Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza; Mvuvi Nigeria atafuna samaki mwenye thamani ya mabilioni ya shilingi bila kujua

Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza; Mvuvi Nigeria atafuna samaki mwenye thamani ya mabilioni ya shilingi bila kujua

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
M1.jpg

Mvuvi mmoja katika kijiji cha Warri, jimbo la Niger Delta nchini Nigeria amevua samaki aina ya Blue Marlin mwenye uzito wa 87 kgs na kumchinja kisha kugawana nyama na wanakijiji wenzie.

Baadae kampuni ya Pacific seafood ya nchini Marekani iliposikia habari za kuvuliwa kwa samaki huyo adimu duniani ilitangaza offer ya 30,000$ kwa kila kilo sawa na TZS 69M kwa kilo, ambapo ingelipa jumla ya 2.6 US$ million sawa na Tshs bilioni 6 kwa kilo zote 87. Lakini wakati kampuni hiyo inatangaza offer hiyo tayari samaki huyo alikua ameshaliwa na kuisha.

Frank Dulcich Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Pacific Seafood amesema kitu ambacho mvuvi huyo hakujua ni kwamba wakati anafurahia kutafuna minofu ya samaki huyo, alitafuna pia urithi wa familia yake vizazi na vizazi.

"As he was eating together with his villagers, he didn't know that he has eaten the wealth for his generations to come" amesema Dulcich!

Blue Marlin ni moja ya samaki adimu sana duniani na wenye thamani kubwa sana baada ya Bluefin Tuna na White Marlin. Wanapatikana bahari ya Pacific tu, na kabla ya huyu aliyepatikana Nigeria, mwingine alipatikana nchini Nicaragua mwaka 2014!

M2.jpg
M3.jpg

 
Mvuvi mmoja katika kijiji cha Warri, jimbo la Niger Delta nchini Nigeria amevua samaki aina ya Blue Marlin mwenye uzito wa 87 kgs na kumchinja kisha kugawana nyama na wanakijiji wenzie.

Baadae kampuni ya Pacific seafood ya nchini Marekani iliposikia habari za kuvuliwa kwa samaki huyo adimu duniani ilitangaza offer ya 30,000$ kwa kila kilo sawa na TZS 69M kwa kilo, ambapo ingelipa jumla ya 2.6 US$ million sawa na Tshs bilioni 6 kwa kilo zote 87. Lakini wakati kampuni hiyo inatangaza offer hiyo tayari samaki huyo alikua ameshaliwa na kuisha.

Frank Dulcich Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Pacific Seafood amesema kitu ambacho mvuvi huyo hakujua ni kwamba wakati anafurahia kutafuna minofu ya samaki huyo, alitafuna pia urithi wa familia yake vizazi na vizazi.

"As he was eating together with his villagers, he didn't know that he has eaten the wealth for his generations to come" amesema Dulcich.!

Blue Marlin ni moja ya samaki adimu sana duniani na wenye thamani kubwa sana baada ya Bluefin Tuna na White Marlin. Wanapatikana bahari ya Pacific tu, na kabla ya huyu aliyepatikana Nigeria, mwingine alipatikana nchini Nicaragua mwaka 2014.!

Kwanini walimhitaji huyo samaki..?? Ana kazi gani.. na faida gani..!!??
 
Kumbe na wewe Mshana Jr huwa ni mwamba wa kuleta taarifa feki JF, kama huyo samaki anapatikana bahari ya Pacific tu, na wakati huo Nigeria hupakana na Atlantic tu, wala si Pacific manake fake news! BTW source of inf hujaweka!
Mkuu Humjui huyu bwana? Kiufupi ni mtu anayejifanya kudandia dandia taarifa ili kutafuta chippu popularity jf
 
Huyo jamaa baada ya kupata taarifa ya thamani ya huyo samaki lazima alipoteza fahamu. Ila sasa nina amini mtu unaweza kurithi hata "UJINGA". Jamaa amerithi kwa mababu zetu waliokua wanatumia "ALMASI" kama kete za bao.

Usishangae siku mbili hizi huyo jamaa akafa kizembe kwa "PRESHA, MSONGO WA MAWAZO colabo na KUJILAUMU"
 
" Blue Marlin ni moja ya samaki adimu sana duniani na wenye thamani kubwa sana baada ya Bluefin Tuna na White Marlin. Wanapatikana bahari ya Pacific tu, na kabla ya huyu aliyepatikana Nigeria, mwingine alipatikana nchini Nicaragua mwaka 2014.!"

Pacific Ocean inafika Nigeria??????? JF members tuwe tuna heshimiana please.
 
Back
Top Bottom