Jamaa aliyeniibia kuku mwaka jana leo amefariki, mtaa unahisi nimemroga

Jamaa aliyeniibia kuku mwaka jana leo amefariki, mtaa unahisi nimemroga

Wakuu habari zenu,
Mwaka jana mwezi March kuna jamaa mtaani hapa aliniibia kuku mchana kweupe kabisa watu wanaona, nilipopata taarifa nikamtafuta mtaani nikamkosa, nikaamua kwenda nyumbani kwako nikamkuta dada zake nikawaeleza jamani fulani kaniibia kuku wangu naomba akija mwambieni arudishe. Hawakutilia sana maanani wakasema wamechoka na habari zake za wizi ila watamwambia arudishe.

Niliporudi mtaani nikapata taarifa kutoka kwa wambea wa mtaa ya sehemu alipouza hao kuku ikabidi nifunge safari mpaka kwa huyo mama aliyeuziwa kuku lakini nae akakataa kabisa kuwa hajauziwa. Basi me nikaondoka, kesho yake mchana nikapewa taarifa kuwa mwizi wangu ameonekana mtaani huko eti ananitafuta ajue kwa nini namchafulia jina lake mtaani, ikabidi sasa nianze kumtafuta hali ya kuwa kichwani tayari nimechafukwa kwa hasira. Muda si mrefu nikakutana nae kabla sijaongea nae akaanza kunipandishia sauti kwa nini nimeenda kwao nimemuita mwizi wa kuku, hapo uzalendo ukanishinda kwa hasira nikavaana nae nikampiga kidogo then nikamchukua nikampeleka mpaka ofisi ya mtaa kushtaki kuwa mwizi wangu huyu naomba anirudishie kuku wangu.

Alipoulizwa kuhusu kuiba kuku akakataa kabisa tena akaniruka kuwa nimempiga sana hali ya kuwa kuku hajaiba, me kuulizwa ushahidi sina zaidi ya kutaka kwenda alipouza kuku, tukaongozana mimi, mwizi wangu pamoja na mtendaji wa mtaa mpaka alipouza kuku, kufika hapo aliyenunua kuku akakataa kabisa kuwa hajauziwa kuku. Hapo nikakosa ushahidi wa kumtia hatiani ikabidi niwe mpole tu ila nikatamka kuwa basi namuachia Mungu kama kweli hajaiba kuku na iwe hivyo lakini kama ameiba basi Mungu atalipa kwa wote waliohusika, nikaondoka zangu.

Sasa ikapita miezi kama sita tukio limeanza kusahaulika, akaja jirani mmoja kunipa habari kuwa yule mwizi wangu anaumwa sana na anaropoka huko usiku wa manane kuwa kuku wamemponza, sikutilia maanani sana habari hizo maana najua umbea wa mtaani labda walitaka kunichimba wajue kama nikisamehe kweli au kuna kitu nilifanya. Baada ya kama wiki mbili hivi habari zikaenea zaidi kuwa jamaa anaumwa sana na amewaambia ndugu zake kuwa anakufa kwa sababu ya kuku. Baada ya siku kadhaa akaja mzee mmoja ni sheikh wa msikiti ninaosali hapo mtaani akaniambia kuwa amefuatwa na familia ya mwizi wangu kuwa yeye sheikh ameitwa kumuombea dua mgonjwa ambaye ndio huyo mwizi wangu, baada ya dua familia imemtuma aje kwangu kuomba msamaha kwa niaba yako maana hali imekuwa ngumu sana. Me nikamjibu sheikh "mzee wangu mimi sihusiki kabisa na ugonjwa wa huyo mtu, tangu nilipokosa ushahidi wa moja kwa moja kuhusu kuku wangu aliowaiba basi nikasamehe kwa maana kwanza kuku wenyewe hawakuwa wengi lakini pia nikiendelea kufuatilia hii issue nitapoteza muda lakini pia nitajijengea ubaya na ndugu zake kwa hiyo nimesamehe kwa roho moja"
Mzee anaondoka.

