Jasusi Honda ndani ya mpango wa Congo

Jasusi Honda ndani ya mpango wa Congo

RIWAYA : MPANGO WA CONGO

SEHEMU YA 27

SIMU 0758573660


***

Mtega nyoka hakuwa mbali na nyumba ya Mwasu ila alishindwa kuingia baada ya kuona tukio fulani akiwa hatua chache kutoka ilipokuwa nyumba ile.

Alikuwa na mwenyeji wake aliemwongoza pale.

Mwenyeji alimwonesha tu wakiwa mbali nyumba ya Mwasu.

Ni wakati akipiga hatua fupifupi ndipo alipoona watu wawili kibalazani.

Mmoja alikuwa amesimama na mwingine amekaa.

Aliekuwa amesimama alikuwa na wajihi sawa na mtu aliepambana nae Buzuruga Plaza siku kadhaa nyuma.

Mtu aliekuwa amesimama alimwona alivyochomoa bastola yake kutoka kiunoni kwa kasi ya ajabu na kumwelekeza jambo mtu aliekuwa amekaa.

Mtu aliekuwa amekaa wakati anasimama ndipo mtega nyoka alipomuona vyema.

Alikuwa ni Malima.

"Kumekucha!!" alijisemea Mtega nyoka..

Alijibanza nyuma ya nyumba iliokuwa jirani.


Haukupita muda mrefu aliona wakitokea vijana wengine wawili na kuingia ndani.

Zilipita dakika tatu ndipo alipoona watu watano wakitoka ndani huku wawili wakiwa ni Malima na Remi.
Na wengine ni mtu mrefu waliepambana Buzuruga Plaza na vijana wengine wawili.

Nyuma yao alitokea Binti mmoja mrembo sana ambae aliishia mlangoni tu na kuwasindikiza kwa macho.

Watu wale ambao walitembea ki kawaida tu bila kuonesha kama kuna mateka kati yao,walipita nyuma ya nyumba walimokuwamo na kutokea kwenye uwanja wa kanisa la Wokovu.

Huko walikuta gari ikiwa imenawangojea!

Wakapanda na kuelekea barabara kubwa kwa kupitia Nyakato shule ya msingi kisha wakakamata barabara kubwa na kuwa kama wanaelekea buzuruga.

Walipofika kona ya Nyakato sokoni,walikunja na kuelekea Meko,walipita karibu na baa ya ShaTemba na kuelekea njia ya vumbi ya Meko majanini.

Nyuma yao alikuwapo Mtega nyoka safari hii akiwa na pikipiki alioendesha mwenyewe huku abiria akiwa ni mwenye pikipiki.

Kwa msaada wa mwenye pikipiki, alimwelekeza kama wenye gari wamepitia njia ya Meko majanini basi wataenda kutokea njia ya Meko shule ya msingi hivyo wao waelekee shuleni na wangoje hapo.

Baada ya dakika kadhaa ilipita gari ya wagonjwa ikitokea Meko majanini.

Mtega nyoka aliona mtu aliekuwa amekaa kushoto mwa dereva.

Alijua wamebadilisha gari!

Akaifuata gari ile ya wagonjwa.

Safari yao ilikuwa ya uangalifu sana ili wasije wakashitukiwa.

Gari ile ilienda kuishia makanisa matatu na ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Mtega nyoka kufika eneo lile.

Hapo ndipo Mtega nyoka alipoona majengo sawa na yale yalioko kwenye kadi alioichukua mifukoni mwa mvamizi aliemuua bwana Kindo Seleman; Mkurugenzi wa Kasuku Contractors.

"Sasa kama ni kanisa ile kadi ya nini?" alijisemea Mtega nyoka huku akielekea kwenye makazi ya mchungaji wa kanisa la Efather.

Bado Mtega nyoka nae alikuwa anashangaa harakati zilizokuwa pale.


Akili yake ilishindwa kabisa kupata walau lililokuwa likiendelea pale.

Kama ni kikao basi ilitakiwa watu waingie na kutulia! Ila watu walikuwa wanaingia na kutoka.

Lakini pia yalikuwa ni mavazi yao.

Mavazi waliovaa ilitakiwa yavaliwe na waumini wa madhehebu ya Roman Catholic ama KKKT na si vinginevyo!!

Kwa mtazamo kanisa lile lilikuwa sawa na kanisa la kakobe ama Mzee wa upako ama wachungaji wenye sifa za utajiri kuliko uwezo wa waumini wao.

Sasa tangu lini makanisa ya aina hiyo yakawa na watawa?

Ajabu hii.


Ilikuwa ni wakati akitoka huko kwa mchungaji ndipo alipomuona mwanamke alievaa hijabu jeusi na kufunika uso wake wote na kubakiza macho tu.

Mwendo!!.

Aliutazama mwendo wa mwanamke yule.

Hata!!

Mwanamke gani huyu anatemebea kama kakanyaga moto!!

Aliachana nae akapanda pikipiki iliomleta pale na kutokomea.

Mwanamke wa hijabu nae akapanda pikipiki iliomfikisha pale na kuondoka.

Huku malipo ya dereva akimwandikia kwenye karatasi na kumuomba dereva afike kituo cha polisi atapewa pesa yake yote endapo akimwonyesha karatasi ile OCCID.

Dereva wa pikipiki akakubali japo roho ilimdunda.

Polisi hakuzoeleki!!


*****

Solomoni Bukaba alirudi ndani kwa Sundi na kuvua yale mavazi kisha akaenda kuyarudisha kama alivyoyakuta na kurudi kule chumbani alikokuwa amelala.

Akalala kama alivyoachwa.

****

Mtega nyoka alikuwa ameona Malima alivyotekwa pamoja na Remi.

Hivyo akapanga kurudi hadi nyumbani kwa Mwasu ili ambane Mwasu.

Hakuchukua zaidi ya saa mbili akawa yupo mlangoni kwa Mwasu.

Akagonga na kutulia.

Punde mlango ukafunguliwa akachomoza binti mrembo mwenye asili ya watu wa Rwanda ama Burundi.


"Nikusaidie nini!" Alisema Mwasu huku akimtizama Mtega nyoka usoni kwa makini.


Mtega nyoka alitabasamu.


"Nikaribishe ndani tuzungumze kidogo," alisema Mtega nyoka.

"Nakuingizaje ndani sikufahamu? Alisema Mwasu.

Mtega nyoka alikaa kimya kisha akatazama kushoto na kulia,alipoona kupo shwari Hakuna mtu akafanya kitendo cha haraka na kasi ya ajabu.

