Jawabu kwa Lord Denning: Mikataba mithili ya IGA inayotaja gharama halisi za miradi ipo hapa Tanzania

Jawabu kwa Lord Denning: Mikataba mithili ya IGA inayotaja gharama halisi za miradi ipo hapa Tanzania

Mama Amon kiasi umepotoka kulinganisha mkataba tambuka wa kampuni kwa kampuni na wa nchi kwa nchi. Hata vile ufafanuzi wako umetoa picha halisi ya tofauti ya mkataba tambuka (IGA )na wa utekelezaji (HGA) kimataifa.

Nakubaliana nawe kuwa TPA na DP World, kwa kuwa tayari wamesaini MoU, waingie kwenye mikataba ya utekelezaji (HGAs) ambayo italindwa na sheria za nchi husika kupitia IGA yenye vifungu vyenye "nipe-nikupe", kulinda maslahi ya Mataifa yote.

Pamoja na pendekezo langu hilo, hoja yangu kuu Serikali iweke na kutekeleza mikakati ya kuwezesha makampuni ya ndani ya kuwekeza na wageni watumike tu kiubia kuongeza ufanisi na tija. Kuendelea kutegemea mataifa ya kigeni, kwa maendeleo, ni kudumisha ukoloni-mamboleo
View attachment 2702526
Picha ya antena za Vodacom, Tigo, Airtel na TTCL zikiwa zimesimikwa kwenye mnara wa Helios baada ya makampuni haya kusaini mkataba wa upangishaji na Helios

Kuna mtu, Lord Denning, ameuliza swali lifuatalo: Je, kuna mkataba mithili ya IGA iliyosainiwa kati ya Tanzania na Dubai unaotaja gharama halisi za miradi kama vile bei ya huduma na kodi ya pango?

Jawabu kwa swali hili ni "ndiyo," na ufafanuzi ufuatao ni kwa ajili ya kuthibitisha hilo.

IGA na HGA ni mikataba mtambuka (framework ontracts)

Mikataba ya IGA na HGA ni mikataba mtambuka, yaani "framework contracts." Kimsingi, mkataba mtambuka unaweza kuwa na sura mbili.

Kwanza, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unahusu mradi unaotambuka nchi nyingi katika utekelezwaji wake na utekelezwaji wake unahitaji maamuzi ya kiserikali na kibunge kwa kufanya mabadiliko ya sheria kadhaa katika nchi zote husika, ambapo wigo wa mradi unafahamika, kiasi kwamba ikishasainiwa HGA hakuna haja ya mikataba mingine.

Mfano mzuri ni ule mradi wa bomba la mafuta linalounganisha Tanzania na Uganda, yaani radi wa EACOP.

Pili, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unahusu mradi unaotambuka nchi nyingi katika utekelezwaji wake na utekelezwaji wake unahitaji maamuzi ya kiserikali na kibunge kwa kufanya mabadiliko ya sheria kadhaa katika nchi zote husika, ambapo wigo wa mradi haufahamiki kikamilifu, kiasi kwamba, kushasainiwa kwa HGA hakuondoi haja ya mikataba mingine. Mchoro ufuatao unatoa picha kubwa kuhusu aina hii ya mikataba mtambuka:

View attachment 2702567

Na tatu, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unatambuka miradi tofauti inayotekelezwa ndani ya nchi ile ile moja, lakini miradi hiyo inatekelezwa kwa nyakati tofauti, katika maeneo tofauti na watekelezaji tofauti, lakini pasipo ulaiza wa kubadilisha sheria za nchi husika, kiasi kwamba kusainiwa kwa "Framework Contract" pamoja na "Project Contracts" kunaondoa mahitaji ya mikataba mingine, na hivyo kuondoa sababu ya uwepo wa IGA na HGA. Mchoro ufuatao unafafanua zaidi.

View attachment 2702566

Mifano ya Mikataba mtambuka isiyohitaji IGA wala HGA

Hapa nchini, kuna mifano mingi ya "mikataba mtambuka" ya aina hii ya pili. Mikataba hii inaonyesha gharama halisi za miradi husika, hata kabla mikataba ya miradi husika kusainiwa. Mifano mizuri hapa Tanzania ni kama ifuatavyo:
  1. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na kampuni ya Vodacom,
  2. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Tigo,
  3. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Airtel,
  4. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya TTCL.
  5. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Halotel.
Makampuni ya Halotel, Vodacom, Tigo, Airtel, na TTCL hutoa huduma za mawasiliano ya simu.

Lakini makapuni haya hayana mitaji ya kutosha kwa ajili ya kujenga minara nchi nzima.

MInara ya kurusha mawimbi ya sauti (signal relay stations) huhitajika kwa ajili ya kusimika antena za kupokea na kurusha upya mawimbi ya sauti kutoka kwa mpigaji hadi kwa mpokeaji.

Lakini, Helios ni kampuni ya Uingereza yenye mtaji wa kujenga na kukodisha minara kwa makapuni mbalimbali.

