JamiiForums Usiku wa manane

Pole atakaa sawa .
Hapana lilikuwa ni suala la kutaka kumchagua mwenyekiti wa kijiwe chetu hasa tunapokutana kunywa ulanzi ,Sasa kinachoniwazisha ni kuwa sikatai kuwa mmoja wa watu wanaohudhuria hili eneo kupata ulanzi ila nimesikitika kuona watu wa Rika kubwa kwangu na vijana wadogo waliojikatia tamaa wanaomba kama ni issue ya uenyekiti wanadai nipewe Mimi .πŸ€”
Hili limenizindua kuwa Sasa kama watu waliojikatia tamaa na maisha na wasio na mawazo ya mbele tena wanaona Mimi ndiye naweza kuwa nsemaji wao ,mwenyekiti wao basi pasina Shaka nami naelekea kuwa kama wao ,hakika nimeumia na nipo katika mawazo ya kukata mguu wangu pale .
 
Amen Mkuu πŸ™

Nashauri kama bajeti itaruhusu hamia kwenye beer tu, ukikaa nasi kwenye viti virefu tunaweza kubadirishana mawazo pengine hata kupeana deals za hela
 
Amen Mkuu πŸ™

Nashauri kama bajeti itaruhusu hamia kwenye beer tu, ukikaa nasi kwenye viti virefu tunaweza kubadirishana mawazo pengine hata kupeana deals za hela
Kwenye bia nilikuwepo mda mrefu ila nina changamoto ya kiafya niliipata ikabidi nipumzike bia ili niende locally ila kwa haya Bora nirudi Bar kunywa maji tu kaka
 
Kuna pombe ya kienyeji inaitwa Komoni, umewahi kusikia? Kama una shida ya kiafya nadhani hii pombe Iko vizuri
Sio ile inakuwa kama maji ? Ambayo pia inapatikana mkoa wa kagera ? Basi ikiwa ni hii nishainywa zamani kidogo ila haikupenda kichwa changu maana kila nilipoinywa nilileta vurugu huko mkoani Kagera kiasi Cha kuhamishwa kituo Cha kazi maana niliwatesa Sana Wana mtaa nilipokuwa nimepanga kaka .
 
Huenda ni hiyo

Mikoa ya Morogoro, Mbeya, Iringa hadi Rukwa kule niliona Wanatumia Mahindi kuipika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…