Akamsukuma Mwasu ndani kwa kasi kisha akatulia na kufunga mlango kwa nyuma.

Mwasu alijinyanyua chini huku akishangaa kasi alionayo bwana yule ambae alikuwa amesimama akimwangalia tu.

"unataka nini kwangu?" aliuliza Mwasu huku akijifuta kitu asichokiona mwilini mwake.

"naomba kufahamu alipo Malima" alisema Mtega nyoka.

Mwasu alishangaa!

"Malima?; mbona simjui!" alisema Mwasu.

Mtega nyoka akacheka kisha akatazama juu ukutani.


"Huyo uliebandika picha yake hapo ukutani ndie ninae mtaka" alisema Mtega nyoka huku akisonta kwa kidole picha kubwa iliokua imebandikwa ukutani.

Mwasu akagwaya huku akijutia uongo wake alioutoa bila kufikiria.

Mwasu alijua yupo matatani hivyo lazima afanye jihada za kujinasua kisha aombe usaidizi kama atashindwa kumdhibiti Mtega nyoka.

"Mi sujui alipo!" alisema Mwasu huku akimtizama usoni Mtega nyoka.

"Na Remi je!" aliuliza tena Mtega nyoka.

Mwasu alikodoa macho huku akishindwa kuelewa dhamira ya mgeni wake huyo.

"Hebu sema shinda yako bwana mana naona sikwelewi; Malima; Remi tuelewe lipi sasa" alikoroma Mwasu.

"Ukinijibu wote kwa pamoja itakuwa vizuri sana" alisema Mtega nyoka.

"watafute mwenyewe utajua walipo" alisema Mwasu.

Mtega nyoka alitulia kimya akimtizama Mwasu.

"Vipi kuna nini pale Makanisa matatu?" lilikuwa swali la mtego ambalo Mwasu hakulitarajia.


Akaingiwa na ubaridi wa gafla.

"Sasa mbona wafahamu mengi, kwanini waniuliza?"


"Kwa sababu na..." Mtega nyoka hakumaliza kauli yake alijiukuta akirudi nyuma kwa kasi na kujipigiza kwenye mlango na kusambaratika chini.


Mwasu alikuwa amemfanyia shambulizi la kushitukiza.

Mtega nyoka aliharakisha kunyanyuka ila alijikuta akienda chini tena baada ya kupigwa teke ubavuni.

Mwasu hakutaka kucheza na mtu kama yule.

Akapaa juu na kurudi na pigo la kifo.

Mtega nyoka aliliona akakwepa kisha akaachia konde zito lililompata Mwasu tumboni.

Mwasu akaenda chini huku akitoa kilio kama cha mwanamke anaebakwa.

Mwasu akasimama ila akajikuta anaingia kwenye wakati mgumu kujiokoa na makaonde mfululizo kutoka kwa Mtega nyoka.

Yapo aliopangua na mengine yalijaa mwilini mwake.


Mwasu akaona akifanya uzembe atakuwa mateka ili aseme anachokijua.

Hakutaka hilo litokee.

Akajifanya kama anaenda chini ila hakufika badala yake alifyatuka kichwa kikali kilichotua tumboni kwa Mtega nyoka na kumpeleka chini. Kisha yeye akasimama haraka na kujirusha mzimamzima na kwenda kulikumba dirisha la vioo lililokuwa sebuleni pale na kusambaratika nalo nje kisha bila kujiuliza akasimama na kutimua mbio za mbwa mwizi.

Mtega nyoka nae aliharakisha kutoka kwa kupitia pale pale dirishani baada ya kuwa wazi kwa kuvunjwa.

Alipotua nje hakuona hata unyayo wa Mwasu.

Alikwama tena.
 
RIWAYA: MPANGO WA KONGO

NA, BAHATI MWAMBA

SIMU: 0758573660.


1
MAUAJI

Ilikuwa ni ndani ya majengo ya ubalozi wa Tanzania yalioko pembeni kidogo mwa mji wa mji mkuu wa Congo DRC katikakati ya mji mdogo wa Ivuba.

Katika moja ya meza zilizokuwa ndani ya vyumba vya juu kabisa ndani ya ubalozi huo kulikuwa kuna mtu amesimama kando ya meza hiyo huku kila mara akijaribu kukuna kichwa chake ambacho hakikuwa na unywele hata mmoja.

Mtu yule hakuwa mtulivu wa nafsi,akili na mwili.Bila shaka kwa sababu kadhaa alizozijua yeye na muda wote aliokuwa amesimama kando ya meza ile alikuwa akitazama dirishani,dirisha ambalo wakati huo lilikuwa lipo wazi na halikuwa limefungwa wala kushushwa pazia kubwa na zito ambalo wakati huo lilikuwa limekunjwa kwa namna fulani hivi kisha likashikizwa na kibanio maalumu ambacho kiliacha pazia lile likiwa limejikunja katikati na kujiachia chini.

Ingekuwa siku zingine bwana huyu angeliweza kumuita mfanya usafi na kumkanya juu ya kusahau kufunga dirisha na kushusha pazia,lakini leo hii hilo hakukumbuka kabisa na badala yake akawa amejielekeza kuwaza na kuwazua jambo fulani tata ambalo kamwe hakudhani linafanyika katika nchi ile ya Congo.

Macho yake yalitazama dirishani tena na hapo akashuhudia jengo lingine refu lililokuwa likitazamana na ofisi zake zile,jengo lile lilikuwa ni hoteli kubwa kabisa ndani ya jiji la Kinshasa na mji ule wa Ivuba.

Tofauti na siku zote ambazo huwa analitazama mara kadhaa huku akiwa na kikombe cha kahawa mkononi,lakini leo hii hakuwa na kikombe na hata yale mawazo yake ya kutaka siku moja yeye au mwanae ajenge jengo kama lile nchini Tanzania hayakuwa kabisa akilini mwake.


Akajikuna kichwa na kujiegemeza kwenye meza iliokuwa kando yake kisha akaketi huku sasa mwili wake ukianza kuhisi joto la ajabu ambalo hakujua ni la uoga ama la joto la ahsubuhi ile ya ajabu kwake.

Akiwa bado anatizama pale dirishani mara mlango wa ofisi yake ukafunguliwa bila mfunguaji kubisha hodi.

Akaingia mwanaume mkakamavu mwenye misuli imara na kusimama nyuma yake.

Balozi Ally Sapi akageuka kutoka kule alikokuwa anaangalia na kumgeukia mwanaume yule.

Walitazamana kwa muda kidogo kisha Balozi Sapi akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa mkupuo.

