Jambo Usilolijua: Nyerere alipokea Taifa la namna gani? Mpango wa Kwanza wa Maendeleo 1961

Jambo Usilolijua: Nyerere alipokea Taifa la namna gani? Mpango wa Kwanza wa Maendeleo 1961

Mikoa ya Kusini WTZ wengi walikuwa wanaishi vijijini kabla ya hata Nyerere kuzaliwa. Nenda ukaone miji kama Rufiji, Kivinje, nk na vijiji karibu yake, vilikuwepo kable ya Nyerere. Mikoa ya Kusini kuna majumba ambayo yapo vijijini yalijengwa tangu miaka ya 1400 na watu walikuwa wanaishi kwa kutumia njia nyingi, kabla Dictator Nyerere kuzaliwa. Maisha ya vijijjini ya Mikoa ya kusini yalikuwa mazuri sana kulinganisha na mikoa mingine. Nyerere na sera zake za Ujamaa alianza kuchukia prosperity ya mikoa ya kusini, na hapo ndipo alipokuja na sera zake kiubaguzi dhidi ya mikoa ya kusini. Let's be honest.

Tunaheshimu mawazo yako, lakini yapo mahali ambapo ni tofauti. Hoja iliyopo mbele yetu ni kuchambua mpango wa mwalimu wa maendeleo.
Tunaomba msianze kuvuruga mada kwa kuingiza hisia, document ipo hapo wazi tuifanyie kazi na si kuanzisha malumbano ya ngano, hadithi au masimulizi ili kutuondoa katika mada. Please, kukaa kimya nako ni sehemu ya kuchangia na kujifunza.
 
Tunamkumbuka Nyerere kwa mengi mazuri aliyoifanyia nchi yetu,hususani msingi wa amani tuliyonayo hadi sasa.Lakini kuna huyu tumemsahau kabisa ktk histori ya nchi yetu.Japokuwa alikuwa mtetezi mkubwa wa wananchi ndani na nje ya bunge.Ndugu Edwadi Moringe sokeine.Ningependa mwenye kuijua historia yakeatuletee hapa javini.
 
Tunaheshimu mawazo yako, lakini yapo mahali ambapo ni tofauti. Hoja iliyopo mbele yetu ni kuchambua mpango wa mwalimu wa maendeleo.
Tunaomba msianze kuvuruga mada kwa kuingiza hisia, document ipo hapo wazi tuifanyie kazi na si kuanzisha malumbano ya ngano, hadithi au masimulizi ili kutuondoa katika mada. Please, kukaa kimya nako ni sehemu ya kuchangia na kujifunza.

mojawapo ya vitu ambavyo utaona wanaogopa kuvifanya wenzetu wanaomchukia Nyerere ni kuangalia ushahidi uliopo mbele yao. Kwa mfano wataleta mambo mengi tu nje ya ushahidi wa wazi ili kukwepa kuuangalia ushahidi huo. Mpango wa kwanza wa maendeleo wa taifa letu tumeuweka hapa ili uangaliwe na kukosolewa na kizazi kipya. So far, karibu kila mtu anayeuangalia leo hii (wengi sidhani kama wamewahi kuuona kabla ya jana) wanakubali kuwa ulikuwa ni mpango mzuri. Siku chache zijazo tutaangalia miaka kumi baada ya Uhuru (yaani baada ya mpango wa kwanza wa maendeleo na ule wa pili wa maendeleo - wa miaka mitano) kulikuwa na mafanikio gani chini ya Nyerere?

Tukiuwaliza huu mpango ulikuwa na makosa gani? Hakuna anayetaka kuangalia wanaleta mambo ya "vijijini n.k) so kama kweli wanataka kuwa wa kweli wakubali kwanza kwamba tuanza na miaka ya mwanzo ya uhuru Nyerere alikuwa sahihi. Tukikubaliana hapo - tukubaliane nao alikuwa sahihi hadi miaka mingapi - so kama alikuwa sahihi hadi 1967.. wakubali hilo kwanza na wampe haki yake. Halafu tutaanza kuangalia the controversial period ya baada ya Azimio la Arusha hadi Vijiji vya Ujamaa (say 1967-1974); na kutoka hapo tutaangalia ngwe ya tatu ambayo ni 1974-1984.
 
Kutoka katika nyaraka:
Health services: Geographical distribution Pg 20-23
Hapa tunaona Hospitali ya Kilwa ilikuwa na uwezo wa kulaza watu 39, yaani chini ya bweni moja la shule. Hospitali ya Mtwara ilikuwa inavuja na hali ni mbaya. Mpango huu wa maendeleo ukatoa kipaumbele. Mtu anayesema maisha ya huko yalikuwa mazuri kabla ya Nyerere sijui kama ameweza kuisoma documet hiyo. Inasikitisha sana

Utaona wilaya kama Muheza, Same, kwasababu huko kulikuwa ima na hospitali nafuu kidogo au za misheni kama zile za Bombo Same, Magila Muheza n.k. hazikutajwa kwa vile mpango mzima ulizingatia vipaumbele katika very limited resources.
Katika Hospitali zote zilizotajwa leo hakuna mtu anayeweza kusema serikali imejenga mpya.

