Japokuwa ni Wakatoliki wenzangu Nashindwa kukielewa Hiki Chama cha Kitume..

Japokuwa ni Wakatoliki wenzangu Nashindwa kukielewa Hiki Chama cha Kitume..

Ryzen

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2012
Posts
7,301
Reaction score
8,706
Tumsifu Yesu Kristu wanaJF!

Kwa wakatoliki wenzangu kuna hawa Jamaa wanajiita Charismatic Catholics, au Karismatiki Katoliki.. hawa Jamaa wamekaa muundo fulani wa kilokole.. Hili Jambo binafsi linanikwaza (Japo sio Big deal).. kwa mfano siku Mkarismatiki akiwa mtoa neno utasikia maneno ya kilokole kama Mpendwa, Bwana asifiwe na Mengine Kadhaa.. sasa mimi binafsi nakuwa mvivu kuwa atentive kwa staili yao Hii..

Juzi kuna sala za Novena (sala za siku 9) nilikuwa nazipitia tukiwa tunajiandaa kwa Novena ya Kushukuru.. Kilichonivunja moyo Niliona mstari umeandikwa Tunasema Asante Baba.. Jambo ambalo wakatoliki awali hatujalizoea..

Sasa wakatoliki wenzangu Nafanyeje ili niweze kudeal vyema na hawa Jamaa..? ili niwe comfortable..

Asanteni!

Divine Khan!
 
Ndo maana wameambiwa siku nyingi watoke huku kati kati yetu watuachie dini yetu lakini hawataki. Paroko wengi tiyari weshawatimua kutoka kati yetu na kama ulipo bado mwambieni baba Paroko awatimulie mbali. Fyekelea mbali. hao mazezeta
 
Ndo maana wameambiwa siku nyingi watoke huku kati kati yetu watuachie dini yetu lakini hawataki. Paroko wengi tiyari weshawatimua kutoka kati yetu na kama ulipo bado mwambieni baba Paroko awatimulie mbali. Fyekelea mbali. hao mazezeta
Kwa Kweli Kaka Mmmefanya Vyemaa..
 
Vatican imesharidhia hiyo kitu na Kuna idara maalum inayoratibu ukarismatic kuanzia vatikan, kitaifa, kijimbo na kiparokia. Mkuu hata hi liturjia unayoiona sasa hivi awali haikuwa hivyo. Mfano kabla ya mtaguso wa Tisa wa vatikan mapadre na waumini wote walikuwa wanaangali kwenye tabernakulo nasio km ilivosasa mapadre wanaipa kisogo tabernakulo. Na Kuna mpango wa kurasimisha baadhi ya maudhui ya karismatic kuingizwa ktk sehemu ya misa kuu za kila jumapili.
 
Huwa hawachelewi kukengeuka hao. Ukipiga ishara ya msalaba utasikia kwenye biblia imeandikwa wapi?
Aisee.. Kuna siku walipiga Ngumi kabisa kwa sababu ya kutofautiana Litrujia
 
Vatican imesharidhia hiyo kitu na Kuna idara maalum inayoratibu ukarismatic kuanzia vatikan, kitaifa, kijimbo na kiparokia. Mkuu hata hi liturjia unayoiona sasa hivi awali haikuwa hivyo. Mfano kabla ya mtaguso wa Tisa wa vatikan mapadre na waumini wote walikuwa wanaangali kwenye tabernakulo nasio km ilivosasa mapadre wanaipa kisogo tabernakulo. Na Kuna mpango wa kurasimisha baadhi ya maudhui ya karismatic kuingizwa ktk sehemu ya misa kuu za kila jumapili.
Watakuwa wameyumba sana, anyway naomba hio Source Mkuu
 
Vatican imesharidhia hiyo kitu na Kuna idara maalum inayoratibu ukarismatic kuanzia vatikan, kitaifa, kijimbo na kiparokia. Mkuu hata hi liturjia unayoiona sasa hivi awali haikuwa hivyo. Mfano kabla ya mtaguso wa Tisa wa vatikan mapadre na waumini wote walikuwa wanaangali kwenye tabernakulo nasio km ilivosasa mapadre wanaipa kisogo tabernakulo. Na Kuna mpango wa kurasimisha baadhi ya maudhui ya karismatic kuingizwa ktk sehemu ya misa kuu za kila jumapili.
hivi mitaguso ni nini mkuu!
 
Nakusikitikia sana, maana nafsi yako imejawa makwazo ya kujitakia. Yaani badala ya KUISHI MAANDIKO wewe UNAISHI MAZOEA na hujisikii vibaya kukiri mbele ya watu.