“Alikuwa sahihi yule bwana mdogo” alisema Balozi huku akimtizama usoni mwanaume yule aliekuwa amesimama mbele yake.

“ina maana ndicho kilichotokea kwako sivyo!”alisaili mwanaume yule.

“Haswaa na tena kinaeza kuniondoa duniani masaa machache yajayo!” alisema Balozi huku akimtizama yule mwanaume na kuuona mshituko wa wazi usoni pake.
Ikawa zamu ya yule mwanaume mkakamavu kujikuna kichwa na kushangaa huku nae kichwa kikijaa moto wa joto ambalo hakujua limetokea wapi ahsubuhi ile.

“aaah ina…” akataka kusema yule mwanume baada ya kuwa anahitaji maelezo zaidi kutoka kwa balozi Ally Sapi,lakini hakumaliza kauli yake tayari balozi Sapi alishaanza kusema.

“Nilipokea ugeni jana jioni wakati natoka hapa ofisini,na kabla sijafika nyumbani yakanipita magari sita kwa kasi na kwenda kusimama mbele kisha gari la mwisho likaanza kupunguza mwendo hali ilionifanya nipunguze na mimi pia na kisha nikaona ishara kutoka kwa dereva wa gari la mwisho kati ya yale magari sita akiniashiria nisimame nami nikatii kwa kusimama pembeni hasa kwa kuhisi inaeza kuwa ni heri tu. Kutoka katika magari yale wakashuka wanaume wanne wakaja karibu na gari langu na bila kusema kwa maneno wakanipa ishara nishuke ndani ya gari,nami nikatii,wakaniongoza hadi kwenye gari moja wapo na humo ndani ya gari sikuamini kabisa nilichokiona aisee” alimalizia kwa kusikitika balozi Sapi.

“kwa ikawa vile tulivyowaza na ulichokiona ni kile kile alichosema marehemu Bulembo!” alisema tena yule mwanaume na hapo ikawa ni zamu ya Balozi Sapi kutumbua macho kwa kutoamini alichokisikia.

“ina maana Bulembo amefariki,lini na wapi!” alihoji Balozi Sapi huku macho yake yakiwa bado yapo yanamtazama mwanaume yule bila kupepesa huku moyo wake ukiruka sarakasi kifuani kwake.
Mwanaume yule akajikuna kichwa na kurudi kumtazama Balozi Sapi huku akijaribu kukwepa kumbukumbu mbaya zilizoanza kumrudia kichwani.

“Nilifika kwake leo mapema kabisa, baada ya kuniandikia ujumbe wakunitaka nifike kwake,nikawahi kufika lakini ikawa kazi bure,nilikutana na maiti yake ikiwa imelala sakafuni na tundu kubwa la risasi shingoni lakini pia nilikuta nyumba yake yote imepekuliwa” alisema mtu yule huku kwa mbali machozi yakizilenga mboni za macho yake,akatumia mgongo wa kiganja chake kujifuta.

“sikijua kama inaeza kuwa namna hii na kwa uharaka mkubwa hivyo” alisema Balozi sapi.

“Hakuna namna lazima tutoe taarifa mapema ofisi kuu mheshimiwa” alisema yule mtu.

Balozi akainama kidogo chini ya meza na alipoinuka alikuwa na mkoba mweusi wa ngozi na bila kutoa kilichomo akamkabidhi yule mwanaume.

“kuuawa kwa Bulembo unamaanisha kuwa kuna msaliti kati yetu hapa ubalozini na pia ni ishara kwetu kuwa tayari tunawindwa tusiifikishe taarifa kunakotakiwa,lakini jitihada za Bulembo zimetuongezea uelewa wa hili jambo,hivyo peleka hivi vielelezo ofisi kuu na hakikisha wanahusika na uzuiaji wa hili jambo,msaliti acha aendelee kuwapo hapa ipo siku kiama kitakuwa juu yake…” Balozi Ally Sapi alisema huku akimkabidhi ule mkoba ambao ulikuwa na nyaraka muhimu sana zilizohusu kile walichokuwa wanakizungumzia pale wakati ule.

“kwa walivyokuteka walitaka uwe miongoni mwao sivyo!” alihoji yule bwana huku akipokea ule mkoba na kuutazama.

“Ndio na nilikataa licha ya kuahidiwa mazuri na bwana yule na kukataa kwangu kunamaanisha kifo kwangu hivi karibuni,hivyo basi hakikisha mpango huo unakoma mara moja,nakuamini Honda” alimalizia kusema Balozi Ally Sapi kisha akageuka na kumwacha Honda akigeuka ili atoke ndani ya ofisi zile za ubalozi wa Tanzania nchini Congo.

****

“kuliaa nyuzi sabiniii…hapo!”

“usijali Mimi ndie Kizibo,hata bila ramani yako tayari wamejaa kwenye jicho la mzungu” alijinadi Kizibo huku mkono wake wa kushoto ukiwa unachezea lenzi ndogo iliokuwa inefungwa juu ya bunduki ya kupiga masafa marefu na mkono wake wa kulia ulikuwa umekamata vyema eneo la kufyatulia risasi ya bunduki ile aina ya K2Lapua magnum rifle,bunduki safi ya kisasa ya kudungulia ukiwa umbali wowote ule. Kizibo hakuwa peke yake alikuwa na mtu mwingine eneo lile ambae yeye akikosa kazi huwa anashika kiona mbali na kisha humsaidia Kizibo kusoma masafa ya windo lao.

“Kojo hawa jamaa wanaongea sana,bila shaka wanajadili hii inshu Mzee” alisema Kizibo huku akijitahidi kufinya jicho lake ili kuhakiisha jicho moja linapata nguvu ya kutazama taswira iliojiweka ndani ya lenzi ya bunduki ile ya kudungulia.

Watu hawa walikuwa kwenye lile lile jengo lililokuwa likitazamana na dirisha la ofisi ya balozi Ally Sapi na wakati huu Kojo na Kizibo walikuwa kwenye moja ya vyumba vya jengo hilo la hoteli huku wakiwa wamekwisha kuweka mtego wao usawa wa lile dirisha ambamo kulikuwa kunafanyika mazungumzo kati ya Balozi Ally Sapi na Honda Makubi,mpelelezi na mfanyakazi ndani ya ofisi za ubalozi.

“Huu nao ni mwanya inabidi uzibwe Kizibo”alisema Kojo huku akishusha kiona mbali.

“Yule bwege anae toka na ule mkoba nenda uuchukue kisha utajua cha kumfanya,huyu kipara mimi bamzibua sasa hivi” alisema Kizibo huku akitema mate pembeni na kidole kikielekea kwenye kifyatulio cha bunduki yake alioipenda na kuihusudu sana.

