Japokuwa ni Wakatoliki wenzangu Nashindwa kukielewa Hiki Chama cha Kitume..

Japokuwa ni Wakatoliki wenzangu Nashindwa kukielewa Hiki Chama cha Kitume..

Mimi ni mkatoliki sio karismatiki. Sijaona tatizo hapo.
 
Vatican imesharidhia hiyo kitu na Kuna idara maalum inayoratibu ukarismatic kuanzia vatikan, kitaifa, kijimbo na kiparokia. Mkuu hata hi liturjia unayoiona sasa hivi awali haikuwa hivyo. Mfano kabla ya mtaguso wa Tisa wa vatikan mapadre na waumini wote walikuwa wanaangali kwenye tabernakulo nasio km ilivosasa mapadre wanaipa kisogo tabernakulo. Na Kuna mpango wa kurasimisha baadhi ya maudhui ya karismatic kuingizwa ktk sehemu ya misa kuu za kila jumapili.
Mkuu samahani kidogo...
Huo "Mtaguso wa Tisa" ulifanyika lini..????maana sijawahi kuusikia.
 
Tumsifu Yesu Kristu wanaJF!

Kwa wakatoliki wenzangu kuna hawa Jamaa wanajiita Charismatic Catholics, au Karismatiki Katoliki.. hawa Jamaa wamekaa muundo fulani wa kilokole.. Hili Jambo binafsi linanikwaza (Japo sio Big deal).. kwa mfano siku Mkarismatiki akiwa mtoa neno utasikia maneno ya kilokole kama Mpendwa, Bwana asifiwe na Mengine Kadhaa.. sasa mimi binafsi nakuwa mvivu kuwa atentive kwa staili yao Hii..

Juzi kuna sala za Novena (sala za siku 9) nilikuwa nazipitia tukiwa tunajiandaa kwa Novena ya Kushukuru.. Kilichonivunja moyo Niliona mstari umeandikwa Tunasema Asante Baba.. Jambo ambalo wakatoliki awali hatujalizoea..

Sasa wakatoliki wenzangu Nafanyeje ili niweze kudeal vyema na hawa Jamaa..? ili niwe comfortable..

Asanteni!

Divine Khan!
Ndugu yangu umesababisha kanisa kutukanwa bure kwenye hii mada yako.

Pole kwa makwazo ila ninaamini wewe ni muumini mlei na sidhani kama akili yako inamapana kuliko maaskofu na mapadre na hata makadnal ambao ndio wazee wakanisa tunaweza kusema ndio wenye kanisa, kwa utashi wao wameruhusu uwepo wa karismatiki na taratibu zao.

Nime kushangaa sana kukosoa wana karismatiki namna wanavyo fanya majukum yao lakini legio maria,moyo wa Yesu , mt yoseph nk haujawakosoa maana wao utaratibu wao na sala zao nje ya mapokeo hazijulikani Kibiblia .


Mimi binafsi nimehudumu karsmatiki kwa miaka 5 nimeona tofouti ya mkrsmatiki na asie karismatiki ndani ya kanisa katoliki.

Karsmatik hufuata mwongozo ambao ni kama katiba ambayo imetungwa na wataalam dini wakiwepo mapadre maaskofu na wanateilojia na kisha kupiwa na baraza la maaskofu kisha kuupitsha uwe mwongozo rasmi wa karsmatiki katoliki.

Ndio nikasema sina hakika kama wewe ni mtaalam sana wa kanisa katoliki za maaskofu kuona mapungufu ya karsmatiki.

Kama karsmatiki wangekua wako nje ya biblia tusinge itetea lakini kwa kua waamini wajikita katika msingi wa liturgia na Biblia kua ya pili ndio maana watu kama nyie hamkosekani.

Ukweli ni kwamba karsmatiki imekua ikimjenga muumini katika msingi wa neno la Mung, karama za Roho Mtakatifu, na kuikimbia dhambi.

Sasa kwa vile waamini wengi pamoja na mapdre ni washirika wa dhambi ni lazima muichukie karsmatiki

Yote ya yote pole sana kwa kukwazika maana Yesu alitahadharisha kwamba mkwazo yapo lakini ole wake ayasabishae.
Pia jua sote wana wa Mungu kwa sababu tumeamini katika Kristo kwa hio haina haja ya mafarakano. Nyumba tunayojenga ni moja na kila mtu anajenga kwa material yake, wengine nyasi wengine fito wengine mawe wengine udongo lakini mwisho wakazi kila kazi itapimwa kwa moto itakayosimama mwenye kujenga atalipwa , kwa hio sote tunajenga katika msingi mmoja nao ni Kristo.
 
Sasa kwa vile waamini wengi pamoja na mapdre ni washirika wa dhambi ni lazima muichukie karsmatiki
Sina neno kama padre ambaye ndie huyo askofu.. Ndiye huyo Kardinali.. Umemuweka kwenye hili kundi.. Tena katika muundo wa kashfa..
 
Sina neno kama padre ambaye ndie huyo askofu.. Ndiye huyo Kardinali.. Umemuweka kwenye hili kundi.. Tena katika muundo wa kashfa..
Raisi wa nchi anakiri kuharibiwa na mapadre wa kikatoliki, anasema si yeye tu. Wote! Wewe umepona kweli? Fungus...
 
Kwa lugha nyepesi ni mabadiliko, maboresho au marejeo ya kanuni, taratibu, Sheria kuhusu swala, tendo au mfumo wa kuabudu, kuhudumu, kuamini Jambo la kikatoliki. Kifupi ni mabadiliko ya kikanuni ya kanisa la Roma ambapo makardinali wote duniani wanakutana vatikani kupitisha.
Sio kweli mtaguso ni mikutano ya mabadiliko inajumuisha viogozi kanisa Kwa mfano mapadre,maaskofu,macardinali na viogozi wengine..!!Kwa mfano mtaguso Wa kwanza wa Vatican..mkutano Wa kwanza wa vatican kwenye hiyo mikutano ndo hayo mabadiliko ujadiliwa..
 
Kanisa linajitahidi kuaccomodate watu wake wote kadri iwezekanavyo.
Eti kanisa. Roman catholic siyo kanisa. Waanzilishi wake wana mission tofauti sana na mnachokiamini. Ndio maana wakiona waumini wanaofuata maandiko wanafyekelewa mbali.
 
Shida kubwa ya kanisa katoliki ni kuwa na wakatoliki wasiojua ukatoliki na wanadai wanaujua, hawa ndio shida kuliko wasioijua imani yenyewe. Mkatoliki kama unajua kusoma lazima utafute maana ya imani yako sio kuwa mvivu wakutafuta masuala ya imani yako halafu unakuja humu unasema unakwazwa tafuta maana ya maandiko yapo mengi ya kujua imani yako. Mungu tuepushie mbali wakatoliki wasiotafuta maana ya imani yao na bado wanajiita wakatoliki
Kwa mfano wanatakiwa wajue kwanini wanaabudu Jumapili, Kwanini wanaabudu sanamu,Je 25.12 ndio siku alizaliwa Yesu waliipata wapi siku hiyo? Kwanini watoto wanabatizwa wakati kubatizwa kunaendana na kuamini je watoto wachanga nao wanaaminije? Kwanini Passover imetafsiriwa kama Easter.
 
Back
Top Bottom