Japan yaipatia Tanzania mkopo wa Shilingi bilioni 761.8. Zanzibar yapata mgao wa Tsh bilioni 218

Japan yaipatia Tanzania mkopo wa Shilingi bilioni 761.8. Zanzibar yapata mgao wa Tsh bilioni 218

Nilichogundua humu JF, MACHOGO wengi hawana elimu ya uraia.

Hoja zao nyingi kuhusu Muungano ni kama wauza nyanya za mafungu magengeni.

Yaani inatia kinyaa kwa kweli.

Halafu mtu anajiona ametoa zinga la point.
Hoja zako zipo wapi?
Je, Zanzibar wana Bajeti ya Ulinzi , Mambo ya ndani, nje, Wizara za muungano na taasisi zake?

Je, mikopo inayochukua ambayo si tatizo, watarudisha kwa utaratibu gani?
Ikiwa hawawezi kumalizana na Tanesco, mabilioni wanayokopa nani atakayelipa? Mtanganyika!

Tunasema, wakati umefika turudi rasimu ya Warioba ya mambo 7 . Tanganyika isimame na kujisimamia na Zanzibar nayo ijisimamie ikakope mtrilioni kadri inavyoweza.
 
Ndio vizuri kwani anakumbatia Muungano ni Zanzibar au Tanganyika?

Pili mbona Zanzibar wanataka kujitenga, kwani hawayaoni hayo? Jibu ni kwamba huu ni uzushi na wao kwa uchache wao wanaona watafika mbali wakiwa peke yao.
Ndio maana tunasema waende kukopa wenyewe hata matrilioni 1000. Mbona wameuza visiwa je, umesikia Mtanganyika akizungumzia hilo.

Habari ya kupitia JMT halafu mzigo wanamwachia Mtanganyika ni mbaya sana.

Tusaidiane kuidai Rasimu ya Mzee Warioba na mambo 7 tu, tena kwasasa Wazanzibar mtasaidia sana maana Rais wa JMT na SMZ ni Wazanzibar! tusaidiane ili muwe huru kuijenga Dubai yenu na Tanganyika izibe mashimo ya barabara zake. Hii habari ya kubebeshana Bill inachosha!
 
Serikali ya Japan imeipatia Tanzania mkopo wa shillingi billion 761.8 kwaajili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo nchini!

Katika mkopo huo kisiwa cha Zanziba kimepewa mgao wa Tsh billion 218+

Kazi iendelee...

=====

View attachment 2108391

Serikali ya Tanzania na Japan zimesaini mikataba mitatu ya mkopo na msaada yenye thamani ya Yen za Japan bilioni 37.9 sawa na takriban shilingi bilioni 761.8 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ukarabati wa Bandari ya Kigoma, uboreshaji wa miundombinu ya maji Zanzibar na Ujenzi wa Barabara ya Arusha-Holili.

Mikataba hiyo imesainiwa jijini Dar es Salaam, kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Shinichi Goto pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan, Bw. Naofumi Yamamura, kwa naiaba ya Serikali ya Japan.

Akizungumza katika hafla fupi ya kusaini mikataba hiyo, Bw. Tutuba alisema kuwa Mradi wa ukarabati wa Bandari ya Kigoma utatekelezwa kwa msaada wa Yen za Japan bilioni 2.73 sawa na takriban shilingi bilioni 54.79, ukihusisha Ukarabati wa gati za mashariki na kaskazini mwa Bandari ya Kigoma, ukarabati wa majengo ya kushushia abiria na mizigo, ukarabati wa barabara zilizopo katika Bandari hiyo na ujenzi wa majengo mapya ya abiria na mizigo.