***
Honda Makubi alifika nje baada ya kuwa ameshasaini kitabu cha mahudhurio na wakati huo huo alikuwa anapitisha mawazo ya kurudi nyumbani kwa marehemu Bulembo ama aendelee na taratibu za kupeleka zile nyaraka kuzihifadhi na kufanya utaratibu wa kuzituma ofisi kuu jijini Dar es laam na wao watajua cha kuzifanyia.

Akaingia ndani ya gari lake na kuliondoa kwenye maegesho maalumu kwa ajili ya wafanyakazi wa pale ubalozini,lakini ambacho hakujua japo alihisi ni kuwa watu wawili ndani ya ofisi zile walikuwa wakimtizama wakati akitoka eneo lile na mmoja kati yao akanyanyua simu na kupiga pahali kisha akarudi kuendelea na taratibu zake za kufanya usafi.

***
Baada ya kuhakikisha Honda ametoka ndani ya ofisi zake balozi Ally Sapi alichukua simu yake na kujaribu kumpigia Rais wa Tanzania,lakini ajabu simu yake ilikataa kutoa mawasiliano nje ya nchi ile ya Congo,akachukua tena simu nyingine maalumu ambayo hutumia kuwasiliana na mkurugenzi wa usalama wa Taifa nayo ikagoma.

Akiwa kashikwa na mashangao na hamaki ya kutoamini,Balozi akaanza kuzunguka ofisi yake kama asie amani uwepo wake mle ndani na hapo ndipo akalikumbuka tena dirisha lake na haraka akataka kuwahi kuishusha pazia.
Doh
Alikuwa amechelewa.
Risasi yenye nguvu ikatua katikati ya paji la uso wake na kusambaratisha kichwa chake kisha kumsukuma nyuma kwa nguvu na mwili wake usio na mhimili wa utimamu ukajibwaga chini kwa kishindo kisha kwa jitihada kidogo ukajitikisa kidogo na kutulia na ukawa mwisho wa Balozi Sapi.

Kule risasi ilikotokea,Kizibo akatema mate mengi chini.
“pyutyaaa”
Kisha akajiramba midomo yake na kuinyanyua bunduki yake na kisha akaanza kuitawanya huku akipiga mluzi hafifu wa ushindi.

*****

Honda Makubi aliegesha gari yake ndani ya geti la la nyumba ya marehemu Bulembo ,kisha akashuka taratibu na huku akiangaza huku na huko kwa umakini wa hali ya juu.

Kama alivyokuwa amepaacha ahsubuh na ndivyo alivyopakuta pakiwa katika utulivu wa kifo huku maiti ya mmliki wa nyumba ile akiwa ndani hana uhai japo wa kupigia chafya.
Honda akasimama kuupisha utulivu katika akili yake na muda huo mikono yake ilikuwa ikifanya jitihada za kujivika mipira maalumu ya viganja vya mikono.

Alipohakikisha amevaa sawia mipira ile,akapiga hatua ndefu na kuufikia mlango kisha akaufungua taratibu huku utulivu ukiwa ni ngao yake muhimu wakati ule.
Taratibu akachungulia ndani kwa tuo, na kutoka pale alipokuwa aliona mwili wa mpelelezi Bulembo ukiwa umelala vilevile alivyouacha na pembeni yake aliona mparanganyiko wa sofa ukiwa kama alivyoacha hapo ahsubuhi,akapiga hatua nyingine kubwa na kwa haraka zaidi kisha katika uharaka huohuo mikono yake ikaurudishia mlango na kuacha ukijibamiza kwa nguvu nyuma yake huku yeye akiwa hana habari nao tena.
Akatazama mazingira ya mle ndani,hakuona mabadiliko yoyote wakati ule. Akapiga hatua na kuufikia mwili wa hayati Bulembo,kisha akainama na kuanza kupekua mifuko ya suruali aliokuwa amevaa hayati Bulembo.
Katika dakika za mwanzo hakuona la maana katika jitihada zake za upekuzi katika mwili ule uliolala bila uhai.
Akasimama huku akili yake ikianza kujutia muda aliopoteza kurudi nyumbani kwa hayati Bulembo.
Hakuwa sahihi katika mawazo yake,hadi pale macho yake yalipo elekea miguuni mwa maiti aliokuwa akiipekuwa wakati ule na hapo tena akili yake ikaganda bila kufanya jitihada zozote za kutaka kujilaumu kama mwanzo.
Bila kufikiri zaidi,mwili ukafanya vitendo.
Haraka akainama na kupeleka mikono yake kwenye mguu wa kulia ambao ulikuwa umevikwa soksi huku ule wa kushoto ukiwa hauna soksi.
Akaivuta ile soksi na wakati ikimalizikia kuvuka akaona kikaratasi kidogo kikianguka kutoka ndani ya soksi ile.
Honda Makubi alitabasamu huku sasa akili yake ikijipongeza kwa kuwaza kurudi tena ndani kwa hayati Bulembo.
Akainama kuikota ile katasi na wakati ikiwa imeenea kiganjani kwake na mwili ukifanya jitihada za kunyanyuka baada ya kuwa umeinamishwa kuanzia tumboni kwenda juu,mwili wa Honda haukumaliza hilo tendo na mara hiyo kikafanyika kitendo cha haraka na wepesi wa hali ya juu kutoka kwa Honda japo matokeo yalikuwa ni kukosea hesabu za gafla.
Wakati akitaka kusimama akaona kivuli kikiwa karibu yake na mara hiyo akasikia msukumo mkubwa kutokea kiunoni kwake na haraka akajirusha mzima mzima kwenda mbele na bahati mbaya hakuwa ameiona meza iliokuwa hatua chache kutoka pale alipokuwa na alipotaka kujigeuza ili aone kilichomsukuma akajikuta akisambaratika chini baada ya kuipamia meza na kusambaratika nayo chini.
Hakuzubaa
Muda huo huo akajigeuza kwa namna ya ajabu kabisa kisha akatumia mkono mmoja kukita chini huku umbo lake refu likiwa wima katika nukta iliofuata na macho yake yakashuhudia kasi ya ajabu ya kiumbe mweusi na mrefu akimfuata kwa kasi ya upepo na kabla hajasimama imara akajikuta akipokea mateke mawili yaliopigwa kwa mtindo wa tandika reli nae hakuwa amajiandaa kwa hilo akaenda chini mazima kwa mara ya pili.
Hakuzubaa tena mana alishaona kasi na ujuzi wa adui yake,haraka akajizoa na kusimama wima huku akisikia maumivu yakimtambaa mwili mzima kuanzia kifuani,na hapo akajikuta akimsifu adui yake yule kwa kuwa na kasi na nguvu ya kumtetemesha namna ile.
Akajipanga.
Adui akausoma usimamaji wa Honda na akajua anapambana na mtu wa kiwango chake nae akafanya haraka ya kuokoa muda na hilo likawa kosa upande wake.
Adui akarusha ngumi kwa ustadi kumwelekea Honda,lakini Honda aliiona na kama utani akahepa na ngumi ikapiga hewa kisha kwa usitadi mkubwa akaachia konde lenye uzani uliokadiriwa na likampata adui ubavu wa kushoto na adui akabweka kama malaya kichochoroni.
Honda akaachia tabasamu la upande kisha akachumpa na kusimama nyuma ya adui aliekuwa anafanya jitihada za kupambana na maumivu ya mbavu zake,kisha akaachia teke moja kali lililojikita usawa wa maungio ya kiuno na uti wa mgongo na adui akabweka tena kwa mara ya pili huku Honda akiachia tabasamu lingine la ushindi na akihepa tena kujiweka mbali na adui aliekuwa anageuka kwa gadhabu.
Kisu.
Honda aliona kisu mkononi mwa adui na hapo akajipongeza kwa zile hesabu zake za kuwa mbali na adui.
Adui alitupa mikono harakaharaka kumchanganya Honda kisha akaachia teke kali lililopanguliwa kistadi na Honda kisha adui akatumia nafasi ile kumchapa konde kali la mbavu kama malipizi na huku akiachia ukelele wa furaha kwa lipizi lake.
Honda akayumba kwa kupoteza malengo kisha akafanya jitihada kusimama imara.
Hakufanikiwa.
Adui akatumia nafasi ile kumshindilia tena mateke mawili ya kifua na kumtupa kwa kishindo sambamba na kabati la vioo lililokuwa sebuleni pale na kusambaratika chini huku vioo vikimjeruhi hapa na pale.
Kutoka pale alipokuwa ameangukia,Honda alimshuhudia adui yake akinesa kwa aina ya ajabu kabisa na kumfikia pale alipokuwa huku kisu kikiwa kimeshikwa imara mkononi,Honda hakutaka kufa kizembe kwa nguvu alizobakia nazo akasimama kwa kasi kisha akajirusha huku mikono yake ikimkumbatia adui usawa wa kiuno na bega likijikita katikati ya tumbo na kumbwaga kwa nguvu chini ya zulia.
Ingekuwa ni mieleka basi hii ingekuwa ni Roman spear,ila hii sasa wakati huo ilikuwa ni Honda spear.
Walipoanguka chini Honda alizisikia kelele za adui yake wazi wazi masikioni mwake na na yeye akajinasua haraka kutoka pale chini akabaki akiwa amesimama huku akitweta kwa maumivu ya majeraha ya kukatwa na vioo vya kabati.

