Uchaguzi 2020 Japo inaniuma lakini kwa kuwa chama changu mmeendekeza sana ubabe sitawapa kura yangu

Uchaguzi 2020 Japo inaniuma lakini kwa kuwa chama changu mmeendekeza sana ubabe sitawapa kura yangu

gimmy's

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2011
Posts
3,312
Reaction score
3,345
Ndugu zangu mimi ni CCM tangu udogo wangu na mwenye kadi hai kabisa nikiwa na maana kadi yangu nailipia kila mwaka.Nilijiunga CCM rasmi kwa maana yakuchukua kadi ya uanachama 2019 mara baada yakufika chuoni mwaka wa kwanza.

Nasisitiza sitahama chama changu kwa kuwa CCM naipenda toka moyoni ila nitakachofanya ni kuwaadhibu kwa kura viongozi kwa mwenendo usiofaa na sina sehemu nyingine yakuwaadhibu zaidi ya sanduku la kura.

Nafanya hivi kwakuwa nimekosa namna tofauti kwani viongozi hawataki kushauriwa wanahisi wao ni malaika lakini watambue awamu ya tano imetesa sana wananchi kuliko hata mkoloni.

Nasisitiza kutumiiza kwakigezo cha ndege, madaraja, umeme, maji nk sio sawa, hali ya maisha imekua ngumu sana huku mtaani.

Nakumbuka yupo mwananchi mmoja alidiriki kumwambia rais kwa uchungu,"mheshimiwa ruhusu pesa hali huku mtaani ni ngumu sana". Majibu ya rais ,"Asiyefanya kazi na asile". Hili sio jibu la kiongozi kwa mwananchi wake badala yake raisi alitakiwa kuwaza kwamba kuruhusu pesa sio kuwapa wananchi pesa mfukoni bali ruhusu ajira serikalini,ondoa kodi za hovyohovyo siku hizi faini imekuwa chanzo cha mapato kuliko hata VAT.

Yote kwa yote huu ni msimamo wangu na sitahama chama changu ila kwa mwaka huu kura mtanisamehe sitapiga kura CCM.

Wakati sisi tunapata tabu na tukiwaambia mnatujibu vibaya nyinyi mnaishi kwa raha na mnajisahau kuwa hio raha mnayoishi nyinyi chanzo ni sisi kuwapigia kura.
Kwa mwenye hofu na mimi juu ya mapenzi yangu kwa CCM apitie post zangu za nyuma.
 
Ushasema ubabe...unadhani hio kura yako itasaidia kitu.....mwendo ni ubabe kura yako kafungie andazi
 
kinachouma zaidi unajua kabisa ccm itashinda mbali na hatua utakayochukua.
 
gimmy's, pole sana kijana, najua hali ya sasa ilivyokukatisha tamaa na nakuhakikishia hauko peke yako. Tofauti na wewe mimi ni kati ya wale ambao toka awali kabisa, tulimkataa kiongozi wetu wa sasa.

Nakukaribisha utuunge mkono katika juhudi zetu za kuuondoa madarakani utawala huu wa kibabe usiozingatia sheria, usiopenda kukosolewa, usiotaka kushauriwa, usiojali utu na uliokosa busara na hekima.

Silaha pekee tuliyo nayo ni kura yetu na tuitumie vema tarehe 28/10/2020. Kumbuka kosa si kosa bali kurudia kosa.
 
Rais ni kama mzazi anapaswa kuwapa tumaini raia wote. Wapo wana ccm wengi wenye hekima hawapendezwi na kauli za mkuu za kibaguzi na dhihaka." Siwafichi" " Mtajuta" " Huwezi kunijibu hivyo wewe" ( Mama DED BK, kupoteza uteuzi kutotaja fungu kiasi barabara akihofia kuposha); " Niliahidi mafuriko" ..." Wa mabondeni wafurike... wauzieni nei kubwa" " siwezi mchagua DED nimpe gari,nyumba,mshahara halafu amtangaze mpinzani" " Hakuna fidia" .." Mtajuta" " Pesa zipo nakamua mafisadi na majizi"( wafanyabiashara).
 
Raisi kuruhusu peasa mtaani siyo kugawa fedha cash kwa watu ni kutumia mbinu za kiuchumi ili kuongeza mzunguko wa fedha: Mbinu za kiuchumi ni Sera ya Fedha " Monetary Policy na Sera ya Kodi " Fiscal Policy"

Monetary policy refers to central bank activities that are directed toward influencing the quantity of money and credit in an economy. By contrast, fiscal policy refers to the government’s decisions about taxation and spending. Both monetary and fiscal policies are used to regulate economic activity over time.

