Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
RIWAYA : MPANGO WA CONGO
SEHEMU YA 23
Zahanati ya Rorya ndio iliowapokea majeruhi wa ajali iliotokea karibu na kiwanda cha samaki cha Nile perch.
Walikufa watu watatu akiwemo ofisa mmoja wa Polisi aliekuwa ndie dereva wa gari ile.
Miongoni mwa majeruhi wale alikuwamo Remi ambae alipata majeraha kichwani na baadhi ya sehemu mbalimbali za mwili.
Kitu pekee alichokumbuka kukihifadhi ni mkoba wake mdogo ambao alitembea nao kila sehemu.
Alitamani kutoka kwenye kitanda hasa baada ya kukumbuka jinsi alivyonusurika kuangukia mikononi mwa Mwendesha pikipiki.
Na ilikuwa ni kukosea hesabu labda upande wa wabaya wa Remi mana ajali ilitokea hatua mia kutoka kilipo kituo kidogo cha polisi cha Mwatex.
Na kwa kuwa gari lililopata ajali lilikuwa ni la Polisi; haikuchukua lau dakika mbili kabla askari Polisi hawajajaa pale hivyo kufanya mwendesha pikipiki akose lengo lake na kutimka.
Remi mwili haikurusu kabisa kuinuka na kuendelea na shuguli zake.
Akaamua kutulia tu..
Upande mwingine Mtega nyoka bado alikuwa hajapata la kuamua kabisa.
Aliona anahitaji kumpata Malima lakini pia aliona ni vyema akimpata Remi. Wote walikuwa muhimu kwake kwa wakati huo na aliwahitaji.
Akanyanyuka na kuligawa gazeti kwa mtu mwingine kisha akaita pikipiki alihitaji kwenda Kasuku Contractors haraka iwezekanavyo.
.
Haikupita hata dakika kumi akawa amefika zilipo ofisi za Kasuku Contractors.
Alimlipa dereva wa Pikipiki na kuelekea ulipo mlango wa utawala..
Alifika kwa binti aliekuwa amekaa mapokezi..
Hakukaa sana ni baada ya kuelekezwa nyumbani kwa mkurugenzi wa kampuni bwana Kindo Selemani na msanifu mkuu bwana Malima ambao wote hakuwakuta ofisini.
Akachomoka kuwahi ilipokuwa zahanati ya Rorya.
Nusu saa tu ilitosha kumfikisha mbele ya zahanati ile ya Rorya.
Ila alichokuwa amekifuata hakukikuta!!
Eba eeh!!
***
Mwasu alizipata taarifa za Remi kupelekwa kwenye zahanati ya Rorya. Vile alipata taarifa haijulikani ama ni kwa kusoma gazeti ama kwa mtu tofauti!
Alijua yeye!!
Baada ya kukamilisha taratibu za kulipia malipo ya huduma aliopokea Remi; Mwasu akapewa nafasi ya kwenda kuonana na mgonjwa wake ambae alijitambulisha kwenye uongozi wa zahanati kama ni Dada yake.!!
Tabasamu lilijijenga usoni mwa Remi baada ya kuomuona Mwasu na Mwasu nae alijawa na tabasamu lisilosemekana baada ya kumuona Remi.
Ilikuwa ni furaha baina yao!!.
"Nimekutafuta sana Dada yangu!!" alisema Remi baada ya kujaribu kuinuka na kuweza kukaa japo kwa shida kidogo.
"Usijali mdogo wangu,tumekwisha kuonana!!" alisema Mwasu huku akienda kumkumbatia Remi.
Walikumbatiana zaidi ya dakika tatu huku kila mmoja akiwa na hisia zake juu ya mwenzake kisha wakatengana.
Remi alijifuta machozi na kumshuhudia Mwasu nae akifanya vivyo hivyo.
Ilikuwa ni furaha iliochanganyikana na huzuni.
"Pole sana mdogo wangu!!" alisema Mwasu huku akikaa karibu na kitanda cha Remi.
Lakini kwa dakika chache tu Remi alizokaa na Mwasu alitambua mabadiliko makubwa kwenye mwili wa Mwasu.
Hakuwa Mwasu yule waliotengana miaka kadhaa kwenye kambi ya wakimbizi. Mwasu ambae alikuwa legelege na nyama uzembe nyingi.
Huyu alikuwa ni Mwasu alietengeneza mwili wake na kuwa wa kuvutia sana huku nyama zote zikiwa zimekaa pahala sahihi.
Mazoezi yalimjenga.