Sasa leo alfajir nikiwa msikitini ndio nikasikia tangazo la kifo cha jamaa aliyeniibia kuku wangu, kibinadamu niliingia huzuni lakini nikahisi sasa watu wamepata cha kusema kuhusu Mimi na huyu jamaa, wakuu tangu muda huo story mtaani ni mimi kuhusika na kifo cha jamaa, wengine wanasema sawa tu jamaa alizidi, wengine wanasema Nina roho mbaya yaani kuku tu ndio natoka roho ya mtu. Basi sina amani na hata msibani kuzika nafikiria nisihudhurie maana hata wasionijua watatambulishwa leo kuwa mimi ndio muhusika.

Cha kushangaza yule mama niliyeambiwa kuwa ndio alinunua kuku niliobiwa, asubuhi kanifuata nyumbani eti kuniomba msamaha, kakiri ni kweli aliuziwa kuku wangu na yule jamaa na sio kuku wangu tu hata kuku wa watu wengine pia huwa anamuuzia na mbuzi alishawahi kununua kwa jamaa. Nikamjibu kuku wangu mimi ni wale weupe akasema ndio aliwanunua ila anaomba msamaha yuko tayari kulipa pesa ya hap kuku ila nisifanye kitu kibaya katika familia yake au yeye maana anajua tego la mwizi huwa linaanza na mwizi, aliyenunua mpaka aliyekula hivyo ana hofu familia yake itaangamia. Nikamjibu mama we kuwa na amani mimi sihusiki na hilo. Ameondoka lakini hana raha kabisa.

Wakuu nakiri mbele yenu nyinyi sijawahi hata kuusogelea ushirikina na sihusiki kabisa na hili lakini ndio hivyo nimeshapata sifa mbaya mtaani, naombeni ushauri wenu katika hali hii nifanye nini angalau niwe na amani.

Shukran.
Hapa napofanya Biashara Kuna ntu aliibiwa kabati la chips Na mwizi alionekana kabisa Na watu
Akakataa Na familia yake haikujali
Yule Jamaa akasema Sawa namuachia Mungu
Jamaa (mtoto mwizi) hakuamka kesho yake
Hilo tukio Ni kama miaka 10 nyuma
Mpaka Leo hiyo stori inarithishwa vizazi Na vizazi
Aisee TUNAMUOGOPA JAMAA yupo Hadi Leo
Kwa hiyo nikushauri kama hujajenga hapo Hama
Ila kama umejenga watu watakua wanakuogopa which Ina two sides
One side hautafanyiwa ujinga ujinga
Ila another side hata Maji ya kunywa watu wataogopa kuomba
 
Nakuombew ujasiri na amani ya moyo. Maneno yanakera ya watu mtaani ila huna jinsi ishatokea. Uzuri wewe ulifuata hatua zote za kinidhamu hadi kuripoti kwao, ungekuwa mbaya wala usingefanya juhudi zote hizo. Usihudhurie msiba kupisha mengi na maisha taratibu yatakuwa kawaida tena
Asante sana mkuu, umenipa ushauri nzuri sana. Acha nivumilie yatapita tu
 
Mkuu umeongea kitu kikubwa sana ambacho nami kinaniumiza kichwa, je baada ya msiba ndugu zake watakubali tu yaishe hali ya kuwa wanahisi me ndio nimemroga ndugu yao? Je wakisema walipe kisasi wanidhuru si itakuwa dakika 0 tu maana sijui mambo ya kishirikina kabisa. Akili nyingine inaniambia nitafute wataalam wanikinge sasa si ndio itakuwa najiingiza kwenye maagano ya kichawi?
Umemuomba Mungu kakulipia dhambi ulofanyiwa mshukuru

Kingine uchawi haumpati asiehusika labda kama umehusika maana wakienda kuroga watanuia aliehusika na kifo cha ndugu yao nae kimpate kitu wewe hautakuepo

