January Makamba: TANESCO sasa wamesitisha miradi ya ujenzi wa maofisi na kuelekeza fedha kukarabati miundombinu ya Ugavi

January Makamba: TANESCO sasa wamesitisha miradi ya ujenzi wa maofisi na kuelekeza fedha kukarabati miundombinu ya Ugavi

Makamba ana wiki 3-4 ofisini

And then you are talking about kuuza umeme nje ya nchi...umetokea wapi kwa wiki 3?

Hivi mna kichaa nyie members wa Mirembe?

January Makamba - sio mimi niliyesema- ni waziri ndio kasema siku ya kwanza alipokuja TANESCO kwamba tutauza umeme nje ya nchi.

Wengine tukamwona huyu mtu ni crackhead au ni vipi? Tanzania haiko electrified, na ambako umeme umefika unakatika masaa sita kati ya 24, we unatueleza habari ya ku export umeme...

Ina maana Makamba hajui extent of crisis ya TANESCO, wala hajataka kujielimisha kabla ya kutoa matamko mbele ya umma yanayomfanya aonekane waziri kituko na hohehahe mwenye pipe dreams za ku export umeme.

Sasa anakuja na twitter story za maintenance. Kwa nini Ulaya umeme haukatiki kufanya maintenance? Mtu anaetuambia umeme lazima ukatwe kufanya maintenance ni mtafuta visingizio, hatufai.

January Makamba, we said early on, is woefully inept at ministry of energy.
 
kuna mchangiaji hapo kwenye twita kachangia vizuri sana na ndio jibu la matatizo mengi...

Apunguze diplomasia na uungwana...hivyo vitu wakati wake haujafika kwa watanzania bado...Ukatili na ushenzi ndio suluhisho kwenye utendaji wa haya mashirika...
 
Sidhani kama ni "mgao"

Mgao wa umeme ni kitu kingine

Anachosema Makamba ni umeme kukatika sababu ya kazi za maintenance ambazo hazikufanyika tangu miaka mitano sita nyuma

Ni umeme KUZIMWA ili wafanya matengenezo na ni mahali mbalimbali nchini katika level za mitaani kabisa

Load Shedding au "Mgao" ni tatizo jingine kabisa ambalo linatokana na "under production of power" kwenye vinu huko,hapo sasa ndio serikali inaweza kulaumiwa!
Sisi wananchi tukiona kila j2 hakuna umeme tunajua ni mgao tu? hayo maelezo tulikuwa tunapewa enzi za JK kwa miaka 10,je ukarabati gani huo usioisha kwa miaka kumi?
 
Namuelewa maana naona sehemu nyingi wanabadili nguzo kuwa za zege badala ya miti.
Hii nchi miaka mitano nyuma iliishi kwa propaganda kuliko Korea kaskazini, unafiki, uzandiki na uongo ambao mwisho wa siku tungekuja kugota sehemu ambayo tusingeweza kurudi nyuma.

Chukulia mfano tu wa jiji la Dodoma kukusanya mapato kuliko DSM, lakini mwaka huu ni la pili kutoka mwisho. Jiwe alikuwa juha kweri kweri
 
