JAYDEE Apanga kununua ndege (aeroplane)


Mkuu Ngalikihinja.

Uko sawa kabisa...

Labda niwapeni kisa kimoja cha mambo haya, na ni kisa cha ukweli nilichoona mwanzo mwisho...

Kuna jamaa ambaye amekuwa pilot wa siku nyingi sana, na ana rating za ndege kibao...Maisha yake yote ya u'pilot alikuwa anawekeza ili aanzishe kampuni ya ndege, na kweli coming of 2006 jamaa akasaidiwa na wazazi wake ambao wako huko majuu, na wako njema, akaanzisha kampuni iliyojulikana kama SAFARI EXPRESS, akaanza na kukodisha ndege ndogo za abiria 12, lakini baadaye akakodisha ndege 2 nzuri sana aina ya Beechcraft-19 (BE19) na BE20 KUTOKA kwa rafiki zake wa South Africa, zikawa zinapiga tenda za mgodini NORTH-MARA na Sasakwa(Hoteli ya Mmarekani tajiri sana huko Serengeti). ..

Ndani ya mwaka 1 wa kuendesha biashara hiyo, aliangukia pua...! Pamoja na uzoefu mwingi wa ndege aliokuwa nao, madeni yakamzidi...Alikuwa anadaiwa mafuta, hadi jamaa wa Air-BP wakagoma kumpa mafuta kwa utaratibu wa kawaida wa cannet, wakamtaka alipe cash!.. .

MADENI YALIPOMZIDI aliamua kiume:
Aliamua kukimbia nchi hii, na mpaka wa leo hapa naandika hajatokea, wengi wakisema alienda kubadilisha sura ili kuwakwepa wadeni wake...
Aliacha ofisi yake ya quality ya juu ikiwa full-furnished,gari, Hiace custom, Macompyuta kibao, jikoni kukiwa na majiko ya kisasa, mafriji ya kisasa, pamoja na mashine ya bei mbaya ya kutengenezea kahawa(kwa wale wanaojua ma'cappuchino, ma'cafe-late, ma'chocochino etc)...

Waliokuwa wafanyakazi hawakuwa na jinsi zaidi ya kuanza kujisevia kila mtu alivyoweza...Mhasibu alikuwa anacheka, maana aliachwa na account ya kampuni...

Kwahiyo tunaongea vitu hivi kwa kuvifahamu sana, na SI KWA KUMDHARAU MTU!...Nawsilisha!
 
Tatizo ni kuwaza KIMASIKINI. Tumezaliwa na kukulia katika mazingira ya kimasikini hivyo kwa kiasi kikubwa yameathiri fikra na mitazamo yetu.Tunawaza kimasikini! Mtu yeyote anaweza kufanya chochote hata kununua ndege.
Hakuna lisilowezeka ukiwa na malengo yawe ya muda mrefu au mfupi.
Obama alipotangaza nia yake ya kugombea uraisi wa marekani wengi walimbeza na kumuona kama anaota ndoto! Ila leo ni RAISI wa marekani hivyo hakuna lisilowezekana chini ya jua.
 
Asifanye mchezo, huyu, hataweza...Ndege si kama Machozi Band, ambayo unaweza kuiendesha kwa kuwakopa wapigaji..huh!

Lau angejua gharama ambazo ndege inakula asingetamka hilo, labda kwa kujifurahisha tu.
Anacheza mdako huyu dada,badala awaze siku moja atapata mtoto anawaza ndege,anafikiri ni machozi band hata akilia washabiki wanashangilia?wakina mbilia bell wenyewe waliishia kuzipanda tuu!!
 
Well said PJ, nikweli kabisa yote hayo, watu walifaidi sana.
 
haaa yaani binadamu tunajua kukatishana tamaa sana yani, nadhani hayo maelezo cjui ya ndege hivi vile yanahitajiki kwa sana, hiyo ni ndoto ya binti wa watu, anatamani awe hivi awe vile, afanye hiki afanye kile, mungu amjalie hiki na kile, sasa shida ipo wapi jamani? ina maana humu ndani hakuna mwenye ndoto zake? ishu ya ndege cjui hivi na vile muachieni mwenyewe yeye ndio anajua atafanyaje afikie malengo yake, yaani ubinadamu kazi ngumu sana haki ya MUNGU.....
 
Unayoyasema ni kweli endapo utafuata taratibu za kupanga malengo........ Kama ni kuropoka tu........... mbona tunapanga mengi.........
Hivi leo hii nikikuambia kuwa nataka kuinunua MAREKANI unaona hii ni
1. REALISTIC...???? au ndoto za alinacha...????
2. ACHIEVABLE...???? au impossible...???
3. ina TIME FRAME...??? au itachukuwa maisha yangu yote nikiwa bado na-plan leave alone to implementing it...????
4. CHALLENGING..??? yes, very challenging to the extend that it is next to impossible to even think of it..........

TUWENI WAKWELI BANAAA...........
 
