Na jibu kufuatana na kichwa cha habari ulichoweka. Tatizo sio Dr Janabi na Dr kuweka viwango hivyo inaweza kuwa sawa, tatizo ni la sirikali yetu kutoweka mifumo ya uchangiaji matibabu ambao ni endelevu Kwa kuweza kuwaingiza asilimia 95% ya watu wenye uwezo wa kuchangia.Ulizeni gharama za matibabu Muhimbili zilivyo kisha mlinganishe na Hospitali za mitaani mtaona kuwa hali ni mbaya sana. Hospital ya Taifa ya Muhimbili kwa sasa imekuwa ya kibiashara zaidi na si kutoa huduma.
Utra Sound ambayo hata mtaani unaweza piga kwa tsh 20,000 Muhimbili ni tsh 35,000. na mkumbuke mtu anayeenda Muhimbili ni mtu ambaye emshindikana mtaani si kuwa anawenda kule kwa kuwa anapenda.
Kumwona specialist ni tsh 30,000 akikuelekeza uende kwa mwingine nako utalipia tsh 30,000 hata kama ni the same day. hujaenda kuonana na Daktari wa magonjwa ya akili kama unafanya clinic. ni tsh 45,000 mnakaa dk 5 anakuuliza unakunywa dawa? unajisikiaje? haya njoo tena baada ya miezi 3 anakuandikia anakuruhusu uende. tayari tsh 45,000 imeenda. hizi kodi zetu zinatumika wapi?
Soma Pia: Rais Samia afanya uteuzi: Masauni apigwa chini Wizara ya Mambo ya ndani, Kabudi apelekwa Wizara ya Habari na Michezo, Janabi kuwa mshauri wa Rais
Nyie mnajinunulia magari ya milion 300 mpaka 500 huku maskini wanakufa kwa kukosa huduma muhimu na kuwaoandishia gharama za matibabu. hali ni mbaya sana kwa watanzania.
Sishangai wanaposhangilia kusikia wabunge wamepata ajali. wanaumia sana kwa mateso wayapatayo huku watu wachache wakifaidi huduma za kijamii bure. wao wanachangia wachache waweze kula keki ya nchi vizuri.
Pili ni upigaji wa viongozi ambao kwa namna moja au nyingine wapo chini ya sirikali, mfano MSD na nhif.
Tatu huduma flani au maslahi flani kutolewa kwa upendeleo, mfano tuna sikia kuna watu wanaenda kutibiwa India, wakati kuna watu matibabu flani hapa hapa nchini, wanaambiwa hayapo kwenye bima Yao kwenye bima ya Afya.
Hivyo kuna ubaguzi54