Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Hebu tupe mchanguo wa urithi ulikuaje? si ndo nyie mnasema Hajra na mwanawe (Ismael) walifukuzwa akiwa bado ni mtoto mchanga?

kwahiyo tuelezee urithi alipewa walipofukuzwa ama Ismail alirudi kudai urithi alipokuwa mkubwa ama Ibrahim alienda kumpa urithi huko walikopotelea baada ya kufukuzwa.
Mwanzo 21:8-21

[8]Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya; Ibrahimu akafanya karamu kuu siku ile Isaka alipoachishwa kunyonya.

[9]Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.

[10]Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.

[11]Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.

[12]Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.

[13]Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.

[14]Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.

[15]Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.

[16]Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.

[17]Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.

[18]Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.

[19]Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.

[20]Mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.

[21]Akakaa katika jangwa la Parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya Misri.
 
Sijui mnaamaanisha nini kubishana.
Biblia imeandika hivi
.............
Mwanzo 22
1 Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.

2 Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.

3 Ibrahimu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu.

4 Siku ya tatu Ibrahimu akainua macho yake, akapaona mahali pakali mbali.

5 Ibrahimu akawaambia vijana wake, Kaeni ninyi hapa pamoja na punda, na mimi na kijana tutakwenda kule, tukaabudu, na kuwarudia tena.

6 Basi Ibrahimu akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja.

7 Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinena, Babangu! Naye akasema, Mimi hapa, mwanangu. Akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?

8 Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. Basi wakaendelea wote wawili pamoja.

9 Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko, akaziweka tayari kuni, kisha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.

10 Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.

11 Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.

12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.

13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.

14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa BWANA itapatikana.

15 Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni

16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

18 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.

19 Basi Ibrahimu akawarudia vijana wake, wakaondoka, wakaenda zao pamoja mpaka Beer-sheba; Ibrahimu akakaa huko Beer-sheba.
..................
Kisa hicho hakisemi popote kuwa Isaka alitolewa sadaka ya kuchinja.

Naomba wanaodai kuwa Ismael alitolewa sadaka
ya kuchinja, watuwekee hicho kisa hapa kama mimi nilivyoweka.
Ikiwa tutaegemea kwenye maandiko tu tukubaliane kutokukubaliana kwa kuwa kila imani imendika kikiwa kinatofautiana na kingine. Tunachopaswa ni kujadili content ya kilichoandikwa hapo ndo tutaelewa kipi kinasema ukweli na kipi ndani yake ukweli umepindishwa.

Kauli ya kusema mtoto wa pekee, Isaac ... hii unai-reconcile vipi na fact ya kuwa Isaac ni mtoto wa pili baada ya kuwa Ibrahim tayari alishakuwa na mtoto mwengine Ismail?
 
Ikiwa tutaegemea kwenye maandiko tu tukubaliane kutokukubaliana kwa kuwa kila imani imendika kikiwa kinatofautiana na kingine. Tunachopaswa ni kujadili content ya kilichoandikwa hapo ndo tutaelewa kipi kinasema ukweli na kipi ndani yake ukweli umepindishwa.

Kauli ya kusema mtoto wa pekee, Isaac ... hii unai-reconcile vipi na fact ya kuwa Isaac ni mtoto wa pili baada ya kuwa Ibrahim tayari alishakuwa na mtoto mwengine Ismail?
mtoto wa pekee kwenye ndoa ya Ibrahimu na Sarah, Maana baada ya Sara kufa Ibrahim alioa mwanamke mwingine naye akamzalia watoto wengine
 
Ikiwa tutaegemea kwenye maandiko tu tukubaliane kutokukubaliana kwa kuwa kila imani imendika kikiwa kinatofautiana na kingine. Tunachopaswa ni kujadili content ya kilichoandikwa hapo ndo tutaelewa kipi kinasema ukweli na kipi ndani yake ukweli umepindishwa.

