Janga la Corona : CAF yaifuta Mechi ya Namungo huko Angola

covid ni serikali 100 % kama serikali ya angola imepanga hivyo basi hiyo ni amri
Tatizo lako unataka kuleta siasa za bongo kwenye mpira wa kimataifa, game haijaahirishwa sababu ya vipimo vya Angola kusema wachezaji 3 wa Namungo wamekutwa na Corona ila wamehairisha sababu ya fitna na sintofahamu iliyoletwa na jeshi la Angola.

Nikukumbushe tu FC platinum walikutwa na Corona walivyokuja Dsm ila timu haikuambiwa ikae quarantine, Simba waliambiwa wana Corona walivyoenda Nigeria wakawa wajanja wakaenda kupima sehemu nyingine kwa gharama zao wakakutwa tena hawana corona, corona kwa sasa ni fimbo ya kuwachapia timu ngeni inapokuja.

CAF inabidi iwe makini, vinginevyo kinachofuata ni fitna za Corona kwa kila timu ngeni, ukija bongo hapa ukiambiwa una Corona na sehemu ya kupimia ni moja unafanya nini?
 
Kila nchi ina sheria zake.
Hata game ya Kaizer na Raja imefutwa.
Sheria inaweza kutumika vibaya kufanyia fitna, ndio maana hadi CAF wamekubali mechi ihairishwe kwa sababu wameona kilichofanyika ni fitna. Tufanye tumekubali wachezaji 3 wa Namungo wapo + Covid, je ni kwa nini wamelazimisha timu nzima iende quarantine tena ndani ya kambi ya jeshi kwa shurti huku abiria wengine waliofika nao kwenye ndege wameruhusiwa kuendelea na shughuli zao?

Rapid PCR test accuracy yake ni ndogo pia inatumia kama dk 15 kutoa majibu, hauwezi toa majibu ya timu nzima ndani ya dk moja, kutokana na maelezo ya Namungo majibu ya timu nzima yalitoka hapo hapo ndani ya dk kitu kinacho onyesha ilikuwa pre planned move.
 
Wakubali kukaa karantini hizo siku ili gemu ipigwe hakuna namna ukizingatia wapo kwenye ko stage na ratiba haiwasubiri, vinginevyo angola watapewa point za mezani. Aibu kwa nchi
Kwani wao hawatakuja bongo? Kutesa kwa zamu.
 
Nchi nyingi tu jeshi linasimamia protocols za Corona.
Halafu Corona unaweza kutest negative leo, baada ya wiki ukatest positive kwa maambukizi ya juzi.
Msilazimishe Kila nchi iwe relaxed, kiss sisi tupo relaxed.
Game ya Kaiser na Raja imefutwa pia sababu Morocco kama nchi nayo ina protocols zake.
Halafu viongozi wafanye kAzi kitaalam kwa kuuliza nini kinahitajika kabla ya kwenda.
 
Kwa nini wamelazimisha msafara mzima kwenda kuwekwa quarantine kwenye kambi ya jeshi kwa shurti huku wasafiri wengine kwenye same flight wakiruhusiwa ?
 
Kwa nini wamelazimisha msafara mzima kwenda kuwekwa quarantine kwenye kambi ya jeshi kwa shurti huku wasafiri wengine kwenye same flight wakiruhusiwa ?
Weka ushahidi, nimesoma statement ya tff hapo juu sijaona haya unayodai, taarifa ya majaliwa haina maelezo haya, nimesoma protocols za angola ukweli wapo strictly na covid. Mnaingiza propaganda kupindisha ukweli kwa malengo maalum
 
Match itaenda kuchezwa kwenye nchi nyingine, Angola watapoteza fursa ya kuwa wenyeji na wakija Tz tunawapiga fitna tena, wachezaji kama 6 hivi watakuwa na Corona.
Unakomaa na mpira wa majitaka 2021
 
Weka ushahidi, nimesoma statement ya tff hapo juu sijaona haya unayodai, taarifa ya majaliwa haina maelezo haya, nimesoma protocols za angola ukweli wapo strictly na covid. Mnaingiza propaganda kupindisha ukweli kwa malengo maalum
Rudi jukwaa la siasa, hujui mpira na hujui kinachoendelea kwenye mpira. Taarifa ya kwanza kutoka ambayo ilikuwa na maelezo yote ni mahojiani ya Rais wa Namungo na mwandishi wa bongo, hiyo clip ndio imetoa taarifa iliyofanyiwa kazi na Serikali ( PM) na TFF. Au ulidhani Majaliwa na TFF wameota tu Namungo wapo ndani ya kambi ya jeshi?

Bado hujajibu swali kwa nini flight nzima wamewekwa quarantine msafara wa Namungo tu huku watu wengine wakiruhusiwa kuendelea, kwa nini kama wapo neg wawekwe quarantine tena chini ya mitutu ya jeshi? Rudi jukwaa la siasa ukapige porojo hujui mpira na hujui siasa za mpira wa Africa.
 
Unakomaa na mpira wa majitaka 2021
Wao Angola walitaka kufanya fitna za kijinga inaenda kula kwao, Simba hapa Jan tu waliwapiga wachezaji 4 wa Platinum FC Corona ili match iliendelea, unajua hata hilo ?

Unajua policy ya CAF dhidi ya Corona, unajua kilichowatokea Gabon last year walivyofanyiwa ujinga kama huu huu wakalala airport karibia siku nzima???
 
Hii ndio taarifa ya sasa kutoka CAF kutokana na sakata la wachezaji watatu na kiongozi mmoja wa Namungo kukutwa na corona

Tusubiri taarifa zaidi kutoka CAF ambalo ndio shirikisho linalosimamia soka barani Africa

View attachment 1701605
CAF nao si waseme wameiairisha kuliko kusema wamefuta.
Ungekua CCM wangecheza ila kwa vile CAF Dah.
 
Kwa nini wamelazimisha msafara mzima kwenda kuwekwa quarantine kwenye kambi ya jeshi kwa shurti huku wasafiri wengine kwenye same flight wakiruhusiwa ?
Usipende kufikiria hujuma. Hujuma huepushwa na good planning.

Hao abiria wengine wametoka Tanzania?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…