“Bwege sana wewe”
Jamaa alibweka pale chini huku akijizoa zoa kutoka chini na hapo Honda akapata kumtazama vizuri adui yake na akaona kovu baya usoni pake ambalo dhahiri lilimpa tabu sana yule jamaa kuliuguza bila shaka na lilielekea kumtoa jicho upande wa kushoto.
Kovu lile liliongezea mvuto mbaya kabisa katika sura nyeusi ya shababi yule.

“aah nusura univunje kiuno haini wewe” jamaa alizidi kulalama huku akifanya jitihada za kuupata mhimili mzuri kwa kusimama.

“unataka nini kwangu!” hatimae Honda aliuliza.
Na hapo akashuhudia yule bwege akikenua vibaya na hapo Honda akapata kuona kinywa kibaya kutoka kwa yule jamaa.
Kinywani hakuwa na meno mawili ya mbele na ulimi ulikuwa mweusi tofauti na ndimi za binadamu wa kawaida.
“nautaka mkoba mweusi komredi”
Jamaa alijibu swali la Honda.
Honda akatumbua macho kwa umakini kisha akauliza tena.
“mkoba upi?”

“ule uliopewa na Balozi”
Eh bana eh
Honda akizubaa kwa nukta kadhaa za kutoamini kilichosemwa na adui yake.
Kwa nini!.

Kwa sababu alipewa mkoba na Balozi Sapi ndani ya nusu saa iliopita na hakuwa amemuonesha yeyote ule mkoba muhimu wakati ule.
Honda akakumbuka aliuacha ndani ya gari huko nje.
Hata!
Akaruka juu kisha akaachia teke kali lilokuwa likimwendea yule jamaa,jamaa akalegea kidogo na kulikwepa lakini hakujua hila za Honda akajikuta anapokea konde zito katikati ya kifua,jamaa akabweka kama ngedere anaeiba mahindi.
Adui akaenda chini mazima.
Honda akamwendea huku akiunguruma kwa gadhabu lakini hakufika kwa adui yake ambae alijiinua kwa mtindo wa aina yake kisha akaruka kama kima na kuufikia mlango na kutokomea nje kwa kasi ya umeme.
Honda hakukubali Nae akapiga tambo kubwa na kuufikia mlango,haraka akatoka,lakini kasi yake haikumpa matunda aliotaka,isipokuwa kitu pekee alichoambulia ni kuona namna yule jamaa alivyokuwa akimalizikia nje ya geti na kuliacha likijipigiza kwa nguvu.
“Mkoba!!” Honda alijisemea huku haraka akikimbilia gari lake na kujilaumu kwa uzembe wa kutokutembea nao.
Akafungua mlango wa gari lake na kitu cha kwanza ni kuelekeza macho yake pale ulipokuwa mkoba ule ambao sasa alianza kuupa manani kwa kuwa kuna adui asie mjua akiuwinda.
Kwanini! Hakujua japo alihisi.
“kina nani hawa?” alijiuliza huku akianza kutoka ndani ya ile nyumba ya hayati Bulembo.
Akiwa tayari ametoka nje ya uzio wa nyumba ile,mara akasikia ving’ora vya magari ya polisi vikielekea kule alikotokea.
“shiit!!!” alimaka kwa gadhabu kwa kutoelewa ni nani aliewapigia polisi wa Congo katika uharaka wa namna ile.
“Mambo yanazidi kunoga aisee” alijisemea huku akiongeza mwendo wa gari lake kurudi kwa balozi Sapi kumpa taarifa ya alichokiona kule kwa Hayati Bulembo.
Hakujua yajayo…
***


Aisee hii kama muvi kabisa..
Inanikumbusha Enzi za akina Joram Kiango,Sargent vata,.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Mwasu kakichafua
RIWAYA : MPANGO WA CONGO

SEHEMU YA 27

SIMU 0758573660


***

Mtega nyoka hakuwa mbali na nyumba ya Mwasu ila alishindwa kuingia baada ya kuona tukio fulani akiwa hatua chache kutoka ilipokuwa nyumba ile.