Lakini kama uliamini na kumuachia Mungu wakati ulipodhurumiwa unashindwa nini kuamini na kumuomba Mungu akukinge na hilo jambo? Kuwa na imani ndugu then umesema unaendaga msikitini huwa unafuata nini kama huna imani na Mungu
 
Umemuomba Mungu kakulipia dhambi ulofanyiwa mshukuru

Kingine uchawi haumpati asiehusika labda kama umehusika maana wakienda kuroga watanuia aliehusika na kifo cha ndugu yao nae kimpate kitu wewe hautakuepo

Lakini kama uliamini na kumuachia Mungu wakati ulipodhurumiwa unashindwa nini kuamini na kumuomba Mungu akukinge na hilo jambo? Kuwa na imani ndugu then umesema unaendaga msikitini huwa unafuata nini kama huna imani na Mungu
Asante mkuu, nitaendelea na Imani yangu kama ulivyoshauri maana kama watataka kurudisha mapigo halitanikuta
 
Heshima imeamua kukufata.....sahivi hata ukisahau kitu mahali watakibeba wakuletee 😹
 
Umemuomba Mungu kakulipia dhambi ulofanyiwa mshukuru

Kingine uchawi haumpati asiehusika labda kama umehusika maana wakienda kuroga watanuia aliehusika na kifo cha ndugu yao nae kimpate kitu wewe hautakuepo

Lakini kama uliamini na kumuachia Mungu wakati ulipodhurumiwa unashindwa nini kuamini na kumuomba Mungu akukinge na hilo jambo? Kuwa na imani ndugu then umesema unaendaga msikitini huwa unafuata nini kama huna imani na Mungu
Asante mkuu
 
Hapa napofanya Biashara Kuna ntu aliibiwa kabati la chips Na mwizi alionekana kabisa Na watu
Akakataa Na familia yake haikujali
Yule Jamaa akasema Sawa namuachia Mungu
Jamaa (mtoto mwizi) hakuamka kesho yake
Hilo tukio Ni kama miaka 10 nyuma
Mpaka Leo hiyo stori inarithishwa vizazi Na vizazi
Aisee TUNAMUOGOPA JAMAA yupo Hadi Leo
Kwa hiyo nikushauri kama hujajenga hapo Hama
Ila kama umejenga watu watakua wanakuogopa which Ina two sides
One side hautafanyiwa ujinga ujinga
Ila another side hata Maji ya kunywa watu wataogopa kuomba
Hata kama jamaa hajahusika hapo itaonekana ni yeye kumbe hamna kitu
 
Wakuu habari zenu,
Mwaka jana mwezi March kuna jamaa mtaani hapa aliniibia kuku mchana kweupe kabisa watu wanaona, nilipopata taarifa nikamtafuta mtaani nikamkosa, nikaamua kwenda nyumbani kwako nikamkuta dada zake nikawaeleza jamani fulani kaniibia kuku wangu naomba akija mwambieni arudishe. Hawakutilia sana maanani wakasema wamechoka na habari zake za wizi ila watamwambia arudishe.

Niliporudi mtaani nikapata taarifa kutoka kwa wambea wa mtaa ya sehemu alipouza hao kuku ikabidi nifunge safari mpaka kwa huyo mama aliyeuziwa kuku lakini nae akakataa kabisa kuwa hajauziwa. Basi me nikaondoka, kesho yake mchana nikapewa taarifa kuwa mwizi wangu ameonekana mtaani huko eti ananitafuta ajue kwa nini namchafulia jina lake mtaani, ikabidi sasa nianze kumtafuta hali ya kuwa kichwani tayari nimechafukwa kwa hasira. Muda si mrefu nikakutana nae kabla sijaongea nae akaanza kunipandishia sauti kwa nini nimeenda kwao nimemuita mwizi wa kuku, hapo uzalendo ukanishinda kwa hasira nikavaana nae nikampiga kidogo then nikamchukua nikampeleka mpaka ofisi ya mtaa kushtaki kuwa mwizi wangu huyu naomba anirudishie kuku wangu.