Niko Dar,maeneo mengi haipiti wiki bila umeme kukatwa,na hali ilizidi kuanzia last year 2020.
Mfano huku kwetu ni guarantee kila alhamisi lazima umeme ukatwe.Ukiwauliza sometimes watakwambia hitilafu,wakati mwingine wanasema ni scheduled maintenance ingawa hawatoagi taarifa eneo husika,ni sisi wakorofi ndio tunajuaga sababu ya kuwasumbua,maana wengine wetu umeme ndio ajira yetu hapa mjini.
I wish ningekuwa na uwezo wa kuzileta post zangu zote nilizoandika kule uzi wa Tanesco kila mara umeme unapokatika maeneo mbalimbali nnapokuwepo.Ni mlolongo wa post za kila wiki,kila mwezi takriban miaka yote miwili ya hivi karibuni.
Sasa mtu kama mimi ninayelipia umeme wangu,nimenunua mita na kufunga,naishi kwa ajili ya umeme,halafu nakutana na hali hii ya kukatika umeme mara kwa mara kwa miaka sio wiki,ni miaka,then nasoma jibu la waziri wa nishati kama hivi,unategemea ntaelewa kweli?
Baadhi yenu mnazungumzia tatizo hili kama vile lina miezi miwili tu,ilhali ni tatizo la muda mrefu tangu miaka ya mwisho ya Magufuli(late 2019 then 2020 baada ya election limezidi mpaka leo) hili lipo.Nani atakuelewa ukisema ni scheduled maintenance?
Uongozi ni kitu cha mwendelezo,sisi tunauliza kiti cha waziri,regardless ni Makamba,Kalemani etc,wawajibike.Ukimrithi Kalemani unapaswa kuyatolea majibu hata yale yaliyofanyika akiwepo yeye.Ni jambo lisilo na mantiki mtu azungumze kama vile kuna mapinduzi yametokea na sasa serikali yake ni mpya.Makamba azungumze kama Waziri wa Nishati,sio kama Makamba.
Tatizo limedumu muda mrefu,halijaanza juzi,so ni scheduled maintenance na hitilafu all through the year?Then tunalipia kitu gani sasa?Hata gari haiendi service kwa kiwango hicho.
Kama Dar umeme unasumbua hivi,then ni wapi Tanesco wanaweza kutuonyesha wanajitahidi kutoa huduma bora?
Halafu kwanini hawasemi hadi waulizwe?
Kitu cha mwisho baadhi yenu mjue watanzania wana makovu.Miaka iliyopita especially before Magufuli waliumizwa sana na umeme.
Unapokuja kwetu kuzungumzia umeme uwe na hoja za kueleweka....SABABU TUNAWAJUENI MAMBO YENU VIZURI TU,mmetuchosha kwa miaka mingi.Shirika lile lilikuwa zuri sana,lakini nyie viongozi mmelivuruga.Kama sio nyie mlioko hivi sasa basi wenzenu waliopita na mzigo wao mnaubeba nyinyi, hamuwezi kubisha,ni matakwa ya uongozi.Kwa hiyo mkija kwetu kuzungumza muongee ukweli,acheni uongo kwa mambo yanaumiza jamii.Umeme ni sensitive,uchumi wa mtu mmoja mmoja na wa taifa.Msiufanyie utani utani!
 
Makamba na Mwigulu ni contenders wa urais 2025,

wamepewa wizara zenye lawama technically ili wawe disqualified.

Hizo
 
Hiyo bil 200 ni makusanyo ya mwezi tu, mbona hili lipo wazi?
View attachment 1991272
Jamaa anajua namba ila kaamua kubishana, na ukiendelea kubishana naye unaweza geuka victim wa matusi yake.

Hakuna kisingizio chochote cha kukatika umeme mara kwa mara, kila kitu kipo planned watu wapige pesa. Na architect wa michongo ndio huyo bwana January.
 
Jamaa anajua namba ila kaamua kubishana, na ukiendelea kubishana naye unaweza geuka victim wa matusi yake.

Hakuna kisingizio chochote cha kukatika umeme mara kwa mara, kila kitu kipo planned watu wapige pesa. Na architect wa michongo ndio huyo bwana January.
Umenena vyema mkuu
 
hahahah nimeona kuna mtu hapa kasema eti kipindi hiki wanaweka nguzo za zege hahahaha hivi wanafikiri watanzania ni wajinga sana eeh? yani wanataka kutudanganya kuwa nguzo za zege zimeanza kuwekwa kipindi cha Samia yani ndani ya hii miezi 6? hahahahahaha

Kwa hiyo mitambo ilikuwa ina muogopa Magufuli na kumsubiri Makamba aje ili ianze kuharibika na kufanyiwa mantainance hahahahaha
 
Na Tanesco ni yako kwani?

Au ya mwananchi yeyote yule?

Mnajidanganya!

Sasa wananchi tunataka umeme na yeye anazingua sababu anazotupa ni za kitoto…anatuona sisi mafala…atokeee wa nini..

Sio mgeni huyo kwa wananchi tunamjua hatuna imani nae….ATOKE
 
Makamba na Mwigulu ni contenders wa urais 2025,

wamepewa wizara zenye lawama technically ili wawe disqualified.

Hizo
Hakuna mwana CCM yoyote hatakaye dhubutu kutia 2025 zaidi ya Samia. Halafu Samia wana CCM watakuja kumwogopa zaidi ya Magufuli ni swala la muda tu!

Uchaguzi 2030 wote Makamba, Mwigulu na Ummy wana nafasi kubwa. Lakini wizara zao ndio mbinde.

Nina nina imani January ili tatizo la umeme atalimaliza lakini akifuata ushahuri wa kuingiza wawezekaji Tanesco itakuwa ni bomu litalomlipukia 2030!
January na Mwigulu hizo wizara zinaweza kuwamaliza wasipokuwa makini!
 
