JamiiForums ni kiboko, imenipa kazi mwenzenu

JamiiForums ni kiboko, imenipa kazi mwenzenu

Anza kazi kijana kwa kampuni ambayo unadhani utaenda practise ulichosoma for Career Advancement.
Pia kumbuka hautakiwi in life kubweteka na mshahara you need to have altenative sources of income could be vibiashara vya apa na pale etc
 
Habari wakuu!,mi ni graduate-2011 na nimekuwa nikifuatilia matangazo ya kazi hapa JF na kutuma application zangu, nimeitwa kwenye interview 5 na sasa nimeitwa kufanya kazi kwenye kampuni 3 tofauti, zote nimepewa mikataba nimeisoma lkn sijaisaini bado, tatizo ni malipo. Yani ina-arange 380,000 mpaka 400,000. Je, kwa maisha ya Dar zinaweza kukidhi? Mi sina uzoefu na jiji hili nimekuja tu kutafuta kazi na nipo kwa ndugu maana yake nikipata kikazi hicho nitalazimika kuanza maisha yangu.
Nenda kapige mchongo huo.
 
nenda kaanze kazi .utakuwa na ujuzi na itakuwa rahisi kupata kazi nyingine.........maisha ni kupanga/kuchagua ukitaka ya hali ya juu hautatosha ukitaka maisha ya kawaida utapanga na utaona mambo yanakwenda kutoka na mshahara wako
 
400,000/= ikikatwa kodi pamoja na nssf unabaki na kama 320,500/= sio mbaya, you should go for it wkt unatafuta maali kwingine!...kuna mshkaj wangu anafanya kule posta analipwa 300,000 net na anaishi kimara mbona anayamudu maisha vizur tu
 
Huo mshahara ni mdogo, lakini ni rahisi kupata kazi nyingine wakati ukiwa na kazi kuliko unapokuwa huna kazi. Uzoefu wangu: Nikiwa graduate nilianza na kazi ya 270,000/= , baada ya miaka miwili nikapata experience wanayo taja kwenye matangazo ya kazi, nikaomba kazi sehemu ingine at least kwa sasa hivi napata mara 4 ya hiyo ya kwako.

Ila usisahau kumchangia huyu kaka yako ambaye umepata kazi kupitia kwake ili naye aweze kuendelea kuishi katika dunia hii......Nina maana ya changia Jamii Forum
 
Hongera mkuu ....!!, chukua hiyo kaz kama pa kuanzia, kisha chakalika mpaka ufikie malengo yako ...
 
Mkuu, ni kupangilia tu, ingawaje huo mshahara sio mkubwa, lakini huwezi ku-suffer on ur way on getting perfect job for u. Binafsi, natumia about TZS 150,000/= kwa mwezi na napiga menu ya maana kabisa kuliko anayetumia 300,000/= kwa mwezi.

Here is how I do (Huwa nafanya yafuatayo mara nipatapo salary yangu):

- Nanunua mchele 15 kg@ 1,500/- = TZS 22,500/-
- Nampa mshikaji wa bucha sh. 28,000/ kwa mwezi ~hapo ni nyama 0.5kg (stake) na 0.5kg(maini). Hizo ni kwa wiki, ambapo natumia 7,000/- kwa wiki na 28,000/- kwa mwezi. Nilichofanya baada ya kuhamia hapa kitaa, nikajenga mazoea na mshikaji wa bucha hadi akawa rafiki yangu na hivyo, ninapomwachia 28,000/- nina uhakika wa kwenda kuchukua nyama kila wiki bila longolongo!
- Watu wa mwambao bila nazi, msosi hauendi...na siku kuna nazi(ya tui) za bakhresa, nina shida gani!!!! Natumia pakti mbili kwa wiki @600, therefore nanunua za mwezi mzima kwa sh. 4,800/-
- Huwa nanunua mafuta ya kula tena yale yale ambayo maskini kama mimi wanayaogopa....ya alizeti kwa sh.18,000/ (lita 3) ambayo nayatumia si chini ya miezi 4 (means kwa mwezi na-spend sh 4,500/-)
- Nanunua in advance sukari 2kg @2000= TZS 4,000/- .
- Nanunua Soya 3 packets @2,000~~~~ TZS 6,000/- kwa mwezi (huwa situmii kabisa majani ya chai)
- Maharage 2kg@ 1,800/= (3,600/- kwa mwezi).... nyama peke yake huwa haipandi kwahiyo lazima nipate maharage kidogo.
- Tambi kwa ajili ya weekend 8pc @ 1000= 8,000/-
- Mafuta ya taa 6lts @ 2000 = 12,000
- Njegele 1,200/- kila weekend...napenda sana hii ki2 na tambi!= 4,800/- kwa mwezi

22,500 + 28,000+4800+4500+4000+6000+3600+8000+12,000+4,800= 98,200/=

Hapo unakuta natumia kama laki tu, lakini napata vitu vyote muhimu for my favorite meal !! Addition point ni kwamba, ninapoenda job, huwa sinywi chai asubuhi, BALI HUWA NAKULA MSOSI!!!