Alipoulizwa kuhusu kuiba kuku akakataa kabisa tena akaniruka kuwa nimempiga sana hali ya kuwa kuku hajaiba, me kuulizwa ushahidi sina zaidi ya kutaka kwenda alipouza kuku, tukaongozana mimi, mwizi wangu pamoja na mtendaji wa mtaa mpaka alipouza kuku, kufika hapo aliyenunua kuku akakataa kabisa kuwa hajauziwa kuku. Hapo nikakosa ushahidi wa kumtia hatiani ikabidi niwe mpole tu ila nikatamka kuwa basi namuachia Mungu kama kweli hajaiba kuku na iwe hivyo lakini kama ameiba basi Mungu atalipa kwa wote waliohusika, nikaondoka zangu.

Sasa ikapita miezi kama sita tukio limeanza kusahaulika, akaja jirani mmoja kunipa habari kuwa yule mwizi wangu anaumwa sana na anaropoka huko usiku wa manane kuwa kuku wamemponza, sikutilia maanani sana habari hizo maana najua umbea wa mtaani labda walitaka kunichimba wajue kama nikisamehe kweli au kuna kitu nilifanya. Baada ya kama wiki mbili hivi habari zikaenea zaidi kuwa jamaa anaumwa sana na amewaambia ndugu zake kuwa anakufa kwa sababu ya kuku. Baada ya siku kadhaa akaja mzee mmoja ni sheikh wa msikiti ninaosali hapo mtaani akaniambia kuwa amefuatwa na familia ya mwizi wangu kuwa yeye sheikh ameitwa kumuombea dua mgonjwa ambaye ndio huyo mwizi wangu, baada ya dua familia imemtuma aje kwangu kuomba msamaha kwa niaba yako maana hali imekuwa ngumu sana. Me nikamjibu sheikh "mzee wangu mimi sihusiki kabisa na ugonjwa wa huyo mtu, tangu nilipokosa ushahidi wa moja kwa moja kuhusu kuku wangu aliowaiba basi nikasamehe kwa maana kwanza kuku wenyewe hawakuwa wengi lakini pia nikiendelea kufuatilia hii issue nitapoteza muda lakini pia nitajijengea ubaya na ndugu zake kwa hiyo nimesamehe kwa roho moja"
Mzee anaondoka.

Sasa leo alfajir nikiwa msikitini ndio nikasikia tangazo la kifo cha jamaa aliyeniibia kuku wangu, kibinadamu niliingia huzuni lakini nikahisi sasa watu wamepata cha kusema kuhusu Mimi na huyu jamaa, wakuu tangu muda huo story mtaani ni mimi kuhusika na kifo cha jamaa, wengine wanasema sawa tu jamaa alizidi, wengine wanasema Nina roho mbaya yaani kuku tu ndio natoka roho ya mtu. Basi sina amani na hata msibani kuzika nafikiria nisihudhurie maana hata wasionijua watatambulishwa leo kuwa mimi ndio muhusika.

Cha kushangaza yule mama niliyeambiwa kuwa ndio alinunua kuku niliobiwa, asubuhi kanifuata nyumbani eti kuniomba msamaha, kakiri ni kweli aliuziwa kuku wangu na yule jamaa na sio kuku wangu tu hata kuku wa watu wengine pia huwa anamuuzia na mbuzi alishawahi kununua kwa jamaa. Nikamjibu kuku wangu mimi ni wale weupe akasema ndio aliwanunua ila anaomba msamaha yuko tayari kulipa pesa ya hap kuku ila nisifanye kitu kibaya katika familia yake au yeye maana anajua tego la mwizi huwa linaanza na mwizi, aliyenunua mpaka aliyekula hivyo ana hofu familia yake itaangamia. Nikamjibu mama we kuwa na amani mimi sihusiki na hilo. Ameondoka lakini hana raha kabisa.

