JamiiForums ina mambo

JamiiForums ina mambo

Mleta mada nilishakuambia. Kwenye mitandao ya kijamii, "unaweza kuwa mtu yeyote tu unayetaka kuwa". Unaweza kuwa:
1. Mwenye hekima
2. Mpumbavu
3. Tajiri
4. Masikini
5. Mgonjwa
6. Mzima
7. Mtakatifu (sana)
8. Mdhambi (sana)
Kwa hiyo endelea tu kuchukuliana nayo mkuu.
 
Namaanisha Kama wengi duniani wanavyotumia google kupata majibu ya kile wanachokitaka pia baadhi ya watanzania wanaitumia jf kupata solution kwa matatizo yao.
Sio ukiitaka JF lazima Ugoogle?

Uzuri ni kuwa ukisearch kitu google kwa lugha ya Kiswahili basi unaletewa kwanza machaguo kutoka Jamiiforums.
N
 
Hiyo #1 kwamba watu wanakomenti kufuata alichokoment mtu wa kwanza sikubaliani nalo hasa ila ila hiyo ya like ni kweli kabisa,ukifungua thread hesabu post nane au kumi za mwanzo hata kama hazi-make sense basi utakutana na like balaa ila baada ya hizo ukisogea sogea hadi #20 hata kama zipo zilizojaa elimu na weledi unakuta zina like 1/2.ila hayo mengine yote mkuu screpa yupo sahihi.
 
Kwa miaka kadhaa ambayo nimekuwa member wa JF nimeweza kuexperience mambo yafuatayo;-

1. Anacho komenti mtu wa kwanza kwenye post maranyingi huwa ndio msimamo wa wengine wanaofatia kukomenti ( yaani wengi ni wafata upepo). Wakwanza kukomenti akikuponda na wengine watakuponda, wakisifia na wengine watasifia.

2. Unaweza ukatukanana na mtu kwenye thread hii then mda huohuo ukamgongea like kwenye thread nyingine na kummwagia sifa kibao.

3. Kwavile tunatumia Fake ID's, si ajabu ukajikuta unabishana na bosi wako na kumvimbia kwamba unahela sana na unauwezo hata wa kuajiri ukoo wao mzima, pia unaweza ukamuita babaako 'dogo' au 'boya' bila kujua.

4. Ukienda kwenye jukwaa la Vyombo vya usafiri unaweza fikiri kila mwana JF anamiliki gari, tena gari kali. Maana ukiulizia VITZ unaambiwa uwe mvumilivu uendelee kujikusanya ununue 'GARI', na uachane na vi'baby-walker'.

5. Ukienda MMU Wanaume wote wanajifanya 'MANDINGO', hakuna anayekubali kwamba yeye kibamia, na akianza kupiga gemu goli 1 ni kuanzia dakika 30, hakuna anayemaliza kwa dakika 5. Hilo ni kwa upande wa wanaume, kwa wanawake wao kila mmoja ni 'MNATO', hakuna Mtera kule.

6. Ukienda kule jukwaa mama 'SIASANI' yaani ndio vurugu tupu, kila mtu anajiona jiniazi na ndio maana ni jukwaa linaloongoza kwa povu. Utasikia "hizo hoja zako za kitotototo peleka kwa watoto wenzio facebook".

7. Watumiaji wa JF wanadhani kila mtu yuko Dar. Hata wanapoweka matangazo yao unaona kabisa akilini mwao wanajua kila mtu anaishi Dar.

8......
9......
10......

Mengine ongeza wewe...
Ndio nini? In Joti's voice.
 
Baada ya kugundua mtu fulani ndugu yangu naye ni member wa Jf huwa namtoa povu kila anacho post kwa kumwambia vitu kwa kujifanya kukisia kumbe ndo ukweli wenyewe ..utakuta namwambia "inaonekana hata elimu yako ni ya kuunga unga kutokana na kufeli". basi atavimba kwa kujidai "bwana mdogo......... " .
Kwahiyo JF wengi wanatoana mapovu kwa makusidi kabisa.
 
Unaweza kukuta ni rafiki yako, mnaongea vizuri, mnajuliana hali n.k lkn JF mna bifu mnatukana matusi makubwa makubwa ya nguon huku mkiwahusisha baadhi ya ndugu zenu.
Lkn upande wa pili utakuta jana tu umehudhuria happybirthday ya mwanae na zawad umetoa
 
Back
Top Bottom