Jaji Warioba: Miaka yote watu wanaelewa kujaza fomu, lakini 2020 ghafla hawajui. Siasa inataka kuingia kwenye Dini

Jaji Warioba: Miaka yote watu wanaelewa kujaza fomu, lakini 2020 ghafla hawajui. Siasa inataka kuingia kwenye Dini

Jaji Warioba akichangia kwenye mkutano wa TCD leo Dodoma, amenena haya

Miaka yote watu wanaelewa na wanajaza fomu vizuri lakini Mwaka 2020, ghafla watu hawajui kujaza fomu (wanaenguliwa). Hapa lazima kuna namna

Msitazame Wajumbe wa Tume pekee, angalieni Mfumo mzima wa Uchaguzi. Wizi wa kura unaanzia mbali. Unaanzia kwenye Kuandikisha wapiga kura, wakati wa kupiga kura na kutangaza matokeo

Siasa inataka kuingia kwenye dini, zamani viongozi tulikuwa tunakwenda kwenye vyumba vya ibada kama waumini, unasikiliza neno la Mungu. Siku hizi viongozi wakienda wanaombwa kutoa salamu za kisiasa, hii inaweza iingiza siasa katika dini tukapata matatizo

Vyama vingi vimekuwa kama makabila, vinaanza kugawa wananchi. Wananchi walikuwa kama jumuiya lakini siku hizi mambo mengi ya kijamii tunaingiza siasa, mfano msiba ni wa jamii lakini baadhi ya misiba unakuta sare za vyama,"

Katika vyama jumuiya zetu nazo zinakuwa kama za uhasama, badala ya kutuleta pamoja. Hali tuliyo nayo sasa utamaduni umetikiswa kidogo na tunapozungumzia maridhiano, nia yake kuturudisha kwenye utamaduni tuliokuwa nao


Viongozi wa kisiasa wangehubiri amani kama walivyofanya viongozi wa dini miaka michache iliyopita, nchi isingekuwa na malalamiko yanayolalamikiwa hivi sasa “kama wangetenda kama viongozi wa dini, nadhani matatizo haya tunayozungumza tusingekuwa nayo.


57F766D0-B76B-4EA5-8FDE-17BD56506BC9.jpeg
 
Kwanini hawakuenda mahakamani?

Kubaki unalialia umeonewa wakati hakuna kesi hata moja mahakamani ya kupinga uchaguzi ni upuuzi na kupoteza muda.
Elitwege please please, kipimo cha busara kitaonekana kwenye ulichokiandika, hebu changia hoja acha inclination za kisiasa. Inamaana wewe ukichaguliwa kwenye kamati hutaweza kutafuta suluhu. Kipimo cha uhalali wa uchaguzi sio namba ya kesi mahakamani hata siku moja. Kuwa mkweli kwa moyo wako.
 
Kwanini hawakuenda mahakamani?

Kubaki unalialia umeonewa wakati hakuna kesi hata moja mahakamani ya kupinga uchaguzi ni upuuzi na kupoteza muda.
Na wewe no mpuuzi no.1 wakati wa magufuli kulikuwepo mahakama? Nani alikuwa yuko tayari kupoteza pesa kwa mawakili wakati ikijulikana wazi kwamba magufuli alijichukulia hatamu zote kuanzia tume ya uchaguzi, bunge, mahakama mpaka magerezani alikuwa akipeleka wapinzani wake na kuwatoa alioona wanakubaliana nae. Muda mchache baada samia kuchukuwa uongozi japokuwa kutoka chama hicho tunaona mabadiliko makubwa kwenye mahakama na vyombo vyengine vya sheria sisi wegine tunashukuru mungu kutuondosha magufuli na mungu aliepushe taifa letu kupata kiongozi kama yule huko tunakoelekea.
 
Back
Top Bottom