Alikuwa na mwenyeji wake aliemwongoza pale.

Mwenyeji alimwonesha tu wakiwa mbali nyumba ya Mwasu.

Ni wakati akipiga hatua fupifupi ndipo alipoona watu wawili kibalazani.

Mmoja alikuwa amesimama na mwingine amekaa.

Aliekuwa amesimama alikuwa na wajihi sawa na mtu aliepambana nae Buzuruga Plaza siku kadhaa nyuma.

Mtu aliekuwa amesimama alimwona alivyochomoa bastola yake kutoka kiunoni kwa kasi ya ajabu na kumwelekeza jambo mtu aliekuwa amekaa.

Mtu aliekuwa amekaa wakati anasimama ndipo mtega nyoka alipomuona vyema.

Alikuwa ni Malima.

"Kumekucha!!" alijisemea Mtega nyoka..

Alijibanza nyuma ya nyumba iliokuwa jirani.


Haukupita muda mrefu aliona wakitokea vijana wengine wawili na kuingia ndani.

Zilipita dakika tatu ndipo alipoona watu watano wakitoka ndani huku wawili wakiwa ni Malima na Remi.
Na wengine ni mtu mrefu waliepambana Buzuruga Plaza na vijana wengine wawili.

Nyuma yao alitokea Binti mmoja mrembo sana ambae aliishia mlangoni tu na kuwasindikiza kwa macho.

Watu wale ambao walitembea ki kawaida tu bila kuonesha kama kuna mateka kati yao,walipita nyuma ya nyumba walimokuwamo na kutokea kwenye uwanja wa kanisa la Wokovu.

Huko walikuta gari ikiwa imenawangojea!

Wakapanda na kuelekea barabara kubwa kwa kupitia Nyakato shule ya msingi kisha wakakamata barabara kubwa na kuwa kama wanaelekea buzuruga.

Walipofika kona ya Nyakato sokoni,walikunja na kuelekea Meko,walipita karibu na baa ya ShaTemba na kuelekea njia ya vumbi ya Meko majanini.

Nyuma yao alikuwapo Mtega nyoka safari hii akiwa na pikipiki alioendesha mwenyewe huku abiria akiwa ni mwenye pikipiki.

Kwa msaada wa mwenye pikipiki, alimwelekeza kama wenye gari wamepitia njia ya Meko majanini basi wataenda kutokea njia ya Meko shule ya msingi hivyo wao waelekee shuleni na wangoje hapo.

Baada ya dakika kadhaa ilipita gari ya wagonjwa ikitokea Meko majanini.

Mtega nyoka aliona mtu aliekuwa amekaa kushoto mwa dereva.

Alijua wamebadilisha gari!

Akaifuata gari ile ya wagonjwa.

Safari yao ilikuwa ya uangalifu sana ili wasije wakashitukiwa.

Gari ile ilienda kuishia makanisa matatu na ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Mtega nyoka kufika eneo lile.

Hapo ndipo Mtega nyoka alipoona majengo sawa na yale yalioko kwenye kadi alioichukua mifukoni mwa mvamizi aliemuua bwana Kindo Seleman; Mkurugenzi wa Kasuku Contractors.

"Sasa kama ni kanisa ile kadi ya nini?" alijisemea Mtega nyoka huku akielekea kwenye makazi ya mchungaji wa kanisa la Efather.

Bado Mtega nyoka nae alikuwa anashangaa harakati zilizokuwa pale.


Akili yake ilishindwa kabisa kupata walau lililokuwa likiendelea pale.

Kama ni kikao basi ilitakiwa watu waingie na kutulia! Ila watu walikuwa wanaingia na kutoka.

Lakini pia yalikuwa ni mavazi yao.

Mavazi waliovaa ilitakiwa yavaliwe na waumini wa madhehebu ya Roman Catholic ama KKKT na si vinginevyo!!

Kwa mtazamo kanisa lile lilikuwa sawa na kanisa la kakobe ama Mzee wa upako ama wachungaji wenye sifa za utajiri kuliko uwezo wa waumini wao.

Sasa tangu lini makanisa ya aina hiyo yakawa na watawa?

Ajabu hii.


Ilikuwa ni wakati akitoka huko kwa mchungaji ndipo alipomuona mwanamke alievaa hijabu jeusi na kufunika uso wake wote na kubakiza macho tu.

Mwendo!!.

Aliutazama mwendo wa mwanamke yule.

Hata!!

Mwanamke gani huyu anatemebea kama kakanyaga moto!!

Aliachana nae akapanda pikipiki iliomleta pale na kutokomea.

Mwanamke wa hijabu nae akapanda pikipiki iliomfikisha pale na kuondoka.

Huku malipo ya dereva akimwandikia kwenye karatasi na kumuomba dereva afike kituo cha polisi atapewa pesa yake yote endapo akimwonyesha karatasi ile OCCID.

Dereva wa pikipiki akakubali japo roho ilimdunda.

Polisi hakuzoeleki!!


*****

Solomoni Bukaba alirudi ndani kwa Sundi na kuvua yale mavazi kisha akaenda kuyarudisha kama alivyoyakuta na kurudi kule chumbani alikokuwa amelala.

Akalala kama alivyoachwa.

****

Mtega nyoka alikuwa ameona Malima alivyotekwa pamoja na Remi.

Hivyo akapanga kurudi hadi nyumbani kwa Mwasu ili ambane Mwasu.

Hakuchukua zaidi ya saa mbili akawa yupo mlangoni kwa Mwasu.

Akagonga na kutulia.

Punde mlango ukafunguliwa akachomoza binti mrembo mwenye asili ya watu wa Rwanda ama Burundi.


"Nikusaidie nini!" Alisema Mwasu huku akimtizama Mtega nyoka usoni kwa makini.


Mtega nyoka alitabasamu.


"Nikaribishe ndani tuzungumze kidogo," alisema Mtega nyoka.

"Nakuingizaje ndani sikufahamu? Alisema Mwasu.

Mtega nyoka alikaa kimya kisha akatazama kushoto na kulia,alipoona kupo shwari Hakuna mtu akafanya kitendo cha haraka na kasi ya ajabu.

Akamsukuma Mwasu ndani kwa kasi kisha akatulia na kufunga mlango kwa nyuma.

