Jamaa aliyeniibia kuku mwaka jana leo amefariki, mtaa unahisi nimemroga

Jamaa aliyeniibia kuku mwaka jana leo amefariki, mtaa unahisi nimemroga

Wakuu habari zenu,
Mwaka jana mwezi March kuna jamaa mtaani hapa aliniibia kuku mchana kweupe kabisa watu wanaona, nilipopata taarifa nikamtafuta mtaani nikamkosa, nikaamua kwenda nyumbani kwako nikamkuta dada zake nikawaeleza jamani fulani kaniibia kuku wangu naomba akija mwambieni arudishe. Hawakutilia sana maanani wakasema wamechoka na habari zake za wizi ila watamwambia arudishe.

Niliporudi mtaani nikapata taarifa kutoka kwa wambea wa mtaa ya sehemu alipouza hao kuku ikabidi nifunge safari mpaka kwa huyo mama aliyeuziwa kuku lakini nae akakataa kabisa kuwa hajauziwa. Basi me nikaondoka, kesho yake mchana nikapewa taarifa kuwa mwizi wangu ameonekana mtaani huko eti ananitafuta ajue kwa nini namchafulia jina lake mtaani, ikabidi sasa nianze kumtafuta hali ya kuwa kichwani tayari nimechafukwa kwa hasira. Muda si mrefu nikakutana nae kabla sijaongea nae akaanza kunipandishia sauti kwa nini nimeenda kwao nimemuita mwizi wa kuku, hapo uzalendo ukanishinda kwa hasira nikavaana nae nikampiga kidogo then nikamchukua nikampeleka mpaka ofisi ya mtaa kushtaki kuwa mwizi wangu huyu naomba anirudishie kuku wangu.

Alipoulizwa kuhusu kuiba kuku akakataa kabisa tena akaniruka kuwa nimempiga sana hali ya kuwa kuku hajaiba, me kuulizwa ushahidi sina zaidi ya kutaka kwenda alipouza kuku, tukaongozana mimi, mwizi wangu pamoja na mtendaji wa mtaa mpaka alipouza kuku, kufika hapo aliyenunua kuku akakataa kabisa kuwa hajauziwa kuku. Hapo nikakosa ushahidi wa kumtia hatiani ikabidi niwe mpole tu ila nikatamka kuwa basi namuachia Mungu kama kweli hajaiba kuku na iwe hivyo lakini kama ameiba basi Mungu atalipa kwa wote waliohusika, nikaondoka zangu.

Sasa ikapita miezi kama sita tukio limeanza kusahaulika, akaja jirani mmoja kunipa habari kuwa yule mwizi wangu anaumwa sana na anaropoka huko usiku wa manane kuwa kuku wamemponza, sikutilia maanani sana habari hizo maana najua umbea wa mtaani labda walitaka kunichimba wajue kama nikisamehe kweli au kuna kitu nilifanya. Baada ya kama wiki mbili hivi habari zikaenea zaidi kuwa jamaa anaumwa sana na amewaambia ndugu zake kuwa anakufa kwa sababu ya kuku. Baada ya siku kadhaa akaja mzee mmoja ni sheikh wa msikiti ninaosali hapo mtaani akaniambia kuwa amefuatwa na familia ya mwizi wangu kuwa yeye sheikh ameitwa kumuombea dua mgonjwa ambaye ndio huyo mwizi wangu, baada ya dua familia imemtuma aje kwangu kuomba msamaha kwa niaba yako maana hali imekuwa ngumu sana. Me nikamjibu sheikh "mzee wangu mimi sihusiki kabisa na ugonjwa wa huyo mtu, tangu nilipokosa ushahidi wa moja kwa moja kuhusu kuku wangu aliowaiba basi nikasamehe kwa maana kwanza kuku wenyewe hawakuwa wengi lakini pia nikiendelea kufuatilia hii issue nitapoteza muda lakini pia nitajijengea ubaya na ndugu zake kwa hiyo nimesamehe kwa roho moja"
Mzee anaondoka.

Sasa leo alfajir nikiwa msikitini ndio nikasikia tangazo la kifo cha jamaa aliyeniibia kuku wangu, kibinadamu niliingia huzuni lakini nikahisi sasa watu wamepata cha kusema kuhusu Mimi na huyu jamaa, wakuu tangu muda huo story mtaani ni mimi kuhusika na kifo cha jamaa, wengine wanasema sawa tu jamaa alizidi, wengine wanasema Nina roho mbaya yaani kuku tu ndio natoka roho ya mtu. Basi sina amani na hata msibani kuzika nafikiria nisihudhurie maana hata wasionijua watatambulishwa leo kuwa mimi ndio muhusika.