Communication: pg 28-32
Mawasiliano hasa ya barabara yalizingatia ukuzaji wa njia muhimu za uchumi na urahisi wa mawasiliano. Katika barabara zinazowekewa lami leo, zote zilijengwa katika wakati wa Nyerere, I mean foundation work. Hawa viongozi wa sasa wanaweka lami hawajengi kwasababu zilishajengwa.
Hata plan za barabara ni za mpango huo w mwanzo wa Nyerere.
Angalia feeder raod ndipo utagundua kuwa wakati huo tulikuwa navichwa vinavyoijali nchi.

Hydro-electric Pg 48 na 70
Hale imejengwa na Nyerere, iliyokuwepo ni Pangani. Nyumba ya mungu ilikuwa katika plan 1961 na ililenga kuwa ya kutoa umeme na umwagiliaji, kuonyesha umuhimu wa umwagiliaji na sio kufuata mvua za Thailand kama akina EL walivyojaribu kutughilibu.

Field assistants: Ukiriguru and Tengeru
Yaani field assistant ni mtu anayejua kuandika japo jina, fikiria hawa ndio Nyerere alianza nao na vyuo hivyo vilitegemewa kuchukua wanafunzi 180.
Leo tuna graduates maelfu tunashindwa kuwatumia lakini bado yupo kiongozi anasema Nyerere hakumaliza shida zetu na yeye hataweza.
Kwa maneno mengine mtu huyu aliyezungukwa na maprofesa anajifananisha na Nyerere aliyekuwa anafanya kazi na field assistant

Land use training: pg 52 (b) soma uone jurnior land surveyors na field assistant. Field assistant ni mtu aliyemaliza darasa la 4, 7 au 8. Leo tuna maelefu ya wahitimu kutoka Ardhi University, hakuna mpango wowote wa kuwatumia kuleta maendeleo. Bado kuna kiongozi aliyezungukwa na maelfu ya wahitimu anasimama na kusema siwezi kumaliza shida zenu hata Nyerere hakuzimaliza!!!!

Irrigation schemes: pg 71
Mbarali irrigation scheme ilikuwepo tangu mwaka 1958 na Nyerere alikusudia kuipanua ili iongeze tija katika kilimo. Nimeshangaa sana wakati wa Ziara ya PM wa India mwaka huu waziri mkuu Pinda amewashukuru wahindi kwa kuja na kutueleza umuhimu wa irrigation scheme na akasema " Inabidi sasa tujipange" Haaa! hivi Pinda aliyefanya kazi Ikulu hakujua irrigation scheme hadi wahindi waje kumshtua. Hivi PM hana muda wa kupitia nyaraka kama hizi kama sehemu ya kujifunza, kama angeipitia asingesema maneno yale.

Tengeru natural resource school: pg 72
"............additional of lecture rooms, recreation facilities, vert lab etc"
Kwa taarifa maprofesa waliofundisha graduate wengi walikuwa ni zao la Tengeru akiwemo waziri mkuu Sumaye.
Je hii si ushahidi wa kile alichokiacha mwalimu!!!

Ukisoma document utaona kuna sehemu Nyerere na wenzake walikiri kuwa mipango hii ni ya muda mrefu na matokeo yake kwa muda mfupi ni kidogo. Mpaka sasa sijaona mahali penye harufu ya ukabila, udini au chuki dhidi ya watu wa kanda fulani. tuendelee kuichambua ili tupate majibu ya maswali yanayotusumbua kila siku.
 
View attachment 32526

Mojawapo ya hoja ambazo hatuzikii mara nyingi kwa wale ambao wanambebesha Nyerere lawama na mzigo wa taifa letu kuwa ni yeye ndiye aliyelivuruga ni kuwa Nyerere alipokea taifa lenye hali gani ile Disemba 9, 1961. Tunapoelekea miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania bara na hasa baada ya kupitishwa kwa mpango wa "nane" wa maendeleo chini ya serikali ya CCM ni vizuri kurudi nyuma kabisa tuone tulipoanzia.

Wiki iliyopita niliwaletea sehemu tu ya mapokezi ya Rais Nyerere Ikulu ya Marekani wakati huo chini ya Rais J. F. Kennedy. Mkutano wao ulikuwa ni mwaka 1963. Hata hivyo kabla ya hapo viongozi hao wawili walikuwa na mawasiliano ya karibu sana. Kuelekea Uhuru serikali chini ya Nyerere ilikaa na kuandaa mpango wa miaka mitatu (ambao ndio mpango wa kwanza wa maendeleo) wa taifa huru. Mpango huu ulikuwa na mambo mengi na ulikuwa na lengo moja tu nalo ni kujaribu kuleta taifa hilo changa katika karne ya ishirini.