Helios wanamiliki minara zaidi ya 1000, katika Afrika mashariki na Kati. Hivyo, haya makampuni yetu yanakodisha nafasi kwenye minara ya Helios ili yaweze kuweka antena zao kwenye minara hiyo, na kuwahudumia wateja wake.

Kampuni inapoanza kukodisha nafasi kwenye minara ya Helios inakuwa haijui kwa uhakika inahitaji minara mingapi na iliyo wapi.

Kwa hiyo, busara ni kukodisha minara ya Helios kwa awamu, kulingana na wateja wanavyopatikana na wanakopatikana.

Hivyo, mchakato wa kuingia mkataba kati ya kampuni ya Helios na kampuni kama vile Vodacom inachukua hatua nne. Yaani:
  1. Kusainiwa kwa mkataba mtambuka mmoja (framework contract) wenye kutaja taarifa chache za jumla, zitakazoweka singi wa mikataba ya saiti moja moja katika siku za usoni.
  2. Kampuni yenye mahitaji kuiandikia Helios ikiomba huduma ya kukodishwa mnara kwenye site mpya.
  3. Kusainiwa kwa mikataba ya saiti maalum (site cocntract), na hivyo kuongeza idadi ya minara ya Helios iliyokodishwa kwa kampuni pale tu mahitaji ya kampuni yanapoongezeka kwa sababu wateja wapya wamepatikana.
  4. Helios kuandaa mnara kwenye saiti kulingana na mahitaji, na hatimaye kampuni kukabidhiwa saiti hiyo.
Kwa ujumla, mikataba mtambuka kati ya Kampuni ya Helios na makampuni yaliyotajwa hapo juu, inafanana katika muundo na maudhui.

KImsingi, kila "mkataba mtambuka" kati ya Helio na kampuni yoyote hapo juu, una sehemu zifuatazo:
  1. Maelezo ya msingi kuhusu makubaliano: Sehemu hii inaongelea wahusika katika mkataba, malengo ya wahusika, na mwongozo wa jumla kuhusu mahusiano ya siku za usoni.
  2. Kiammbatanisho cha kwanza ("schedule 1"): Kinaongelea "configuration", yaani aina ya huduma ambazo Helios anapaswa kuhakikisha zinapatikana kwenye kila saiti. Mfano:-- kuna sharti kwamba, kama mnara unaotaka kukidishwa uko sehemu ambako hakuna umeme wa gridi ya Taifa, basi Helios aweke jenereta; -- kuna sharti kwamba, kampuni itapewa ukubwa wa eneo la meta moja ya mmraba kwa ajili ya kusimika antena yake; -- kuna kifungu kinataja ukomo wa muda wa mkataba tambuka; -- kuna kifungu kinataja ukomo wa muda wa mkataba mahsusi utakaosainiwa katika siku za usoni; -- na kadhalika.
  3. Kiambatanisho cha pili ("schedule 2"): Kinaongelea kodi ya pango inayotajwa kwa kutumia kizio cha "TZS/site/month". Gharama hizi ziko katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni bei za kukodisha mnara ulioko kwenye maeneo yenye umeme wa gridi ya Taifa (bei nafuu). Na Kundi la pili ni bei za kukodisha mnara ulioko kwenye maeneo yasiyo na umeme wa gridi ya Taifa (bei kubwa).
  4. Kiambatanisho cha tatu ("schedule 3"): Kinaongelea muundo na maudhui ya mkataba utakaosainiwa kwa ajili ya kukidisha saiti moja tu, yaani kukodisha mnara mmoja pekee. Kwa hiyo, kama kampuni ya Vodacom itakodisha minara 100, kutasainiwa mikataba mahsusi 100.
  5. Kiambatanisho cha nne ("schedule 4"): Kinaongelea utaratibu wa kuongeza mnara mpya, yaani jinsi kampuni yenye mahitaji itakavyowasiliana na Helios na kuonyesha huduma ya mnara mpya ianze kutolewa lini.
  6. Kiambatanisho cha tano ("schedule 5"): Kinaongelea utaratibu wa kukabidhiana huduma kwenye saiti.
  7. Kiambatanisho cha sita ("schedule 6"): Kinaongelea protokali ya kutumia saiti, maana kwenye mnara mmoja kuna wakodishaji wengi. Yaani, unakuta kuna antena za Tigo, Airtel, Vodacom, na kadhalika.
Hitimisho

Mkataba mtambuka (framework contract) kati ya Helios na makampuni ya simu ni kama mkataba kati ya nchi na nchi (IGA). Na mkataba wa saiti kati ya Helios na makampuni ya simu ni kama mkataba wa ngazi ya miradi kati ya nchi mwenyeji na mwekezaji wa kigeni (HGA).

Kwa hiyo, inawezekana, na ni lazima, kutaja gharama za mradi kama vvile kodi ya pango na pia ukomo wa muda kwenye IGA. Timu ya Johari Hamza haikuwa na weledi katika mambo haya.

Na kama ambavyo Helios na makampuni ya simu yanasaini "Framework Agreements" na baadaye "Project Site Agreements," vivyo hivyo DPW na TPA wanaweza na wanapaswa kusaini nyaraka za aina hii.