Cha kushangaza yule mama niliyeambiwa kuwa ndio alinunua kuku niliobiwa, asubuhi kanifuata nyumbani eti kuniomba msamaha, kakiri ni kweli aliuziwa kuku wangu na yule jamaa na sio kuku wangu tu hata kuku wa watu wengine pia huwa anamuuzia na mbuzi alishawahi kununua kwa jamaa. Nikamjibu kuku wangu mimi ni wale weupe akasema ndio aliwanunua ila anaomba msamaha yuko tayari kulipa pesa ya hap kuku ila nisifanye kitu kibaya katika familia yake au yeye maana anajua tego la mwizi huwa linaanza na mwizi, aliyenunua mpaka aliyekula hivyo ana hofu familia yake itaangamia. Nikamjibu mama we kuwa na amani mimi sihusiki na hilo. Ameondoka lakini hana raha kabisa.

Wakuu nakiri mbele yenu nyinyi sijawahi hata kuusogelea ushirikina na sihusiki kabisa na hili lakini ndio hivyo nimeshapata sifa mbaya mtaani, naombeni ushauri wenu katika hali hii nifanye nini angalau niwe na amani.

Shukran.
We kuwa na amani madam haukuhusika,. Apo Sasa ni Fanya TU jitihada ya kuongeza kuku hakuna atakayekuibia. Utaumiza kichwa Bure Kwa kitu ambacho huwezi kukibadilisha
 
Kaza mkuu kazaaa usiachie wapukutike wooote...nakuomba kaza

mganga nitampataje huyo
 
Samahani sana mkuu, wana JF wamenituma nikuulize, namna ya kumpata mtaalamu wako?..🤔
 
ni zaidi ya mke wa mtu,...😂😂🤣
Hata majambazi sugu, wanamuogopa kuku🤔🤔🧐😂
🤓 🤓 🤓, Kabisa mkuu, kuna jamaa alienda kuiba kuku usiku, Sasa baadala ya kuwanyonga shingo ili asipige kelele, yeye akakosea akanyonga mguu 😂😂. Wacha kuku apige makelele ya kiwango cha lami.

Mpaka leo ni R. I. P
 
Mkuu hilo eneo kwako si salama na hata kwenye mazishi ya huyo mwizi wa kuku wako usikanyage kwa sababu zifuatazo; familia ya huyo jamaa hawana amani wanahisi kinaweza kuwatokea kama kilichomtokea ndugu yao hivyo wanaweza wakafanya mpango wa kukupoteza kwa lengo la kujilinda na kulipa kisasi

Kumbuka alikuja ostadhi kuomba msamaha kwa niaba ya mwizi ukasema wewe uhusiki na matatizo yake mwisho wa siku mwizi alipoteza maisha pia huyo mama aliyenunua kuku wa wizi alikuja kwako kuomba msamaha ili awe na amani lakini amepata majibu ambayo hakutegemea kutoka kwako hivyo bado umemuacha na wasiwasi atahisi kitamtokea kilichomtokea aliyeiba kuku

Kwa vyovyote huyo mama atatafuta namna ya kukumaliza ili awe na amani maana anahisi na yeye atafuata njia aliyopita mwizi wa kuku, mkuu nakushauli kama huna nguvu za kiroho hama hilo eneo haraka iwezekanavyo la sivyo itakugharimu
 
Wakuu habari zenu,
Mwaka jana mwezi March kuna jamaa mtaani hapa aliniibia kuku mchana kweupe kabisa watu wanaona, nilipopata taarifa nikamtafuta mtaani nikamkosa, nikaamua kwenda nyumbani kwako nikamkuta dada zake nikawaeleza jamani fulani kaniibia kuku wangu naomba akija mwambieni arudishe. Hawakutilia sana maanani wakasema wamechoka na habari zake za wizi ila watamwambia arudishe.