Uzuri wa mpango huu unatupa mwanga wa hali ilikuwaje 1961 katika Tanganyika na mzigo mkubwa ambao Nyerere alibebeshwa na wananchi wenzake. Tunapojaribu kumhukumu leo hii kuwa aliiacha nchi katika "hali mbaya" - kitu ambacho si cha kweli - ni lazima tujaribu kujibu swali pia nchi aliyoipokea ilikuwaje? Changamoto za taifa changa hilo ilikuwaje (wengine wanafikiria hali ilivyokuwa Dar ndivyo ilivyokuwa mikoani). Hivyo kwa kupitia mpango huu utaweza kupata mwanga kidogo wa hali yetu ya kiuchumi ilikuwaje, kijiografia ilikuwaje na raslimali watu ilikuwaje.

Ukishapitia mpango huu swali moja ni LAZIMA ujiulize: Watendaji wa kutekeleza mpango huu walikuwa watoke wapi? Na je walikuwepo?

Wiki ijayo, inshallah tutaangalia nyaraka za CIA kuhusu Nyerere. Yote hii ni katika kuelekea kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika. Please do Enjoy. Kama umepitia mpango "wao" wa maendeleo wa miaka mitano unaweza kulinganisha kitu ambacho naweza kukiita 'motivation' ya mipango hii miwili ni nini. Only then you'll glance (like from a far) the thinking and making of a great leader. Kumbuka hakukuwa na MKUKUTA wala MKURABITA kabla yake.

NB:
1. Nashauri uongeze ukubwa wa PDF wakati unaangalia kwa karibu 700% kuweza kusoma vizuri.
2. Mistari iliyopigwa kwenye kijitabu hiki ni reaction ya serikali ya Marekani walipopitia mpango huu.
Kazi unayoifanya MKJJ ni ya kihistoria hapa,na inaupeleka mtandao huu juu zaidi.
Kwenye hili nina maoni mengi sana tu,however nimeonelea nianze kwa kusema kuwa "Sifungamani na upande wowote" kwenye suala hili.Sababu mojawapo ambayo naamini ni kubwa ni kwamba kuna nchi zimeongozwa na vichaa lakini sasa zina maendeeleo sana kutushinda.Pia nakubaliana kwa kiasi kikubwa sana na Nyambala.Inawezekana matukio ya kiunyanyasaji pamoja na kuuwawa kwa wale ma anti ubepari kipindi cha nyuma kulimfanya achukue hatua za tofauti kama vile kufuata mfumo wa ujamaa nk.

Mwalimu alifanya mengi mema,na kuna matokeo mengine yalikuwa mabaya.Hilo liko wazi na ushahidi ni ufisadi,kutokuwajibishana na umasikini tulionao....However i will always love mwalimu kwasababu nia yake ilikuwa njema kwa Taifa na amekufa masikini bila kujirundikia mali za watanzania.

However,ni lazima tuelewe pia nafasi aliyokuwa nayo ya kutu andalia viongozi bora na si wa ndiyo mzee peke yake kwasababu hao ndo walimwangusha.

Mfumo huo wengi wanaamini kuwa ulitokana na lack of expertise tuliyokuwa nayo baada ya uhuru.Hilo wakoloni hawakulifanya kwa bahati mbaya.Hili lilimtatiza mwalimu na ndio maana watumishi wengi wa serikali walipofanya mabaya walihamishiwa sehemu nyingine badala ya kuwa fired ama kuwa accountable.Hilo nalo limerithiwa kwa sababu tunaona wanachofanyiwa mafisadi.Ule udugu wa kuvumiliana hata tukiharibu na kufuja mali za Taifa ume tucost dearly.

Mwalimu alisema walikuwa wakali na aliwatandika viboko.Hata hivyo alitakiwa ajue kuwa nchi itaongozwa kwa msaada wa watanzania wengine pia na si individual.He said that he had power and we didnt have nothing to do with him,yani alijuwa katiba ilimpa nguvu sana.Sasa mwalimu pia alitakiwa aelewe tofauti kati ya katiba ya mkoloni na katiba ya mpata uhuru.
Kwasasa naishia hapa mkuu coz mambo ni mengi.Ntarudi hapa nikipata nafasi.
 
Kwenye ukurasa wa 9 inapozungumzia suala la "Finance" kuna kauli ambayo kwa mchumi yeyote au hata aliyepitia kwa juu juu ina uzito mkubwa sana. Mpango unasema hivi:

The world bank has pointed out that financial stringency and budgetary limitations will be determining factors in any planning for the future. These budgetary limitation are due to the very small taxable capacity of Tanganyika's low-income economy.

Hii ina maana gani? Ina maana ya kwamba kwa miaka 40 ambayo wakoloni walikuwa wanaendesha uchumi wa Tanzania hawakutengeneza uchumi ambao ni sustainable enough kuweza kujiendesha wenyewe. Sehemu ya uchumi iliyolipa kodi ilikuwa ni ndogo sana. Kwa maneno mengine mafanikio yoyote ya maendeleo wakati ule yangetegemea sana kile kinachoitwa kama "tax base" yaani sehemu ya uchumi inayotozwa kodi (iwe ni watu, au sekta fulani).