Hakuhitajiki IGA wala HGA kamwe ili kuiwezesha DPW au kampuni yoyote iwayo kuwekeza katika bandari za Tanzania!

Mama Amon Desk
"Summbawanga Town"
Sumbawanga.
30 Julai 2023.
View attachment 2702527


Siitaji technicality yeyote au kuwa Mwanasheria, sijui, IGA, HGA or anything....

Mkataba huu mwenye common sense akisoma anajua hizi ni hamnazo kabisa.
 
View attachment 2702526
Picha ya antena za Vodacom, Tigo, Airtel na TTCL zikiwa zimesimikwa kwenye mnara wa Helios baada ya makampuni haya kusaini mkataba wa upangishaji na Helios

Kuna mtu, Lord Denning, ameuliza swali lifuatalo: Je, kuna mkataba mithili ya IGA iliyosainiwa kati ya Tanzania na Dubai unaotaja gharama halisi za miradi kama vile bei ya huduma na kodi ya pango?

Jawabu kwa swali hili ni "ndiyo," na ufafanuzi ufuatao ni kwa ajili ya kuthibitisha hilo.

IGA na HGA ni mikataba mtambuka (framework ontracts)

Mikataba ya IGA na HGA ni mikataba mtambuka, yaani "framework contracts." Kimsingi, mkataba mtambuka unaweza kuwa na sura mbili.

Kwanza, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unahusu mradi unaotambuka nchi nyingi katika utekelezwaji wake na utekelezwaji wake unahitaji maamuzi ya kiserikali na kibunge kwa kufanya mabadiliko ya sheria kadhaa katika nchi zote husika, ambapo wigo wa mradi unafahamika, kiasi kwamba ikishasainiwa HGA hakuna haja ya mikataba mingine.

Mfano mzuri ni ule mradi wa bomba la mafuta linalounganisha Tanzania na Uganda, yaani radi wa EACOP.

Pili, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unahusu mradi unaotambuka nchi nyingi katika utekelezwaji wake na utekelezwaji wake unahitaji maamuzi ya kiserikali na kibunge kwa kufanya mabadiliko ya sheria kadhaa katika nchi zote husika, ambapo wigo wa mradi haufahamiki kikamilifu, kiasi kwamba, kushasainiwa kwa HGA hakuondoi haja ya mikataba mingine. Mchoro ufuatao unatoa picha kubwa kuhusu aina hii ya mikataba mtambuka:

View attachment 2702567

Na tatu, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unatambuka miradi tofauti inayotekelezwa ndani ya nchi ile ile moja, lakini miradi hiyo inatekelezwa kwa nyakati tofauti, katika maeneo tofauti na watekelezaji tofauti, lakini pasipo ulaiza wa kubadilisha sheria za nchi husika, kiasi kwamba kusainiwa kwa "Framework Contract" pamoja na "Project Contracts" kunaondoa mahitaji ya mikataba mingine, na hivyo kuondoa sababu ya uwepo wa IGA na HGA. Mchoro ufuatao unafafanua zaidi.

View attachment 2702566

Mifano ya Mikataba mtambuka isiyohitaji IGA wala HGA

Hapa nchini, kuna mifano mingi ya "mikataba mtambuka" ya aina hii ya pili. Mikataba hii inaonyesha gharama halisi za miradi husika, hata kabla mikataba ya miradi husika kusainiwa. Mifano mizuri hapa Tanzania ni kama ifuatavyo:
  1. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na kampuni ya Vodacom,
  2. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Tigo,
  3. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Airtel,
  4. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya TTCL.
  5. Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Halotel.
Makampuni ya Halotel, Vodacom, Tigo, Airtel, na TTCL hutoa huduma za mawasiliano ya simu.

Lakini makapuni haya hayana mitaji ya kutosha kwa ajili ya kujenga minara nchi nzima.

MInara ya kurusha mawimbi ya sauti (signal relay stations) huhitajika kwa ajili ya kusimika antena za kupokea na kurusha upya mawimbi ya sauti kutoka kwa mpigaji hadi kwa mpokeaji.

Lakini, Helios ni kampuni ya Uingereza yenye mtaji wa kujenga na kukodisha minara kwa makapuni mbalimbali.

Helios wanamiliki minara zaidi ya 1000, katika Afrika mashariki na Kati. Hivyo, haya makampuni yetu yanakodisha nafasi kwenye minara ya Helios ili yaweze kuweka antena zao kwenye minara hiyo, na kuwahudumia wateja wake.

Kampuni inapoanza kukodisha nafasi kwenye minara ya Helios inakuwa haijui kwa uhakika inahitaji minara mingapi na iliyo wapi.

Kwa hiyo, busara ni kukodisha minara ya Helios kwa awamu, kulingana na wateja wanavyopatikana na wanakopatikana.