“Bandari ya Kigoma ilijengwa katika kipindi cha mwaka 1912–1927 na imekuwa bandari muhimu katika kusafirisha mizigo na abiria kwenda nchi jirani za Burundi, DR Congo, Zambia na mikoa iliyopakana na Kigoma, hivyo kukamilika kwa utekelezaji wa mradi huo kutachangia kuongeza ufanisi wa Bandari, kutoa fursa za ajira, kupanua wigo wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali, kuchochea shughuli za kiuchumi na kuchochea biashara kati ya Tanzania na nchi hizo jirani” alisema Bw. Tutuba

Alisema kuwa Mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Maji Zanzibar, utatekelezwa kwa mkopo wa masharti nafuu wa kiasi cha Yen za Japan bilioni 10.86 sawa na takriban shilingi bilioni 218.382 ambapo mradi huo utahusisha kujenga na kukarabati miundombinu ya maji Mjini Zanzibar.
Ukigawanya kila mkoa wa bara utapata bil 22, mfano tabora irapata bil 22 wakazi zenji inalamba bil 231
 
Serikali ya Japan imeipatia Tanzania mkopo wa shillingi billion 761.8 kwaajili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo nchini!

Katika mkopo huo kisiwa cha Zanziba kimepewa mgao wa Tsh billion 218+

Kazi iendelee...

=====

View attachment 2108391

Serikali ya Tanzania na Japan zimesaini mikataba mitatu ya mkopo na msaada yenye thamani ya Yen za Japan bilioni 37.9 sawa na takriban shilingi bilioni 761.8 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ukarabati wa Bandari ya Kigoma, uboreshaji wa miundombinu ya maji Zanzibar na Ujenzi wa Barabara ya Arusha-Holili.

Mikataba hiyo imesainiwa jijini Dar es Salaam, kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Shinichi Goto pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan, Bw. Naofumi Yamamura, kwa naiaba ya Serikali ya Japan.

Akizungumza katika hafla fupi ya kusaini mikataba hiyo, Bw. Tutuba alisema kuwa Mradi wa ukarabati wa Bandari ya Kigoma utatekelezwa kwa msaada wa Yen za Japan bilioni 2.73 sawa na takriban shilingi bilioni 54.79, ukihusisha Ukarabati wa gati za mashariki na kaskazini mwa Bandari ya Kigoma, ukarabati wa majengo ya kushushia abiria na mizigo, ukarabati wa barabara zilizopo katika Bandari hiyo na ujenzi wa majengo mapya ya abiria na mizigo.

“Bandari ya Kigoma ilijengwa katika kipindi cha mwaka 1912–1927 na imekuwa bandari muhimu katika kusafirisha mizigo na abiria kwenda nchi jirani za Burundi, DR Congo, Zambia na mikoa iliyopakana na Kigoma, hivyo kukamilika kwa utekelezaji wa mradi huo kutachangia kuongeza ufanisi wa Bandari, kutoa fursa za ajira, kupanua wigo wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali, kuchochea shughuli za kiuchumi na kuchochea biashara kati ya Tanzania na nchi hizo jirani” alisema Bw. Tutuba

Alisema kuwa Mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Maji Zanzibar, utatekelezwa kwa mkopo wa masharti nafuu wa kiasi cha Yen za Japan bilioni 10.86 sawa na takriban shilingi bilioni 218.382 ambapo mradi huo utahusisha kujenga na kukarabati miundombinu ya maji Mjini Zanzibar.
We need to step up,mikopo hii kidogo ni aibu
 
Kwani huu Muungano sisi tunaung'ang'ania una faida gani na sisi, kidhati kabisa mie sioni faida kwetu kwenye huu muungano, halafu kibaya zaidi ni sisi ndio tunafosi, wazanzibar wakitaka nchi yao inakuwa msala.
Kwa hili,tunaomba tuwaaxhe jamaa waende zao.no longer material,wale wazee waliwaza nini jamani kwenye muungano
 
Ndio maana tunasema waende kukopa wenyewe hata matrilioni 1000. Mbona wameuza visiwa je, umesikia Mtanganyika akizungumzia hilo.

Habari ya kupitia JMT halafu mzigo wanamwachia Mtanganyika ni mbaya sana.