Mpango huu pia kwenye sehemu hiyo hiyo unatuonesha kuwa Nyerere mwenyewe kama mchumi - tukumbuke kasoma uchumi - anatoa somo la msingi sana kwa mchumi wowote - unatumia kulingana na mapato yako. Mpango unasema hivi:

The size of recurrent expenditure (matumizi ya kawaida-MM) which is limited by recurrent revenue , i.e by the amount of money that Government collects each year in various taxes places in turn a limit on the size of development expenditure.

kwa maneno mengine, mapato ya kawaida tunayoyapata kutoka katika kodi mbalimbali yanatumika zaidi kugharimia matumizi ya kawaida ya serikali (mishahara, malipo mbalimbali ya kuendeleza vilivyopo n.k) kabla ya kiasi kinachobakia kwenda kwenye matumizi mapya -yaani ya maendeleo. Kama tax base yako ni kidogo na kama matumizi uliyonayo tayari ni makubwa, ni wazi kuwa ni fedha kidogo sana ya kodi yako itakayoenda kwenye maendeleo. Hili haliitaji shahada ya kwanza ya uchumi toka UDSM kuweza kulielewa. Mtu yeyote aliyejifunza classical economy - lile likitabu fulani likubwa hivi - anaweza kuelewa siku ya kwanza darasani.

Na kutoka hapo mpango unaeleza kitu kingine cha wazi sana, kwamba hata ukiingiza fedha kwenye mpango fulani wa maendeleo kwa mfano kujenga hospitali au shule, mpango ule ukikamilika unageuka kuwa ni mpango wa kudumu na hivyo utatakiwa uingizwe kwenye bajeti ya matumizi ya kawaida; kwa maneno mengine, mipango ya maendeleo inazidi kubebesha mzigo katika bajeti ya kawaida ya matumizi kila mwaka.

For example, capital expenditure on hospitals and schools provided for in development plan will generate after their completion recurrent expenditure on staff, nurses, and doctors and on teachers and students respectively. Such a recurrent expenditure has to be accommodated in recurrent budgets long after its origin - the building of hospitals and schools has been completed.

Ni kutokana na ukweli huo ilionekana wazi kuwa uchumi wetu usingeweza kukuwa kwa zaidi ya asilimia 5 kwa mwaka. Siyo maoni ya Nyerere hayo bali ya Benki ya Dunia ambao walishiriki sana katika kuandaa mpango huu. Leo hii watu wanazungumzia kukua kwa asilimia 7 kama lengo! Wakati wana tax base kubwa zaidi, wasomi wengi zaidi, na sababu nyingi zaidi za kufanya vizuri.

Kutokana na uelewa huu mpango wa maendeleo unasema hivi (Uk.12):

The total increast of some 3-4M poundsin recurrent expenditure will no doubt represent a heavy burden on Tanganyika's budget. It is thie recurrent commitment which limits the size of the Development Plan itself and within the Plan restricts the development of those services that give rise to particularly heavy recurrent expenditure such as Education and Medical services. These two services alone account for more than half of the total increase in recurrent expenditure arising from the plan.

Sasa hapa hatuna budi kuwauliza wale wanaomkosa Nyerere, what is wrong with reasoning background of this plan? Kauli hizo zina uongo gani wa kiuchumi. Watu wanasema Nyerere angeweza kujenga mashule mengi na mahospitali bwelele kila kijiji labda na kila mji tena ya kisasa kabisa.. well.. angetoa wapi hela? Angechagua nini? Kati ya shule mpya na barabara mpya au hospitali mpya serikali ya mwanzo ingechagua nini hasa kama bajeti yake iko limited hivyo?

Kama hawa wakosoaji wangekuwa na ukweli huo wao wangechagua kufanya nini?

Sasa juzi wamepitisha mpango wao wa maendeleo; angalia mgawanyo wa jumla wa mpango wa Nyerere (Uk. 13) :

Asilimia 60 ya fedha zote zilizokuwa zinaombwa kwa ajili ya mpango huu ilikuwa ni kwa ajili ya maendeleo
Asilimia 20 Huduma za jamii
Asilimia 20 kwenda Jeshi, Polisi, Mambo ya Nje, Majengo ya serikali na mengineyo.


Je katika bajeti ya mwaka huu peke yake asilimia ngapi inapelekwa kwenye maendeleo kulinganisha na fedha zinazoenda kuhudumia matumizi ya kawaida?

Kuhusu suala la barabara Nyerere na mpango wa serikali yake wanatuonesha walivyokuwa wanaona mbali!

