Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Ni mjakazi wa Sara,kwa mujibu wa bible ndiyo maana akampa Ibrahim apige,na ndiyo maana Ibrahim anasema 'mjakazi wako'..
 
Amesema nani alitakiwa kuchinjwa?
Hakuna yeyote aliyetakiwa kuchinjwa, watafsiri wa Qur'an wamekosea sana tafsiri, sijuwi hilo la kuchinjwa mtoto wamelitowa wapi.


Nijuavyo limetumika neno "dhabih" ambalo kitafsida linamaanisha kukatwa jando.

MAJIBU YA FAIZFOX HAYO
 
Kuna din inilikuja miaka 650 baada ya dini kongwe kuwepo

Ilibidi wakopy na kuedit mambo ya watangulizi wao

Kuna nabii wa mwisho alimaliza Kila kitu, sidhani kama nabii mwingine angelkuja baadaye miaka 650 na jambo jipya.

Huyu nabii alituachia amri kuu ya upendo akisema mpende jirani yako kuliko unavyojipenda

Kwa kutambua kuwa binadamu alimkosea Mungu ilihitaji upatanisho wa damu akakaamua kujitoa afe atoe damu ili awakomboe binadamu kwa damu yake

Wale wa copy and paste hii iliwashinda ikabidi waamrishe kuchinja wanyama kama ibaada ya kafara yao ya upatanisho

Lakini wasichojua Hawa wakuiga ni kwamba Mungu wa mbingini alishaachana na utaratibu wa kusamehe nakutoa Baraka kwa kafarara ya damu za wanyama

Ibaada za Kuchinja wanyama ni kupotea kiimni
 
Umese
Umesema Sinai iko Arabuninya Saudia?
 
Hakuna yeyote aliyetakiwa kuchinjwa, watafsiri wa Qur'an wamekosea sana tafsiri, sijuwi hilo la kuchinjwa mtoto wamelitowa wapi.


Nijuavyo limetumika neno "dhabih" ambalo kitafsida linamaanisha kukatwa jando.
Kukatwa Jando sio Dhabih faiza!

Hapo nitawatetea Waislam unawaonea..
Neno "khitan" au huandikwa kiarabu "ختان" ndo humanisha Jando au Kutairiwa na mtu aliyetahiriwa Huitwa "Makhtun"

Na Faiza Huwa unasoma Quran yako??
Nifatilize..

Soma Surah As-Saffat aya ya 102

فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعْىَ قَالَ يَٰبُنَىَّ إِنِّىٓ أَرَىٰ فِى ٱلْمَنَامِ أَنِّىٓ أَذْبَحُكَ فَٱنظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِىٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ


Inatamkwa hivi ..

"Falamma balagha maAAahu alssaAAya qala ya bunayya innii ara fii almanami annee athbahuka faunthur matha tara qala ya abati ifAAal ma tumaru satajidunii in shaa Allahu mina alssabiriina"

Ambayo maana yake ni hii..

Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.

nimeshangaa Kuona Neno أَذْبَحُكَ inatamkwa adhbahuka..... Unasema Tafsiri yake ni Jando ulisoma Wapi Arabic Grammar walizokufundisha hivyo??? mpaka kesho Hilo neno Humaanisha Kuchinja Au kuua Wewe umepata wapi maana tofauti na hiyo..
 
Dini kongwe dini gani?..unajua bible ilikuwepo kabla hata yesu hajazaliwa!?
 
Unasema Hakuwa mke ila biblia Inasema alikuwa Mke sasa Tumuamni nani weeewe Au biblia unayoifuata au ulipotoa kisa...?

Bilha na zilpa wana status tofauti na Hajiri na ndo maana Umeona anadiskasiwa kwa mapana..

Nakurudisha tena kusoma Mwanzo 16:3 ambayo huchangii chochote kuihusu..

Mwanzo 16:3

"Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe."

And Sarai Abram's wife took Hagar her maid the Egyptian, after Abram had dwelt ten years in the land of Canaan, and gave her to her husband Abram to be his wife.


Hakuna Kijakazi yoyote Aliwahi kupewa Hii status Kwenye Biblia kama ulimpata Nionyeshe Andiko nijifunze kitu kipya ambaye alikuwa kijakazi halafu akaitwa mke

Nimekujibu kwamba Sheria Za kiyahudi au sheria za kiebrania zimepitia Mapito mengi sana Na zimekuwa zikibadilisha na kutiliwa mkazo...

Sheria za Musa na torah na Sheria za Halakha (Sheria za sasa za kiyahudi) ni tofauti na sheria kipindi cha Ibrahimu na kina Yakobo..

Ni sawa ufananishe Sheria ya Kipindi cha Kinjikitile ngwale na kipindi hiki cha sasa Eti kwa sbabu tu zote ni Tanganyika ....Hapana..
 
Mkuu mimi nimekuelewa! Kuna watu wanaofundishwa Ukweli na kuna watu wanaodanganywa!
Lakini Mungu nayemfahamu ni Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa ISAKA na Mungu wa Yakobo alijitambulisha kwa Musa kuwa
(Kutoka 3:6)-Mimi ni Mungu wa baba zako,na Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.
Sifahamu kama Mungu wa Ibrahimu alijidhihrisha kama ni Mungu wa Ishmael!
Lakini Biblia imeweka wazi kabisa kuwa mtoto aliyetolewa na Ibrahimu kama Sadaka ya kuteketezwa kwa agizo la Mungu mwenyewe ni Isaka,(Mwanzo22:1-14)
Kwa habari ya Ishmael Mungu alimwambia Ibrahimu aisikilize sauti ya mkewe Sarah amfukuze Hajir kijakazi na Ishmael kwa sababu hatarithi pamoja na Isaka, katika Isaka uzao wa Ibrahimu utaitwa,
(Mwanzo21:10-12)
Mwisho Mungu siyo kigeugeu hata kwenye Biblia aseme hivi harafu ageuke aseme vile kwenye Quran!
Ili kuleta amani kila mtu afuate mafundisho ya dini yake.
 
Sifahamu kama Mungu wa Ibrahimu alijidhihrisha kama ni Mungu wa Ishmael!
Lakini Biblia imeweka wazi kabisa kuwa mtoto aliyetolewa na Ibrahimu kama Sadaka
Qur'an imefutwa hio ikaandikwa Mungu wa Ishmael na vizazi vyake waliofuatia maana Bible haijamzungumzia Ishmael hivyo
 

Ishmael hakupewa urithi ila sikatai alibarikiwa na Mungu na pia alimzika Babaake
 

Tumia Quran iliyoandikwa na waarabu.
Sijakuzuia Mkuu.

Unajua Fika kuwa Quran hazijitoshelezi na hata nikikuulizà maswali quran haiwezi kujibu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…