Kauli ya kusema mtoto wa pekee, Isaac ... hii unai-reconcile vipi na fact ya kuwa Isaac ni mtoto wa pili baada ya kuwa Ibrahim tayari alishakuwa na mtoto mwengine Ismail?
Na Isaka ndiye mtoto wa Agano kwa watoto wote wa Ibrahimu
 
Wanabodi,
Leo ni sikukuu ya Eid El Haji, Iddi ya Kuchinja.

Leo ni siku ya Sikukuu ya Idd El Haj, ni iddi ya kuchinja, asubuhi nilikuwa naangalia matangazo ya mubashara ya Baraza la Iddi kupitia TBC, kutoka Msikiti wa Mfalme Mohammed VI wa Morroco, Bwakwata, Kinondoni jijini Dar es Salaam, kumbe Msikiti Mkuu wa Bakwata, sasa umebadilishwa jina!, na kupewa jina la Mfalme wa Morroco!.

Mgeni rasmi kwenye Baraza la Iddi ni Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, ambaye ameandamana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye amesilimishwa na kupewa jina la Aboubakar Chalamila!, na mawaziri akiwemo Waziri Mhe. Mohamed Mchengerwa. Baadhi ya watu maarufu niliowaona ni pamoja na Alhaj Sheikh Ali Nguruko, Alhaj Chande, Idda Azan, Shaweji Abdalah, Salum Mwalimu, Juma Simba Gadafi, Salum Abladaha "TRY Again", Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Mruma, Kadhi wa Dar es Salaam, Shamin Khan, mwenyekiti wa JUAKITA, pia kulikuwa na mabalozi wa Balozi wa Moroko, na wa Comoro.

Katika salam zake, Sheikh Aboubakar Chalamila alisema utulivu wa jiji la Dar es Salaam, unawategemea sana viongozi wa Dini.

Salaam za Waislamu, zimetolewa na Alhaj Sheikh Nuru Mruma, Katibu Mkuu wa Bakwata ambaye amewasisitiza Waislamu kudumisha amani na kuilinda amani. Wazazi watakiwa kulea watoto wao kwa tabia njema, kujenga taifa la kizazi cha watu wema ambao hawatapokea rushwa wala kufanya ufisadi.

Amesema kupanda miti na utunzaji wa mazingira ni ibada muhimu kwa Waismamu wote.

Pia amewataka Waislamu kujitokeza kwa wingi, kujiandikisha kwenye uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.
na wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya kidemokrasia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Salaam za Mufti, zimetolewa na Kaimu Mufti Sheikh Ali Muhidin Mporogore, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, Bwakwata. Aamezungumzia Watanzania tutafakari, sadaka ya kuchinja siku ya Iddi El Haj, ni iddi ya kuchinja. Zamani ilikuwa sio kuchinja tuu wanyama, bali walichinja hata binadamu ana akatolea mfano Sadaka ya Nabii Ibrahim kutaka kumtoa mwanae Ismail, kwa sadaka ya kuchinja.

Hakuna ubishi kuhusu Wakristo na Waislamu, kuwa ni watoto wa Baba mmoja, Nabii Ibrahim hivyo huu ni uthibitisho wa Mungu wa Wakristo na Waislamu ni Mungu Mmoja, ila kuna watu wanafundishwa ukweli na kuna watu wanadanganywa!.

Hakuna ubishi kuwa mtoto wa kwanza wa Ibrahim ni Ismail aliyezaa na mjakazi wa Kimisri, Hagir, na Isaka ni mtoto wa pili wa Ibrahim, aliyemzaa na mkewe Sarah.

Hakuna ubishi Ibrahim alitaka kumtoa mtoto wake Sadaka ya kuchinja.

Waislamu na Kitabu chao Kitukufu cha Quran Tukufu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Ismail.
Wakristo na Kitabu chao Kitakatifu cha Biblia Takatifu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Isaka.