The Mission's view that the main trunk road system is virtually complete is not accepted by the Government. The present main road system looks outwards, particularly in the noth and facilititaes the flow of purchasing power from the rich provinces in teh north to Kenya and Uganda rather than inwards to Tanganyika. Also, there is no direct road connecting the prosperous Lake and West Lake provinces (Mwanza, Kigoma, Shinyanga of the time- MM) with the Northern Province and with Tanganyika searports so that the main flow of imports and exports has to make a detour via kenya and Uganda. Similarly, there is no convenient link with teh potentially rich Southern Highlands and the Kilombero valley.


The government's view is that the new main road system should connect the areas of agricultural and mineral production (taking into sonderation their future potential) with the main outlets in Tanganyika. Also, there is little point in starting an ambitious feeder roads programme if there are no railheads and main roads to feed to. However, the Government accepts the Mission's view, that gradually the emphasis should shift to feeder roads and this factor will be taken into consideration in the next plan.

Ndugu zangu, hii ndio reasoning ya great leader. Hakuitaji kuuma maneno bali kuita vitu jinsi villivyo. Kuna watu wanataka tuamini kuwa wakoloni walitutandikia barabara kila kona ya nchi na Nyerere akaja akaziharibu; wanataka tuamini kuwa mtu uliweza kutoka Tanga hadi Mahenge au Ilula hadi Magu kwenye barabara za lami! Wanataka tuamini kuwa ilikuwa rahisi kutoka Ifakara kwenda Morogoro mjini kwenye barabara za kuvutia zilizoachwa na wakoloni. Ukweli uko wazi kwa Mtanzania mwenye fikra huru kuamua; yule ambaye yuko tayari kufungua macho yake baada ya kupewa hiki kidonge kama alichopewa Neo kwenye "The Matrix".

Ili kuweza kutoa hukumu ya haki ya uongozi wa Nyerere ni lazima kwanza mtu afungue hisia zake, kukataa aliyoimbishwa na watu wengine na kwa macho meupe asome yeye mwenyewe kama mwanadamu mwenye fikra huru na kuanza kuangalia ushahidi ulioko mbele yake. Ni katika kufanya hivyo tu mtu ataanza kujenga ile balance ya kweli na siyo extremes view za "uovu, ubaya" wa Nyerere ambazo zinamuondoa Nyerere kutoka katika context of historical paradigm of which he was part of.
 
Ndiyo; na nilikuwa wa kwanza kuiweka hapa JF. Ni miongoni mwa mipango mibovu kabisa iliyowahi kubuniwa na watu wenye akili timamu. Ukiisoma huu mpango wa kwanza na mpango huu wa nane utaona tofautii ya vinavyodhaniwa ni kama usiku na mchana.

Kuna rafiki yangu mmoja wa karibu (kipindi chetu cha uvulana) alitokea kuwandikia barua ya kumtaka kimapenzi binti ambaye kwa bahati naye alikuwa rafiki yangu/

Ile barua ilipomfikia yule binti ikamkasirisha kwa mambo mengi sana, alichofanya yule binti akaniita na kuanza kunisomea ile barua.

Barua ilianzwa kusoma....wakati anaendela nikayaona makosa ya 'kiufundi' nikahisi kuona aibu mimi....baadaye nikaanza kuumia jinsi ninavyosikiliza utumbo alioumwaga. Baada ya kufika mwisho, nikamshauri yule binti kwa heshima yangu aichane ile barua.....aibu ya yule jamaa ilikuwa kama vile yangu ...ikanivaa ikanikamata

Nimekuuliza swali la kizushi...najua ulisoma kwani fani yako inakuruhusu kusoma kila kitu

Ila jibu lako la NDIYO...linaendana na swali lingine LA KIZUSHI kutoka kwangu

KWANI ULITEGEMEA NINI KWENYE HUU MPANGO WA KIKWETE???

Huwa sisomi kabisa vitu vinavyonajisi ubongo wangu!! pole kaka, yaani aibu ingenishika kama barua ya yule rafiki yangu kipenzi
 
Kuna rafiki yangu mmoja wa karibu (kipindi chetu cha uvulana) alitokea kuwandikia barua ya kumtaka kimapenzi binti ambaye kwa bahati naye alikuwa rafiki yangu/

Ile barua ilipomfikia yule binti ikamkasirisha kwa mambo mengi sana, alichofanya yule binti akaniita na kuanza kunisomea ile barua.

Barua ilianzwa kusoma....wakati anaendela nikayaona makosa ya 'kiufundi' nikahisi kuona aibu mimi....baadaye nikaanza kuumia jinsi ninavyosikiliza utumbo alioumwaga. Baada ya kufika mwisho, nikamshauri yule binti kwa heshima yangu aichane ile barua.....aibu ya yule jamaa ilikuwa kama vile yangu ...ikanivaa ikanikamata

Nimekuuliza swali la kizushi...najua ulisoma kwani fani yako inakuruhusu kusoma kila kitu

Ila jibu lako la NDIYO...linaendana na swali lingine LA KIZUSHI kutoka kwangu

KWANI ULITEGEMEA NINI KWENYE HUU MPANGO WA KIKWETE???

