Ng'azagala
JF-Expert Member
- Jun 7, 2008
- 1,288
- 222
Msiangushe udini huyu jaji anafaa, ila tatizo langu lipo kwa huyo aliyeandika taarifa hii. Mbona amejitaja kama MWANDISHI WA HABARI WA RAIS MSAIDIZI. Hapa kuna uhakika kweli? Tuna Rais Msaidizi? Au angetakiwa kusema ni MWANDISHI WA HABARI MSAIDIZI WA RAIS? Kweli tutaona mengi mwaka huu na ujao.
Conflicts of intrest ! Unataka kutwambia kuwa katika familia moja akipata cheo mmoja basi wengine wasfanye kazi serikalini?
Hongera Chande, kwanza nakupa hongera kama swahib yako, pili nakupa hongera kama mtoto wa mjini Dar. Ntakuja nyumbani kukuletea hongera zangu za dhati, waambie hao maaskari mzee Dar akija wasimletee taabu getini!
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi
MWANDISHI WA HABARI MSAIDIZI WA RAIS?
hapa nafikiri ni tatizo la lugha yetu labda angeweka mkato kati ya Rais na Msaidizi kwani hata option uliyotoa bado ina mkanganyiko
Othman ni mwanasheria mzuri competent among all three names, well he has international and local experience.
JK for the second time you made a good choice kama ulivyofanya first time kwa Magufuli
Mengine yote ni Udini tu taratibu watazoea tu..ukumbuke tangu uhuru 1961 ni wale wale tu..
Watazoea na kwamba Tanzania ni wote sote (kila moja)
"Ni "coincidence" tu kwamba kaka mtu ni bosi wa TISS. Tatizo la neno hili ambalo maana yake ni tukio au matukio kutokea kwa wakti mmoja ni kwamba kuna wakti tukio hilo linaweza kuchukua muda kama tunaovyoona kwamba kaka mtu alikwishaukwaa ukurugenzi wa TISS na mdogo pengine akawa nae ana hamu ya kuwa mtu fulani katika Tanzania."
Bw. Richard na wengineo who went to school and can actually read and understand!!!!...
For the umpteenth time, hawa jamaa SIO NDUGU KABISA..... The newspaper report got it totally wrong here!
Ni wazawa wa Tanga. Rashid Othman is actually much younger than judge Moh'd Chande.
ili kusave muda naomba utuambie mtoa mada amedanganya wapi je hawa jamaa sio ndugu??????
Ifike mahala tuache kutia nyongo kila jambo linalofanywa na watawala. Nimesoma kwa makini wasifu wa Jaji Mkuu mpya Othman Chande. Inajitokeza waziwazi kwamba huyu ni mtu mwenye wasifu na sifa za juu kabisa katika maswala ya sheria na mahakama. Ana uzoefu wa hali ya juu kitaifa na kimataifa. Mamlaka ya uteuzi wangekuwa ni wajinga kama wangemuacha kwa sababu tu kaka yake ni Mkurugenzi Mkuu wa TISS. Tony Blair na Gordon Brown waliwahi kuwateua mtu na mdogo wake kuwa katika baraza la mawaziri. Juzijuzi Chama cha Labour kiliwapitisha mtu na kakake kugombea nafasi ya Kiongozi wa labour.
Ni ujuha na ujinga kumteua mtu kwa sababu ya dini, udugu, ukabila, n.k. Vilevile ni ujuha na ujinga wa kutisha kuacha kumteua mtu kwa sababu tu ndugu yake alishatangulia huko serikalini hata kama ana sifa. Haya mambo ya ku-balance kidini, kikabila, kidugu, kikanda na kimokoa ndiyo yanaletekeza mijitu mingine kuteuliwa kuwa mawaziri hata kama haina sifa ili wateuzi waonekane walizingatia mgawanyo wa kimkoa, kidini, kikabila, n.k. Kama mtu ana sifa basi ateuliwa, na kama hakuna mtu mwenye sifa kwa nafasi husika kutoka hiyo dini au kabila au mkoa basi na iwe hivyo. Si lazima kila dini au mkoa uwakilishwe katika nafasi za uteuzi.
