Jamani bodi ya mikopo hivi hela yetu ya field lini?

Jamani bodi ya mikopo hivi hela yetu ya field lini?

KILLERS KISS GUY

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2013
Posts
718
Reaction score
258
kwa kweli bodi ya mikopo ifike hatua muwe na aibu hivi hela zetu bado munafanyia biashara tu?

Nani asiyejua udhalimu uliopo ndani ya bodi ya mikopo mtu akiajiliwa leo baada ya miezi yaa mitatu ana gari la kukata na shoka hivi hela munazito wapi kama hela zetu munaenda kuzizungusha,,, UDSM, UDOM, SAUT, Mzumbe tuungane kwa pamoja tukadai hela zetu.
 
kwa kweli bodi ya mikopo ifike hatua muwe na aibu hivi hela zetu bado munafanyia biashara tu? nani asiyejua udhalimu uliopo ndani ya bodi ya mikopo mtu akiajiliwa leo baada ya miezi yaa mitatu ana gari la kukata na shoka hivi hela munazito wapi kama hela zetu munaenda kuzizungusha,,, UDSM, UDOM, SAUT, mzumbe tuungane kwa pamoja tukadai hela zetu

hahahahaha.
 
kwa kweli bodi ya mikopo ifike hatua muwe na aibu hivi hela zetu bado munafanyia biashara tu? nani asiyejua udhalimu uliopo ndani ya bodi ya mikopo mtu akiajiliwa leo baada ya miezi yaa mitatu ana gari la kukata na shoka hivi hela munazito wapi kama hela zetu munaenda kuzizungusha,,, UDSM, UDOM, SAUT, mzumbe tuungane kwa pamoja tukadai hela zetu

ni kweli hawa jamaa wamezid sasa. Hela hawato hadi sasa sijui wana mpango gani. Sijui wanataka wanachuo wakajiuze kwao ili wapate hela ya kuendeshea maisha yao au vip?
 
kwa kweli bodi ya mikopo ifike hatua muwe na aibu hivi hela zetu bado munafanyia biashara tu? nani asiyejua udhalimu uliopo ndani ya bodi ya mikopo mtu akiajiliwa leo baada ya miezi yaa mitatu ana gari la kukata na shoka hivi hela munazito wapi kama hela zetu munaenda kuzizungusha,,, UDSM, UDOM, SAUT, mzumbe tuungane kwa pamoja tukadai hela zetu

Haya ndio maandalizi ya BRN, ni aibu. Wanafunzi wamesaini form za kupatiwa pesa hizo kwenye akaunti zao toka wiki ya tatu ya mwezi wa sita, huku wakielezwa kuwa pesa wangepatiwa baada ya siku tatu toka wasaini. Leo hii napoandika ni wiki ya tatu imepita. Hivi akina Mwigulu Nchemba wanafanya nini??? Mwigulu, Malima na Saada Mkuya, hebu jaribuni kufikiria kuwa kama mngelikuwa ni nyinyi mngefanyaje???. Ninawanafunzi nimewapangia kituo cha Field Ifakara, na huko hawana ndugu hata mmoja. Kwa ahadi ya Bodi ya mikopo kuwa watawekewa pesa baada ya siku tatu toka wasaini, wanafunzi hawa walipomaliza mitihani yao tu tarehe 4 July, walikopa pesa ili waende kuripoti field tarehe 8/July siku ambapo walitakiwa kuripoti. Wanafunzi hao walifika huko kituoni Ifakara na baada ya siku tatu walizokaa huko pesa yote waliyokuwa nayo imewaishia.Kumbuka huko hawana ndugu.Wanapanga vyumba na kujinunulia chakula. Hadi hapa napoandika ujumbe huu wanaishi kwa msaada wa wasamalia wema.Je hii ni haki kweli??? Kama Serikali inajua kuwa pesa hazipo kwa nini wasitoe taarifa mapema ili hizo field zika ahirishwa hadi hapo watakapopata hizo pesa kuliko kuwatesa watoto wa watu namna hii???
 
Kiukweli hali ni tete sana huku fild!! Maana kuna wanafunzi ambao wameenda kufanyia fild ktk mikoa ambayo sio kwao wala kuwa nandugu. Naisihi serikali ilichukulie tatizo hili serious maana kuna mwalimu mmoja jana ktk kituo fulani alianguka darasani kwa kukosa chakula siku mbili
 
mtoa mada inaelekea umepa field Tanesco ambako hata .... ya maji hakuna?
 
niliweza kuenda field siku tatu za mwazo baada ya hapo nikaishiwa na kwenda kwa rafiki wa mzazi wangu toka hapo sijaonekana maana hata hela ya nauli sina
 
Mm Nipo CRDB hapa posts Lakin Hal tete hatupewi hata chai hayo mengine ndo usiulize hela mpaka sasa Hamna yan ... Ninamagadhabu vbaya mno tunakula kama mbwa
 
nmechoka kwenda kwenye ATM kucheki kama wameweka yani sio poa nimechoka
 
The government is for us or we are here for the government??!,kwasababu tumezoea kukausha na vyuo vimefungwa hawana cha kupoteza kwani hatuwezi kugoma kisa watu wamesambaratika,,,leo nimesikia redion kuwa hawana hera ila kwanini kwenye mabunge yao hawasemi kama hawana hela
 
Ni wiki ya tatu sasa tangu field zianze kwa wanafunzi mbalimbali wa elimu ya juu lakini katika hali ya kusikitisha mpaka sasa hawajapata fedha ya kujikimu kwa ajili ya field baadh waliotangulia kwa gharama zao wenyewe wako ktk hali mbaya sana kifedha na wengine bado hawajawasili katika maeneo mbalimbali waliyopangiwa kwa ajili ya field.....

bodi ya mikopo wanasema hawana fedha wanasubiri hazina iwapelekee na hazina nayo haijatoa majibu ya kueleweka kwamba lini wataipa bodi fedha hiyo......Tunataka kusikia kauli ya serikali lini fedha hizi zitapelekwa kwa wahusika.....wadau wa Elimu na wanaharakati mbalimbali saidieni hambo hili
 
Jumla ya vyuo 13 vimekumbwa na tatizo hili vyuo hivi ni;
UDSM,
UDOM,
SAUT main campus mwanza,
IFM
SAUT songea
mkwawa iringa,
Chuo kikuu Tumaini tawi la mbeya,
SAUT mbeya,
Mzumbe tawi la mbeya,
Chuo cha kodi Dar es salaam
DUCE,
Jordan university-morogoro

Field work ni muhimu kwa kila mwanafunzi wa elimu ya juu ili aweze kuhitimu......hivi serikali ina nia dhati ya kupata wataalamu katika kada mbalimbali kutoka elimu ya juu kwani inashangaza kuona wanafunzi kutoka vyuo zaidi ya kumi na tatu wanakosa fedha za field lakini serikali iko kimya......Source mtanzania na majira ya ijumaa tarehe 17/7/2014 tamko lilitolewa na mwenyekiti wa Tahliso
 
Duh! Hii serikali ni majanga tu! Wanakera sana. kwa mtindo huu hauwezi kutoa wasomi wenye uelewa.
 
mkuu wanaandamanaje wakiwa mmoja mmoja makazini wanakofanyia field! Nakushauri uwe unatafakari kabla ya kupost comment yako
Ni tungo tata hiyo dadangu, ungeitafakari kwa mapana ungeelewa namaanisha nini....KWA KUWA UNATAFAKARI SANA..UTAELEWA TU..
 
Back
Top Bottom