Huwa sisomi kabisa vitu vinavyonajisi ubongo wangu!! pole kaka, yaani aibu ingenishika kama barua ya yule rafiki yangu kipenzi

hahahah nimecheka sana; ila ukweli ni kwamba sikutarajia lolote jema zaidi ya kile kilichokuwemo. Kwa vile kuna watu wazima na akili zao walijitokeza kuupigia debe mpango huu wa kina Kikwete nililazimika japo kuupitia kwa mbali tu kuangalia kama ni kweli unastahili sifa hizo. Kweli ningejua mapema nisingeusoma. Lakini kama nisingeusoma nisingekuwa na uwezo wala haki ya kuukosoa.
 
Nyamba usiwe na shaka, siku chache zinavyokwenda nitaweka hata barua za mawasiliano kati ya Kennedy na Nyerere.. nadhani unachosema kina ukweli sana.

This is not entirely true, Oscar Kambona advised Mwalimu not go through the Ujamaa route but he refused and undermined Mr Kambona..
 
This is not entirely true, Oscar Kambona advised Mwalimu not go through the Ujamaa route but he refused and undermined Mr Kambona..

Ujamaaa route haikuwa idea mbaya . Sasa hivi inakosolewa sababu kuna matatizo fulani fulani yalitokwa . Na ha hata idea hiyo ya kambonaingefuatwa watoto wengi wa wakulima leo wasingeweza hata kufika dar wala kusoma CHUO Kikuu.

Kwenye ujaa kuna watu walikuwa ni koo za maskini wamekuwa matajiri au familia za kawaida. Hyo routte ya kambaa ni wachache wangeweza kubadili maisha yao.

So usidhani kushidwa kw aidea ya mwalimu kuna justify kwamba Idea ya kambona ingefanikiwa. No. Kwa miaka ile mazingira yale Idea ya Nyerere ilikuwa ndo sahihi.
 
Shamu,
Mkuu wangu kidogo natofautiana nawe pale unaposema Nyerere ali fail wakati unashindwa kabisa kutuhusisha sisi wenyewe na failure ile. Na hatuwezi kuendelea ku fail ikiwa sababu zote tunazoamini zilifanya Nyerere afail tumeziondoa lakini bado tunashuka chini..
Kuwepo kwa sabau na sukari ya modification ambazo zimejaa madwa haina maana ndio manendeleo ikiwa maradhi yanazidi na watu wanakufa haraka kuliko wakati wowote ule. Hata ukoma umerudi tena kwa sana tu natunashindwa hata kuutibu.

Hivyo, sielewi kipimo cha failure ikiwa mimi naamini kabisa kwamba hata hao ma economist wanaoaminika duniani ni zuga tu. Hakuna statistics za kiuchumi ambazo zina ukweli ktk utabiri wake. hakuna hata siku moja wachumi wanaweza kusema kwa uhakika uchumi wa Tanzania au hata Marekani mwaka kesho, utakuwa kwa kiasi gani mara zote huwa wanakosea kwa sababu mafanikio sio swala la kujumlisha na kutoa.

Ila tunaposoma malengo kama haya ni jukumu letu kuyafanyia kazi na labda nikukumbushe tu kwamba kabla ya vita ya Uganda unajua kwamba uchumi wa tanzania uliwahi kukua hadi asilimi 10, a record ambayo haijawahi kutokea tena!.

Sasa iweje leo tuseme Nyerere hakufanikiwa wakati kaweza kuongoza hadi kaondoka kakabidhi urithi na chama chake CCM bado kinatawala!. Jambo ambalo ni adimu sana ktk tawala za kidunia hasa baada ya utandawazi. Na labda nikwambie tu kwamba hata huyo Kennedy wenyewe Wamarekani wanamwona he was a failure kiuchumi na wengine kumwita Socialist! inategemea wewe unamtazama vipi kiongozi na maendeleo gani unayozungumzia lakini kwa kifupi Nyerere alifanikiwa kwa mengi alotaka kuyafanya iwe mabaya kwako ama kwa mazuri kwa wengine lakini he did it! List ya mengi aloyafanya unaiona hapo juu! Wee nipe ya Mkapa, Mwinyi au JK kama yatajaa hata mkononi!
 
Mikoa ya Kusini WTZ wengi walikuwa wanaishi vijijini kabla ya hata Nyerere kuzaliwa. Nenda ukaone miji kama Rufiji, Kivinje, nk na vijiji karibu yake, vilikuwepo kable ya Nyerere. Mikoa ya Kusini kuna majumba ambayo yapo vijijini yalijengwa tangu miaka ya 1400 na watu walikuwa wanaishi kwa kutumia njia nyingi, kabla Dictator Nyerere kuzaliwa. Maisha ya vijijjini ya Mikoa ya kusini yalikuwa mazuri sana kulinganisha na mikoa mingine. Nyerere na sera zake za Ujamaa alianza kuchukia prosperity ya mikoa ya kusini, na hapo ndipo alipokuja na sera zake kiubaguzi dhidi ya mikoa ya kusini. Let's be honest.