Lina ubaya gani neno MPENDWA? Sasa wewe una tofauti gani kiitikadi na hao walokole?, kwani nao wanakwazika tukisema TUMSIFU YESU KRISTO!

Wanaposema BWANA ASIFIWE, ni Bwana mwingine tofauti na Yesu? Ya nini kugombea fito na tunajenga nyumba moja?
 
Tumsifu Yesu Kristu wanaJF!

Kwa wakatoliki wenzangu kuna hawa Jamaa wanajiita Charismatic Catholics, au Karismatiki Katoliki.. hawa Jamaa wamekaa muundo fulani wa kilokole.. Hili Jambo binafsi linanikwaza (Japo sio Big deal).. kwa mfano siku Mkarismatiki akiwa mtoa neno utasikia maneno ya kilokole kama Mpendwa, Bwana asifiwe na Mengine Kadhaa.. sasa mimi binafsi nakuwa mvivu kuwa atentive kwa staili yao Hii..

Juzi kuna sala za Novena (sala za siku 9) nilikuwa nazipitia tukiwa tunajiandaa kwa Novena ya Kushukuru.. Kilichonivunja moyo Niliona mstari umeandikwa Tunasema Asante Baba.. Jambo ambalo wakatoliki awali hatujalizoea..

Sasa wakatoliki wenzangu Nafanyeje ili niweze kudeal vyema na hawa Jamaa..? ili niwe comfortable..

Asanteni!

Divine Khan!

Kama unaishi imani yako vizuri, kwa nini ukwazike na wanaoishi imani yao (vizuri)? Jenga imani yako kwenye mwamba na siyo kwenye mchanga Matayo 7:24-27.
 
hivi mitaguso ni nini mkuu!
Kwa lugha nyepesi ni mabadiliko, maboresho au marejeo ya kanuni, taratibu, Sheria kuhusu swala, tendo au mfumo wa kuabudu, kuhudumu, kuamini Jambo la kikatoliki. Kifupi ni mabadiliko ya kikanuni ya kanisa la Roma ambapo makardinali wote duniani wanakutana vatikani kupitisha.
 
hivi mitaguso ni nini mkuu!
Mkuu Mitaguso ni Kama Vikao Fulani vya kutoa maamuzi kuhusu utata fulani.. sema vya Kikanisa.. Kwa Mfano Mtaguso wa kwanza kuwahi kufanyika ni ule wa Nicea 325 A.D
 
Sasa mtoa maada kusema asante baba inakuuma? Kusema mpendwa unawashwa? Kusema Bwana Yesu asifiwe unakonda? Kweliwewe zao la shetani unaona masanamu hayo mnayo fukizia ubani nimhimu sana duu kweli tabu ipo
Asante Mtakatifu..
 
Vatican imesharidhia hiyo kitu na Kuna idara maalum inayoratibu ukarismatic kuanzia vatikan, kitaifa, kijimbo na kiparokia. Mkuu hata hi liturjia unayoiona sasa hivi awali haikuwa hivyo. Mfano kabla ya mtaguso wa Tisa wa vatikan mapadre na waumini wote walikuwa wanaangali kwenye tabernakulo nasio km ilivosasa mapadre wanaipa kisogo tabernakulo. Na Kuna mpango wa kurasimisha baadhi ya maudhui ya karismatic kuingizwa ktk sehemu ya misa kuu za kila jumapili.

Sikumbuki kama Kanisa Katoliki lilishawahi kuwa na 'Mtaguso wa Tatu wa Vatican' na huo wa Tisa je? Lakini ninavyojua hadi sasa kumekuwa na mitaguso ya Vatican miwili tu. Mtaguso wa Kwanza wa Vatican (Vatican I) 1869–70 na Mtaguso wa Pili wa Vatican (Vatican II) October 11,1962-December 8, 1965. Hata hivyo, kumekuwa na sinodi nyingi na mabaraza mengi.
 
Sikumbuki kama Kanisa Katoliki lilishawahi kuwa na 'Mtaguso wa Tatu wa Vatican' na huo wa Tisa je? Lakini ninavyojua hadi sasa kumekuwa na mitaguso ya Vatican miwili tu. Mtaguso wa Kwanza wa Vatican (Vatican I) 1869–70 na Mtaguso wa Pili wa Vatican (Vatican II) October 11,1962-December 8, 1965. Hata hivyo, kumekuwa na sinodi nyingi na mabaraza mengi.
Loo my mistake. Kumbe nimeandika mtaguso wa Tisa. Of course mitaguso so far ipo miwili tu.
 
Back
Top Bottom