Nimeeleweka?

Sinywi chai; NAPIGA MSOSI! Always, ingawaje sikai mbali na town, huwa naamka saa 11 alfajiri na kuanza kupika WALIIIIIIIII......! Nikishapiga menu yangu ya adabu asubuhi, wala sihangaiki lunch time; by the way, nikishatulia kwenye kiti changu huwa sipendi usumbufu!

Eti unakuta mtoto wa kiume anasema "eti siwezi kula asubuhi.....!" mtu ukiwa na hayo mawazo then be prepared kuolewa mambo yatakapobana! Nasikitika sana kwamba hamna daladala ambazo naweza kulipa in advance, otherwise, I'd do it....sipendi stress kwenye maisha, hususani kwa vitu vya kipuuzi kama basic needs!

Try it, utakuja gundua maisha is very easy sema hatuyajulii tu!!!
You must be jinias aiseeeeee........ila mkuu wewe noma unaamka na kuanza kupika??
 
...1)Hiyo uliyopiga 6*12*300,000 ni umezidisha tu 300,000 kwa miaka sita, haujaweka interest .

Hapo nilikuwa najaribu kusema hata kama ukiamua kuweka hiyo pesa yote ambayo ungeweka kila mwezi kwa miaka sita wakati unaanza (badala ya kufanya hivyo kila mwezi!) huwezi kupata interest itakayo kufanya uwe na kiasi cha pesa cha shiling milioni 150 baada ya miaka sita (katika rate hiyo ya 8% pa, compounded monthly).

..5) Formula rahisi ya kutafuta pato kwa kutumia compound interest ni P(1+r/n)^ nt (for one-time investment)

...Au ngoja nikurahisishie: 300,000 monthly, for 6 yrs at 8% compound interest, compounded annually

6x3.6M + 5x3.6Mx1.08+ 4x3.6Mx1.08^2 + 3x3.6mx1.08^3 + 2x3.6Mx1.08^4+ 1x3.6mx1.08^5 = aprox. 90M
If u compound it monthly, inaenda to 100m+ coz u deposit monthly too!!..

Hiyo fomula A = P(1+r/n)^ nt (A ni amount including interest baada ya ya miaka hiyo sita, P ni principal, let say unaweka hizo 21,600,000 (=6x12x300,000) zote kwa mkupuo mmoja wakati unaanza badala ya kila mwezi ambayo kwa hoja yako tunategemea ilete amount kubwa zaidi, halafu r ndio rate yaani 0.08 (8%) kwa mwaka, n ni mara ngapi katika mwaka compunding inafanyika, let say ni kila mwezi na hivyo n itakuwa 12, halafu t ni muda (katika miaka) wa hiyo fixed deposit, yaani miaka 6).

Mimi nilifanya hivi hiyo hesabu:

P=21,600,000
[r/n = 0.08/12=0.0066667, nt =12x6=72]
1+r/n = 1+0.0066667=1.0066667
(1+r/n)^nt=(1.0066667)^72= 1.6135060140746 (type kwenye excel "=power(1.0066667,72)" au hivi "=1.0066667^72")
A = P(1+r/n)^ nt = 21,600,000 x 1.6135060140746 = 34,851,729.9040113

Labda kama kuna mahala ninakosea katika fomula hiyo!

Ukitaka kuitizama vema ni lazima uzingatie kuwa bank baada ya wewe kufanya deposit wanampa mtu mwingine anayehitaji mkopo (say kwa kipindi hicho cha miaka 6) kwa interest ambayo itakuwa kubwa kuliko 8% (i.e. kunakuwa na 'spread')...so strictly speaking anayekulipa interest sio bank bali ni mteja aliyekopa hiyo pesa ambayo wewe ume deposit bank. Sasa jaribu kufikiria leo hii mtu akikopa bank tzs 21,600,000 anaweza fanya biashara gani katika miaka sita ili akuze mtaji huo hata kufika zaidi ya tzs 150m (ili yeye abakie na mtaji/faidia, arudishe bank pesa yote aliyokopa na interest juu -bank ipate faida yake na baadae pia kukupa wewe uliye deposit tzs 21,600,000 kiasi cha tzs 150m karibia faida ya shiling 128m!). Hapana....labda kuna kitu sijaelewa/sielewi hapa.
 