Du hii historia mpya au?!, Mkuu labda utueleweshe ni kipi hasa kilivurugwa au kuporwa kutoka mikoa ya kusini na sera za ujamaa?
 
Ndio maana tunapochangia humu utawezas kuwajua watoto wa juzi juzi kutokana na maneno yao. Nakupongeza kwa kukiri hilo hio wazi wazi.

Mkuu unaweza kufafanua kuhusu the "benchmark ya watoto wa juzi juzi, jana jana au leo leo?" Vipi kuhusu watanzania na watoto wao waliokuwa wakiishi nje ya nchi miaka hiyo ya mwanzoni mwa sabini nao wanahesabika ni wa juzi juzi simply kwa sababu hawakuona in first hand some of the development projects in those early beginnings? Just for your information, There were so many people of Mbeya origins in Malawi, Rhodesia and as far as South Africa before independence and after. Likewise so many Tanganyikans of Kilimanjaro origins in Kenya also Tanganyikans from Kagera and around who resided in Uganda.
 
Shamu,
Mkuu wangu kidogo natofautiana nawe pale unaposema Nyerere ali fail wakati unashindwa kabisa kutuhusisha sisi wenyewe na failure ile. Na hatuwezi kuendelea ku fail ikiwa sababu zote tunazoamini zilifanya Nyerere afail tumeziondoa lakini bado tunashuka chini..
Kuwepo kwa sabau na sukari ya modification ambazo zimejaa madwa haina maana ndio manendeleo ikiwa maradhi yanazidi na watu wanakufa haraka kuliko wakati wowote ule. Hata ukoma umerudi tena kwa sana tu natunashindwa hata kuutibu.

Hivyo, sielewi kipimo cha failure ikiwa mimi naamini kabisa kwamba hata hao ma economist wanaoaminika duniani ni zuga tu. Hakuna statistics za kiuchumi ambazo zina ukweli ktk utabiri wake. hakuna hata siku moja wachumi wanaweza kusema kwa uhakika uchumi wa Tanzania au hata Marekani mwaka kesho, utakuwa kwa kiasi gani mara zote huwa wanakosea kwa sababu mafanikio sio swala la kujumlisha na kutoa.

Ila tunaposoma malengo kama haya ni jukumu letu kuyafanyia kazi na labda nikukumbushe tu kwamba kabla ya vita ya Uganda unajua kwamba uchumi wa tanzania uliwahi kukua hadi asilimi 10, a record ambayo haijawahi kutokea tena!.

Sasa iweje leo tuseme Nyerere hakufanikiwa wakati kaweza kuongoza hadi kaondoka kakabidhi urithi na chama chake CCM bado kinatawala!. Jambo ambalo ni adimu sana ktk tawala za kidunia hasa baada ya utandawazi. Na labda nikwambie tu kwamba hata huyo Kennedy wenyewe Wamarekani wanamwona he was a failure kiuchumi na wengine kumwita Socialist! inategemea wewe unamtazama vipi kiongozi na maendeleo gani unayozungumzia lakini kwa kifupi Nyerere alifanikiwa kwa mengi alotaka kuyafanya iwe mabaya kwako ama kwa mazuri kwa wengine lakini he did it! List ya mengi aloyafanya unaiona hapo juu! Wee nipe ya Mkapa, Mwinyi au JK kama yatajaa hata mkononi!


Hapo ndipo linapokuja suala muhimu la uongozi. CCM inatawala mpaka sasa hivi kwa sababu gani? Jibu Nyerere, ok. Sasa unaona kwamba Nyerere alifanya makosa ktk uongozi kwa wananchi. Nchi sasa hivi inaongozwa na Elite (vigogo) wachache ambao wanabadilishana madaraka kupitia system hiyo iliyoanzishwa na Nyerere (CCM). Makosa ya Nyerere ni kuwanyima haki ya msingi Wananchi wa TZ ambao wengi wao ni maskini. Kama Nyerere angewapa WTZ elimu, knowledge ktk mambo ya research & development, economic prosperity tusingekuwa tulipo sasa hivi.

Alichotuachia Nyerere ni system ya Elite (Vigogo) CCM ambao hawatoweza kutoka madarakani kwa muda mrefu. Tunapoangalia quality za good leader lazima tujue kwamba anafuata misingi ya sheria, heshimu haki za binadamu, maadili mema kwa wananchi wake, Nyerere kafeli ktk hilo.
 
Tunaheshimu mawazo yako, lakini yapo mahali ambapo ni tofauti. Hoja iliyopo mbele yetu ni kuchambua mpango wa mwalimu wa maendeleo.
Tunaomba msianze kuvuruga mada kwa kuingiza hisia, document ipo hapo wazi tuifanyie kazi na si kuanzisha malumbano ya ngano, hadithi au masimulizi ili kutuondoa katika mada. Please, kukaa kimya nako ni sehemu ya kuchangia na kujifunza.


