Jamani kaka yangu; hayo unayomfanyia wifi yangu, Mungu anakuona!

Jamani kaka yangu; hayo unayomfanyia wifi yangu, Mungu anakuona!

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
1,679
Reaction score
2,123
Kila siku wifi anaamka alfajiri, anakuchemshia maji ya kuoga. Anafanya usafi wa nyumba, anapika chai, anaogesha watoto. Anaenda kutafuta mkaa, anahakikisha familia imepata chakula.

Sokoni anakazana—anauza maandazi ili watoto wapate ada ya shule maana wewe huwalipii. Jioni inamkuta bado kwenye mishe mishe. Anarudi nyumbani hoi, jua limempiga kutwa nzima. Anaandaa tena chakula cha usiku.

Loo, kaka. Mbona unajiona mfalme? Unaondoka asubuhi kwenda kazini baada ya kunywa chai aliyokupikia wifi. Ukitoka kazini unaenda unakokujua, unarudi usiku wa manane unanuka pombe, na harufu ya wanawake wengine inakufuata. Bila haya, unampiga wifi makonde na kumshutumu eti amechelewa kukufungulia geti. Badala ya kumshukuru amekesha akisubiri urudi, unatishia kumtimua na kumpa talaka.

Anakukaribisha chakula mezani, unakataa kula, eti chakula kibichi wakati hata huonji. Wifi yangu mvumilivu, anakuandalia tena maji ya kuoga. Anakuhudumia kwa heshima unalala fofofo.

Wifi yangu anateseka, siku nyingine analala njaa na watoto, wakati wewe unakula vinono hotelini na hao malaya. Unasahau wifi ndiye anayekufulia nguo, ukienda kazini unaonekana "smart"

Kaka, mara hii umesahau? Wifi yangu alikuvumilia wakati huna pesa. Ni yeye aliyekufuta machozi ulipofukuzwa kazi. Sasa umepata kazi mpya, shukrani yako imekuwa mateke?

Kaka, usisahau: ulikaa ndani ya tumbo la mama miezi 9. Ulinyonya maziwa ya mama. Ulilelewa kwa mikono ya mama. Mheshimu mke wako, yeye naye ni mama.

Kaka, nakuheshimu, lakini nakuambia ukweli: Unayoyafanya, Mungu anakuona. Kilio cha wifi yangu, Mungu anakisikia. Machozi ya wifi yangu, Mungu anayaona. Naomba ubadilike, usisubiri Mungu alipize kisasi.

"Enyi waume, wapendeni wake zenu." (Waefeso 5:25)
==================

Tunaadhimisha siku ya Wanawake Duniani.
Tunakumbushana thamani ya Mwanamke.
 
kama ni kweli kaka yake anamtendea hayo mkewe na watoto haifai na haipendezi kabisa, ila nawe shughulika na yako ya kwake muachie mwenyewe na mke wake. hongera kwa my late mother, my wife na wanawake wote wenye utu ulimwenguni.
 
ila nawe shughulika na yako ya kwake muachie mwenyewe
Duh, kama kila mtu atasema 'shughulika na yako'(mind your own business), basi watu wengi wataendelea kuteseka bila kupata msaada. Kuuona uovu na kunyamaza sio hekima, ni sawa na kushiriki huo uovu. Mungu mwenyewe anatuagiza kuwapenda na kuwatetea wanaodhulumiwa.

Mithali 31:8
"Fumbua kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu; uwatetee watu wote walioachwa peke yao."

Isaya 1:17
"Jifunzeni kutenda mema, tafuteni haki. Wateteeni waliodhulumiwa..."
 
Ngoja waje...
Wenyewe wanasema hayanaga muongozo haya...
 
Nyie mawifi wa Kibongo mnakuwaga wanafki sana..

Kaka yako akianza kumjali na kumuhudumia mkewe, mtaanza kusema amepewa limbwata.

Kaka yako akibadilika lazima utakuja na uzi mwingine. Hamnaga jema ninyi
Jamani, sio kila wifi ni mnafiki, wala sio kila mke ana limbwata. Tunapozungumza kuhusu unyanyasaji wa wanawake, hatumaanishi kuwa kila mume ni mbaya. Lakini tukiwanyamazia wanaowatesa wenzetu, tunakuwa sehemu ya tatizo.

