DOKEZO Jamanii Shule ya Msingi Sinza ni chakavu, madarasa yamebomoka na Ofisi ya Walimu nayo imebomoka

DOKEZO Jamanii Shule ya Msingi Sinza ni chakavu, madarasa yamebomoka na Ofisi ya Walimu nayo imebomoka

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
photo_2025-01-22_10-48-21 (2).jpg

photo_2025-01-22_10-48-22.jpg
Nimefika Shule ya Msingi Sinza iliyopo Sinza, Dar es Salaam, kwa ajili ya kumuandikisha Mtoto wa Dada yangu ili kuanza masomo ya Darasa la Kwanza, lakini nasikitika kusema nilichokutana nacho ni huzuni kubwa kama sio mshangao, hali hiyo imenifanya nibadili uamuzi na kuamua kumpeleka kwenye Shule nyingine.

Kuanzia Ofisi za Walimu, wamejibana kwenye chumba kimoja ambacho ubora wake unatia mashaka.

Eneo lingine la ofisi limeporomoka kutokana na uchakavu, hali hiyo inawalazimu Walimu kubanana kwenye kipande kidogo cha chumba kilichobakia.

Hali hiyo nimeambiwa kwamba imedumu kwa muda sasa, ambapo Walimu wakati mwingine wanalazimika kukaa kwenye kibalaza ili kutekeleza majukumu yao mfano wakiwa wanasahihisha madaftari ya Wanafunzi.

Nimesikitika sana kwa kuwa Shule hiyo Mjini Jijini tena katikati ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, eneo ambalo kikawaida nilitegemea miundombinu yake ingekuwa rafiki na yenye hadhi, kibaya zaidi hata baadhi ya vyumba vya madarasa vinaonekana kuchoka na kuchakaa.

Kwa hali niliyoshuhudia kwa macho yangu nitumie jukwaa hili kutoa wito wangu kwa mamlaka za Kiserikali ikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, TAMISEMI wafuatilie suala hilo na kufanya marekebisho ambayo yatawaweka Walimu na Wanafunzi katika mazingira salama na rafiki.

Kuacha hali hiyo iendelee ni kuhatarisha usalama wa Walimu na Wanafunzi lakini vilevile inaweza kuchangia kushusha morali za Walimu katika kuwafundisha Wanafunzi wetu.
photo_2025-01-22_10-48-19.jpg

photo_2025-01-22_10-48-21.jpg

photo_2025-01-22_10-48-16.jpg

photo_2025-01-22_10-48-23.jpg
 
Ndio haina hata Paa siku zote au ipo kwenye matengenezo?

Vipi ikija mvua au kukiwa na jua kali?
 
Nimefika Shule ya Msingi Sinza iliyopo Sinza, Dar es Salaam, kwa ajili ya kumuandikisha Mtoto wa Dada yangu ili kuanza masomo ya Darasa la Kwanza, lakini nasikitika kusema nilichokutana nacho ni huzuni kubwa kama sio mshangao, hali hiyo imenifanya nibadili uamuzi na kuamua kumpeleka kwenye Shule nyingine.

Kuanzia Ofisi za Walimu, wamejibana kwenye chumba kimoja ambacho ubora wake unatia mashaka.

Eneo lingine la ofisi limeporomoka kutokana na uchakavu, hali hiyo inawalazimu Walimu kubanana kwenye kipande kidogo cha chumba kilichobakia.

Hali hiyo nimeambiwa kwamba imedumu kwa muda sasa, ambapo Walimu wakati mwingine wanalazimika kukaa kwenye kibalaza ili kutekeleza majukumu yao mfano wakiwa wanasahihisha madaftari ya Wanafunzi.

Nimesikitika sana kwa kuwa Shule hiyo Mjini Jijini tena katikati ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, eneo ambalo kikawaida nilitegemea miundombinu yake ingekuwa rafiki na yenye hadhi, kibaya zaidi hata baadhi ya vyumba vya madarasa vinaonekana kuchoka na kuchakaa.