Hivyo, mchakato wa kuingia mkataba kati ya kampuni ya Helios na kampuni kama vile Vodacom inachukua hatua nne. Yaani:
  1. Kusainiwa kwa mkataba mtambuka mmoja (framework contract) wenye kutaja taarifa chache za jumla, zitakazoweka singi wa mikataba ya saiti moja moja katika siku za usoni.
  2. Kampuni yenye mahitaji kuiandikia Helios ikiomba huduma ya kukodishwa mnara kwenye site mpya.
  3. Kusainiwa kwa mikataba ya saiti maalum (site cocntract), na hivyo kuongeza idadi ya minara ya Helios iliyokodishwa kwa kampuni pale tu mahitaji ya kampuni yanapoongezeka kwa sababu wateja wapya wamepatikana.
  4. Helios kuandaa mnara kwenye saiti kulingana na mahitaji, na hatimaye kampuni kukabidhiwa saiti hiyo.
Kwa ujumla, mikataba mtambuka kati ya Kampuni ya Helios na makampuni yaliyotajwa hapo juu, inafanana katika muundo na maudhui.

KImsingi, kila "mkataba mtambuka" kati ya Helio na kampuni yoyote hapo juu, una sehemu zifuatazo:
  1. Maelezo ya msingi kuhusu makubaliano: Sehemu hii inaongelea wahusika katika mkataba, malengo ya wahusika, na mwongozo wa jumla kuhusu mahusiano ya siku za usoni.
  2. Kiammbatanisho cha kwanza ("schedule 1"): Kinaongelea "configuration", yaani aina ya huduma ambazo Helios anapaswa kuhakikisha zinapatikana kwenye kila saiti. Mfano:-- kuna sharti kwamba, kama mnara unaotaka kukidishwa uko sehemu ambako hakuna umeme wa gridi ya Taifa, basi Helios aweke jenereta; -- kuna sharti kwamba, kampuni itapewa ukubwa wa eneo la meta moja ya mmraba kwa ajili ya kusimika antena yake; -- kuna kifungu kinataja ukomo wa muda wa mkataba tambuka; -- kuna kifungu kinataja ukomo wa muda wa mkataba mahsusi utakaosainiwa katika siku za usoni; -- na kadhalika.
  3. Kiambatanisho cha pili ("schedule 2"): Kinaongelea kodi ya pango inayotajwa kwa kutumia kizio cha "TZS/site/month". Gharama hizi ziko katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni bei za kukodisha mnara ulioko kwenye maeneo yenye umeme wa gridi ya Taifa (bei nafuu). Na Kundi la pili ni bei za kukodisha mnara ulioko kwenye maeneo yasiyo na umeme wa gridi ya Taifa (bei kubwa).
  4. Kiambatanisho cha tatu ("schedule 3"): Kinaongelea muundo na maudhui ya mkataba utakaosainiwa kwa ajili ya kukidisha saiti moja tu, yaani kukodisha mnara mmoja pekee. Kwa hiyo, kama kampuni ya Vodacom itakodisha minara 100, kutasainiwa mikataba mahsusi 100.
  5. Kiambatanisho cha nne ("schedule 4"): Kinaongelea utaratibu wa kuongeza mnara mpya, yaani jinsi kampuni yenye mahitaji itakavyowasiliana na Helios na kuonyesha huduma ya mnara mpya ianze kutolewa lini.
  6. Kiambatanisho cha tano ("schedule 5"): Kinaongelea utaratibu wa kukabidhiana huduma kwenye saiti.
  7. Kiambatanisho cha sita ("schedule 6"): Kinaongelea protokali ya kutumia saiti, maana kwenye mnara mmoja kuna wakodishaji wengi. Yaani, unakuta kuna antena za Tigo, Airtel, Vodacom, na kadhalika.
Hitimisho

Mkataba mtambuka (framework contract) kati ya Helios na makampuni ya simu ni kama mkataba kati ya nchi na nchi (IGA). Na mkataba wa saiti kati ya Helios na makampuni ya simu ni kama mkataba wa ngazi ya miradi kati ya nchi mwenyeji na mwekezaji wa kigeni (HGA).

Kwa hiyo, inawezekana, na ni lazima, kutaja gharama za mradi kama vvile kodi ya pango na pia ukomo wa muda kwenye IGA. Timu ya Johari Hamza haikuwa na weledi katika mambo haya.

Na kama ambavyo Helios na makampuni ya simu yanasaini "Framework Agreements" na baadaye "Project Site Agreements," vivyo hivyo DPW na TPA wanaweza na wanapaswa kusaini nyaraka za aina hii.

Hakuhitajiki IGA wala HGA kamwe ili kuiwezesha DPW au kampuni yoyote iwayo kuwekeza katika bandari za Tanzania!

Mama Amon Desk
"Summbawanga Town"
Sumbawanga.
30 Julai 2023.
View attachment 2702527
Jibu mujarabu
 
Siitaji technicality yeyote au kuwa Mwanasheria, sijui, IGA, HGA or anything....

Mkataba huu mwenye common sense akisoma anajua hizi ni hamnazo kabisa.
Kitu kama hiki ndicho anakitumia huyu tapeli Lord denning ili kuulinda ule mkataba wa hovyo.