Othman Chande, chapa kazi. Una nafasi ya kujitengenezea legacy ya pekee kwa kutoa msukumo muhimu ili hatimaye nchi yetu iwe na Katiba Mpya yenye kuzingatia misingi ya demokrasia na haki za binadamu.
Lakini baada ya hapo Wamarekani wakabadilisha sheria. Hakuna cha kuteua ndugu, mjomba, etc katika kazi za serikali.Mkuu usisahau pia kwamba J.F Kennedy alimteua mdogo wake Bobby Kennedy kuwa Attorney General.. na kazi zilienda fresh tu!
Lakini kumchagua Jaji Othman kuwa Jaji Mkuu haitoshi considering judiciary yetu ilivyogawanyika. Infact kwa nini watu hawajiulizi about the exclusivity ya Ukabila uliopo ndani ya Judiciary?
Of course kama tutakuwa hatuko makini kwenye kujadili hili itakuwa yale yalee ya sweeping statements kama vile 'ohhh WACHAGGA wamejazana kwenye judiciary ndio maana kuna nuka rushwa' lakini hakuna anayetaka kuangalia chanzo cha hili. Its quite unfortunate kuwa hata hao the so called University Students hawaji kuchangamsha hili baraza rightly or wrongly kutuelezea tena kwa sababu za kisomi kwa nini Judiciary yetu iko ONE SIDED.......maana kushakuwa so polarised humu and I can also understand pessimism kama ipo.
Nadhani kuna myriad factors ambazo tunaweza kusema kuwa zimeweza ku produce a Tanzanian judiciary with kwa mtazamo wa karibu ni haki kusema kuwa ni:
1.distinctly elite
2.non-representative demographics.
3.Born into families of wealth and privilege
4. Ivy League types
Hiyo point ya 4 ni muhimu kuifafanua kwa sababu most of our judges received their basic education good schools, their law training from either UK or U.S (Mara nyingi ni from the Golden Triangle ya UK ambayo inacombine:OXFORD na CAMBRIDGE, kwa upande mmoja, upande wa pili ni Vyuo ambavyo viko chini ya University of London kama KINGS COLLEGE, LONDON SCHOOL OF ECONOMICS, IMPERIAL COLLEGE na ukiangalia kwa sana utaona the others wamesomea kwenye Ivy League za North East wenyewe wanaziita ambazo kuna BROWN COLUMBIA, CORNELL,DARTMOUTH,HARVARD,PRINCETON na bila kusahau UPENN...hivyo piga ua utaona majaji wakuu wetu hawakoso at least a degree from the above institutions.
Sasa after that wengine waliobtain coveted pupilage at a prominent chambers of barristers kwa waliosoma UK. Na after a long and financially rewarding careers at the highest ranks of the bar, including appointments mbali mbali ndipo hawa waheshimiwa waliiingia kwenye full-time judiciary at the end of their practicing career.Given formal eligibility requirements, informal entrance barriers, and other restrictions, the Tanzania bench is overwhelmingly comprised of mainly older males (kwa sababu ya mfumo dume), Christian and from the most privileged stratum of society. So mtu kama Jaji Othman kuwa Jaji mkuu will always bring eyebrows kwa sababu HE DOESNT FIT THE PROFILE. Thats why nimesema kuwa tokana inbalance tulionayo katika Jamii Rais amefanya uamuzi wa busara kwani anaondoa zile stereotypes kuwa Mswahili tena Muislam hawezi kuwa Jaji mkuu na akatoa Haki sawa kwa wote. Mchukieni tuu Jakana lakini on this, I give him big up japo kama nilivyoelezea kuwa hii fani iko very elitist huko juu .