Walakini uko wapi, wakati unapewa jibu la kisomi...mlikuwa mnaongopewa huku mfumo mzima wa umeme unaharibika... Huwa nafikiria Hayati alikuwa na dhumuni gani na hii Nchi.
pumbavu

so hatupaswi kuwa na mfumo sahihi?? yaani sisi ni watu wa kukatikiwa umeme?

mama yako ana hasara sana
 
Walakini uko wapi, wakati unapewa jibu la kisomi...mlikuwa mnaongopewa huku mfumo mzima wa umeme unaharibika... Huwa nafikiria Hayati alikuwa na dhumuni gani na hii Nchi.
"usomi" uchwara huo...ni wizi tu tu!
Kwani mlitegemea nini Makamba afanye zaidi ya kuturudishia mawazo ya kuwa na jenereta?
Huyu bibi naona kafika ukomo kabisa....of all 60 mil people, Makamba!!?
 
Yaaano wakati wa kikwete miaka 10 ulikiwa unakatika kwa sbb walikiwa wanarepair,sasa bado unasema maoaka mitano umeme haukukatika kwa kuwa watu walikuwa wanaogopa kutumbulia..sasa walichorepair miaka 10 yakikwete ilikuwa ninini?
VERY smart argument...kwa ufupi ilikuwa balaa..kelele za majenereta kila sehemu ya nchi hii...anyways mwenye akili yeyote akikujibu plse tag me..ila kwa ufupi comment yako ni 5*. January anabebwa tu na viongozi ila hamna kitu. Dont expect much kwa mtu alipata zero form 4.
 
Namuelewa maana naona sehemu nyingi wanabadili nguzo kuwa za zege badala ya miti.
Hii nchi miaka mitano nyuma iliishi kwa propaganda kuliko Korea kaskazini, unafiki, uzandiki na uongo ambao mwisho wa siku tungekuja kugota sehemu ambayo tusingeweza kurudi nyuma.

Chukulia mfano tu wa jiji la Dodoma kukusanya mapato kuliko DSM, lakini mwaka huu ni la pili kutoka mwisho. Jiwe alikuwa juha kweri kweri

Yes Nchi iliishi kwa propaganda but hizo hizo propaganda zilifanya umeme usikatike ovyo ovyo.Tunazihitaji hizo propaganda tena kuliko sasa kuleta blah blah ambazo hazina mashiko na umeme si wa uhakika.

Hayo mengine ya ujuha wa mtu hata wewe hapa kwa comment yako waonekana ni juha haswa tena punguwani wahedi
 
Sasa wananchi tunataka umeme na yeye anazingua sababu anazotupa ni za kitoto…anatuona sisi mafala…atokeee wa nini..

Sio mgeni huyo kwa wananchi tunamjua hatuna imani nae….ATOKE
Inaumiza sana
 
hahahah nimeona kuna mtu hapa kasema eti kipindi hiki wanaweka nguzo za zege hahahaha hivi wanafikiri watanzania ni wajinga sana eeh? yani wanataka kutudanganya kuwa nguzo za zege zimeanza kuwekwa kipindi cha Samia yani ndani ya hii miezi 6? hahahahahaha

Kwa hiyo mitambo ilikuwa ina muogopa Magufuli na kumsubiri Makamba aje ili ianze kuharibika na kufanyiwa mantainance hahahahaha

Utawaweza hawa Chawa wa January? Kwamba nguzo za zege zimetengenezwa ndani ya miezi sita na kuanza kusimikwa.Hao ndio wanaomdanganya kuwa anafaa kuwa Rais na yeye bila aibu anajiona kweli atakuwa Rais wa JMT
 
Yes Nchi iliishi kwa propaganda but hizo hizo propaganda zilifanya umeme usikatike ovyo ovyo.Tunazihitaji hizo propaganda tena kuliko sasa kuleta blah blah ambazo hazina mashiko na umeme si wa uhakika.

Hayo mengine ya ujuha wa mtu hata wewe hapa kwa comment yako waonekana ni juha haswa tena punguwani wahedi
Baadhi ya watanzania wajinga unapoteza mda. Kipindi chote cha miaka 6 ya JPM umeme kukatika ilikuwa nadra sana. Na wakati anachukuwa nchi suala la umeme ilikuwa shida, umeme kukatika, mgao, sasa miaka 10 yote ya JK Tanesco walikuwa wanafanya repair? kama ilikuwa ni propaganda basi ziendelee sababu zilileta matokeo. Umeme ulikuwa haukatiki.
 
Back
Top Bottom