetu Kutoka Nchini Kenya.

Mkuu Lakini Kama sikosei Tunamhusisha Jaji Kaijage na TUZO juu ya HAKI AMANI NA MARIDHIANO wakati wa mchakato wa Uchaguzi na Kipindi Cha Matokeo.....
 
Back
Top Bottom