They can be used to accelerate growth when an economy starts to slow or to moderate growth and activity when an economy starts to overheat. In addition, fiscal policy can be used to redistribute income and wealth.
 
Ushasema ubabe...unadhani hio kura yako itasaidia kitu.....mwendo ni ubabe kura yako kafungie andazi
Mhindi akiwa na duka anasalimia majirani zake wote na kuwafanya wateja wake. Wenyewe wanasema “ every penny counts “ hapa ni kuwa “every vote counts”.
 
Ndugu zangu mimi ni CCM tangu udogo wangu na mwenye kadi hai kabisa nikiwa na maana kadi yangu nailipia kila mwaka.Nilijiunga CCM rasmi kwa maana yakuchukua kadi ya uanachama 2019 mara baada yakufika chuoni mwaka wa kwanza.

Nasisitiza sitahama chama changu kwa kuwa CCM naipenda toka moyoni ila nitakachofanya ni kuwaadhibu kwa kura viongozi kwa mwenendo usiofaa na sina sehemu nyingine yakuwaadhibu zaidi ya sanduku la kura.

Nafanya hivi kwakuwa nimekosa namna tofauti kwani viongozi hawataki kushauriwa wanahisi wao ni malaika lakini watambue awamu ya tano imetesa sana wananchi kuliko hata mkoloni.

Nasisitiza kutumiiza kwakigezo cha ndege, madaraja, umeme, maji nk sio sawa, hali ya maisha imekua ngumu sana huku mtaani.

Nakumbuka yupo mwananchi mmoja alidiriki kumwambia rais kwa uchungu,"mheshimiwa ruhusu pesa hali huku mtaani ni ngumu sana". Majibu ya rais ,"Asiyefanya kazi na asile". Hili sio jibu la kiongozi kwa mwananchi wake badala yake raisi alitakiwa kuwaza kwamba kuruhusu pesa sio kuwapa wananchi pesa mfukoni bali ruhusu ajira serikalini,ondoa kodi za hovyohovyo siku hizi faini imekuwa chanzo cha mapato kuliko hata VAT.

Yote kwa yote huu ni msimamo wangu na sitahama chama changu ila kwa mwaka huu kura mtanisamehe sitapiga kura CCM.

Wakati sisi tunapata tabu na tukiwaambia mnatujibu vibaya nyinyi mnaishi kwa raha na mnajisahau kuwa hio raha mnayoishi nyinyi chanzo ni sisi kuwapigia kura.
Kwa mwenye hofu na mimi juu ya mapenzi yangu kwa CCM apitie post zangu za nyuma.

Safi sana, mimi napenda sana watu wenye mawazo huru ambao misimamo yao haibase kwenye ushabiki kama wa Simba na Yanga bali kwenye issues.

Utawala wa awamu ya tano ni utawala uliojaa kiburi na jeuri ya mamlaka, umebomolea watu nyumba kwa ukatili wa kutisha, umetumbua watu hadharani bila staha za inidhamu za kikiazi zilizoko kisheria, ni dhalimu umeharibu chaguzi serikali za mitaa, umebambikizia watu kesi, kupora hela za wafanyabiashara kwa kuwafungulia kesi nzito za uhujumu uchumi and then kuwaambia watoe hela wawaachie, Hauheshimu utawala wa sheria, unapoka hata mamlaka za bunge kwenye kuidhinisha matumizi, Umeminya uhuru wa habari na kulazimisha vyombo vyetu vya habari kuwa ama Kasuku wa kuimba sifa za Jiwe, Watu wametekwa na kupotezwa katika utawala huu, Utawala huu una kauli chafu hasa dhidi ya wanawake. Diplomasia yetu imeyumba chini ya utawala huu, Utawala ulioonea wakulima wa korosho kwa kupora korosho zao. Ni utawala unaonuka udini, teuzi za utawala huu zinekaa kidini mpaka aibu, Pia ni utawala wa kiunduguization na ukabila, mtoto wa dada ndiye paymaster wa serikali, Miradi mikubwa inafanywa na mtu waliyeoa nyumba moja na jiwe!.

Ni utawala wa kudhibiti dhibiti watu

Kiufupi umefanya jambo la maana kuukataa utawala huu dhalimu.

Yeyote ambaye hajafanya maamuzi afanye tafakuri yeye mwenyewe bila ushabiki wa ukada wa kivyama, Atagundua kuwa utawala huu umepwaya sana!
 
Back
Top Bottom