Jambazi akamatwa akitubu dhambi Kanisani

Jambazi akamatwa akitubu dhambi Kanisani

Ana bahati sana huyo njemba, kwa ninavyowajua polisi wetu, yaani mpaka wamfuate kote huko ilikua wamuue afie mbali, labda jamaa kashtukia na kujipeleka kanisani ili apate pakutokea, na ile kwamba hakimu amemhukumu miaka mitano itakua jamaa hakuungamana madhambi yake yote, kataja vitu vidogo vidogo vya ksababisha afungwe kifungo cha muda mfupi.

Polisi wetu wahangaike kutoka kituoni ili wakufuatilie, raslimali zote hizo uwahangaishe, lazima wakutolee nje nje ufe wakipata mwanya au fursa, ila jamaa kacheza ndefu kwa kuingia kanisani na kumwaga mbele ya nyomi na kuwaacha mapolisi wakiwa solemba bila la ziada ila kumkamata kikawaida kawaida.

Jamaa akinyoosha tabia zake akiwa gerezani, kifungo kinaweza kikapungua hadi hata mwaka mmoja, kimsingi asome Biblia humo, ahubiri hubiri na kuimba nyimbo za sifa na asijiingize kwenye ugomvi wowote, sema kunao wanachama wenzie waliobaki nje wanaweza kuunda njama za kumdhuru ili asimwage mtama.
Pamona na kwamba mimi sio Mkenya but police wanafanana utendaji kazi wako kwa nchi nyingi; sometimes kumkamata mwizi/jambazi sugu hua kuna tafsiri mbili, moja wapo ni hili sugu ambalo limeamua kuacha madhambi yake litaje basi MTANDAO wao, marafiki au majambazi yenzie ili na yenyewe yaingizwe kwa tageti, sababu nyingin ya pili ni kutaka kuionesha jamii kwamba sio kweli kwamba wao police ni mara zote hua wanaua, wakati mwingine hua wanawapeleka mahakamani, na usidhani huko magereza ndio mwisho wa mchezo, bado watatuma watu wao waendelee kumpeleleza hadi kieleweke
 
Back
Top Bottom