Mithali 31:8-9
"Fungua kinywa chako kwa ajili ya bubu, kwa ajili ya haki ya wote walioachwa peke yao. Fungua kinywa chako, hukumu kwa haki, mtetee mnyonge na maskini."

Tuwe na mioyo ya kupinga mabaya, bila kujali ni nani anayeyafanya.
 
Tuondolee ujinga wako humu.
Watu wabaya Sana nyie mnaojiita feminists mmechangia pakubwa uharibifu kwny ndoa.
 
Tuondolee ujinga wako humu.
Watu wabaya Sana nyie mnaojiita feminists mmechangia pakubwa uharibifu kwny ndoa.
Ukinitukana, unanipongeza🙂 Tena ndio unanipa nguvu zaidi ya kuandika.

Inaonekana umeudhika au labda umeuelewa ujumbe wangu vibaya; pengine unahisi nashambulia ndoa badala ya kutetea haki.

Mkuu, kutetea haki za wanawake sio kuharibu ndoa, bali ni kuziimarisha. Ndoa yenye upendo na heshima inakua, lakini ndoa yenye mateso na unyanyasaji inaharibika.

Waefeso 5:25
"Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda kanisa, akajitoa kwa ajili yake."
 
Dada angu shemeji tumemkuta bar analalamika kuwa unampelekesha sana kama mtoto

Halafu amegundua unamcheat.....suluhisho hana zaidi ya mambo mawili kichwani kwake ajiue au akuue

Kuelekea siku ya wanawake kumbushaneni kuwa mna mchango mkubwa katika kuharibu maisha ya wanaume
 
Kila siku wifi anaamka alfajiri, anakuchemshia maji ya kuoga. Anafanya usafi wa nyumba, anapika chai, anaogesha watoto. Anaenda kutafuta mkaa, anahakikisha familia imepata chakula.

Sokoni anakazana—anauza maandazi ili watoto wapate ada ya shule maana wewe huwalipii. Jioni inamkuta bado kwenye mishe mishe. Anarudi nyumbani hoi, jua limempiga kutwa nzima. Anaandaa tena chakula cha usiku.

Loo, kaka. Mbona unajiona mfalme? Unaondoka asubuhi kwenda kazini baada ya kunywa chai aliyokupikia wifi. Ukitoka kazini unaenda unakokujua, unarudi usiku wa manane unanuka pombe, na harufu ya wanawake wengine inakufuata. Bila haya, unampiga wifi makonde na kumshutumu eti amechelewa kukufungulia geti. Badala ya kumshukuru amekesha akisubiri urudi, unatishia kumtimua na kumpa talaka.

Anakukaribisha chakula mezani, unakataa kula, eti chakula kibichi wakati hata huonji. Wifi yangu mvumilivu, anakuandalia tena maji ya kuoga. Anakuhudumia kwa heshima unalala fofofo.

Wifi yangu anateseka, siku nyingine analala njaa na watoto, wakati wewe unakula vinono hotelini na hao malaya. Unasahau wifi ndiye anayekufulia nguo, ukienda kazini unaonekana "smart"

Kaka, mara hii umesahau? Wifi yangu alikuvumilia wakati huna pesa. Ni yeye aliyekufuta machozi ulipofukuzwa kazi. Sasa umepata kazi mpya, shukrani yako imekuwa mateke?

Kaka, usisahau: ulikaa ndani ya tumbo la mama miezi 9. Ulinyonya maziwa ya mama. Ulilelewa kwa mikono ya mama. Mheshimu mke wako, yeye naye ni mama.

Kaka, nakuheshimu, lakini nakuambia ukweli: Unayoyafanya, Mungu anakuona. Kilio cha wifi yangu, Mungu anakisikia. Machozi ya wifi yangu, Mungu anayaona. Naomba ubadilike, usisubiri Mungu alipize kisasi.

"Enyi waume, wapendeni wake zenu." (Waefeso 5:25)
==================

Tunaadhimisha siku ya Wanawake Duniani.
Tunakumbushana thamani ya Mwanamke.
Pole wifi mtu ila huu ujumbe ungemsomea kaka yako mchana kweupe kabla hajanywa pombe
 
Wanawake wengine mmezid unafik. Huyo Kaka hana jema hata moja?

Iweje uamin kila neno litokalo kinywani mwa wifi yako?
 
Back
Top Bottom