Mwasu alijinyanyua chini huku akishangaa kasi alionayo bwana yule ambae alikuwa amesimama akimwangalia tu.

"unataka nini kwangu?" aliuliza Mwasu huku akijifuta kitu asichokiona mwilini mwake.

"naomba kufahamu alipo Malima" alisema Mtega nyoka.

Mwasu alishangaa!

"Malima?; mbona simjui!" alisema Mwasu.

Mtega nyoka akacheka kisha akatazama juu ukutani.


"Huyo uliebandika picha yake hapo ukutani ndie ninae mtaka" alisema Mtega nyoka huku akisonta kwa kidole picha kubwa iliokua imebandikwa ukutani.

Mwasu akagwaya huku akijutia uongo wake alioutoa bila kufikiria.

Mwasu alijua yupo matatani hivyo lazima afanye jihada za kujinasua kisha aombe usaidizi kama atashindwa kumdhibiti Mtega nyoka.

"Mi sujui alipo!" alisema Mwasu huku akimtizama usoni Mtega nyoka.

"Na Remi je!" aliuliza tena Mtega nyoka.

Mwasu alikodoa macho huku akishindwa kuelewa dhamira ya mgeni wake huyo.

"Hebu sema shinda yako bwana mana naona sikwelewi; Malima; Remi tuelewe lipi sasa" alikoroma Mwasu.

"Ukinijibu wote kwa pamoja itakuwa vizuri sana" alisema Mtega nyoka.

"watafute mwenyewe utajua walipo" alisema Mwasu.

Mtega nyoka alitulia kimya akimtizama Mwasu.

"Vipi kuna nini pale Makanisa matatu?" lilikuwa swali la mtego ambalo Mwasu hakulitarajia.


Akaingiwa na ubaridi wa gafla.

"Sasa mbona wafahamu mengi, kwanini waniuliza?"


"Kwa sababu na..." Mtega nyoka hakumaliza kauli yake alijiukuta akirudi nyuma kwa kasi na kujipigiza kwenye mlango na kusambaratika chini.


Mwasu alikuwa amemfanyia shambulizi la kushitukiza.

Mtega nyoka aliharakisha kunyanyuka ila alijikuta akienda chini tena baada ya kupigwa teke ubavuni.

Mwasu hakutaka kucheza na mtu kama yule.

Akapaa juu na kurudi na pigo la kifo.

Mtega nyoka aliliona akakwepa kisha akaachia konde zito lililompata Mwasu tumboni.

Mwasu akaenda chini huku akitoa kilio kama cha mwanamke anaebakwa.

Mwasu akasimama ila akajikuta anaingia kwenye wakati mgumu kujiokoa na makaonde mfululizo kutoka kwa Mtega nyoka.

Yapo aliopangua na mengine yalijaa mwilini mwake.


Mwasu akaona akifanya uzembe atakuwa mateka ili aseme anachokijua.

Hakutaka hilo litokee.

Akajifanya kama anaenda chini ila hakufika badala yake alifyatuka kichwa kikali kilichotua tumboni kwa Mtega nyoka na kumpeleka chini. Kisha yeye akasimama haraka na kujirusha mzimamzima na kwenda kulikumba dirisha la vioo lililokuwa sebuleni pale na kusambaratika nalo nje kisha bila kujiuliza akasimama na kutimua mbio za mbwa mwizi.

Mtega nyoka nae aliharakisha kutoka kwa kupitia pale pale dirishani baada ya kuwa wazi kwa kuvunjwa.

Alipotua nje hakuona hata unyayo wa Mwasu.

Alikwama tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Riwaya :Mpango WA kongo

Sehemu ya nane


Lakini mbali na hivyo alikuwa na mtego wake kwa yule mhudumu mana kama mhudumu akisimama kutoa chenji asimkute, basi lazima atatoka nje kumtafuta na ndio mana alikuwa anaelekea kwenye nyumba za kanisa ili atizame vizuri harakati za kuingia na kutoka ndani ya mgahawa ule wa Tunde.

Haikuwa dakika nyingi alichokitarajia alikiona!!

****

Mhudumu alipigwa na butwaa bada ya kuinuka na kumkosa mteja wake.

Akapagawa!!.

Alipagawa kwa sababu hakudhani, sekunde chache vile mtu ampotee kirahisi tu.
Akajaribu kungojea dakika moja au zaidi, lakini tofauti na matarajio yake hakumuona Honda.

Akaamua kutoka nje lau aone uelekeo aliopitia ili tarifa yake ikamilike kwa wakubwa wake.

Mhudumu yule alitoka hadi nje, akaangaza kushoto na kulia hakuona mtu wala kivuli chake.

Shiiit!!” mhudumu akamaka huku mikono ikiwa imeshika kiuno asijue afuate lipi.

Akiwa hajui lipi afanye mara gari ikasimama karibu na miguu yake na hakujiuliza mara mbili akasogea kwenye kioo cha upande wa dereva,akasikiliza kidogo kisha akarudi akandoka kurudi mgahawani.

Kutokea pale alipokuwa ametulia; Honda aliyaona yote yaliofanywa na mhudumu yule nje ya mlango wa mgahawa wa Tunde.

Hata wakati gari inakuja na kusimama na kisha kuzungumza na walioko ndani ya gari, yote Honda aliyaona na sasa alitaka kuona watu wale waliokuwa ndani ya gari wangelifanya nini, lakini pia hakujua wapo wangapi japo aliamini ni zaidi ya mtu mmoja.

Aliendelea kusubiri hadi aone hatima ya watu wale.

Baada ya dakika kadhaa milango ya nyuma ya ile gari ikafunguliwa na kutoka kila upande wakashuka wanaume wawili waliojazia kimazoezi hasa. Wanaume wale wakaangaza huku na huko kisha wakaingia ndani ya mgahawa ule wa Tunde.

Katika hesabu za Honda aliamini ndani ya gari kutakuwa bado na watu wawili,mmoja dereva na mwingine yupo upande wa pili wa dereva.

Kwa kasi aliambaa na kuta za nyumba kadhaa kisha bila kuonesha tashwititi yoyote akavuka barabara huku hesabu zake zikiwa ni namna ataweza kuifikia ile gari bila kutiliwa shaka.

Alipovuka barabara tu akainamisha uso chini kisha akaanza kutembea kama mlemavu mwenye mguu mmoja mfupi na mwingine mfupi huku mkoba ukiwa unaning’inia mgongoni.