Ameshindwa kujua mazingira yetu kisiasa kati yetu na wenzetu hayafanani, wenzetu wapo accountable kisheria, wa kwetu wako huru hata wakikosea..

Licha ya vifungu vingine vyote vibovu kwenye ule mkataba, huyu tapeli ameokota hicho kimoja tu aje kujiliwaza nacho hapa, akiamini atatudanganya.
 
Kitu kama hiki ndicho anakitumia huyu tapeli Lord denning ili kuulinda ule mkataba wa hovyo.

Amwshindwa kujua mazingira yetu kisiasa kati yetu na wenzetu hayafanani, wenzetu wapo accountable kisheria, wa kwetu wako huru hata wakikosea..

Licha ya vifungu vingine vyote vibovu kwenye ule mkataba, huyu tapeli ameokota hicho kimoja tu aje kujiliwaza nacho hapa, akiamini atatudanganya.
Jifunze kusikia na yale usiyopenda kusikia.

Jifunze pia kuwa sio kila jambo unalosimamia liko sahihi.

Ukishajua haya utaishi vizuri sana!
 
Jifunze kusikia na yale usiyopenda kusikia.

Jifunze pia kuwa sio kila jambo unalosimamia liko sahihi.

Ukishajua haya utaishi vizuri sana!
Nijibu tu kile nilichokuuliza, hayo mafunzo unayonipa naona hata nawe yanakuhusu zaidi.

Huwezi kuuliza swali mtu mwenye akili timamu, asitake kujua your motive behind, na hilo sio kosa.

Wewe wakati unatengeneza hilo swali lako, ulifanya utafiti kidogo kuona tofauti ya kimazingira, na kiuwajibikaji, iliyopo kati ya viongozi wetu na hao wengine?
 
Kweli lugha yetu inatuficha mengi. Kwa uelewa wangu hapa ni kwamba kama mambo hayataenda vizuri, na ikiwa kushitakiana kutakuja basi, IGA ndio itatumika mahakamani. Kwahiyo wote tunaoamini katika HGAs kuwa zitakuwa na vipengele vizuri kulinda nchi tunajidanganya.
Am I correct?

IGA ni makubaliano ya uwekezaji katika bandari zetu.

Katika IGA nchi zimekubaliana DP World ndio kampuni itakayowekeza ikiwakilisha Dubai na TPA kampuni pokezi ya uwekezaji huo ikiwakilisha JMT.

Mikataba ya utekelezaji miradi (HGAs) itaandaliwa kwa misingi ya makubaliano (IGA) na si vingenevyo. Kama kutakuwa na vifungu nje ya hayo makubaliano, hakuna shaka kutazuka mgogoro. Kumbuka baadhi ya vifungu neno shall limetumika ambalo kisheria ni "ulazima" wa kutimiza kilichokusudiwa. Kwa kuwa shauri liko mahakamani tusubiri hatima yake ila natoa mfano wa nguvu ya IGA wakati wa kuandaa HGAs

Article 8: Land Rights
1. The Government of Tanzania
(na siyo Union Republic of Tanzania) shall take all necessary actions to ensure the acqusition and grant of rights to DPW or the relevant project company. Kitakachofuata hapo ni kuamini kuwa DPW hawataomba ardhi yenye maslahi mapana kitaifa kwa ajili ya shughuli zao.
 
Mleta mada amezunguka mbuyu baada amerudi pale pale, mwisho wa siku hakujibu swali lililoulizwa.
Muulizaji alitaka mfano wa IGA ambayo itakuwa na HGAs kisha ikataja gharama halisi ya uwekezaji.

Alipaswa amjibu IGA kati ya nchi x na y ilihitaji HGAs na ilitaja gharama halisi za uwekeza.

Ukalinganishe IGA na framework contracts baina ya kampuni na kampuni kweli??.
Mleta mada anakusudia kutuambia nini hapa??

Hoja ya mleta mada hii hapa:

Hakuna haja ya IGA kati ya Tanzania na Dubai

Baada ya kusema hayo hapo juu sasa nafanya majumuisho muhimu kwa kuzingatia hoja yafuatayo:

Njia mojawapo ya kusanifu hoja, ni kuanzia kwenye ufanano wa vitu viwili. Njia hii huzalisha hoja yenye muundo ufuatao:
  1. Kitu X na kitu Y vinafanana kwa sababu kila kimoja kinazo sifa a, b, and c.
  2. Kitu X pia kinaonekana kuwa na sifa nyingine d.
  3. Kwa hiyo, kitu Y pia kinapaswa kuwa na sifa hiyo d.
Kwa kutumia mantiki hiyo hapo juu, sasa nawea kukujibu kikamilifu kama ifuatavyo:

Mosi, Kampuni ya HELIOS kutoka Uingereza na kammpuni ya DPW kutoka Dubai zinafanana kwa kuwa zote ni Kampuni za wawekezaji wa Kigeni wanaotaka mazingira tulivu ya uwekezaji ili wafanikiwe kuwekeza, kuvuna na kuhamisha faida kutoka nchini Tanzania, ambapo HELIOS anajenga na kuendesha minara kwa kuikodisha kwa makampuni yanayosafirisha mawimbi ya simmu hapa Tanzania, wakati DPW anajenga na kuendesha bandari za mmajini na nchi kavu kwa kuzikodisha kwa watu wanaosafirisha mizigo.