Piga mzigo huo ili upate uzoefu, hakuna mtu atakaye anza kukulipa 4 mil. wakati huna uzoefu, jenga njia kwanza ndiyo upite. unataka kupita kwenye njia wakati hujaisafisha?
 
Hivi kwani ulipokuwa unatafuta kazi ulitarajia mshahara wa kiasi gani??? Na nani aliyekuroga kuwa mshahara huo hautoshi?? Acha dhihaka wewe...Usijaribu kulinganisha maisha yako na ya watu wengine?? Wewe ndo unayejua kwa kiasi gani unahitaji kazi..Ndo maana ukatoka huko kijijini ukaja mjini!!! Kama sivyo ungebaki hukohuko uendeleze kilimo kwanza!!! Chukua kazi hiyo wewe acha uzembe na ukianza kazi usiwe FISADI kwa kujitafutia UTAJIRI na MAFANIKIO ya WIZIWIZI....Na ukianza kazi tu hama mara moja kwa huyo jamaa yako....Maana kama yeye anamshahara wa mamilioni utajiona kazi yako haikufai wewee!!!!
 
Walimu na wauguzi wanaishije? Acheni kujifanya sio watanzania, huu ni ubwege. Ni kweli huo mshahara si mkubwa lkn si kweli kwamba hauwezi kuishi. Sasa hivi hana hata senti anaishije? Umbea wa kiume hauna hata mashiko. Kwa bajeti hiyo mimi enzi zangu mbona ningemiliki hata nyumba ndogo 2. Tupunguze mashauz, huyu anayeuliza hana mtoto wala mjukuu, ni yeye, sehemu zake za siri na tumbo, atashindwa vipi kuishi kama sio kutaka kuleta ujuaji hapa?

WEWE BWANA MDOGO, KAANZE KAZI WA NOTI NDEFU UTAKUKUTA HUKO HUKO UKIWA KAZINI. NDIO WAKATI WAKO WA KUJIFUNZA MAISHA NA BAJETI

Haya majibu ni ya kijinga sana. Ulitakiwa kuweka mchanganuo wa jinsi hiyo hela inavyoweza kutumika kwa mwezi na siyo kujaza ujinga wako wa kuhudumia nyumba ndogo. Yaani unataka mtu aanze kupokea rushwa au kuiba siku ya kwanza kazini?

Kwa aliyeomba ushauri
Daima mwanzo ni mgumu. Jaribu kujinyima vitu visivyo vya msingi huku ukitengeneza jina na CV yako. With time utapata kazi yenye kulipa vizuri zaidi.
 
Mkuu, ni kupangilia tu, ingawaje huo mshahara sio mkubwa, lakini huwezi ku-suffer on ur way on getting perfect job for u. Binafsi, natumia about TZS 150,000/= kwa mwezi na napiga menu ya maana kabisa kuliko anayetumia 300,000/= kwa mwezi.

Here is how I do (Huwa nafanya yafuatayo mara nipatapo salary yangu):

- Nanunua mchele 15 kg@ 1,500/- = TZS 22,500/-
- Nampa mshikaji wa bucha sh. 28,000/ kwa mwezi ~hapo ni nyama 0.5kg (stake) na 0.5kg(maini). Hizo ni kwa wiki, ambapo natumia 7,000/- kwa wiki na 28,000/- kwa mwezi. Nilichofanya baada ya kuhamia hapa kitaa, nikajenga mazoea na mshikaji wa bucha hadi akawa rafiki yangu na hivyo, ninapomwachia 28,000/- nina uhakika wa kwenda kuchukua nyama kila wiki bila longolongo!
- Watu wa mwambao bila nazi, msosi hauendi...na siku kuna nazi(ya tui) za bakhresa, nina shida gani!!!! Natumia pakti mbili kwa wiki @600, therefore nanunua za mwezi mzima kwa sh. 4,800/-
- Huwa nanunua mafuta ya kula tena yale yale ambayo maskini kama mimi wanayaogopa....ya alizeti kwa sh.18,000/ (lita 3) ambayo nayatumia si chini ya miezi 4 (means kwa mwezi na-spend sh 4,500/-)
- Nanunua in advance sukari 2kg @2000= TZS 4,000/- .
- Nanunua Soya 3 packets @2,000~~~~ TZS 6,000/- kwa mwezi (huwa situmii kabisa majani ya chai)
- Maharage 2kg@ 1,800/= (3,600/- kwa mwezi).... nyama peke yake huwa haipandi kwahiyo lazima nipate maharage kidogo.
- Tambi kwa ajili ya weekend 8pc @ 1000= 8,000/-
- Mafuta ya taa 6lts @ 2000 = 12,000
- Njegele 1,200/- kila weekend...napenda sana hii ki2 na tambi!= 4,800/- kwa mwezi