Ni nonesense kustudy plan ya documents ya nchi wakati wa Nyerere, wakati matokeo yake tushaona. Muhimu ni kustudy Result ambazo zimesababishwa na hiyo plan ya Nyerere. My opinion.
 
Alichotuachia Nyerere ni system ya Elite (Vigogo) CCM ambao hawatoweza kutoka madarakani kwa muda mrefu. Tunapoangalia quality za good leader lazima tujue kwamba anafuata misingi ya sheria, heshimu haki za binadamu, maadili mema kwa wananchi wake, Nyerere kafeli ktk hilo.

Ni sheria gani Nyerere alizivunja nipe mfano mmoja tu kuwa "kulikuwa na Sheria hii, na Nyerere aliivunja hivi au vile.
 
mojawapo ya vitu ambavyo utaona wanaogopa kuvifanya wenzetu wanaomchukia Nyerere ni kuangalia ushahidi uliopo mbele yao. Kwa mfano wataleta mambo mengi tu nje ya ushahidi wa wazi ili kukwepa kuuangalia ushahidi huo. Mpango wa kwanza wa maendeleo wa taifa letu tumeuweka hapa ili uangaliwe na kukosolewa na kizazi kipya. So far, karibu kila mtu anayeuangalia leo hii (wengi sidhani kama wamewahi kuuona kabla ya jana) wanakubali kuwa ulikuwa ni mpango mzuri. Siku chache zijazo tutaangalia miaka kumi baada ya Uhuru (yaani baada ya mpango wa kwanza wa maendeleo na ule wa pili wa maendeleo - wa miaka mitano) kulikuwa na mafanikio gani chini ya Nyerere?

Tukiuwaliza huu mpango ulikuwa na makosa gani? Hakuna anayetaka kuangalia wanaleta mambo ya "vijijini n.k) so kama kweli wanataka kuwa wa kweli wakubali kwanza kwamba tuanza na miaka ya mwanzo ya uhuru Nyerere alikuwa sahihi. Tukikubaliana hapo - tukubaliane nao alikuwa sahihi hadi miaka mingapi - so kama alikuwa sahihi hadi 1967.. wakubali hilo kwanza na wampe haki yake. Halafu tutaanza kuangalia the controversial period ya baada ya Azimio la Arusha hadi Vijiji vya Ujamaa (say 1967-1974); na kutoka hapo tutaangalia ngwe ya tatu ambayo ni 1974-1984.

Unajua siasa, Wanasiasa wote wanakuwa na plan nzuri za miundo mbinu. Tatizo linakuja kwenye utekelezaji. Hapo ndipo utakapoona viongozi wetu especially in Africa si watekelezaji akiwemo Nyerere.

Kama unataka kumjaji Nyerere kwa nyakati, sawa. Lakini, I hope conclusion yako itakuwa, Nyerere alishindwa kuliondoa taifa ktk ujinga, umskini uliopita mipaka.
 
However i will always love mwalimu kwasababu nia yake ilikuwa njema kwa Taifa na amekufa masikini bila kujirundikia mali za watanzania.
Hiki ndicho haswaa kinachomtofautisha mwalimu na viongozi wa leo, na pia hiyo nia yake njema haikuwa compromised na ufisadi wa aina yeyote ile, fisadi wala mtoto wa fisadi. Sasa as of today utasemaje una nia njema na taifa halafu marafiki zako wa karibu ni Rostam, EL na Chenge?
 
Are you sure; ushauri huu ulitolewa wapi?

Mzee Mwanakijiji, here is an excerp I have taken from wikipedia on Oscar Kabmona, Oscar Kambona - Wikipedia, the free encyclopedia. Kambona advised him to test the ' Ujamaa ' system in a small scale but Mwalimu refused and the results are evident today?..


" After Nyerere came out of seclusion, he publicly thanked Oscar Kambona, whom he called "my colleague," for defusing a potentially dangerous situation.
In fact, when the soldiers remained defiant, it was Oscar Kambona who persuaded Nyerere to seek immediate assistance from the former colonial power, Britain, to suppress the mutiny.
The two leaders had been close political allies and personal friends since the days of the independence struggle when they were the main leaders of the independence movement. In fact, when Kambona got married to a former Miss Tanganyika at a cathedral in London, Nyerere was his best man.
But the two leaders started drifting apart a few years after independence. The first rift occurred in 1964 during the army mutiny, and then in 1965 when Tanzania officially became a one-party state.
As a cabinet member, Oscar Kambona supported the transition to a one-party state but did so reluctantly, only as a team player.
He was opposed to the change because he said there was no mechanism guaranteeing change of government by constitutional means in a country dominated by one party. He also contended that there were no constitutional safeguards to make sure that the country did not drift into dictatorship.
The next split with Nyerere came in February 1967 when Tanzania adopted the Arusha Declaration, an economic and political blueprint for the transformation of Tanzania into a socialist state.
Kambona was opposed to this fundamental change and argued that the government should first launch a pilot scheme to see if the policy was going to work on a national scale......."
 
Back
Top Bottom