Pili, Kampuni ya HELIOS kutoka Uingereza inao uwezo wa kuendesha biashara zake kwa kutummia "mkabata mtambuka" (framework agreement) na "mikataba ya miradi mmahsusi" (project site agreements), pasipo kuhitaji mkataba wa IGA kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya Uingereza.

Na tatu, kwa hiyo, Kampuni ya DPW kutoka Dubai inapaswa kuwa na uwezo wa kuendesha biashara zake kwa kutummia "mkabata mtambuka" (framework agreement) na "mikataba ya miradi mmahsusi" (project site agreements), pasipo kuhitaji mkataba wa IGA kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya Dubai.

Yaani, timu ya Johari Hamza haikuwa na weledi katika mambo haya.
 
Huo ni mjadala mwingine ambao unaweza kuanzisha uzi ili ujadiliwe kivyake.

Swali langu linasema hivi;
Kuna IGA au BIT gani iliyowahi kuingiwa Duniani (POPOTE PALE) ambayo imetoa nafasi ya kuingiwa kwa HGA ( Mkataba mahsusi wa uwekezaji) alafu still ikaonyesha kiwango cha uwekezaji, aina ya uwekezaji na mgawanyo wa mapato?

Na nimesema hapa atakayeweza kulijibu hili swali vizuri atanilazimu kuondoa fake I'd yangu niliyokaa nayo humu tangu mwaka 2012 kwenye account zangu mbili tofauti. Ingawa moja siitumii tena nimebaki nayo hii ya Lord Denning

Nimelijibu swali hilo kama ifuatavyo:

Hakuna haja ya IGA kati ya Tanzania na Dubai

Baada ya kusema hayo hapo juu sasa nafanya majumuisho muhimu kwa kuzingatia hoja yafuatayo:

Njia mojawapo ya kusanifu hoja, ni kuanzia kwenye ufanano wa vitu viwili. Njia hii huzalisha hoja yenye muundo ufuatao:
  1. Kitu X na kitu Y vinafanana kwa sababu kila kimoja kinazo sifa a, b, and c.
  2. Kitu X pia kinaonekana kuwa na sifa nyingine d.
  3. Kwa hiyo, kitu Y pia kinapaswa kuwa na sifa hiyo d.
Kwa kutumia mantiki hiyo hapo juu, sasa nawea kukujibu kikamilifu kama ifuatavyo:

Mosi, Kampuni ya HELIOS kutoka Uingereza na kammpuni ya DPW kutoka Dubai zinafanana kwa kuwa zote ni Kampuni za wawekezaji wa Kigeni wanaotaka mazingira tulivu ya uwekezaji ili wafanikiwe kuwekeza, kuvuna na kuhamisha faida kutoka nchini Tanzania, ambapo HELIOS anajenga na kuendesha minara kwa kuikodisha kwa makampuni yanayosafirisha mawimbi ya simmu hapa Tanzania, wakati DPW anajenga na kuendesha bandari za mmajini na nchi kavu kwa kuzikodisha kwa watu wanaosafirisha mizigo.

Pili, Kampuni ya HELIOS kutoka Uingereza inao uwezo wa kuendesha biashara zake kwa kutummia "mkabata mtambuka" (framework agreement) na "mikataba ya miradi mmahsusi" (project site agreements), pasipo kuhitaji mkataba wa IGA kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya Uingereza.

Na tatu, kwa hiyo, Kampuni ya DPW kutoka Dubai inapaswa kuwa na uwezo wa kuendesha biashara zake kwa kutummia "mkabata mtambuka" (framework agreement) na "mikataba ya miradi mmahsusi" (project site agreements), pasipo kuhitaji mkataba wa IGA kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya Dubai.

Yaani, timu ya Johari Hamza haikuwa na weledi katika mambo haya.
 
Nikupongeze Mama Amon kwa uchambuzi wako mzr, ila kuna maelekzo umeyatoa na mifano ya mkataba ambayo inakinzana na hoja iliyopo na hoja ya mtu uliyemnukuu kwenye andiko lako hili.

Kwanza, ufafanuzi wako umeanza kwa kuandika bayana "Mifano ya Mikataba isiyohitaji IGA na HGA.." Kisha ndio ukaanza kuitaja kwa kuchambua Mikataba ya Kampuni ya Helios na Mitandao ya Simu ya Tanzania na ukaenda kueleza na vifungu vya ghrama, Pango nk. (Kwa maelezo yako, mifano hiyo ya mikataba ndio hiyo ya kundi hilo ulilokoleza la kutohitaji IGA na HGA).