Niliporudi mtaani nikapata taarifa kutoka kwa wambea wa mtaa ya sehemu alipouza hao kuku ikabidi nifunge safari mpaka kwa huyo mama aliyeuziwa kuku lakini nae akakataa kabisa kuwa hajauziwa. Basi me nikaondoka, kesho yake mchana nikapewa taarifa kuwa mwizi wangu ameonekana mtaani huko eti ananitafuta ajue kwa nini namchafulia jina lake mtaani, ikabidi sasa nianze kumtafuta hali ya kuwa kichwani tayari nimechafukwa kwa hasira. Muda si mrefu nikakutana nae kabla sijaongea nae akaanza kunipandishia sauti kwa nini nimeenda kwao nimemuita mwizi wa kuku, hapo uzalendo ukanishinda kwa hasira nikavaana nae nikampiga kidogo then nikamchukua nikampeleka mpaka ofisi ya mtaa kushtaki kuwa mwizi wangu huyu naomba anirudishie kuku wangu.

Alipoulizwa kuhusu kuiba kuku akakataa kabisa tena akaniruka kuwa nimempiga sana hali ya kuwa kuku hajaiba, me kuulizwa ushahidi sina zaidi ya kutaka kwenda alipouza kuku, tukaongozana mimi, mwizi wangu pamoja na mtendaji wa mtaa mpaka alipouza kuku, kufika hapo aliyenunua kuku akakataa kabisa kuwa hajauziwa kuku. Hapo nikakosa ushahidi wa kumtia hatiani ikabidi niwe mpole tu ila nikatamka kuwa basi namuachia Mungu kama kweli hajaiba kuku na iwe hivyo lakini kama ameiba basi Mungu atalipa kwa wote waliohusika, nikaondoka zangu.

Sasa ikapita miezi kama sita tukio limeanza kusahaulika, akaja jirani mmoja kunipa habari kuwa yule mwizi wangu anaumwa sana na anaropoka huko usiku wa manane kuwa kuku wamemponza, sikutilia maanani sana habari hizo maana najua umbea wa mtaani labda walitaka kunichimba wajue kama nikisamehe kweli au kuna kitu nilifanya. Baada ya kama wiki mbili hivi habari zikaenea zaidi kuwa jamaa anaumwa sana na amewaambia ndugu zake kuwa anakufa kwa sababu ya kuku. Baada ya siku kadhaa akaja mzee mmoja ni sheikh wa msikiti ninaosali hapo mtaani akaniambia kuwa amefuatwa na familia ya mwizi wangu kuwa yeye sheikh ameitwa kumuombea dua mgonjwa ambaye ndio huyo mwizi wangu, baada ya dua familia imemtuma aje kwangu kuomba msamaha kwa niaba yako maana hali imekuwa ngumu sana. Me nikamjibu sheikh "mzee wangu mimi sihusiki kabisa na ugonjwa wa huyo mtu, tangu nilipokosa ushahidi wa moja kwa moja kuhusu kuku wangu aliowaiba basi nikasamehe kwa maana kwanza kuku wenyewe hawakuwa wengi lakini pia nikiendelea kufuatilia hii issue nitapoteza muda lakini pia nitajijengea ubaya na ndugu zake kwa hiyo nimesamehe kwa roho moja"
Mzee anaondoka.

Sasa leo alfajir nikiwa msikitini ndio nikasikia tangazo la kifo cha jamaa aliyeniibia kuku wangu, kibinadamu niliingia huzuni lakini nikahisi sasa watu wamepata cha kusema kuhusu Mimi na huyu jamaa, wakuu tangu muda huo story mtaani ni mimi kuhusika na kifo cha jamaa, wengine wanasema sawa tu jamaa alizidi, wengine wanasema Nina roho mbaya yaani kuku tu ndio natoka roho ya mtu. Basi sina amani na hata msibani kuzika nafikiria nisihudhurie maana hata wasionijua watatambulishwa leo kuwa mimi ndio muhusika.

Cha kushangaza yule mama niliyeambiwa kuwa ndio alinunua kuku niliobiwa, asubuhi kanifuata nyumbani eti kuniomba msamaha, kakiri ni kweli aliuziwa kuku wangu na yule jamaa na sio kuku wangu tu hata kuku wa watu wengine pia huwa anamuuzia na mbuzi alishawahi kununua kwa jamaa. Nikamjibu kuku wangu mimi ni wale weupe akasema ndio aliwanunua ila anaomba msamaha yuko tayari kulipa pesa ya hap kuku ila nisifanye kitu kibaya katika familia yake au yeye maana anajua tego la mwizi huwa linaanza na mwizi, aliyenunua mpaka aliyekula hivyo ana hofu familia yake itaangamia. Nikamjibu mama we kuwa na amani mimi sihusiki na hilo. Ameondoka lakini hana raha kabisa.

