JamiiForums Usiku wa manane

😁😁😁😂😂😂 ndiwoo wengi tunakoga, wateule wachche ndiyo wanaoga 😂😂😂😂🤣🤣🤣
Hakika,waogaji ni wachache mno,Mtu anaoga masaa matatu kajiloweeka wee na shower gel na maji ya uvuguvugu pembeni ana wine,kawasha mishumaa ya kunukia halafu anasikiliza blues,Wakogaji Sasa na makopo yetu,kipande Cha jamaa mixer doffi ,unaanza tu kopo la kwanza Mende huyo kapanda mguuni,unaruka unaparamia tumaji twenyewe twa chumvi halafu nusu ndio tunamwagika tunabaki robo ndoo,hapo ni chap chap dakika mbili na sekunde 47 uko nje umeSHAKOGA😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…