Yes najua kutakuwa na defenders wa mfumo huu au Judiciary yetu as it is lakini ukweli itabaki pale pale kuwa our Judiciary is SOCIALLY BIASED pili iko OUT OF TOUCH WITH ORDINARY LIVES na mbaya zaidi it LACKS PUBLIC CONFIDENCE THAT JUSTICE IS FAIRLY DISPENSED. Sasa kama mnataka tu we na mjadala ambao utaangalia beyong personalities sawa lakini upande wangu nadhani kuna umuhimu wa kufanya reform katika mhimili huu muhimu kwetu kama taifa kwaili kuongeza vitu vitatu:
1. TRANSPARENCY
2. ACCOUNTABILITY
3. DIVERSITY
Naweza kusema kuwa Post Cold War na mpaka miaka ya hivi karibuni kumekuwa na various 'forces' ambao wamekuwa wakitaka kuwepo kwa reforms ambazo zingeangalia au zingeshed light on issues kama vile a) appointment process b)adopting modern personnel management techniques andof course diversifying the bench to more fairly reflect the general population ili kuondoa minongono (rightly or wrongly) kuwa Wachagga au Wakristo wamejikita kwenye hili eneo/ Ninavyofahamu mimi kuwa pressure inatoka from within kwa maana Tanganyika Law Society, and non- legal professionals and governmental actors (kisirisiri au in private) as well as a broad range of social critics such as SHIVJIS and the like na pia bila kusahau SERIOUS press na bila kusahau wale vocal academics.
Its common ukimuuliza mtu wa mtaani atakuwambia kuwa issues zinazochefua judiciary yetu ni 1.criticisms of insider-preferences
2.political cronyism,
3. na bila kusahau the antiquated appointment system
Anyway najua Jaji Othman atakuwa na kazi kubwa ila kama nikipata nafasi ya kuzungumza naye nitamshauri azingatie mambo matatu na si mengine bali nilishatya mention na ndio yata underline reforms zozote tutakazo kuwa nazo kwenye judiciary nazo ni
1. TRANSPARENCY
2. ACCOUNTABILITY
3. DIVERSITY
Mniwie radhi post yangu ndefu kiasi lakini nimeona si vijabaya nikaongezea hayo niliyoyasema hapo awali
hawa jamaa hawana undugu kabisaaaaaa, hilo jina la othman ndilo lilowachanganya. Watu wanaifanya jf kama sio ya great thinkers kwa kuandika vitu ambavyo havina upembuzi yakinifu, tuumize vichwa jamani......as great thinkers.
Ni mtu mwenye akili zenye kuenea kwenye kizibo cha soda tu ndie anaweza asione walakini kwenye huu uteuzi!
Kwa suala la udini kwangu sidhani kama lipo ILA ni wehu wa hali ya juu kuwapa ndugu wawili (kama kweli ni ndugu kama inavyosemwa) nyadhifa sensitive kama hizi. i.e. Directore wa Usalama wa taifa na jaji mkuu. Inabidi bunge liingilie kati mapema sana kabla mambo hayajaharibika!!
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116539
E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT'S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Jaji Mohamed Chande Othman kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, kuanzia tarehe 28 DIsemba, 2010.
Jaji Othman anachukua nafasi ya Jaji Augustino Ramadhani anayestaafu kwa mujibu wa sheria tarehe 27 DIsemba, 2010.
Kwa sasa Jaji Othman ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa na pia ni mtaalamu binafsi juu ya hali ya Haki za Binadamu huko Kusini mwa Sudan, hadi mwezi Agosti 2011.
Jaji Othman alizaliwa tarehe 1 Januari, 1952, ana shahada ya kwanza ya Sheria (LLB) ya Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam na Shahada ya Uzamili (MA) kutoka katika Chuo Kikuu cha Webster, Geneva-Uswisi.
Amewahi kuwa Makamu wa Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Rwanda huko Arusha na amewahi kushika nafasi sawa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali huko Timor Mashariki.
Jaji Othman pia, amewahi kufanya kazi ndani na nje ya nchi katika Mashirika mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa kama vile Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) na Shirika la Msalaba Mwekundu.
Jaji Othman ataapishwa kesho tarehe 27 Disemba, 2010 katika viwanja vya Ikulu saa 4:00 asubuhi.
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi
Ikulu
Dar es Salaam
26 Disemba, 2010