Wakuu nakiri mbele yenu nyinyi sijawahi hata kuusogelea ushirikina na sihusiki kabisa na hili lakini ndio hivyo nimeshapata sifa mbaya mtaani, naombeni ushauri wenu katika hali hii nifanye nini angalau niwe na amani.

Shukran.
Ninakusihi sana Kwa unyenyekevu Mkubwa kushinda Ukubwa wenyewe .


Kama umepanga tu, HAMA.

Na kama ni Mji wako mwenyewe, Sijui nikushauri nini.

Ila WATAKUUA Kwa namna yoyote inayowezekana labda MUNGU ASIMAME MBELE YAKO.


Upo kwenye Mtihan mgumu sana unaohitaj utulivu wa kimaamuzi kwakua ndio yatakayoamua Maisha yako ya kesho yaan UHAI..

Wala MTU asikuambia, Kwa Sasa wanakuogopa, hawatakuchezea tena n.k .


Ikiwezekana nenda Polisi , Tafuta Wazee wa Eneo Hilo , shirikisha viongozi wa Dini wa eneo hili,wakukutanishe na Ndugu au wanajumuia wako , NACHOMAANISHA TUMIA NAMNA YOYOTE ILE UTENGENEZE AMANI NA KUAMINIWA UPYA KWENYE JAMII HIYO.

Kuna Watu wanaweza kua ni WABAYA WAKO, wameamua kupitia kwenye Hilo au watu waloibiwa na Jamaa wamemuondoa ila hekaheka zako za kufatilia kuku ,zmekufikiaha hali.
 
Kuna mtu wa karibu ameamua kukusaidia kazi kijana,the thing ni kuwa huyo jamaa alikuwa anaiba sehemu nyingi kuku mtaani kwa hiyo unatakiwa ufahamu ya kwamba sio wewe peke yako uliyewahi kuibiwa kuku kitaa,kwa hyo Kuna mtu katika circle yenu mlioibiwa kaamua kusafisha mtaa.vinginevyo iwe ni wachawi wa mtaani kwenu kwa kuwa wanafahamu uhasama wenu .Impact ya jambo Hilo ni kuwa ndugu zake watataka kukumaliza wewe,siku sio nyingi utarogwa na ndugu zake au na wachawi wa mtaani kwenu.kama ni wachawi wa kitaa the next round inakuhusu wewe kufa ili ionekane kuwa kisasi kimelipwa na ndugu.wachawi Huwa wanatumia akili kubwa sana kwenye mambo yao ndugu,usione furaha huyo mtu kufa .Hakuna mtu ataiba Tena kitu nyumbani kwako ila fahamu kuwa haupo salama wewe na familia yako.mara nyingi watu wa pwani hata kama watoto wao Wana makosa hawawezi kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa.Hapo jambo la msingi unatakiwa kuhama.Vinginevyo mama aliyenunua kuku anahisi kufa tuu wakati wowote ,kwa hiyo lazima ahakikishe anakutanguliza ili awe safi.kama unarafiki yako wa karibu anayefanya fanya ibada mara tano kwa siku na ulimweleza jambo Hilo fahamu kuwa aliamua kukulipia kisasi kimya kimya.
Uzi ufungwe,majibu yote yako hapa nilitaka kumwambia kama hivi mtoa mada.
Hapo kilichofanyika ni kwamba kuna mtu mwingine jirani ambaye alikerekwa na kuchoka tabia ya huyo mwizi kwa hiyo akautumia huo mwanya kufanya hicho kisasi halafu akajificha nyuma akijua kwa vyovyote mtu atakayehisiwa ni wewe mtoa mada kwa sababu ulijitokeza waziwazi na kukwaruzana na huyo mwizi.
Sasa kitakachofuata kuna wachawi watakuja kukujaribu waone nguvu yako inaishia wapi kwenye mambo ya giza na kama ni mwepesi mwepesi watakudhuru.
Ili kuepuka hayo madhara kwanza inabidi uhame huo mtaa lakini haimaanishi kwamba ukihama wachawi hawatokupata la hasha wachawi wakikuhitaji wana uwezo wa kukufuata popote hata iwe Ulaya tena ndani ya dakika moja tu isipokuwa ukihama itafanya watu wakusahau na kusahau tukio kwa haraka kuliko ukiwa hapohapo ukinyooshewa vidole kila siku.
Jambo lingine kwa vile umedai wewe ni muislamu tafuta wataalamu wa dua usomewe visomo vikali vya kujilinda tena inabidi usafirie sio kwa wataalamu wa mjini watakulia tu pesa yako na kukudanganya kuwa uko na kinga kumbe hamna kitu,hapa usiwe bahili wala kuwaza gharama kwa usalama wako.
Maoni yangu ni hayo zingatia haya kumbuka kuishi na walimwengu hasahasa wa uswahilini ni kazi sana ndugu inahitaji akili za ziada.
 
