Hilo siyo tatizo maana wa mama na mawifi huwa Hawakubali kwamba mtoto Wa kiume akioa anakuwa na majukumu pia. Wao hasa mawifi huwa hawamuheshimu mke Wa kaka yao yaani wana muona kama house girl tu wa kaka yao. Ndugu huwa wana mdharau wifi hadi na yeye sasa anaamua kusimama kidete. Ukiisoma hiyo story inaonekana hao 4 wame team up against huyo wifi kwamba ame mtwist kaka yao. Ukweli hapo unaanzia kwenye dharau za ndugu ndio maana na yeye amefikia hadi kujibu meseji. Kitu kama jiko si la kumuomba kaka Hilo ni madada na wifi wanalimaliza. Haiwezekani jiko tuu la elfu 50 sijui mama atume meseji kwa mwanae. Hiyo meseji ingetumwa kwa mke wa kaka yao jiko lingenunuliwa siku hiyohiyo na kupelekwa. Wadada ukiwachekea watakuja kubeba hata vitunguu kisa VYA KAKA YETU. Huyo wifi yuko sahihi KABISA.Maoni yangu samahani kama nimemkwaza mtu.
kakolo inategemea hali na mazingira kama uwezo wa kumsaidia mama yako upo kwanini asisaidiwe
Na unaweza kuta ktk familia labda mwenye hali nzuri ni Kaka yao.
Hivi kama mama anaona ana uweza wa kupata pesa sehemu nyingine kwa nini aombe kwa mwanae wa kiume?
Pesa ni nini lakini mie simtetei huyo mwanamke bado naona ana makosa
Kwa mie Binafsi mama aliyenizalia mme wangu namuheshimu na kumuona kama ni mama yangu mzazi.
najua binadamu wote tunamapungufu lakini"lile neno lilosema mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake"
mwenyewe ni kama hili"Hivi leo akipata tatizo na mmewe wa kwanza kumkimbilia ni mama mkwe.
Kwa nini amjibu mama mkwe wake majibu ya ajabu namna hiyo
Kwanza hana adabu
Pili hana hekima
Tatu naona kama hafai kuwa mke ambaye anaweza kujenga ndoa yake.
Nne huyo atakuwa sio mama bora hata watoto anaozaa atakuwa anawafundisha uchoyo na tabia mbaya
Kuna leo na kesho ataacha watoto wake katika mazingira magumu sana