Lakini, mkataba wa DPW na Tz una IGA na pia inaelezwa kuwa utakuwa na HGA. Sasa tulitegemea kuwe na Mkataba wenye nature ya namna hiyo aidha serikali ilishawahi ingia huko nyuma hapa Tz au nchi nyingine ambayo imeingia mkataa wa namna hii halafu ndani ya hiyo IGA kuwe na vifungu vya gharama, malipo, muda, mgawanyo wa fedha, na mengine yote kama ambavyo itakuwa ktk actual site contracts/aggreement.

Mifano uliyotoa sio sahihi na inajicontradict.

Asante kwa angalizo. Kwa uelewa zaidi somma aya hizi hapa:

Hakuna haja ya IGA kati ya Tanzania na Dubai

Baada ya kusema hayo hapo juu sasa nafanya majumuisho muhimu kwa kuzingatia hoja yafuatayo:

Njia mojawapo ya kusanifu hoja, ni kuanzia kwenye ufanano wa vitu viwili. Njia hii huzalisha hoja yenye muundo ufuatao:
  1. Kitu X na kitu Y vinafanana kwa sababu kila kimoja kinazo sifa a, b, and c.
  2. Kitu X pia kinaonekana kuwa na sifa nyingine d.
  3. Kwa hiyo, kitu Y pia kinapaswa kuwa na sifa hiyo d.
Kwa kutumia mantiki hiyo hapo juu, sasa nawea kukujibu kikamilifu kama ifuatavyo:

Mosi, Kampuni ya HELIOS kutoka Uingereza na kammpuni ya DPW kutoka Dubai zinafanana kwa kuwa zote ni Kampuni za wawekezaji wa Kigeni wanaotaka mazingira tulivu ya uwekezaji ili wafanikiwe kuwekeza, kuvuna na kuhamisha faida kutoka nchini Tanzania, ambapo HELIOS anajenga na kuendesha minara kwa kuikodisha kwa makampuni yanayosafirisha mawimbi ya simmu hapa Tanzania, wakati DPW anajenga na kuendesha bandari za mmajini na nchi kavu kwa kuzikodisha kwa watu wanaosafirisha mizigo.

Pili, Kampuni ya HELIOS kutoka Uingereza inao uwezo wa kuendesha biashara zake kwa kutummia "mkabata mtambuka" (framework agreement) na "mikataba ya miradi mmahsusi" (project site agreements), pasipo kuhitaji mkataba wa IGA kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya Uingereza.

Na tatu, kwa hiyo, Kampuni ya DPW kutoka Dubai inapaswa kuwa na uwezo wa kuendesha biashara zake kwa kutummia "mkabata mtambuka" (framework agreement) na "mikataba ya miradi mmahsusi" (project site agreements), pasipo kuhitaji mkataba wa IGA kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya Dubai.

Yaani, timu ya Johari Hamza haikuwa na weledi katika mambo haya.
 
Narudia tena. Soma swali vizuri!

Kuna IGA au BIT gani iliyowahi kuingiwa Duniani (POPOTE PALE) ambayo imetoa nafasi ya kuingiwa kwa HGA ( Mkataba mahsusi wa uwekezaji) alafu still ikaonyesha kiwango cha uwekezaji, aina ya uwekezaji na mgawanyo wa mapato?
IGA ya Italia na Algeria mwaka 2022 kwenye masuala ya nishati iliwekwa wazi kwamba Italia wangwekeza $4billions kwenye mashirikiano hayo.

Unauliza swali la kitoto sana, hata watu kukujibu wanaona uvivu. Kuna malaki ya IGA dunia na wewe sio ajabu hujawahi kuona hata zaidi ya tatu, halafu IGA za uwekezaji haziwezi kuwa sawa na za utamaduni, sheria, mazingira n.k
 
IGA ni makubaliano ya uwekezaji katika bandari zetu.

Katika IGA nchi zimekubaliana DP World ndio kampuni itakayowekeza ikiwakilisha Dubai na TPA kampuni pokezi ya uwekezaji huo ikiwakilisha JMT.

Mikataba ya utekelezaji miradi (HGAs) itaandaliwa kwa misingi ya makubaliano (IGA) na si vingenevyo. Kama kutakuwa na vifungu nje ya hayo makubaliano, hakuna shaka kutazuka mgogoro. Kumbuka baadhi ya vifungu neno shall limetumika ambalo kisheria ni "ulazima" wa kutimiza kilichokusudiwa. Kwa kuwa shauri liko mahakamani tusubiri hatima yake ila natoa mfano wa nguvu ya IGA wakati wa kuandaa HGAs