Remi hakujua ni mazoezi ya kawaida ama ni zaidi ya mazoezi ya kawaida.
Lakini pia Remi aliisikia mikoni imara ya Mwasu wakati wakikumbatiana.
Kwanini!? Hakutaka kujua hilo.
"Ahsante Dada" Hatimae alisema Remi.
"Jana nilipata taarifa zako,ila nilipofika pale nilipoambiwa upo sikukuta, nilihangaika hadi niliposoma gazeti ahsubuhi hii ya kuwa upo hapa na Majeruhi wengine kwenye ile ajali" alisema Remi huku bado akimtizama Remi.
Remi alitizama pembeni,kumbukumbu mbaya ya kilichotokea usiku ule ilimrudia, akajikuta chozi la uchungu linamtoka.
"Usijali mdogo Wangu,pumzika kwanza kisha utanisimulia tu!!" alisema Mwasu huku akimfuta machozi kwa upande wa Kanga aliokuwa amevaa.
Mwasu alitoka kidogo na baada ya dakika kadhaa alirejea.
"Mdogo wangu inabidi hapa tuondoke ukatibiwe sehemu nyingine! Huduma za hapa ni chini ya kiwango" alisema Mwasu.
Remi alishukuru kwa ukarimu wa ndugu yake huyo.
Kwa msaada wa matabibu wawili waliomsaidia kutembea kwa kumshika huku na huku,walifanikiwa kumuingiza ndani ya gari iliokuwa imesimama nje ya uzio wa Zahanati ile.
Wakati gari ile inaondoka pale ni wakati huohuo ambao pikipiki iliombeba Mtega nyoka iliingia ndani ya zahanati ile.
"Dakika chache zilizopita kuna mtu kasema ni Dada yake, amemchukua kwenda kwenye matibabu zaidi" alieleza Tabibu mmoja..
"Kasema ni hospitali gani wataelekea?" aliuliza Mtega nyoka.
"Hapana!!" alijibu Tabibu.
"naombeni kuona taarifa zake huyo aliemchukua mgonjwa!" aliongea kimamlaka Mtega nyoka.
Tabibu alibabaika kidogo! Ila baada ya kukutana na jicho kavu la Mtega nyoka; alitoa kitabu cha wageni.
Mtega Nyoka alisoma vyema namba za simu na mtaa alioishi Dada wa Remi;Mwasu.
.
Akaondoka kurudi Kasuku Contractors.
****
"Ni nani anahusika na usajili wa magari ya kampuni!" alihoji Mtega nyoka punde tu alipofika kwenye meza ya mapokezi.
"Kila kitu hufanywa na mkurugenzi!" alijibu binti aliekuwa mapokezi.
Ndilo jibu alilohitaji Mtega nyoka.
Akapitiliza hadi ofisi iliokuwa imeandikwa "MKURUGENZI" huku nyuma hakuzijali kelele zilizopigwa na dada wa mapokezi aliehitaji aombwe ruhusa y kuelekea huko ofisi za utawala.
Baada ya kugonga mlango na kuruhusiwa kuingia; Mtega nyoka akasukuma mlango na kuingia ndani.
Alikutana na sura ya Mzee wa makamo na kibao kilichokuwa mbele yake kilichokuwa na jina la Kindo Selemani.
"Kilichonileta kwako ni jambo dogo ila linaweza kuchukua muda kidogo kama..." alisema Mtega nyoka ambae alikatishwa na sauti ya majivuno ya Kindo.
"Sema shida yako moja kwa moja kijana tusipotezeane muda"
"Naomba kujua idadi ya gari zinazomilikiwa na kampuni yako tafadhali" alisema Mtega nyoka.
Kindo alishituka baada ya kusikia swali hilo.
Mshituko ambao Mtega nyoka aliuona dhahiri shahiri.
"Wewe ni nani! Polisi?" aliuliza kwa jaziba Kindo.
"Ni polisi ndio na ninayo ruhusa ya kukuhoji kuhusu umiliki wa magari ya kampuni" alisema Mtega nyoka huku akisimama kutoka alipokuwa.
"Unatakiwa kuongea na mwanasheria wa kampuni na si mimi!" alisema Kindo huku akianza kupeleka mkono ilipokuwa simu ya mezani.
Mtega nyoka aliwahi kumzuia.
"Nisingependa tusumbuane kwa jambo dogo hili ndugu!" alisema kwa upole Mtega nyoka.
Kindo akagwaya!
