Jamani Mungu anawaona kwa mnayowafanyia kondoo hawa!

Jamani Mungu anawaona kwa mnayowafanyia kondoo hawa!

Nduna shujaa

Senior Member
Joined
Aug 14, 2022
Posts
163
Reaction score
134
Inasikitisha sana kwakeli yani baadhi ya wachungaji wanawaaminisha wanatibu vvu na kuwafanya watu wanaacha dawa hatimaye kufa. Lakini pia niwape kisa kingine nje na hapo juu.

Kwanza nikiri wapo wachungaji wachache wenye karama ya uponyaji, wengine wapiga dili tu.Kisa cha kweli ila sitataja jina la mhanga wala jina la kanisa ila ni kanisa la kilokole pale songea tanga mwenye jina linalofanana na chaji.Wagonjwa wengi waendao kwa mara ya kwanza wanaagizwa wabebe 30000.

Halafu baada ya kukaa naye mezani na kuona tatizo la mhusika akamwambia wewe na mwenzako leteni 200000 wakatowa wale waumini wagonjwa akawa anawaombea mwezi mzima wakiwa wanakaa hapo eneo la ibada hawakupona hatimaye wakaaga kuondoka.

Mchungaji akawambia ataenda nyumbani kwao kutoa madudu yaliyopo pale nyumbani,wahusika walipofika nyumbani wakampigia unakuja lini mchungaji akawambia tuma ela ya mafuta ya gari ikatumwa 50000.Sasa toka hapo walipotuma wakimkumbusha aende anawapa kalenda mwisho wa siku anakuwa mkali na kusema hawezi kwenda kwajili yao labda wao wagonjwa waumini waende tena kanisani.

Wachungaji wa namna hii wanawaharibia cv wenzao na kujipatia kipato na si huduma.Ifike wakati serikali iyachunguze makanisa yote yanayomilikiwa na watu binafsi kuanzia kiutendaji na akaunti zao ili walipe kodi.
 
Mtu isipomfaa akili yake,,,,basi utamdhuru ujinga wake...

Hapa Duniani UJINGA wako ni fursa kwa mtu mwingine,,,Mchungaji anachofanya ni ametumia Fursa ya Ujinga wa wengine kujinufaisha...,
 
Mtihani sana, mnawaamini vipi hao wachungaji!! Kuna mdada mmoja alikua akiumwa, alipelekwa kwa watu wenu wamtibu ikashindikana, narudia tena ilishindikana, wakampereka kwa sheikh, mbona alipona!
 
...Kwanini unamficha jina lake Mchungaji Tapeli huyo? Au Habari Yako Sio Kweli??
 
Unavyokataa kumtaja maana yake unabariki matendo yake Kwa kukataa kumtaja.

Kama habari Yako ni ya kweli unaogopa Nini kumtaja Sasa
 
Kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake, sisi serakali tunajua mnakula (kanisa) ila msivimbewe!!
 
...Kwa Nini unamficha jina lake Mchungaji Tapeli huyo? Au Habari Yako Sio Kweli??
Nimetaja hapo jina lafanana na chaji.Hata ukiuliza maenen hayo mchungaji anayefanana na jina la chaji utamata.Na locationi nimetowa.
 
Unavyokataa kumtaja maana yake unabariki matendo yake Kwa kukataa kumtaja.

Kama habari Yako ni ya kweli unaogopa Nini kumtaja Sasa
nimesema jina lafanana na chaji .Na locationi nimeitaja.
 
Back
Top Bottom