22,500 + 28,000+4800+4500+4000+6000+3600+8000+12,000+4,800= 98,200/=

Hapo unakuta natumia kama laki tu, lakini napata vitu vyote muhimu for my favorite meal !! Addition point ni kwamba, ninapoenda job, huwa sinywi chai asubuhi, BALI HUWA NAKULA MSOSI!!!

Nimeeleweka?

Sinywi chai; NAPIGA MSOSI! Always, ingawaje sikai mbali na town, huwa naamka saa 11 alfajiri na kuanza kupika WALIIIIIIIII......! Nikishapiga menu yangu ya adabu asubuhi, wala sihangaiki lunch time; by the way, nikishatulia kwenye kiti changu huwa sipendi usumbufu!

Eti unakuta mtoto wa kiume anasema "eti siwezi kula asubuhi.....!" mtu ukiwa na hayo mawazo then be prepared kuolewa mambo yatakapobana! Nasikitika sana kwamba hamna daladala ambazo naweza kulipa in advance, otherwise, I'd do it....sipendi stress kwenye maisha, hususani kwa vitu vya kipuuzi kama basic needs!

Try it, utakuja gundua maisha is very easy sema hatuyajulii tu!!!
Mkuu kweli wewe ni mzee wa budget,...ila siku ukioa kumbuka kubadilika maake_mmmmmmh
 
Nenda kafanye kazi. Cha maana zaidi ni kuweka mipango juu ya (1) Career development (2) Personal development. Members wengi wameshauri juu ya umuhimu wa kuepuka matumizi mabaya na kutafuta njia zingine za kuongeza kipato. Elewa kuwa muda ni kitu muhimu sana tafadhali uwe na mipango mbalimbali juu ya maisha, ikianzia ya muda mfupi na ya muda mrefu na kila mpya lazima ufanye monitoring & review.
 
Hongera sana .
Kama huna kazi kabisa ni bora ukasign contract na moja ya hizo kampuni,leo na kesho utapata kazi nyingine kwani utakuwa upo ndani ya soko la ajira .Uzoefu na social capital utakayoitengeneza ukiwa kazini itakuweka sehemu nzuri baadae.
 
Au ngoja nikurahisishie: 300,000 monthly, for 6 yrs at 8% compound interest, compounded annually

6x3.6M + 5x3.6Mx1.08+ 4x3.6Mx1.08^2 + 3x3.6mx1.08^3 + 2x3.6Mx1.08^4+ 1x3.6mx1.08^5 = aprox. 90M
If u compound it monthly, inaenda to 100m+ coz u deposit monthly too!!

BON CHANCE!!


Kwa hii hesabu naomba mkuu ufungue benki ili nije kuweka pesa zangu. Kwa kifupi mkuu kwenye hii computation yako umefanya kitu kinaitwa 'Multiple inclusion of entries' ambayo imekusababishia kupata 'Exaggerated output'.

Ukifanya hiyo hesabu vizuri kwa formula yako ya P(1+r/n)^nt huwezi kupata zaidi ya 35M kwa kipindi cha miaka 6. Kama namba hazikwei siku hizi kuna software kibao. Mfano hii hapa:


