Jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Nyerere 1982/1983

Jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Nyerere 1982/1983

It's true tuna tatizo la kutoweka kumbukumbu za matukio muhimu kwa taifa letu.
Kesi ilipoanza mwanzo ilikuwa na washitakiwa 46, washitakiwa 23 waka confess na kugeuzwa mashahidi wa jamhuri wakabaki washitakiwa 23, wawili wakaachiwa kwa no prima facie wakabaki 21, kwenye hukumu wawili were aquited 19 ndio wakakutwa na hatia. Nimesearch majina yao online sikufanikiwa.
P
Na taratibu za kuziweka wazi taarifa kama hizi zipo vipi kwa taifa letu?
 
Marekebisho:

Huyo komandoo aliyeuawa hakuuwawa jirani na ubalozi wa Marekani sijui kwa nini watu wanapotosha.Na hii habari ilikuwa wazi kabisa.

Mimi nikuwa naishi O/bay jirani sana na huo ubalozi wa USA wa zamani kwa nyuma.

Huyo Kamandoo aliuawa kinondoni pale inapoanza down ya kwenda magomeni , alidandia pickup ya wazi baada ya kuwatoroka ghafla waliomkamata..

Nakumbuka kama alikuwa anaitwa Tammim
Taharuki ilikuwa ya ukubwa gani wakati huo kwa watu wa kawaida waliokuwa maeneo jirani?
 
Ilikuwa ghafla tulivyofuatilia inaelekea askari walitonywa wakamnasa . Wakati wanamsindikiza ali escape akadandia hiyo pickup, hiyo barabara ya kinondoni to magomeni haikuwa nzuri namna hii nadhani ilichangia wakamuai akapigwa risasi akiwa kwenye pickup. Ni tukio la mud mfupi tu. TV hazikuwepo wala , smart phone na traffic jams zilikuwa hamna.


Nakumbuka pia kuna mmoja ali escape toka Ukonga. Alihukumiwa kufungwa pale. Aliondoka na ofisa magereza mmoja nadhani walichonga dili walimfungulia geti tu. Hii story ilikuwa kwenye magazeti ya kawaida. Wakati ule ukitaka story ambao haina longolongo una subiri BBC saa 12.

Kwa mfano wakafi RTD walikuwa hawatangazi kwamba ATC imetekwa na akina Memba na iko wapi BBC walikuwa wanatoa habari zote.

Taharuki ilikuwa ya ukubwa gani wakati huo kwa watu wa kawaida waliokuwa maeneo jirani?
 
Uzi huu hauwezi kukamilika bila kutaja mchango wa shahidi wa serikali, jasusi mzoefu aliyesambaratisha ngome ya uhaini, aliyetambukiwa kwa jina la siri "Mr. X" katika kesi ya uhaini.

Ambaye leo ni Waziri wa Sheria, balozi Augustine Philip Mahiga.
Huyu jamaa alikuwa miongoni mwao wale walio asi au?
 
Ukweli wa haya yote utakuja kuusikia CHADEMA wakiingia Mjengoni
Ni kweli mkuu maana siku moja nlikua IRINGA cha ajabu ni kuwa historia ya mtemi Mkwawa tunayoisoma kwenye vitabu inaonekana ni ya kupikwa sana si kile ambacho wenyeji wanakifahamu.

Mkwawa anaonekana kuwa alikuwa ni kiongozi aliyetumia diplomasia sana na uchawi sana kutaka kupata suluhu na wajerumani lakini tunaambiwa alikua shujaa aliyepambana na wajerumani mpaka dakika ya mwisho wakati ukweli ni kuwa aliwakimbia wajerumani kwa kutaka kujiokoa baada ya diplomasia na utabiri wa mganga wake wa kienyeji kuwa atawashinda wajerumani kushindwa.

Ninachojiuliza hapa je ni kweli kuwa historia ya nchi hii nyingi ni ya kupika??
kwa nini matukio mazito kama haya ya mapinduzi ya kijeshi hayatajwi katika historia ya hii nchi?
 