Tusaidiane kuidai Rasimu ya Mzee Warioba na mambo 7 tu, tena kwasasa Wazanzibar mtasaidia sana maana Rais wa JMT na SMZ ni Wazanzibar! tusaidiane ili muwe huru kuijenga Dubai yenu na Tanganyika izibe mashimo ya barabara zake. Hii habari ya kubebeshana Bill inachosha!
Aliyekwambia hawawezi Kukopa nani? Wakitaka Kukopa wanalazimika kuomba kibali Bara,na Bara ndio wanatoa final decision..

Binafsi napenda Zanzibar ikae peke yake Ili iwe kama Dubai tuache kufuata mizigo mbali huko wakati tunaweza ifuata hapo Zanzibar tuu.
 
Hivi tutakapoanz kulipa mkopo Zanzibar nayo italipa fungu lake au ni bara tu itakayobeba mzigo wa deni?
Inayokopa ni Tanzania.
Inayolipa au kutakiwa kulipa ni Tanzania hiyo hiyo.
Hakuna sehemu Tanganyika au Zanzibar inalipa au itatakuwa kulipa madeni yaliyokopwa na TANZANIA.

Mkitaka kuhuisha hizo ndogo zenu kwanza vunjeni Muungano kila nchi iwe huru, halafu kama mnaona bado Muungano mnauhitaji anzisheni shirikisho full stop


Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Well,kwani kuna tatizo gani kwasasa? Rais si Mzanzibar

Hii habari ya kuondoka si njema maana nusu ya Wazanzibar wanaishi bara , wanakila haki
Ipo siku utaangali nyuma na kujutia

Sasa kama Zanzibar inaelewa haina sovereign, kwanini Othman Masoud, AG wakati huo aliongoza jitihada za kutaka Zbar ipewe nafasi ya kukopa? Je, CUF hawakuwa na uelewa?
Unataka kusema AG wa Zanzibar na VP kwasasa hakuwa na weledi unaousema?

Kwasasa Zbar si ina SMZ na taasisi zake sasa nini kinashindika kusema hawataki muungano?
Muungano tukiuvunja Wazanzibari wanaoishi bara watakuwa kama Wazanzibari wanaoishi UK, US, Canada, Sweden, Afrika Kusini n.k. Watahesabika kama Wazanzibari wengine wa diaspora, watakaribishwa nyumbani wasaidie kuwekeza na kujenga nchi. Michango yao itahitajika sana kuendeleza na kujenga Zanzibar. Mkiwafukuza huko watahamia nchi nyingine au watarudi nyumbani. Si unaona jinsi Wayahudi dunia nzima wanavyoisadia Israel kupata maendeleo?

SMZ inatambulika na CCM tuu. Haitambuliki umoja wa mataifa (UN), haitambuliki Arab League, haitambuliki pengine popote. Vunja rasmi huo unaoita muungano Zanzibar ijiendeshe. Nyie machogo mliochoka na muungano wapeni ushauri watu wa CCM waache fikra kama za huyu hapa

 
Sawa,suala hapa ni kwenye marejesho ya mkopo,Je Zanzibar inajilipia mkopo iliochukua Kwa koti la Muungano?
Suala kutengana ni sawa,ila CCM hawataki!Wananchi tulipendekeza Muungano wa serikali 3 ila CCM kazuia Kwa nguvu zote!
Huu muungano sioni hata faida yake Kwa mtanganyika!
Hapa nakuunga mkongo. Ukiwauliza wanaoulinda huo muungano umeleta faida gani hawana majibu. Umaskini Zanzibar umezidi. Zanzibar ingeungana na nchi mama yao Oman leo hii Zanzibar ingekuwa kama Muscat. Utajiri wa mafuta ungechuruzika mpaka kufika Zanzibar. Makosa ni kuungana na nchi fukara iliyoitwa Tanganyaika iliyojaa watu wenye ukabila, ukanda, udini, ubaguzi, ufukara wamebaki kuirudisha nyuma Zanzibar na siasa chakavu.

#FreeZanzibar
 
Back
Top Bottom