"Tatizo hujui unaongea na nani bwana mdogo nita..." hakumaliza kauli yake akajikuta akipokea bonge la Mkofi, uliomfanya aone shilingishilingi na kufumba macho na alipofungua hakuziona.
"Nisingependa tufike huko unakotaka ndugu" aliongea tena Mtega nyoka.
Kindo alibaki akitetemeka tu.
"Unajua unalofanya litakugarimu kijana" alisema Kindo huku sauti ikimkwama.
"Haya naomba kujua unamiliki magari mangapi" alihoji tena Mtega nyoka.
Kindo akainama kwenye droo na kutoa karatasi moja iliokuwa imenakishiwa na karatasi nyingine kwa juu yake.
Mtega nyoka aliichukua na kuisoma.
Alikutana na orodha ndefu ya magari ya kampuni ile na wanaoyatumia.
Hakuona gari namba T117DHJ.
Sijaona gari lilioungua moto huko Kitangili. Au halimilikiwi na kampuni yako." alihoji Mtega nyoka huku akimtizama usoni Kindo ambae alianza kutokwa jasho jepesi licha ya kuwa na kiyoyozi ndani ya ofisi ile.
"Afu kuna nini huko Dekuku!" alihoji tena Mtega nyoka.
Ilikuwa ni kabla ya jibu likatokea tukio moja matata lililohitaji akili na uwezo kulikwepa.
Mlango ulisukumwa kwa nguvu huku ukifuatiwa na mvumo wa kitu kilichokua kimemlenga katikati ya uti wa mgongo Mtega nyoka ambae bila kujiuliza alijipinda na kuangukia ubavu na kuacha kitu kile kiende kujikita kwenye kifua cha Kindo ambae alitoa mguno wa uchungu.
Kutoka alipoangukia; Mtega nyoka aliona mtu akiingia kwa kasi na bastola mkononi huku akiwa ameziba uso wake kama ninja.
Mtega nyoka nae kwa utalamu akawahi kuinuka pale chini na kutaka kumvaa mvamizi.
Mvamizi nae akaona kitendo kile haraka akarudi nyuma na kumpisha Mtega nyoka kisha akaachia risasi moja ilioenda kutua kwenye paji la uso la Kindo na kisha haraka akamgeukia Mtega nyoka.
Alichelewa!
.
Mvamizi alijikuta akipaa juu na kusukumwa kwa nguvu hadi ukutani na alipotaka kuanguka alijikuta akipokea mateke mengine mawili ya harakaharaka yaliomtia kiwewe.
Akataka kuinuka ajipange zaidi ila hakupewa nafasi na Mtega nyoka; akajikuta akipokea mateke mengine mawili chini ya magoti na kujikuta akitepweta kama aliepigwa na denda na kichaa.
Mvamizi alihusudu uwezo wa Mtega nyoka kwa vile alivyojua kucheza na nafasi alioipata.
Akagwaya!!
Mtega nyoka alijikuta amesimama peke yake baada ya kuona mwenzie aliepambana nae akienda chini bila upinzani zaidi.
Aliona damu ikimwagika.
"*****, what the fuc...!!" alisema mtega nyoka baada ya kuona adui aliechukua uhai wa Kindo nae uhai wake umechukuliwa.
Akabaki amesimama peke yake katikati ya chumba kilichokuwa na maiti mbili.
Haraka haraka akamkagua mvamizi,mfukoni alikuta kadi iliomshangaza kidogo!!
"inakuwaje hii!!"
Hakukuwa na wa kumjibu.
****
Wengine wanaendelea kujipatia uhondo wa riwaya hii na nyingine tatu kwa pesa ya Tsh3000/=
Yani unapata riwaya nne zilizokatika ubora kwa Tsh 3000/=tu.
Walionunua sasa wote wamejipatia nakala zao kwa email ama whatsapp.
Hujachelewa lipa hapa 0758573660 jina Bahati Mwamba upate riwaya.
Karibuni na ahsanteni kwa sapoti yenu
Barikiwa mkuu kudoRIWAYA: MPANGO WA CONGO
SEHEMU YA 24
Na Bahati Mwamba
Kitambulisho kile alikigeuza huku na huko bila kupata maana ya kile alichokiona.
Kitambulisho kilikuwa kina picha ya Makanisa yaliojengwa pamoja huku milango ikiwa inajitegemea na kila mlango ulikuwa na msalaba juu yake!
"Ina maana gani hii!!" Mtega nyoka alijiuliza bila kupata majibu sahihi.