Wakuu nakiri mbele yenu nyinyi sijawahi hata kuusogelea ushirikina na sihusiki kabisa na hili lakini ndio hivyo nimeshapata sifa mbaya mtaani, naombeni ushauri wenu katika hali hii nifanye nini angalau niwe na amani.

Shukran.
Jinyamazie wala usihangaike.

Hiyo siyo sifa mbaya, ni sifa nzuri ya kutisha vibaka.

kifo hicho kitakuheshimisha sana, pia jamii itakuheshimu na kukuogopa.

Hakuna kibaka atakayekuja kukuchezea tena.

Hakuna haja ya kutumia nguvu kujisafisha kwa jambo usilolitenda, iache dunia itakusafisha kwa nguvu ya Karma.

Kama alikuwa makwapu kwapu, kuna sehemu aloenda kuiba wakamkwamisha, maana kuna watu hawataki ujinga.

Potezea wala usihangaike.
 
Ndugu katika Imani Kuna neno zito sana ulitamka ambalo ni "MIMI NAMUACHIA MUNGU", huenda ndio matokeo ya yote hayo.
Kama ulipanga Fanya uhame, ila kama ni kwako dah sijui nini nikushauri, ila ni vizuri ukasogea eneo hilo
Nimejenga kabisa na ufugaji wangu naufanyia hapa
 
Mkuu umeongea kitu kikubwa sana ambacho nami kinaniumiza kichwa, je baada ya msiba ndugu zake watakubali tu yaishe hali ya kuwa wanahisi me ndio nimemroga ndugu yao? Je wakisema walipe kisasi wanidhuru si itakuwa dakika 0 tu maana sijui mambo ya kishirikina kabisa. Akili nyingine inaniambia nitafute wataalam wanikinge sasa si ndio itakuwa najiingiza kwenye maagano ya kichawi?
Ushauri wangu jambo zuri unafanya ibada, jikinge kwa Allah kwa ubaya wowote uliokusudiwa kwako,na mtake rehma yake

Amka mida ya saa nane au tisa usiku swali hata rakaa mbili na utake rehma ya Allah

Fanya hivyo hata mara tatu kwa wiki,kumbuka hakuna mchawi atakayekudhuru pasina idhini ya Allah

Lingine ikitokea labda umeitwa huko serikali ya mtaa pamoja na hao ndugu,waambe upo tayar kuapa kwa Mungu kwamba hujafanya chochote na kama umefanya laana ya Mungu ikushukie

Pili jaman muwe makini sana kuonyesha uadui au hasira yenu hadharani,kuna mtu huenda ana ubaya na mimi,sasa anasubiri wewe ukisema utaniua basi anachukua nafasi hiyo kuniua mm na ubaya unakuja kwako

Muwe makini sana juu ya mambo haya,naamini kabisa huyo ni mwizi mzoefu kwahiyo alikuwa na maadui wengi pia
 
Aisee hiyo ni hatari na nusu, kitaa wataanza kukugwaya kama mwanga kumbe kijana swafi swala tano.

Bila shala mwizi jambo la kukuibia na kukukana waziwazi lilimkereketa nafsi yake
 
Mkuu umeongea kitu kikubwa sana ambacho nami kinaniumiza kichwa, je baada ya msiba ndugu zake watakubali tu yaishe hali ya kuwa wanahisi me ndio nimemroga ndugu yao? Je wakisema walipe kisasi wanidhuru si itakuwa dakika 0 tu maana sijui mambo ya kishirikina kabisa. Akili nyingine inaniambia nitafute wataalam wanikinge sasa si ndio itakuwa najiingiza kwenye maagano ya kichawi?
Acha uoga sisi wakristo biblia imeandikwa x365 usiogope kwahiyo kila siku iambie nafsi yako usi ogope maana Mungu yu pamoja Nami amen 🙏
 
Pole sana jirani, hata mimi niliposikia kifo cha jamaa nikajua umemroga kweli.
 
Back
Top Bottom