Jee ukweli halisi ni upi?.
Hii maana yake
Kama tukio la Ibrahim kutaka kumchinja mwanae kumtoa sadaka ni tukio moja, then
1. Hii maana yake ni kuna watu wanadanganywa, haiwezekani kwa Waislamu mtoto huyo awe ni Ismail na kwa Wakristu mtoto huyo awe ni Isaka, hii maana yake kuna kitabu hapo kinasema kweli na kuna kitabu kinasema uongo!, jee ukweli ni upi?.

Umuhimu wa kuujua ukweli huu, unakupa fursa ya kujua ukweli ni upi, hivyo ufuate mafundisho yapi ambayo ndio mafundisho ya kweli!.

Bandiko hili linakutaka kwanza uwe open minded, kama wewe ni mfia dini, unaamini dini yako ni ya ukweli mtupu, bandiko hili halikufai.

Pili unatakiwa uwe na ngozi ngumu ya kuukubali ukweli halisi hata uwe mchungu vipi!, ikitokea ni dini yako unayoiamini kuwa ni dini ya kweli, kumbe ni dini ya uongo, uwe na uwezo wa kustahimili maana...

Nawatakia Waislamu wote,
Iddi Mubarak njema ya kuchinja.

Paskal
MUNGU WA WAKRISTO NA WA WAISLAMU NI MIUNGU MIWILI TOFAUTI KABISA. HAWAFANANI HATA KIDOGO. SIFA ZAO NI TOFAUTI NA HATA MBINGU ZAO NI TOFAUTI.
 
Mimi nina swali kwako Che Mittoga !

Kipindi Isaka anazaliwa Ishamael alikuwa na miaka mingapi?
Biblia haijaandika hiyo miaka.

Mimi nimeomba andiko linalo mtaja kwa jina Ismaeli kutolewa sadaka maana sijawahi kuliona popote.
Na nimeweka andiko la Mwanzo 22: likimtaja Isaka.
Kutokana na Biblia.
Ismaeli aliondoka nyumbani kwa Ibrahimu katika Mwanzo 21: kabla ya Mungu kumjaribu Ibrahimu amtoe sadaka Isaka.
Ina maana Ibrahimu aliambiwa hivyo wakati Ismaeli kesha ondoka na mama yake Hajiri kwa Ibrahimu.

Hivyo lingewekwa kwanza hilo andiko linalo mtaja Ismaeli kwa jina lake kutolewa sadaka ndio tuendelee kujadili hii mada.
La sivyo haitakuwa na mantiki.

Katika visa vya Biblia mtoto wa kwanza mala nyingi tu tunasoma anakosa urithi anaostahili.
Esau alikosa baraka kama mtoto wa kwanza na akapewa Yakobo mdogo wake, Nk.
 
Surah Al-saffat (37), soma kuanzia aya ya 99 mpaka ya 113.

Baadaya kukombolewa huyo mtoto alitaka kumchinja then immediately Quran inasema na tukambashiria Ibrahim kupata mtoto amnbaye ni Isaac (ametajwa kwa jina). So it's clear that amepewa bishara ya kumpata Isaac baada ya kukombolewa mtoto wa kwanza halafu then ubakie unasema bado aliyetaka kuchinjwa ni Isaac wakati tukio la kutaka kuchinjwa mtoto lilikuja kabla ya Isaac kuzaliwa.

Iweke hiyo aya hapa.
Ushahidi unaletwa mahakamani na sio mahakama kuufuata
 
Mwanzo 21:8-21

[8]Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya; Ibrahimu akafanya karamu kuu siku ile Isaka alipoachishwa kunyonya.

[9]Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.

[10]Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.

[11]Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.

[12]Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.

[13]Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.

[14]Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.

[15]Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.

[16]Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.

[17]Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.

[18]Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.

[19]Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.

[20]Mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.