Hila za Honda zikazaa matunda, hadi analifikia lile gari hakuna aliekuwa amemtilia shaka na kwa kasi ya hewa akafungua mlango wa nyuma na bila kujiuliza akakaa kwenye kiti huku akiwa amewaelekezea bastola wale watu wawili waliokuwa wamekaa viti vya mbele wakiwa na mzubao usio semekana huku dhahiri hofu ikiwa juu yao.

“ondoeni gari hapa!” alisema Honda huku akiwa makini ili asifanyiwe fitina.

Hakuna aliemjibu wala kutekeleza amri yake nae akajua jamaa wanapoteza muda ili wale mabaunsa watokee na wakitokea hatari ipo kwake tu.
Hilo kamwe hakutaka litokee.

Bastola yake iliokuwa na kiwambo cha kuzuia sauti ikatema jiwe la moto na kupenya katikati ya uti wa mgogo wa mtu aliekuwa upande wa kushoto wa dereva na wala mtu yule hakuomba hata maji akawa hana mawasiliano huku damu ikimwagika kama bomba bovu.

Dereva hakuwa na namna, akaiondoa gari bila kujua ni wapi anapaswa kuelekea.

“endesha hadi nitakapokupa maelekezo mengine.” Sauti kavu ya Honda ikaunguruma bila chembe ya mzaha.

****
Safari ya Honda ilikuwa imegubikwa na ukimya wa kutisha na baada ya kitambo kidogo Honda akamwelekeza pahali alipopswa kugesha gari.

Mateka aliegesha gari kando kidogo ya nyumba ya marehemu Bulembo na
Baada Yakuhakikisha mateka wake amezima gari, kwa kasi ya radi akampiga kwa kitako cha bastola chini kidogo ya kisogo na mateka wake akapoteza fahamu hivyo ndani ya gari akawa na watu wawili, mmoja hana fahamu na mwingine bila uhai.

Haraka akashuka na kulekea lango la kuingilia ndani ya nyumba ya Bulembo na alitegemea kukuta utepe wa polisi wa kuzuia aisehusika kuingia pale na ndivyo ilikuwa.

Licha ya kuwapo utepe, pia kuliwa kimya sana kuashiria hakuna askari anaelinda pale na kuhakikisha zaidi akaingia hadi ndani ya utepe na kujaribu kuita ila hakuitikiwa zaidi alisikia sauti yake tu ikitengeneza mwangwi kwenye eneo pweke.

Haraka akarudi kwenye gari na kumchukua mateka wake ambae bado alikuwa amepoteza fahamu, akaingia nae moja kwa moja ndani na huko akamfunga vizuri kwenye kiti kisha akarudi ndani ya gari na kuliondoa kurudi walikotokea ambapo kwa kitambo fulani akaingia njia za vichochoro kulitelekeza gari ile na maiti yake. Huku akichukua baadhi ya vitu alivyodhani vinaweza kumsaidia.

Alikodi usafiri binafsi na kurudishwa hadi karibu na nyumba ya Bulembo, akalipa pesa kisha akaelekea kwenye kichochoro fulani lengo likiwa ni kumchanganya dereva endapo akibanwa huko ili atoe taarifa zake.

Huko huko alikopitia akajikuta yupo ndani ya mitaa yenye nyumba anayoihitaji.

Alipokwisha kuingia ndani, moja kwa moja akaanza upekuzi wake huku akiwa amemweka mateka wake kama kiporo.

Licha ya kukuta ukaguzi wa hali ya juu lakini bado aliamini kuna kitu kitakuwa mle ndani chenye kuweza kumsaidia hasa katika mambo matatu makubwa.

La kwanza ni kujua mhusika wa mauaji ya Bulembo na balozi Aly Sapi, lakini kubwa zaidi ni kuhusu tetesi za kuwapo mtu ambae historia hailezi wazi kuhusu kifo chake, na sasa tarifa za mwanzo za marehemu Bulembo zinasema yupo hai na anampango wake mahususi juu ya nchi ya Tanzania.

Mpango gani;?

Ndilo lilihatajika kufumbuliwa na mpelelezi Honda.

Honda alikuwa ametumia zaidi ya dakika kumi na tano bila kupata hata dalili ya maelezo yenye kumsaidia.
Alijishika kiuno huku akitembeza macho kila kona ya chumba kilichotumiwa na Bulembo kulala huku kichwani akifikiria kuacha kufuatilia njia aliotumia Bulembo mana inazidi kumwacha njia panda na muda unazidi kwenda.
Alitamani sasa kuingia kivingine na kwa njia zake ili apate ukweli wa sakata lile.

Wakati akili ikitafakari maamuzi; macho yakanasa kitu ukutani juu kidogo ya mto na mto huo ulionekana ndio ulikuwa unatumiwa na marehemu Bulembo kwa kuwa ulikuwa unaonekana kuwa na mafuta ya nywele yaliotengeneza weusi kidogo kwa kulaliwa mara kwa mara.
Juu kidogo ya tendegu la kitanda aliona mikwaruzo, akasogea kwa hatua za aste aste na alipofikia karibu aliona maandishi ila yalikuwa ni maandishi yale yale alioyaona kwenye kikaratasi alichokitafuna wakati akiwa mikononi mwa Sajini Kebu.

Na yalikuwa yamepangiliwa vile vile kama yalivyokuwa kwenye karatasi alioitafuna.

“142BOULEVARD DU JUIN
B. P. 1612
KINSHASA CONGO (81)”

Aliyatazama tena maandishi yale, bado hakuwa amepata walau wazo la kujua Bulembo alitaka kumaanisha nini japo alijua hii ilikuwa ni anuani ya ubalozi wa Tanzania Lakini kilichomchangaya zaidi ni ile alama ya mabano kisha zikafuatia namba (81) ilimaanisha nini hii namba! Hakujua wala kufikiria mbali zaidi ya kuzidi kuchanganyikiwa na asijue afuate lipi katika anuani ile

***
Angalizo ; Mnaosoma na kupita kimya kimya hamtendi haki kabisa, kama haivutii sema, umependa sema pia huo ndio ujira wangu wala sihitaj pesa yako ili niendelee kuweka hapa mtaji Pekee ni koment yako ambapo itasaidia watu wengi kuisoma.

Au mnataka na kusibiri isitishwe ndo muibuke na kutoa mitusi? Wakati inapopostiwa hatuwaoni?
Karibuni kwa maoni


Hili ni zaidi ya stori


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Safi sana, mambo yazidi kunoga. Kitendawili kinaanza kuteguliwa taratibu
 
Aisee hatari sana asije akaenda kule aliko Solomon Hahaha kitumbua kimeingia,mchanga
 
Back
Top Bottom