Wick
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 8,313
- 12,170
Tukielekea sherehe za Christmass na Mwaka mpya, kuna madereva wapya na wale wa zamani watakaokuwa safarini sehemu mbalimbali, Iwapo ikatokea upo kwenye mwendo na breki kwenye gari zimefeli, jaribu kufanya haya!. Kumbuka kila moja linajitegemea katika kulifanya!.
1. USIPANIC, ikiwezekana hata abiria wako wasijue tatizo unalohangaika nalo (kuepusha kukuchanganya zaidi).
2. Washa taa za double hazard kuwajulisha madereva wenzio una tatizo. Wenye akili watakaa mbali nawe.
3. Endelea kupump brake inawezekana zikashika au kusaidia punguza mwendo wa gari.
4. Vuta taratibu hand brake, usijaribu kuivuta yote kwa mara moja, ukivuta kwa mara moja utasababisha gari kugeuka ghafla. Kumbuka tumia hand brake iwapo upo chini ya speed 50km/h tu.
4. Iwapo unaendesha Automatic weka gari yako kwenye gia ndogo (L), au kama gari ni Manual shusha gia mpaka 1 hakikisha unadownshift kwenda gia 2 kabla ya 1, usiitoe 4-1 moja kwa moja, hii inaitwa 'engine breaking'.
5. Muda mwingine kuipeleka gari kwenye Neutral (N) itaweza kukusaidia ingawa si salama sana.
6. Washa air conditioning, ipeleke AC ya gari yako mpaka mwisho kwenye ubaridi wake, itaipa uzito mkubwa engine na kukusaidia punguza mwendo wa gari yako. Pia washa taa zote na kila kitu kwenye gari itafanya umeme mwingi zaidi utumike na kuipunguzia nguvu gari.
7. Hii ni hatari lakini inaweza kukusaidia, switch funguo kama unataka zima engine lakini weka kwenye 'Ignition On' sio kwenye 'Engine OFF' juwa kuzitofautisha!.
8. Tafuta eneo salama kugongesha gari yako (unapogongesha lenga upande wa kushoto kwenye kona ili kuzuia dereva usije banwa na steering).
PS: Iwapo upo eneo baya, tegesha gari yako kufunga barabara nzima (utasaidika haraka zaidi).
1. USIPANIC, ikiwezekana hata abiria wako wasijue tatizo unalohangaika nalo (kuepusha kukuchanganya zaidi).
2. Washa taa za double hazard kuwajulisha madereva wenzio una tatizo. Wenye akili watakaa mbali nawe.
3. Endelea kupump brake inawezekana zikashika au kusaidia punguza mwendo wa gari.
4. Vuta taratibu hand brake, usijaribu kuivuta yote kwa mara moja, ukivuta kwa mara moja utasababisha gari kugeuka ghafla. Kumbuka tumia hand brake iwapo upo chini ya speed 50km/h tu.
4. Iwapo unaendesha Automatic weka gari yako kwenye gia ndogo (L), au kama gari ni Manual shusha gia mpaka 1 hakikisha unadownshift kwenda gia 2 kabla ya 1, usiitoe 4-1 moja kwa moja, hii inaitwa 'engine breaking'.
5. Muda mwingine kuipeleka gari kwenye Neutral (N) itaweza kukusaidia ingawa si salama sana.
6. Washa air conditioning, ipeleke AC ya gari yako mpaka mwisho kwenye ubaridi wake, itaipa uzito mkubwa engine na kukusaidia punguza mwendo wa gari yako. Pia washa taa zote na kila kitu kwenye gari itafanya umeme mwingi zaidi utumike na kuipunguzia nguvu gari.
7. Hii ni hatari lakini inaweza kukusaidia, switch funguo kama unataka zima engine lakini weka kwenye 'Ignition On' sio kwenye 'Engine OFF' juwa kuzitofautisha!.
8. Tafuta eneo salama kugongesha gari yako (unapogongesha lenga upande wa kushoto kwenye kona ili kuzuia dereva usije banwa na steering).
PS: Iwapo upo eneo baya, tegesha gari yako kufunga barabara nzima (utasaidika haraka zaidi).