Article 8: Land Rights
1. The Government of Tanzania
(na siyo Union Republic of Tanzania) shall take all necessary actions to ensure the acqusition and grant of rights to DPW or the relevant project company. Kitakachofuata hapo ni kuamini kuwa DPW hawataomba ardhi yenye maslahi mapana kitaifa kwa ajili ya shughuli zao.
Daa! Kila nikikaribia kuelewa najikuta tena Chali! "Katika IGA nchi zimekubaliana DP World ndio kampuni itakayowekeza ikiwakilisha Dubai na TPA kampuni pokezi ya uwekezaji huo ikiwakilisha JMT." Ni nchi gani hizi tena? Mi mbona naona IGA ni kati ya Tanzania na DP WORLD!? Ngoja niisubirie mahakama tu. Ila mleta bandiko kwangu upande wangu ni moja ya watu waliolieleza jambo hili kwa rugha rahisi sana kueleweka (kwa anayetaka kujifubza)
1. Hakukuwa na haja ya IGA katika issue hii.
2. Kinachotafutwa kwenye IGA na HGA kipo kwenye framework contract na project contracts
3. IGA hii inatengeneza hatari kwa Tanzania
4. Mkataba ulipaswa uwe kati ya TPA na DPW na si vinginevyo.
5. Swali la Lord denning linatafuta UBISHI zaidi kuliko kuleta weredi kwa wadau.
 
IGA ya Italia na Algeria mwaka 2022 kwenye masuala ya nishati iliwekwa wazi kwamba Italia wangwekeza $4billions kwenye mashirikiano hayo.

Unauliza swali la kitoto sana, hata watu kukujibu wanaona uvivu. Kuna malaki ya IGA dunia na wewe sio ajabu hujawahi kuona hata zaidi ya tatu, halafu IGA za uwekezaji haziwezi kuwa sawa na za utamaduni, sheria, mazingira n.k
Iweke hapa

Tuone kama ilisema kutakuwa na HGA na ikasema hayo
 
Hakuna ulichojibu

Jibu ni kuweka IGA au BIT inayoeleza kutakuwa na HGA alafu still ikaweka mgawanyo wa mapato. Ni bora ungesema tu sina jibu

Naona kanuni ya REASONING BY ANALOGY inakupiga chenga.
Recap:

The process of analogical inference involves noting the shared properties of two or more things, and from this basis concluding that they also share some further property. The structure or form may be generalised like so:

1. P and Q are similar in respect to properties a, b, and c.
2. P has been observed to have further property x.
3. Therefore, Q probably has property x also.

Source: Argument from analogy - Wikipedia
 
N
Nijibu tu kile nilichokuuliza, hayo mafunzo unayonipa naona hata nawe yanakuhusu zaidi.

Huwezi kuuliza swali mtu mwenye akili timamu, asitake kujua your motive behind, na hilo sio kosa.

Wewe wakati unatengeneza hilo swali lako, ulifanya utafiti kidogo kuona tofauti ya kimazingira, na kiuwajibikaji, iliyopo kati ya viongozi wetu na hao wengine?
Nimetengeneza swali langu purposely kuelimisha watu juu ya upotoshaji unaofanyika.

IGA yetu imeweka nafasi ya kuingiwa kwa HGA zitakazoweka rights za kila upande. ikiwemo masuala ya uwekezaji na mgawanyo wa mapato.

Unaposema mkataba mbovu eti haujaonesha mgawanyo wa mapato ndo hapo unaulizwa ili uweke ushahidi wako wa kuleta mkataba uliosema kutakuwa na HGA na bado ukaelezea mgawanyo wa mapato.

Alichofanya mjibu hoja ni kupuyanga sio kutoa jibu la kilichoulizwa.
 
Naona kanuni ya REASONING BY ANALOGY inakupiga chenga.
Recap:

The process of analogical inference involves noting the shared properties of two or more things, and from this basis concluding that they also share some further property. The structure or form may be generalised like so:

1. P and Q are similar in respect to properties a, b, and c.
2. P has been observed to have further property x.
3. Therefore, Q probably has property x also.

Source: Argument from analogy - Wikipedia
Huku ndo kupuyanga kwenyewe sasa. Kama huna jibu sema sina jibu sio unapuyanga. Kwenye taaluma yetu jibu unachoulizwa ukujibu vingine ni kupuyanga tu
 
N
Nimetengeneza swali langu purposely kuelimisha watu juu ya upotoshaji unaofanyika.

IGA yetu imeweka nafasi ya kuingiwa kwa HGA zitakazoweka rights za kila upande. ikiwemo masuala ya uwekezaji na mgawanyo wa mapato.

Unaposema mkataba mbovu eti haujaonesha mgawanyo wa mapato ndo hapo unaulizwa ili uweke ushahidi wako wa kuleta mkataba uliosema kutakuwa na HGA na bado ukaelezea mgawanyo wa mapato.

Alichofanya mjibu hoja ni kupuyanga sio kutoa jibu la kilichoulizwa.

Swali lako linafutika kwa sababu ya mantiki kwammba hakuna haja ya IGA katika uwekezaji wa bandari. TICTS hawakusaini IGA na walisonga mbele. Kwa nini IGA leo?
 
Huku ndo kupuyanga kwenyewe sasa. Kama huna jibu sema sina jibu sio unapuyanga. Kwenye taaluma yetu jibu unachoulizwa ukujibu vingine ni kupuyanga tu

Ungetuliza akli yako ungegundua kuwa swali lako linafutika kutokana na jibu la swali hili: IGA inahitaji kwa ajili gani katika uwekezaji wa bandari?
 
Back
Top Bottom