Hii kesi hukuwa ukihudhuria mahakamani?
It's true tuna tatizo la kutoweka kumbukumbu za matukio muhimu kwa taifa letu.
Kesi ilipoanza mwanzo ilikuwa na washitakiwa 46, washitakiwa 23 waka confess na kugeuzwa mashahidi wa jamhuri wakabaki washitakiwa 23, wawili wakaachiwa kwa no prima facie wakabaki 21, kwenye hukumu wawili were aquited 19 ndio wakakutwa na hatia. Nimesearch majina yao online sikufanikiwa.
P
 
Na taratibu za kuziweka wazi taarifa kama hizi zipo vipi kwa taifa letu?
Tuna sheria ya national achieves ambapo documents muhimu zote za serikali zinatakiwa kuhifadhiwa kwenye idara ya kumbukumbu za taifa ili ziweze kuwa accessed in future including classified documents kama confidential reports, secret documents na top secret documents ambazo zinaendelea kuwa classified kwa miaka 33, 66 na 99 na muda huo ukipita zinakuwa declassified hivyo kuwa open kwa public.

Exemption ya kupeleka documents za serikali achives ni kwa documents za military intelligence, Tiss operations na documents za Ikulu za rais ambazo hizi zinakuwa na achieved separately and not open to public for life.

Kwa vile uhaini huu umetokea 1982 na sasa kimeisha pita kipindi cha miaka 33, hii inamaanisha documents za kesi hii ya uhaini kwa sasa tayari ni declassified na ziko open to public pale national achieves.
P
 
Mkuu Shwari asante sana kwa hii achieve, mwanzo washitakiwa walikuwa 46 wakaenda wakipungua hadi kesi inaanza kusikilizwa walibaki 23. Wakati huo nilikuwa form II Tambaza tukiishi Drive In Flats tukikaa flat moja na Banyikwa ni next door tumetenganishwa na ukuta tuu. Hawa Banyikwas ni Wahangaza na walikuwa na na mabinti 4 striking beutiful, hivyo you can imagine Msukuma chapa ng'ombe na majirani wa hivyo next door!. Nyumba hiyo ndipo kulifanyikia vikao. Binti wa nyumba hiyo Kesi ilipotatwa kwa mara ya kwanza hawa jirani zangu walikuwa wote wawili Mr & Mrs na binti yao mkubwa Hope alikuwa PW kwenye kesi against wazazi wake!.

Halafu yule Muchwampaka alikuwa ni mume wa mwalimu wetu Tambaza Mwalimu Muchwampaka, kesi ilipotajwa the Muchwampakas walikuwa ndugu wawili kama walivyo the Hans Pope's.

Mwandishi huyo Charles Kizigha yupo ni mzee retired na binti yake alikuja kuwa mbunge wa EALA.

Kiukweli Tanzania tumetoka mbali.
P.
 
Mwanzo washitakiwa walikuwa watu 46 mostly jnr offices at around 21-25 years hiyo 1982 hivyo sasa watakuwa around 60s, nimesema some wapo kwa sababu mmoja ni maarufu anajulikana sana yupo hai na ninamfahamu.
P
Sawa Mkuu Pascal wengine wapo hai kwa mfano yule Mkude aliyekuwa mkufunzi wa mgambo Morogoro, mimi nilipanga nyumba yao kule Morogoro na nilikuwa napiga nae story jioni.

Nilishangaa nilipokutaa amekamatwa lwa uhaini na nilikuwa sijawai kumsikia akiongoea mambo ya kiukashifu serikali hata siku moja.

Ila baadae nikakumbula mpangaji mwenzangu alikuwa usalama wa Taifa. Hakujitambulisha kwangu ila Kaka yangu alifahamu Na alimiliki pikipiki yenye namba za kawaida.

Huyo jamaa aliyekuwa serkalini usalama sikuwai kumwona akiongea na Mkude. Na sijui yule mjeda mkude kama alikuwa na mpango huo alijua yule jamaa anafanya kazi gani.
 
Asante sana ndugu Pascal kwa maelezo hayo. Ni ya kusisimua.
Nimefahamiana na Charles Kizigha kwa miaka mingi sana.
Charles Kizigha anapaswa aandike kitabu, mimi nilimsoma nikiwa chuo cha journalism TSJ, aliripoti kutekwa kwa ndege ya ATC, ndie mwandishi wa kwanza na labda wa pekee nchini Tanzania niliyemfahamu mimi, kumiliki gari brand new kutoka show room, alimiliki gari ya Musso new brand kutoka dukani!, waandishi wengine wote gari zetu ni used, ila sijui kwa waandishi wadada, maana wenzetu hawachelewi kununuliwa magari na ma source!.
P
 
Back
Top Bottom