Hali hii ilimkuta mzee wangu alikuwa yeye na rozari rozari na yeye. Mwaka 2001 tukaibwa ng'ombe mkubwa maksai wa kulimia alituuma sana kama familia hakuna aliyekula isipokuwa watoto wadogo. kipindi hicho tuna ng'ombe kama sabini na ushee hivi lakini huyo alituuma sana.

Baasa ya siku mbili tukimtafuta maporini kutwa nzima bila mafanikio siku3 mzee akaitwa ofisi ya kijiji.Kufika akaulizwa mzee wewe ndo makanya charo? akasema mimi ndiye. Wakamwambia ng'ombe wako kapatikana shilela watu wa huku watakuwa wanapaju hapo shilela karibu na lunguya barabara ya kwenda kahama ukiwa unatoka kakola na walio leta taarifa ni mgambo (sungusungu) wa huko baada ya kumtilia shaka mwizi na kumbana hatimae alikiri kaiba.

Mzee alienda kumchukua ng'ombe ni kweli ni yeye kumbuka alienda na sungusungu wa kijijn kwetu pia jamaa yule mwizi akapigwa viboko na kuogeshwa kwenye tope na faini ya ng'ombe wa kijiji wale. Ikawa hivyo.

Mzee akaulizwa kama ana hitaji kulipwa alipwe lakini aligoma akasema kwa sababu ng'ombe wangu kapatikana na kijiji kimefuata taratibu zake mimi yameisgha kabisa.

baada ya miezi kadhaa jama aliugua kafa...Mchawi akaambiwa ni mzee. unaambiwa siku anakata roho alikuwa anawaambia kamwiteni flani aje mzee hata hajafika kwa jamaa akakuta kashafariki.


wengine wizi wa sola panel nao walikufa wakisema hivyohivyo mwiteni mzee flani.

Baada ya hapo watu wakaanza miminika kuja kununua dawa kwa mzee wakimwambia akiwapa watampa ng'ombe au hadi ng'ombe watatu.....mzee kila akiwaambia hahusiki wala hawakuamini. tangu hapo hatujawahi ibwa tena.

Huwa nafuga kuku kule sifungii kuku na muda myingine wanalala nje lakini hutasikia wameiba lakini kuna watu wanibwa vibaya mno.


2012 Walikuja wezi pia japo hawakuiba na hatukujua walikuwa wanataka waibe nini ila walikuwa wameiba na miji mingine. walipofika home hatujui kiliwatokea nini baiskeli zao wakaziacha wakaanza kukimbia ovyo sisi tumelala...bahati mbaya wanakimbilia kule walikoiba huku wanalia walikamatwa wakapigwa na kuchomwa moto

kati ya hao3 mmoja alipewa muda kwanini walikuwa wanakimbia mbio huku wanalia akasema mzee fln na vijana wake ndo walikuwa wanatukimbiza.


Mimi nilimuibia mzee 100 zile za note nafikiri mwishoni mwa miaka 90 hivi......Alinipiga vibaya mno huku akisema unataka ufe? Sijui siri ya mzee kuhusu haya ila ni mtu wa dini na nusu hata hivyo angekuwa na dawa basi mimi angekuwa kashanipa au kunielekeza.(Nipo karibu nae mno)


Mara kdhaa huwa ansema kigoma huwa hawaibwi na yeye amewahi ishi kule miaka ya 60-70 kama .....
 
Asante mkuu, nitaendelea na Imani yangu kama ulivyoshauri maana kama watataka kurudisha mapigo halitanikuta
Mkuu usidanganyike ukizubaa kitakukuta kitu.
Wachawi hawanaga hiyo akili ya kuanza kuthibitisha kwamba kweli umehusika au hujahusika.
Kwa vile wameshakushuku wewe hawapotezi muda wao wanachukua tu majina yako wanaenda kuyafanyia kazi.
Kwa hiyo kutokuwa na hatia kwako haiwezi kuwa kinga ila ni lazima upambane kujikinga,Mungu alikupa akili ili ujipambanie usikae kinyonge na kumbuka hata mwizi na mchawi wakienda kwenye shughuli zao pia wanamuomba Mungu ili wasikamatwe,kitu kingine inabidi ujue ya kuwa Mungu ni wa viumbe vyote na hana upendeleo kwa mtu mmoja kwa hapa duniani hata ufanye madhambi kiasi gani hakudhulumu haki zako hadi pale itakapofika siku ya hesabu ndipo tutahukumiwa kwa yale tuliyoyafanya duniani.
 
