James Mbatia: CHADEMA wamenifanyia fujo kwenye chama changu na jimboni kwangu wakati wote tupo UKAWA, ulisikia nalalamika?

Nyimbo zenu sasa ni zilipendwa
 
Asubiri moto atakao pelekewa mwaka huu. Hata akisaidiwa na CCM
Vunjo sio maboya
 
Hizo ndizo kauli za kiume na kiungwana

Na ndiyo maana nasema viongozi wa CDM na wafuasi wao hupenda sana kudeka na kuonewa huruma hata wanapopaswa wao kutafuta ugali utasikia sisi kazi yetu kuandaa Meza na maji ya kunawa!
 
Sio kwa kura, bali matumizi mabaya ya madaraka. Tunaoikubali cdm tupo wa kutosha, na hatudanganyiki. Ile 1.5t mpaka leo bado inatuuma.
Ni kawaida boss, kuna wakati nguvu inatumika ili kuondoa watu au mfumo mbovu. Nchi haiwezi kwenda kwa kutegemea kura za wapuuzi wanaompigia mpuuzi mwenzao.
 
Ni kawaida boss, kuna wakati nguvu inatumika ili kuondoa watu au mfumo mbovu. Nchi haiwezi kwenda kwa kutegemea kura za wapuuzi wanaompigia mpuuzi mwenzao.

Tunaposema kuwa huwa mnategemea nguvu kukaa madarakani, inakuwaje mishipa ya shingo inawatoka kwa kulazimisha kuwa mnakubalika?
 
CHADEMA tabia zao kama watoto wa mwisho wanapenda kuonekana wao wapo sawa kwa kila kitu na hawataki kujishusha walisahau kuwa NCCR na CUF viliwahi kuwa vyama vikuu vya upinzani kosa lao walipokuwa chama kikuu cha upinzani walikosa mikakati ya kufanya bado wawe juu
 
Huyu mbunge wangu lakini acha tuu, hakuna la maana amefanya, kwa sehemu ya jimbo langu labda huko kwengine, kule bara bara ya kwenda kahe night mbovu toka miaka ya huko mbali sana na kule tunafanya kilimo haswa lakini sijawahi sikia jamaa hata Akiongelea hili jambo bungeni ili hata tupate barabara ya kuchonga tuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili ndio jibu la ulichouliza kutoka kwa Mbatia.

"Ni haki yao na ni haki ya chama kilicho sajiliwa kina haki ya kufanya kazi mahali popote pale."

Hakuongea kipindi hicho kwa sababu ilikuwa ni haki yao na hivyo hakuwaona kuwa wamenunuliwa na ccm.
 
Huyu anatakiwa aonyeshwe kwamba Vunjo sio mapandikizi.. Haja fanya kitu popote sio Kahe tuu.
Kama ni kurudi bungeni arudishwe kwa viti vya wavaa sketi. Sio kwa sanduku la kura..
 
yaani sio fair kabisa
Huyo Mbatia anajushuku tu. Anatakiwa afanye kazi aliyotumwa na ccm kwa ufanisi, vinginevyo arudishe hela.
Noma sana. Kuna wapinzani hawataki wapinzani wenzao wafanye siasa za upinzani. Nadhani mwenye nguvu na mbinu apite tu.
Mbati usalama wake upo kwenye kusapot CHADEMA tu kinyume na hapo asifike kabisa Moshi.
 
Anachosema wasubiri nao dawa iwaingie
 
Nina maswali 2 ya kuuliza hapa.

1. Hiyo sare ya NCCR haisadifu kuwa wao ni CCM B ? Maana tofauti yao na CCM A ni rangi za juu (mashati/t-shirts); Wao wana blue,Lumumba wana green au yellow. Ila chini sare sare maua.

2. Kwanini Mbatia anapoongea huwa anabetua mdomo? Wanaume huwa tunaongea vile kweli?
 
Hivi mtu ni bidhaa anaibwa tu?

Yaani mtu mwenye akili hadi kashawishi watu elfu wakampa kura leo anaibwa inakuaje? Fafanua mkuu
 
Chadema.hawajawahi kuwa serious

Ukawa walikubaliana Mtatiro agombee Segerea, dakika za mwisho chadema. Wakabadili gia angani wakamteua Anatropia nae kugombea ubunge Segerea, kura zikagawanyika, CCM ikashinda
 
Vyama vyote vilivyopo TZ ni vyama vya upinzani wanapinzana ili watanzania wote tupate maendeleo ya kweli...

Sasa elimu ni muhimu sana Sisi wote bado hatujapaa elimu ya kutosha kutafsiri maana ya upinzani

Make mkijua ccm pia ni chama cha upinzani watanzania amkeni kuipenda nchi yenu sio vyamaa...mtu yeyote mwenye uwezo wa kuongoza maliasili zetu inabidi awe kiongozii tu sio kusemezana maneno ya kijingaa jingaa

Pia hakuna chama chenye madaraka juu ya vyama vingine...sema kwasababu ya njaa zetu acha tu tupelekane wote hawa watakufaaa tanzania ya kweli itabak kwa vjana kwaiyo vijana someni na muelewe mengii kuhusu kuongoza maliasili za nchi
 
Tunaposema kuwa huwa mnategemea nguvu kukaa madarakani, inakuwaje mishipa ya shingo inawatoka kwa kulazimisha kuwa mnakubalika?
Inua ubora wa Upinzani, basi! Huwezi kuruhusu kila mjinga aliye na wafuasi atake kutawala nchi. Never!
 
Inua ubora wa Upinzani, basi! Huwezi kuruhusu kila mjinga aliye na wafuasi atake kutawala nchi. Never!

Tuinue ubora wa upinzani kwa vigezo vya kiccm!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…