Haraka akatoka ndani ya ofisi ile na kuelekea mapokezi kisha akatimka kutoka ndani ya Kasuku Contractors.
Haraka akadandia pikipiki iliokuwa inashusha abiria ndani ya buzuruga plaza.
Lengo lilikuwa ni kuwahi ilipo Kanisa ya wokovu kama ananuani ya Mwasu ilivyoonesha.
.
Alipanga kumuwahi Remi.
*****
Mwasu na Remi walifika salama ndani ya makazi ya Remi. Hii ilikuwa ni tofauti na maelezo aliyopewa ya kuwa anaenda kutibiwa kwenye kituo kikubwa cha matibabu.
"Usijali mdogo wangu,nitakupeleka hospitali kisha tutarudi tena hapa na utakuwa ukitibiwa hapa hapa." Mwasu alimtoa wasiwasi Remi.
Remi hakuwa na usemi alibaki mtazamaji.
Ndani ya nyumba ya Mwasu kulikuwa kuna mtu mwingine na walipoonana na Remi wote hawakutambuana.
Alikuwa ni Malima.
Malima alifika nyumbani kwa Mwasu ili atafute nyaraka alizopoteza kwa kuhisi huenda aliwahi kuziacha pale.
Na sasa ilikuwa imepita saa nzima huku akiwa amepekua kila pahali bila kuona alichokihitaji.
Malima hakumtabua Remi kabisa licha ya kuongea usiku wa siku iliopita.
Malima alishangaa kidogo kisha akahoji.
"Kabla hata sijajua mnaendeleaje,nadhani huyu mgeni hakustahili kuwapo hapa, alitakiwa awe anapewa matibabu sasa hivi"
Mwasu hakumjibu badala yake alikuwa anafanya jitihada za kumkaliza Remi kwenye sofa.
"Hauna pesa ya matibabu nikupe?" aliendelea kuhoji Malima.
"Pesa ninayo ila nina sababu zangu za kumleta hapa kwanza." alijibu Mwasu.
"Sababu gani kwa mtu alieumia kiasi hiki?" alimaka Malima.
"Unataka kuijua?!" alihoji Mwasu huku akimtizama Malima usoni bila kupepesa macho yake.
"Sina shida ya kuijua Mwasu; zaidi ya afya ya huyu binti kuzingatiwa, akifia hapa je!!" alisema Malima huku akitanabaisha wasiwasi wake.
Mwasu akitikisa kichwa tu huku akielelea chumbani kwake ambako alikuta kumevurugwa vya kutosha.
Mwasu alitabasamu!!
Alijua nini Malima alitafuta.
Dakika tatu badae Mwasu aliungana na Remi sebuleni huku wakimwomba Malima awapishe kidogo.
Hakuuliza akatoka kwenda kibalazani.
"Ni nini kimekukuta Remi!!" alisema Mwasu huku akikaa kwenye sofa lililokuwa kando ya sofa alilokalia Remi.
Remi alikaa kimya kidogo kisha akasema;
"Tangu tulipoachana pale kambini, kulitokea sintofahamu kadhaa hivi ambazo inasemekana zilianza kuwapo hata wakati upo..." alinyamaza Remi baada ya kujikuta roho yake inakuwa nzito kuendelea kuzungumza.
Hata yeye mwenyewe hakujua ni kwanini.
"Aah nitakweleza siku nyingine Dada!!" alisema Remi huku akishika kichwa kuashiria hajisikii vizuri.
"Ooh pole sana!!" alisema Mwasu huku akinyanyuka na kwenda kumshika kichwa Remi kwa kutumia mgongo wa kiganja chake.
***
Malima aliendelea kuwaza ni vipi atamwambia mkurugenzi wake kuhusu upotevu wa nyaraka za jengo muhimu sana.
Alijikuna kichwa akiwa haelewi ni lipi afanye.
Malima kila alipofikiria bado akili yake ilimpa kumbukumbu ya mwisho ni Mwasu alieondoka na gari huku kukiwa na nyaraka.
"Ziko wapi!!" Malima alijigonga kichwa huku akishindwa kabisa kuchanganua mambo yalivyo kuhusu nyaraka zile.
Kama ni akili kugoma,basi za Malima ziliamua kusimama kabisa kutatua kitendawili kile.
Alihofu!!
Alihofia kazi yake kupotea.
****
Mwasu bado walikuwa wamekaa wanazungumza mambo mbalimbali ya huko nyuma na jinsi walivyotokea kushibana pindi walipokuwa pamoja.