Compound Interest Calculator
 
Piga kazi wewe acha utani. Ngoja nikupe story kidogo

mimi nilimaliza shule 2009 nikapata mchongo Arusha. kama mnavyojua Arusha hakunaga mchezo hakuna njegere za 150 wala 200 ni noma lakini nilianza na Mshahara basic 395,000 na niliripoti mzigoni bila kujishauri...nikapiga mzigo huku natafuta better position, uzuri waliniweka sehemu nzuri ya Creditors kwa hiyo nikawa nawasiliana na supplier wengi sana na nilikuwa napiga kazi kwelikweli....baada ya miezi sita nikaitwa na kampuni moja baada ya kuappriciate kazi yangu kwenye kampuni nililokuwa... wakaniahidi kunipa Net ya 420,000 faster nikasepa maana kwanza nilikuwa bado nipo Probation.... nikachapa kazi pale mpaka probation ikaisha....ilipoisha jamaa waliniappriciate na kunipa gross ya 828,000 na hapo sasa ilikuwa ni 2010. wakanipa chance kama junior accountant tu. baada ya miezi sita ikafika increement na wakanipa 850,000 net. wakati huo pia nilikuwa napiga kazi huku naangalia upepo..... ilipofika April 2011 nikakutana na jamaa ambao nilikuwa nadeal nao sana ( infact waliomba nikutane nao wanataka Accountant) sikuvunga...nikakutana nao full maujanja ni kama ilikuwa interview hivi japo sikujua wanataka nini, wakaniuliza nafanya nini na napata ngapi? baada ya week mbili wakaniletea nisign Appointment ya 1.4M net wananitaka nifanye kazi kwao....sikuvunga nikasepa nikaenda kuanza nao......leo hii hata sikwambii napata ngapi tena...kwahiyo cha msingi ni wewe upate kazi kwanza then ujimarket mwenyewe ile mbaya.
 
Kwa hii hesabu naomba mkuu ufungue benki ili nije kuweka pesa zangu.
Hata mimi nipo tayari kukopa sehemu yoyote hata milioni 100 na kuweka kwenye hiyo benki yake!
 
Sikiliza mkuu,

380,000/= na 400,000/= hakuna tofauti yoyote. Maana yangu ni kwamba, kama range ya mshahara ndio hiyo basi hapo usiangalie kigezo cha mshahara, bali angali ni kazi gani ambayo itakuuza vizuri hapo baadae. You get wht I mean?

Assume kampuni A ni benki ambayo wamekupa nafasi ya Teller na salary offer ya sh. 400,000/= na company B, nayo ni reputable company na wameku-offer post ya Marketing Officer kwa mshahara wa sh. 370,000/= ! Kwa ushauri wangu, accept offer ya marketing officer kwa 370,000/= coz' marketing officer inauzika kuliko teller.

Kama salary inatosha au haitoshi, ni kwamba huo mshahara ni mdogo lakini usiache coz' hapa town sio kwenu na umekuja kutafuta. Tatizo lenu watu kama nyinyi (yaani mliokuja Dar karibuni) mna ujinga wa kuangalia washikaji zenu wanakaa wapi badala ya kuangalia una salary kiasi gani. Utakuta mtu kamaliza UDSM, washikaji zake wanaishi Mwenge/Sinza/Ubungo (nyumbani kwao) nanyi mnataka kupanga maeneo hayo. Utaumia broda!

Mahali kama Kwa Azizi Ally, unapata chumba kwa sh.30, 000/- tena kizuri tu kwa mtafuta maisha. Mahali penyewe karibu na town, una uhakika wa kutumia 600/- tu kwa nauli; sehemu za kula bata hadi uzisumbukie..... unadhani basic ya 380,000/= haiwezi kukusogeza wakati unatafuta better post?! it can broda!

Akili za mbayumbayu, changanya na za kwako!!!

kama jama amekusoma sasaivi anaenda kusaini mkataba maana maneno uliyompa ni mazito sana.
 
You must be jinias aiseeeeee........ila mkuu wewe noma unaamka na kuanza kupika??

Ahaaaaa, mkuu! hilo tu?! kama kuna jambo gumu ktk kazi zangu binafsi basi hilo la kuamka saa 11 alfajiri na kupika c moja wapo!!! mbona cmpo tu wangu! kwanza, b4 cjaenda kulala, nahakikisha nimesafisha sufuria la kupikia pamoja na kuosha mchele ( na kuchuja maji yote). Nikiamka tu saa 11, ki2 cha kwanza ni kuchemsha maji kwa jagi la umeme, dak 1 yanakuwa tayari kisha nayatumia maji haya niliyochemsha kubandikia msosi wangu! Nikishaweka tu sufuria jikoni, nakimbia mara moja bafuni kwa ajili ya kuoga na ninaporudi huko nakuta tayari msosi ushakaukia! Nikisharudi toka bafuni, ki2 cha kwanza ni kupunguza moto na kugeuza ubeche na kufunika.....ninapomaliza kujipangusa maji, msosi nao unakuwa tayari.....no one minute is lost unutilised! jaribu hiyo ki2, utakuja gundua maisha iz very ize, ni kujipanga tu!
 
Back
Top Bottom