[21]Akakaa katika jangwa la Parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya Misri.
What a contradiction! ... yani katika same story line Mungu awe upande wa Sara kutaka kumnyima urithi Ismail na kubariki kuwa afukuzwe yeye na mama yake lakini huko walikopotelewa akawatendee miujiza ya kuwaletea kisima cha maji palipokuwa hakuna maji ili kumuokoa huyo mtoto.

Something doesn't add up to this story, ila ukiwa open minded utagundua kuwa Mungu amewatukuza watoto wote wa Ibrahim hapo then nyinyi mnapata wapi biasness ya kumchagua Isaac na mkamkataa Ismail?

Ila sijaona mgao wa urithi hapo, au ndo kile kiriba cha maji walichopewa?
 
Rejea kwenye video,

View: https://youtu.be/79NTc1Qfgrw

  1. anzia dakika ya 43
  2. MC anamuita mtu wa ku recite Quran
    .Ustaadh anakuja na ku recite kwa Kiarabu kwa muda wa dakika 6 mpaka dakika ya 49

    Kisha msikilize Kaimu Mufti Sheikh Ali Muhidin Mporogore, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, Bwakwata akitafsiri kwa lugha ya Kiswahili maneno ya Quran kuhusu kuchinja.
    P

Nimesikiliza "qari" yaani msomaji, kasoma Surat Saffat aya ya 100 mpaka aya ya 105. Nimesikiliza na aliyepewa kutafsiri, hapo ndipo alipoboronga. Na yeye kwa kuwa anajuwa anahokisema akamsukumia mtafsiri mwengine aitwae Ibn kathir, akasema huyo mtafsiri ndiye kasema huyo mtoto ni "Ismail". Hayo Yanabaki kuwa ni maneno ya mtafsiri (commentator) na siyo ya Qur'an.

Maana yake nini hiyo? Maana yake hakuna katika hizo aya zilizosomwa alipotajwa Ismail.

Ndiyo maana post ya juu huko nikasema yamepachikwa maneno kutoka nje ya Qur'an. Hata wewe ukiisikiliza aya inaposomwa hutosikia jina la Ismail, hilo utalisikia kutoka kwa "mtafsiri (commentator). Kayatowa wapi hayo aliyoongezea kama hayapo kwenye Qur'an? Hilo ndilo swali la kujiuliza.
 
What a contradiction! ... yani katika same story line Mungu awe upande wa Sara kutaka kumnyima urithi Ismail na kubariki kuwa afukuzwe yeye na mama yake lakini huko walikopotelewa akawatendee miujiza ya kuwaletea kisima cha maji palipokuwa hakuna maji ili kumuokoa huyo mtoto.

Something doesn't add up to this story, ila ukiwa open minded utagundua kuwa Mungu amewatukuza watoto wote wa Ibrahim hapo then nyinyi mnapata wapi biasness ya kumchagua Isaac na mkamkataa Ismail?

Ila sijaona mgao wa urithi hapo, au ndo kile kiriba cha maji walichopewa?
hujaona baraka ya kumfanya kuwa uzao, sisi tunaamini uzao wa Ismaili ndio wote wakaao jangwani,
 
Iweke hiyo aya hapa.
Ushahidi unaletwa mahakamani na sio mahakama kuufuata
Sawa mahakama, mtoririko wa hizo aya ni huo hapo chini

99 - And [then] he said, "Indeed, I will go to [where I am ordered by] my Lord; He will guide me.

100- My Lord, grant me [a child] from among the righteous."

101 - So We gave him good tidings of a forbearing boy.

102 - And when he reached with him [the age of] exertion, he said, "O my son, indeed I have seen in a dream that I [must] sacrifice you, so see what you think." He said, "O my father, do as you are commanded. You will find me, if Allah wills, of the steadfast."

103 - And when they had both submitted and he put him down upon his forehead,

104 - We called to him, "O Abraham,

105 - You have fulfilled the vision." Indeed, We thus reward the doers of good.