"Dada hakuna aliekushitukia kwamba wewe ni mgeni hapa jijini?" alihoji Remi.
"unajua mdogo wangu, Tanzania sio kama nchi zingine. Ni ngumu sana mgeni kuulizwa ukazi wake, hivyo nilipofika hapa wala hakuna aliehangaika kujua ubini wangu,hivyo nami sasa ni Mtanzania." alijibu Mwasu.
"Mh!! vipi sasa ukishitukiwa?" alihoji tena Remi.
Mwasu aliachia cheko dogo huku akijifuta midomo kwa kiganja cha mkono wa kulia.
"Ni ngumu sana mdogo wangu,nimeshakuwa Mtanzania kabisa sasa,najua lugha yao na ninajua tamaduni zao,hivyo si rahisi kabisa" alijibu Mwasu.
Remi aliguna tu.
"kwanini hujiulizi kuhusu wewe Remi!!" alihoji Mwasu.
"Basi tu imenibidi na ni bora nikamatwe!" alijibu bila shaka yoyote Remi.
Mwasu akatafakari kwa kauli ile kisha akahoji tena.
"Kwanini ulikuja huku?"
Remi alibabaika kidogo kujibu huku akijiuliza kama ni sahihi kwake kumwambia yaliomsibu dada yake huyo wa hiyari.
"Mmh nadhani kwa sasa ningepona kwanza halafu tutazungumza kwa kina kabisa hili suala." alisema Remi.
Mwasu akapandisha mabega kisha akatazama saa yake na kutaka kunyanyuka ila Remi akauliza swali.
"Hivi Amokachi nae nilisikia kalowea huku,mliwahi onana?"
Lilikuwa swali la mtego ambao Mwasu hakujua autegue vipi. Akababaika kidogo kisha akageuka na kumjibu.
"Nadhani hana hata mawasiliano yangu,hivyo ni ngumu kuonana. Mwanza kubwa hii!!"
Remi akatikisa kichwa kukubali bila kuongeza neno.
"aah hujala bado,ngoja niandae chakula ule na shemeji yako!!" alisema Mwasu huku akielekea upande wa jiko lililokuwa ndani ya nyumba ile.
Remi alibaki na maswali kadhaa baada ya kubaki peke yake.
Siku anaingia Mwanza na kuelekea Igoma alikoambiwa ni ofisini kwa Mwasu; macho yake mwenyewe yalimuona Amokachi na Mwasu wakiteta jambo na ndio sababu yeye akatimua mbio ili asiingie mikononi mwa Amokachi anaemtafuta kwa udi na Uvumba.
Sasa alishangaa Mwasu kumwambia hawajawahi kuonana.
Utata!!
Jambo lingine ni vile alivyoona maisha safi ya Mwasu ambayo ni tofauti na kazi anayofanya ya umama ntilie hadi watu wakamwita Mama Ujazo.
Hapo akamfikilia Malima ambae anaeza kuwa ndie mtu aliempangia Mwasu.
Hapo napo akabaki njia panda.
Remi akabaki na fumbo.
***
Nje bado mawazo yalimzonga Malima akabaki amejiinamia tu bila kufanya lolote huku mara kwa mara akichorachora chini bila kujua alichokichora.
Mara akaona kiatu kikubwa(Buti) kikisimama miguuni pake.
Malima akanyanyua uso wake ili aone mmiliki wa buti ile ya jeshi.
Alishuhudia mwanaume mwembamba mrefu aliejenga kimazoezi akiwa amesimama akimtizama yeye.
Kwa utazamaji ule; Malima akagwaya.
"Simama!!" Malima aliamriwa kwa sauti kavu.
Akatii!!
"Haya geuka rudi ndani!!" aliamrisha tena yule mtu.
"Kiongozi tungetambuana kwa..." Malima alitaka kujitetea akaishia njiani baada ya kuona bastola ikimwangalia.
Malima alishikwa na tumbo la kuhara gafla huku akishindwa hata kupiga kelele.
Akajikuta akinyanyua mikono juu kusalimu amri huku akigeuka na kuelekea ndani.
Kule ndani Remi alipitisha wazo moja tu.
Alihitaji kutoroka pale!!
Akajaribu kusimama bado hakuwa na utimamu sawia.
Akajaribu tena.
Mara hii akaweza kusimama na akaanza kupiga hatua ili afike mlangoni.
Wala hakumalizia hatua zote mbili akajikuta akiingiwa na ubaridi wa gafla baada ya kuona Malima akiingia huku akiwa amenyoosha mikono na nyuma yake kukiwa na mtu alieshika bastola.