Hali hii ilimkuta mzee wangu alikuwa yeye na rozari rozari na yeye. Mwaka 2001 tukaibwa ng'ombe mkubwa maksai wa kulimia alituuma sana kama familia hakuna aliyekula isipokuwa watoto wadogo. kipindi hicho tuna ng'ombe kama sabini na ushee hivi lakini huyo alituuma sana.

Baasa ya siku mbili tukimtafuta maporini kutwa nzima bila mafanikio siku3 mzee akaitwa ofisi ya kijiji.Kufika akaulizwa mzee wewe ndo makanya charo? akasema mimi ndiye. Wakamwambia ng'ombe wako kapatikana shilela watu wa huku watakuwa wanapaju hapo shilela karibu na lunguya barabara ya kwenda kahama ukiwa unatoka kakola na walio leta taarifa ni mgambo (sungusungu) wa huko baada ya kumtilia shaka mwizi na kumbana hatimae alikiri kaiba.

Mzee alienda kumchukua ng'ombe ni kweli ni yeye kumbuka alienda na sungusungu wa kijijn kwetu pia jamaa yule mwizi akapigwa viboko na kuogeshwa kwenye tope na faini ya ng'ombe wa kijiji wale. Ikawa hivyo.

Mzee akaulizwa kama ana hitaji kulipwa alipwe lakini aligoma akasema kwa sababu ng'ombe wangu kapatikana na kijiji kimefuata taratibu zake mimi yameisgha kabisa.

baada ya miezi kadhaa jama aliugua kafa...Mchawi akaambiwa ni mzee. unaambiwa siku anakata roho alikuwa anawaambia kamwiteni flani aje mzee hata hajafika kwa jamaa akakuta kashafariki.


wengine wizi wa sola panel nao walikufa wakisema hivyohivyo mwiteni mzee flani.

Baada ya hapo watu wakaanza miminika kuja kununua dawa kwa mzee wakimwambia akiwapa watampa ng'ombe au hadi ng'ombe watatu.....mzee kila akiwaambia hahusiki wala hawakuamini. tangu hapo hatujawahi ibwa tena.

Huwa nafuga kuku kule sifungii kuku na muda myingine wanalala nje lakini hutasikia wameiba lakini kuna watu wanibwa vibaya mno.


2012 Walikuja wezi pia japo hawakuiba na hatukujua walikuwa wanataka waibe nini ila walikuwa wameiba na miji mingine. walipofika home hatujui kiliwatokea nini baiskeli zao wakaziacha wakaanza kukimbia ovyo sisi tumelala...bahati mbaya wanakimbilia kule walikoiba huku wanalia walikamatwa wakapigwa na kuchomwa moto

kati ya hao3 mmoja alipewa muda kwanini walikuwa wanakimbia mbio huku wanalia akasema mzee fln na vijana wake ndo walikuwa wanatukimbiza.


Mimi nilimuibia mzee 100 zile za note nafikiri mwishoni mwa miaka 90 hivi......Alinipiga vibaya mno huku akisema unataka ufe? Sijui siri ya mzee kuhusu haya ila ni mtu wa dini na nusu hata hivyo angekuwa na dawa basi mimi angekuwa kashanipa au kunielekeza.(Nipo karibu nae mno)


Mara kdhaa huwa ansema kigoma huwa hawaibwi na yeye amewahi ishi kule miaka ya 60-70 kama .....
Kwa maelezo yako haya huyo mzee wako ni kweli kuna dawa anayo ila wewe anakuficha ila utakuja kuujua ukweli mwaka atakaofariki utaitwa ili urithishwe hiyo dawa.
Haiwezekani matukio zaidi ya mara mbili itokee hapohapo kwenu.
 
Wabongo wanawazaga mambo ya ajabu mara wawaze yesu, Allah, Muhammad, shetani,mapepo,majini,nafsi,roho,mizimu,vibwengo yaani ni vitu visivyoingia kwenye ubongo wangu
 
Back
Top Bottom