Hivi we miss Judith ulivyosoma maelezo yangu uliyaelewa? au ulikimbilia tuu kutoa coment? Maana sijasema nimemuomba hela akaninyima kwahiyo ndio nimemind ila nimesema hana time na mimi kanitenga watoto wake wote wanajua dingi yupo swafi ila mimi hajawahi kunidokezea nasikia pembeni tuu nanikikausha kama bado sijasikia nikijidai kumpa vijiela vyangu kama zamani anapokea kama vile hana haniambii lolote. Sasa wewe naona uko nje ya mstari sana coments zako zipo kama mtu
anayeropoka ovyo. au kama vipi ingia jukwaa la dini
mpendwa Loly,
maelezo yako nayo yamekuwa cummulative in nature. mtu akisoma post # 1 anapata picha fulani, akiendelea kusoma majibu yako kwa wachangiaji picha inabadilika, kwa hiyo na wewe unachangi watu wasikupate sawasawa kutokana na presentation yako.
1. hapa mwiishoni unasema we ndio mdogo kuliko wote,
2. katikati ulisema hao ndugu zako (unaoona anaowasaidia huku wewe kakutenga) wa uwezo mkubwa zaidi yako kimaisha/kifedha.
3. post zingine unasema ukijifanya kumpa hela zako kidogo anachukua na wewe unasikia kuwa ana hela nyingi toka kwa watu ila wewe hakuambii,
4. post nyingine unasema ananunua/anabadilisha magari kila anapotaka,
5. sasa hapa kwenye majibu yangu unaruka tena kuwa shida yako siyo pesa, shida yako hazungumzi na wewe!
kwa ujumla unasema baba yako kapata bingo, mara kapata mkwanja hadi anabadili magari lakini husemi huu mkwanja ni nini? ashinda bahati nasibu, kapora hela benki, kafanya biashara ikafanikiwa, kapata kazi nzuri zaidi, kapanda cheo? kusema tu mkwanja kwa kweli hueleweki!
hivi unawezaje kumsaidia (vihela kidogo) mtu anayebadilisha magari wakati wewe huwezi kubadilisha magari?, je hao ndugu wenye uwezo mkubwa zaidi yako anawasaidia mitaji wewe anakuacha, je wana uwezo mkubwa zaidi ya baba yao au baada ya kupewa mitaji ndio wakahangaika na biashara zikawakubali? je una wivu wa mafanikio ya baba yako na ndugu zako wengine? au hukutaka wainuke kimaisha?
je ulitaka kwa kuwa unaamini baba yako ana hela kukuzidi wewe basi ukimpa hata 1000/= akatae? je hapo usingekimbilia jamvini kusema baba yako kakudharau na kakataa zawadi yako kwa kuwa ni ndogo? je unajua kuwa mzazi hakatai chochte toka kwa mtoto hata kama ni kidogo iasi gani?
unasema hakuna tatizo kati yake na mama yako, je unayajua mambo yao hata ya liyotokea chumbani kwao kabla wewe hujazaliwa?
unasema baba yako haongei na wewe, we ulishamuomba kuongea naye akakataa? ulishawahi kumwambia kuwa una hamu ya kutaka kuongea naye akapuuza? ulishawahi hata kumuandalia luch/dinner maalum ili upate nafasi ya kuongea naye na umueleze unavyofeel mahusian yenu?
unaonekana unapuuza sana ushauri wangu na wengine tunaokutaka 'usimfungie vioo" baba yako na unachekelea sana ushauri wa wanaokuambia mpotezee, achana naye nk. kuna mtu wiki chache zilizopita alikuja hapa kusema kuwa hampendi mama yake, leo na wewe unaleta kioja kumhusu baba yako kwa sababu ya pesa!
angalieni wapendwa, shetani yuko kazini hata sasa, anapepeta watu kama ngano, naam yumkini hata walio wateule.
kuweni macho!
Mungu akubariki sana Loly
Mungu awabariki wapendwa wote mlionisoma
Amina.