Jambo gani la kushtusha la kitaifa liliwahi kumwibua hadharani Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango?

Kilichomuibua hadharani ni Corona
 
Aliongea hadharani kipindi kile anazushiwa kuwa amekufa.
Akasema alishangazwa na kiongozi mkubwa kuwasha mshumaa kuwa amekufa.
Sijui huyo kiongozi mkubwa ni nani hajamtaja leo!!
 
Alishapewa maelekezo akar kimya. Si unakumbuka kipindi amekula kiapo cha u VP alianza kama yeye ndiye mkuu wa ikulu.
 
Hukumsikia may mosi 2024?
 
Naamini Mpango ndie Mtu pekee CCM inaweza msimamisha kugombea URAIS baada ya SSH kuondoka

Huyu mshua kama anaandaliwa hivi maana nahisi ndio kombora pekee lisilo na makando kando CCM
 
Sina uhakika kama wakati wa utawala wa Magufuli mambo yalikuwa yanaenda vizuri sana, ninachojua yalakuwa yanaenda anavyotaka, lakini sio lazima iwe yalikuwa yanaenda kwa usahihi.
Kila mtu anajua ni Bora wakati wake kuliko Sasa....
Kwa kila kitu.
 
Kila mtu anajua ni Bora wakati wake kuliko Sasa....
Kwa kila kitu.
Mimi ni mmojawapo wa kila mtu, ila sioni huo ubora usemao. Kwangu hofu, na nidhamu za kinafiki sio ubora wa uongozi. Huenda tunatumia vipimo tofauti kufikia hitimisho.
 
Huyu Mkatukumeni na Mlei mwenzangu ambaye ni Makamu wa Rais wa JMT sijawahi kumsikia aki address jambo lolote liwe kubwa au dogo hasa kama linagusa maisha na hisia za Raia.
Alishawaambia yeye anaogopa na anatetemeka hata akiachiwa nchi hajui pakuanzia
 
Naamini Mpango ndie Mtu pekee CCM inaweza msimamisha kugombea URAIS baada ya SSH kuondoka

Huyu mshua kama anaandaliwa hivi maana nahisi ndio kombora pekee lisilo na makando kando CCM
Labda Rais wa nyie waha, huyo hafai hata kidogo,

Ni bora tu samia aongoze hadi 2056 kuliko huyo asiyejua hata kuongea
 
Huyo Mwamba haelewi na haelewani na wengi huko koridoni. Sema tu basi!
 

Yeye anahusika na mambo ya mazingira na muungano. Kikatiba anasema kama nani?
 

Ila udini unakusumbua sana. Unaangalia watu kwa dini zao badala ya matendo yao. It falls short....
 
Alipopatwa na kupona Uviko 19 then akaja hadharani huku akilia na kutokwa na makamasi na udenda akitusihi watanzania wenye viburi na ubishoo kuvaa barakoa. Toka hapa sijamuona tena na sijuwi kama bado yupo.
Duh, nimecheka sana kwa ujumbe wako.
Au labda fuse zilikata toka kipindi kile.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…