106- Indeed, this was the clear trial.

107 - And We ransomed him with a great sacrifice,

108 - And We left for him [favorable mention] among later generations:

109 - "Peace upon Abraham."

110 - Indeed, We thus reward the doers of good.

111 - He was truly one of Our faithful servants.

112 - We ˹later˺ gave him good news of Isaac—a prophet, and one of the righteous.

113 - We blessed him and Isaac as well. Some of their descendants did good, while others clearly wronged themselves.
 
Nimesikiliza "qari" yaani msomaji, kasoma Surat Saffat aya ya 100 mpaka aya ya 105. Nimesikiliza na aliyepewa kutafsiri, hapo ndipo aliporonga. Na yeye kwa kuwa anajuwa anahokisema akamsukumia mtafsiri mwengine aitwae Ibn kathir, akasema huyo mtafsiri ndiye kasema huyo ni mtoto ni "Ismail".Hayo Yanabaki kuwa ni maneno ya mtafsiri (commentator) na siyo ya Qur'an.

Maana yake nini hiyo? Maana yake hakuna katika hiyo aya alipotajwa Ismail.

Ndiyto maana post ya juu huko nikasema yamepachikwa maneno kutoka nje ya Qur'an. Hata wewe ukiisikiliza aya inaposomwa hutosikia jina la Ismail, hilo utalisikia kutoka kwa "mtafsiri (commentator). Kayatowa wapi hayo aliyoongezea kama hayapo kwenye Qur'an? Hilo ndilo swali la kujiuliza.
"Kayatowa wapi hayo aliyoongezea kama hayapo kwenye Qur'an? Hilo ndilo swali la kujiuliza"
 
hujaona baraka ya kumfanya kuwa uzao, sisi tunaamini uzao wa Ismaili ndio wote wakaao jangwani,
Mbona una generalize kiasi hicho kamanda? ... kumbukua kweye hilo jangwa palifanywa kisima na Mungu kwa ajili ya huyo mtoto (Ismail)! ... just for your information, hayo maji ndo yanaitwa maji ya "zamzam", mpaka leo yapo kuthibitisha kuwa Mungu aliagiza Ibrahim awapeleke pale kwa malengo maalum ya baadae. Hivi hii haikuoneshi wewe kuwa hii ilikuwa ni foundation ya future prophet to come in Ismail's generation?

Halafu pia ukisema uzao wa Ismail ndo wanaokaa jangwani does this include mpaka na sahara desert?
 
Ibrahim ni Muebrania kiasili lakini dini yake ni Myahudi na ndie muanzilishi wa dini ya wayahudi.

Mungu wa Ibrahim, isaka ma Yakobo ambaye ni Yahwe ndiye alimchagua Ibrahim kuanzisha dini ya Kiyahudi
Wewe tubaki kwenye kufanya UCHAWA kwenye siasa. Haya mabo ya dini waachie werevu.

Judaism ni dini ya Wayuda. Yuda ni mtoto wa Yakobo. Hivyo, UKWELI unabaki pale pale kwamba Ibrahimu hakuwa Myahudi.
 
"Kayatowa wapi hayo aliyoongezea kama hayapo kwenye Qur'an? Hilo ndilo swali la kujiuliza"
Aulizwe yeye mpotoshaji, msikilize vizuri "sheikh" aliyepewa kutafsiri, yeye kamsukumia "Ibn Kathir", anaelewa kuwa hapo kwenye aya hizo zilizosomwa halijatajwa jina la Ismail.

Hapo juu kidogo neno "sheikh" nimeliweka kwenye mabano kwa sababu naamini Sheikh wa kweli hawezi kuwa mpotoshaji na kupachika majina yasiyokuwepo kwenye aya zilizosomwa.

Hiyo ni tafsiri inayopogtosha na kubadilisha maana.
 
Back
Top Bottom