"Amokachi!!?" alijikuta akitamka bila kupenda..
"Ulidhani unaweza kukimbia kuliko mimi Remi!!?" alihoji amokachi huku akimalizikia kuingia ndani.
Muda huohuo Remi alimshuhudia Mwasu akitokea kule jikoni akiwa hana wasiwasi na kile alichokiona pale sebuleni.
"Kazi nzuri Mwasu; Pimbi wote wamenaswa" alisema Amokachi huku akitabasamu.
Mwasu nae alitabasamu huku akienda haraka na kuuchukua mkoba aliokuwa nao Remi na kuufungua.
Hola!!
Haukuwa na kitu ndani yake! Ulikuwa tupu.
"Viko wapi ulivyochukua?" alikoroma Mwasu huku akiukunguta mkoba ule bila mafanikio zaidi ilidondoka pedi moja tu.
Amokachi na Mwasu walibaki wamepigwa na butwaa.
"Hii ndio sababu ya kumleta mgonjwa hapa!?" alihoji Malima huku akitetemeka.
Mwasu alicheka kidogo.
"Ningeshangaa kama usingeikumbuka hii sababu!!" alijibu Mwasu.
"Niacheni mana nadhani sihusiki!!" alijitetea Malima.
Amokachi alicheka kwa kebehi.
"Yani ungejua wala usingejisumbua kujitetea kunguni wewe!!" alisema Amokachi.
Malima akapigwa na butwaa. Anaingiaje kwenye mkasa asiojua?
Jibu halikukawia!!
"Ramani sahihi iko wapi?" alihoji tena Amokachi.
Malima alitoa macho kwa mshangao kama changudoa aliedondosha simu yenye namba muhimu.
"Hata mimi naitafuta,tena wewe unai..." Malima alikatishwa na mluzi uliopigwa na Mwasu.
Punde wakaingia vijana wengine wawili ambao waliwaziba midomo kwa vitambaa fulani na punde Remi na Malima walijikuta hawana fahamu.
Walibebwa kama mizoga.
Majibu wangeenda kuyatoa huko huko wanakopelekwa.
*****
Bado unaweza kupata riwaya hii na nyingine tatu kwa Tsh 3000/=
Namba ya malipo ni, 0758573660 jina Bahati Mwamba.
Sio kweli mkuu ipo hewani kila dakika na kila sms inayoingia najibu. Hakuna alieboeka na aina yangu ya ujibuji on time.Hii namba uliyoweka haipatikani na ikipatikana haiko active Sana.mtu anataka kununua simulizi anakusms hajibiwi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nishamaliza Mambo na Sasa hivi nimekuja ku- unsubscribe kwenye huu uzi. Ila sijavutiwa na mwisho wake yule jamaa kujifia kabla hajalipa mabaya aliyotenda.Sio kweli mkuu ipo hewani kila dakika na kila sms inayoingia najibu. Hakuna alieboeka na aina yangu ya ujibuji on time.
Kama huipati basi piga hapa 0624155629 ila malipo fany hapa 0758573660 nipo hewani hata saa nane usiku
Hahaa ilikuwa lazima afe kwa kihoro sio kwa timu ile ilioingiaNishamaliza Mambo na Sasa hivi nimekuja ku- unsubscribe kwenye huu uzi. Ila sijavutiwa na mwisho wake yule jamaa kujifia kabla hajalipa mabaya aliyotenda.
Ila uko safiiiii safiiiii Sana.
Ukiwa na simulizi nyingine mpya nitag please mr KUDO.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kongole sana " hii kitu sio mchezo Usaliti kila mahali naona hapo kuwa sundi na yeye ni Mafia .. So huyo jamaa aliye kikimbia Kifo nyumbani kwake " naona amekifuata mikononi kwa sundi " ..... labda itokee sundi amuonee huruma " nahisi sundi ndiye mdada aliyehusika na kwenda kuzichoma zile nyaraka ... Ila kwakuwa alikuwa amevaa kininja Jamaa alishindwa kujua kwamba aliye mvamia nimpenzi Wake "
Yeah anaweza kuwasaliti mafia wenzake kwaajili ya kuzidiwa na penzi ..ila yatakayo mfika lazima atakwenda kuhadithia kuzimuUko sawa mkuu, nilikua sijawaza hili, ila Sundi atafanya mistake kubwa ya kumuacha hai jamaa, tusubiri.
Sent using Jamii Forums mobile app