SMARTER GHOST
JF-Expert Member
- May 22, 2021
- 298
- 1,258
Niko na muda acha nitie neno!
Kila MC huwa wanakua na kitu fulani anachokiwezea zaidi. Kuna wanoweza kufreestyle sana, kuna wanaoandika lyrics kuntu zenye kuelimisha (edutainment), kuna wazee wa punchlines, alafu kuna wababe wa flow and delivery!
J Moe ni moja kati ya MC's wa kibongo wenye uwezo mkubwa sana wa kuandika mashairi yenye ujumbe. Ni rapper anaeweza kuijadili mada moja kwenye wimbo mzima kwa mvuto wa aina yake. Kasikilize story tatu, kasikilize kimyakimya, au kasikilize money na famous.
Chidi Benzino a.k.a King Kong, ni rapper mwenye flow na delivery kali zaidi kuwahi kutokea kwenye bongo hip hop. Nadhani Ulamaa Solo Thang ndio anaweza kushindana nae kwenye suala la flow and delivery. Sauti yake nzito, uwezo wa kunata na beat, vitakufanya uendelee kumsikiliza Chidi bila kujali anachokiimba kina mantiki au hakina!
Nikirudi kwenye hoja kuu ya mleta mada, Yes mimi pia naamini J Moe is a better MC than Chidi Benz. J Moe sio mnyonge pia kwenye flow, ila kwenye mashairi anamuacha Chid benz pakubwa. Pia J Moe anaweza kubadilika badilika kuendana na theme ya wimbo husika. Akiimba mambo ya starehe anafanya poa, na akiamua kuielimisha jamii pia anafanya poa bila shida. Chidi benz anabamba zaidi kwenye nyimbo za starehe pekee!
Mwisho kabisa, mifano ya nyimbo ulizozitaja hazina uhalisia. Nadhani kwakua unamkubali sana J Moe ndio maana ukatumia hisia zaidi kusema J Moe alifunika kwenye hizo ngoma.
Ukisikia paah (remix), walifunika zaidi JCB na Fid Q. Walielewa mada husika na nashairi yao yakabeba matukio yanayoendana na theme ya wimbo. J Moe alifanya kawaida tu. Kwa upande wa Chid benz, alienda chaka. Nadhani hakuelewa mada husika. Alichokiimba hakikuendana na wenzie kabisa
Mchizi wangu (remix), wengi walifanya poa hasa Fid Q na Lord Eyez. Alizingua Mh Temba tu na kisauti chake (ni maoni yangu), sijui nani alimuita. Pia kwenye hii ngoma, naona Chid benz alimfunika J Moe. Verse ya Benzino ilikua moto sana.
Mimi ya Geez Mabovu, naona kama ilikua 50/50. Verse ya J Moe ilikua na mistari kuliko ya Chidi, ila verse ya Chidi ikawa na flow kali kuliko ya J Moe.
Mwisho kabisa, kuna kitu kinaitwa Longevity. J Moe amekaa kwenye game kwa muda mrefu na kutoa hit songs nyingi kumzidi Chidi benz. Consistency ya J Moe inafanya nimpe nafasi mbele ya Chidi benz!
Adiós.
Kila MC huwa wanakua na kitu fulani anachokiwezea zaidi. Kuna wanoweza kufreestyle sana, kuna wanaoandika lyrics kuntu zenye kuelimisha (edutainment), kuna wazee wa punchlines, alafu kuna wababe wa flow and delivery!
J Moe ni moja kati ya MC's wa kibongo wenye uwezo mkubwa sana wa kuandika mashairi yenye ujumbe. Ni rapper anaeweza kuijadili mada moja kwenye wimbo mzima kwa mvuto wa aina yake. Kasikilize story tatu, kasikilize kimyakimya, au kasikilize money na famous.
Chidi Benzino a.k.a King Kong, ni rapper mwenye flow na delivery kali zaidi kuwahi kutokea kwenye bongo hip hop. Nadhani Ulamaa Solo Thang ndio anaweza kushindana nae kwenye suala la flow and delivery. Sauti yake nzito, uwezo wa kunata na beat, vitakufanya uendelee kumsikiliza Chidi bila kujali anachokiimba kina mantiki au hakina!
Nikirudi kwenye hoja kuu ya mleta mada, Yes mimi pia naamini J Moe is a better MC than Chidi Benz. J Moe sio mnyonge pia kwenye flow, ila kwenye mashairi anamuacha Chid benz pakubwa. Pia J Moe anaweza kubadilika badilika kuendana na theme ya wimbo husika. Akiimba mambo ya starehe anafanya poa, na akiamua kuielimisha jamii pia anafanya poa bila shida. Chidi benz anabamba zaidi kwenye nyimbo za starehe pekee!
Mwisho kabisa, mifano ya nyimbo ulizozitaja hazina uhalisia. Nadhani kwakua unamkubali sana J Moe ndio maana ukatumia hisia zaidi kusema J Moe alifunika kwenye hizo ngoma.
Ukisikia paah (remix), walifunika zaidi JCB na Fid Q. Walielewa mada husika na nashairi yao yakabeba matukio yanayoendana na theme ya wimbo. J Moe alifanya kawaida tu. Kwa upande wa Chid benz, alienda chaka. Nadhani hakuelewa mada husika. Alichokiimba hakikuendana na wenzie kabisa
Mchizi wangu (remix), wengi walifanya poa hasa Fid Q na Lord Eyez. Alizingua Mh Temba tu na kisauti chake (ni maoni yangu), sijui nani alimuita. Pia kwenye hii ngoma, naona Chid benz alimfunika J Moe. Verse ya Benzino ilikua moto sana.
Mimi ya Geez Mabovu, naona kama ilikua 50/50. Verse ya J Moe ilikua na mistari kuliko ya Chidi, ila verse ya Chidi ikawa na flow kali kuliko ya J Moe.
Mwisho kabisa, kuna kitu kinaitwa Longevity. J Moe amekaa kwenye game kwa muda mrefu na kutoa hit songs nyingi kumzidi Chidi benz. Consistency ya J Moe inafanya nimpe nafasi mbele ya Chidi benz!
Adiós.