Kwa hali niliyoshuhudia kwa macho yangu nitumie jukwaa hili kutoa wito wangu kwa mamlaka za Kiserikali ikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, TAMISEMI wafuatilie suala hilo na kufanya marekebisho ambayo yatawaweka Walimu na Wanafunzi katika mazingira salama na rafiki.

Kuacha hali hiyo iendelee ni kuhatarisha usalama wa Walimu na Wanafunzi lakini vilevile inaweza kuchangia kushusha morali za Walimu katika kuwafundisha Wanafunzi wetu.
Hapo sio Kilwa kweli 😛
 
Subirini kwanza tukamilishe uagizaji wa mabasi ya Utong na maandalizi ya mengine ya uchaguzi, hizo shule sio kipaumbele chetu..ukiona hazifai peleka mwanao private..ebo!
 
Mbaya zaidi sasa hv wazazi inimladi tumeambiwa elimu Bure hata ukiambiwa mchangie mfuko wa cement mnataka serikali inunue
 
Ngoja kwanza Lucas Mwashambwa aje akuletee ile picha ya mabasi ya chama chake cha ccm yakipeleka wajumbe Dodoma kutapanya hela za walala hoi, ili tulinganishe.
 
Kikubwa Tuendelee na pambio za kusifu, kuabudu na kujipendekeza.
 
Mbona mna makelele hivi, hela iliyopo serikalini ni kwa ajili ya goli la Mama na si vinginevyo, naomba tuelewane.
 
Nimefika Shule ya Msingi Sinza iliyopo Sinza, Dar es Salaam, kwa ajili ya kumuandikisha Mtoto wa Dada yangu ili kuanza masomo ya Darasa la Kwanza, lakini nasikitika kusema nilichokutana nacho ni huzuni kubwa kama sio mshangao, hali hiyo imenifanya nibadili uamuzi na kuamua kumpeleka kwenye Shule nyingine.

Kuanzia Ofisi za Walimu, wamejibana kwenye chumba kimoja ambacho ubora wake unatia mashaka.

Eneo lingine la ofisi limeporomoka kutokana na uchakavu, hali hiyo inawalazimu Walimu kubanana kwenye kipande kidogo cha chumba kilichobakia.

Hali hiyo nimeambiwa kwamba imedumu kwa muda sasa, ambapo Walimu wakati mwingine wanalazimika kukaa kwenye kibalaza ili kutekeleza majukumu yao mfano wakiwa wanasahihisha madaftari ya Wanafunzi.

Nimesikitika sana kwa kuwa Shule hiyo Mjini Jijini tena katikati ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, eneo ambalo kikawaida nilitegemea miundombinu yake ingekuwa rafiki na yenye hadhi, kibaya zaidi hata baadhi ya vyumba vya madarasa vinaonekana kuchoka na kuchakaa.

Kwa hali niliyoshuhudia kwa macho yangu nitumie jukwaa hili kutoa wito wangu kwa mamlaka za Kiserikali ikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, TAMISEMI wafuatilie suala hilo na kufanya marekebisho ambayo yatawaweka Walimu na Wanafunzi katika mazingira salama na rafiki.

Kuacha hali hiyo iendelee ni kuhatarisha usalama wa Walimu na Wanafunzi lakini vilevile inaweza kuchangia kushusha morali za Walimu katika kuwafundisha Wanafunzi wetu.
k Mamake! CCM, nilisoma hapa, 90s, waalimu wali kuwa wanajari kuuza uji na visheti tu! Wakijichokea, wanawaambia wanafunzi waendelee na mapumziko mpaka muda Wa kutoka
 
Nenda TAMISEMI kwa waziri husika kama kweli una uchungu.

Kuna shule huko hazina madawati na kuna mwalimu mmoja na watu wanasoma wewe unasema hapa sinza kwenye masomo ya ziada kibaoo.

Tena jirani na Tasisi ya Elimu. Wewe mwenyewe nahisi ni mwalimu. Ngoja Mpwayungu village aje...
 
Inasikitisha sana na watawala busy kununua mabasi ya chama
 
Back
Top Bottom