Jamal Malinzi: Natukanwa sana JamiiForums, Facebook na redio mbali mbali

kumbe!? wanamichezo jf kuanzia Leo Malinzi hataki mmuite janga mwiteni neema, na siyo hovyo Bali ni kiongozi bora kuwahi kutokea...
hapo lazima likes hii post..
 
Malinzi ni mpiga dili kama kina mzee akilimali pale yanga,
Huwezi kufananisha TFF ya Tenga na huyu Malinzi kwa lolote
 
MH. President Yakupasa Ujichunguze Kwa Umakini Mno!! HAKUNA Kelele Ambazo Hazina Chanzo, Lazima Kuna Suala Ambalo Wadau Wa Mchezo Huu Wameliona Ni Tatizo Kwako Na Taasisi Unayoiongoza!! HAYA Mh. PM MAJARIWA Naye Alikuwa Anakutusi!!!?? Pale Aliposhangaa Na Kukemea Mpango Wa Malinzi Na Taasisi Yako, Kutaka Kumrudisha Nchini Kocha Mliyemfukuza KIM POULSON!!!??
 
Kuna matusi mengine sio fair kabisa

kama wale waliomtukana kisa mama yake Samata alikaa chini airport...

sasa Malinzi alihusikaje na kutokuwepo viti airport ?
Mkuu, mbona Samatta kila siku anasema angetamani MAMA yake angekuwa hai aone mafanikio yake. Au mama mdogo!
 
Kwa kifupi, huyo Boss wa TFF hajui uongozi wa soka, na uongozi wowote ule...!

Yaani kwenye press conference uliyoitisha mwenyewe unaongea huku umefura..! Ajab kabisa
 
Mimi nilishamsamehe siku nyingi baada ya kubaini kuwa hafai.
 
Malinzi ajiulize haya:
1. Ile taifa stars maboresho iko wapi?
2. Nyasi bandia kwa nini kaitaba bukoba na si ccm kirumba mwanza uwanja wenye hadhi ya kimataifa?
3. Hivi Yanga wapo juu katiba ya uendeshaji mpira wa nchi hii? Wakati TFF wanaikomalia TEFA juu ya suala la uchaguzi, lakini kama wasimamizi wa soka na vilabu vya nchi hii TFF wamekuwa vipofu juu ya sakata la uchaguzi wa Yanga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…