Jamaa aelezea safari yake ya biashara miaka 13 kwa picha nne

Yani kuna watu tayari washalemaa kiakili. Yaani hawaamini kama huyo jamaa kaweza yeye mwenyewe, hawakubali, yani hawataki, maana washaona kila mtu ana ulemavu wa kusaidiwasaidiwa kama yeye.

The hustle is real.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaonekana wengi kwenye hii Thread hawajui maana ya "connection".

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. DISCIPLINE
2. PERSISTANCE
character za KIKINGA lazima utoboe
Character za kikinga naomba niwasaidie wadau KWA ufafanuzi: 1. Hakuna kugegeda maana utamaliza pesa kwa kuhonga.
2. Mlo mmoja kwa siku na ikiwezekana vipande viwili vya muhogo wa kukaanga unashushia na maji ya moto.
3. Mavazi yako usizidishe zaidi ya suruali 3/ kaptula 3 na shati au T-shirt 3.
4. Biashara yako isiwe ya ukoo! Mfano wa biashara ya ukoo kila mwandugu aliekabika na tatizo wewe unakuwa kimbele mbele wa kumsaidia.
Nb. Kama kuna niliyoisahau unaweza kuongezea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Mkinga mume anaenda makambako kufungasha mke amemwacha dukan..atapika hapo hapo au bek 3ataleta msos dukan...ss huku mume yuko dukani mke yuko hom tu anasogoa...usk mara akuibie elfu 20 ya mauzo...kila sherehe unataka uwepo😄😄..unaendeleaje hapo!
 
Nina mdogo wangu yeye alianza 2008 kupanga sabuni chini,sasa hivi ni hatari
 
Ukishakuwa na mindset kama hii yako huwezi kutoboa !!
Kubali tu juhudi binafsi zinaweza kuleta mabadiliko, pia.
Bila connection hapa duniani huwez kutoboa...huwez jua wakat anaanza ni watu gan wa muhimu katika kupata taarifa walikuwa wamemzunguka...amekomaa na ameweza bigup

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muda mwingine haiko hivyo , kunna watu wanajua kukomaaa . Kinachotuangusha wengi wetu ni nidhamu ya pesa , hasa unapoanza kuzikamata , unakuta na matumizi nayo yanaongezeka ,

Katika ujasiliamali ukiweza kuwa na nidhamu ya pesa pamoja na juhudi ya kuzitafuta, Lazima uwe kama dogo hapo.
kutoka hatua ya kwanza mwaka 2005 kwenda hatua ya pili mwaka 2009 lazima kuna mtu alimshika mkono kwa kumuongezea mtaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukishajiona kuwa una connection Jua kuwa ipo kwenye daraja flan. kuna watu mjini hapa hamjui mtu wala pa kuanzia yet wanatoboa
connection ktk life ni muhim sana mkuu
mi binafsi kuna mamb nishaangaika nayo ila baada ya kupata connection fasta tu yame tiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo picha hazitoshi kutoa picha kamili. Watu wana-pose mbele ya asset na kupiga picha kisha kudanganya wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…