Kama ni kweli basi ni aibu
Club iliyokusanya zaidi ya 200M kwenye goli la mama leo hii inapatwa na skendo za madeni?
Halafu mwanzo tulivyoona vilio kwa Princess tukadhani labda sababu itakuwa focus yao ipo kwenye timu ya wanaume, na kwamba upande huu hauna hayo malalamiko kwasababu ndiko nguvu zote zilipowekezwa.
Hela zote hizo wanazitumia kufanya nini kama mishahara tu ya wachezaji wanashindwa kulipa kwa wakati?
Sasa zile ahadi zao za kutuambia watajenga uwanja tuendelee kuziamini kuwa ni kweli, kama tu pesa ndogo ya kulipa wachezaji inatolewa kwa kusuasua vipi kwenye jambo kubwa kama uwanja?