JamiiForums ina mambo

JamiiForums ina mambo

Ukiweka bandiko unalalamika kutapeliwa elfu 10 au 50 kila mmoja anakuona kamaskin sana kasiko na mbele wala nyuma ila mishahara ikitoka na makato juu hata yawe elfu nne zitaanzishwa threads mia kidogo, bandiko litajaa malalamiko na kejeli kwa serikali(kuwatapeli hela zao)
Ha ha ha ha hatarr tupu.
 
10.Wengine hawajuagi hata kah mishahara imetoka au inatoka lini,ila akiingia JF anakuta watu wanasema mi mshahara nimeshakula au umetoka zamaniii.kumbe wengne wanasema mishahara ya jobs ambazo sio official.....mtu anajilipa mwenyew.
 
JF hatari.....
...
Kuna kipindi nilikuwa nje.. Nikawa natafuta namba ya headmaster wangu wa Galanosi.
Alikuwa ameshahama shule kitambo.
Nikaweka thread hapa..
Nilipata namba yake zaidi ya watu kumi tofauti na nikapewa details za kuhusu yeye kuliko hata nilivyokuwa sitarajii..
JF usiichezee hata mkeo yuko hapa akikuta uzi unaokuhusu anatapikaaa
Vijana wanasema ''JF sio poa''... Hahahah
 
jf bn kila mtu kasoma chuo ila haijalish cha upish au vp
 
Subiria majibu ya mwendokasi yatakayokuachanisha taya...Kuna watu wana majibu ya kushangaza mno humu ndani! Bingwa wao akiwa huyu jamaa MO11
Majibu ya kukata na shoka halafu mubasharaaa
 
Kwa miaka kadhaa ambayo nimekuwa member wa JF nimeweza kuexperience mambo yafuatayo;-

1. Anacho komenti mtu wa kwanza kwenye post maranyingi huwa ndio msimamo wa wengine wanaofatia kukomenti ( yaani wengi ni wafata upepo). Wakwanza kukomenti akikuponda na wengine watakuponda, wakisifia na wengine watasifia.

2. Unaweza ukatukanana na mtu kwenye thread hii then mda huohuo ukamgongea like kwenye thread nyingine na kummwagia sifa kibao.

3. Kwavile tunatumia Fake ID's, si ajabu ukajikuta unabishana na bosi wako na kumvimbia kwamba unahela sana na unauwezo hata wa kuajiri ukoo wao mzima, pia unaweza ukamuita babaako 'dogo' au 'boya' bila kujua.

4. Ukienda kwenye jukwaa la Vyombo vya usafiri unaweza fikiri kila mwana JF anamiliki gari, tena gari kali. Maana ukiulizia VITZ unaambiwa uwe mvumilivu uendelee kujikusanya ununue 'GARI', na uachane na vi'baby-walker'.

5. Ukienda MMU Wanaume wote wanajifanya 'MANDINGO', hakuna anayekubali kwamba yeye kibamia, na akianza kupiga gemu goli 1 ni kuanzia dakika 30, hakuna anayemaliza kwa dakika 5. Hilo ni kwa upande wa wanaume, kwa wanawake wao kila mmoja ni 'MNATO', hakuna Mtera kule.

6. Ukienda kule jukwaa mama 'SIASANI' yaani ndio vurugu tupu, kila mtu anajiona jiniazi na ndio maana ni jukwaa linaloongoza kwa povu. Utasikia "hizo hoja zako za kitotototo peleka kwa watoto wenzio facebook".

7. Watumiaji wa JF wanadhani kila mtu yuko Dar. Hata wanapoweka matangazo yao unaona kabisa akilini mwao wanajua kila mtu anaishi Dar.

8......
9......
10......

Mengine ongeza wewe...
umeshahau watu wanatongoza avatar wanadhani ni muhusika
 
Wengine ata week hatujamaliza,
[emoji205] Tutulie tusikilize wenyej
 
Kuna jamaa alitoa povu ktk uzi wa mshana jr kuhusu nguvu za giza, alipovuka eti mambo ya kishirikina hayana nafasi kwa wanakondoo, lakini baaada ya dk chache baadae, nikamkuta katika uzi mwingine anawatetea jamaa zake Kaoge, nikashindwa kujua idadi Ya miungu anayoabudu Jamaa!
 
16464427_1871489053063402_5198701382277791744_n.jpg

umeshahau watu wanatongoza avatar wanadhani ni muhusika
 
Ukiandika Uzi kwa lugha ya kiingereza ukakosea kidogo kila mtu atakuambia
Mkuu ulisomea magu nini?
 
Back
Top Bottom