Tatizo ni kuwaza KIMASIKINI..
Kumbe unajua hilo ee?.
Tumezaliwa na kukulia katika mazingira ya kimasikini hivyo kwa kiasi kikubwa yameathiri fikra na mitazamo yetu..
.Hilo ni moja.Lakini kitu kingine ni lazima tuangalie na mwelekeo wa mtu, sio mtu anamention tu kitu, then we clap hands, right?
Tunawaza kimasikini! .
Nimekupa mfano mzuri hapo juu, sijui kama umeusoma.
Mtu yeyote anaweza kufanya chochote hata kununua ndege. .
.Hilo lawezekana, lakin hapo kuna walakini, si mtu yeyote.
Hakuna lisilowezeka ukiwa na malengo yawe ya muda mrefu au mfupi..
..Lakini hayo malengo peke yake si kitu, ni lazima yawe achievable, right?
Obama alipotangaza nia yake ya kugombea uraisi wa marekani wengi walimbeza na kumuona kama anaota ndoto!
Usilinganishe business na Siasa weweee!
 
Kumbe unajua hilo ee?..Nimekupa mfano mzuri hapo juu, sijui kama umeusoma..Hilo lawezekana, lakin hapo kuna walakini, si mtu yeyote. ..Lakini hayo malengo peke yake si kitu, ni lazima yawe achievable, right?

Usilinganishe business na Siasa weweee!


PJ nakuelewa ila member wengi humu wanachangia kwa ushabiki na hisia ndege sio HIACE, hata ya IKULU yenyewe bado inasuasua, umewapa mfano mzuri jinsi jamaa alivyoshindwa kumudu ile ya biashara je hii ya binafsi? Ni vizuri kuwa na malengo lakini yawe archivable kwa sisi wa imani za dini tunasema do not ask GOD too much that cant give you.
 
"Siku moja MUNGU akipenda nitakuwa na ndege yangu labda" .toka lini kuweka malengo kukawa kosa ndugu zangu tunaojiita great thinkers? nilitegemea watu watamtakia kila kheri sana sana kwenye ukumbi huu wa "great thinkers" lakini inaonekana kuna comments za roho ya korosho flani kama zile comments za kwa michuzi.hesabu zako zinakwambia hawezi kununua ndege sawa lakini si kosa kwake kuwa na lengo hilo.kilakitu kinawezekana dunia hii kwahio badala ya kumkatisha tamaa mwambieni akaze buti na mshaurini kimawazo afanye nini hili kufanikiwa.


hakuna mtu anayejua plan zake za maisha kazipanga vipi kwahio sio mbaya kwake kusema kauli kama hio ni bidii zake tu.kila kitu kinawezekana.


penye nia hapakosi njia.
 
hatumkatishi tamaa ila hatutaki kusema uwongo ahalafu aje atuulize baadaye tushindwe cha kujibu
 
hatumkatishi tamaa ila hatutaki kusema uwongo ahalafu aje atuulize baadaye tushindwe cha kujibu
mimi nina huakika ana akili timamu na anajua anacho kisema.na maneno yake hakusema lazima nije kununua ndege baadae hapana katumia maneno mazuri tu nakilamtu ana maisha yake na malengo yake.chochote utachomwambia hakitobadilisha nia yake kwani hakishindwa atakuwa kajaribu hio pia ni hatua kulikoni kukata tamaa from the scratch.


na labda kasema for fun kuchangamsha kijiwe na naona kweli watu wanachangamka na maneno kibao.hayo ni maisha yake haina haja watu kasema maneno kibao.


wewe mwenyewe sikazi una malengo kibao ambayo ukisema watu wengine wanaweza kufikiri haiwezekani lakini moyoni mwako unahisi inawezekana.
 
kwa mawazo haya yakutojiamini basi ni moja kwa moja siwalaumu viongozi wa nchi kushindwa fanya maamuzi ya tija kama kuinvest kwenye heavy industries kwa sababu wana mawazo yakutojiamini kama hayahaya na sababu hizi hizi ninazoziona hapa JF toka kwa great thinkers wakibongo kwani na wao ni wabongo.like dady like son.
..JD MAMA U CAN DO IT AND SAY IT MILLION TIMES..GOD BLESS U IN EACH AND EVERY STEP U MOVE NA MALENGO YAKO YATIMIE....
....pana watu walianza na baiskeli,pikipiki Rav 4 baada ya miaka wakanunua Bmw na leo wanapush cadillac pamoja na majumba ya millions of money why ndege isiwezekane?????...

ok mimi ninaswali kwa wote wanaomshangaa na kumbeza jd kwa ku-wish nunua ndege.
. { NI BINADAMU GANI ANAYEFAA NUNUA NDEGE?}
 

So Jay Dee kutaka kununua ndege ni Unrealistic, unachievable and a DAY DREAM au...? Time frame sio kikwazo coz kuna malengo yaliyopo kwenye short and long time frame.
Au kwa sababu ni Jay Dee kasema ndio maana inaonekana kuwa haiwezekani...?
Mfano uliotoa wa kutaka kuinunua america ni impossible but alichosema Jay Dee ni POSSIBLE.
 

Umenena vilivyo mkuu.
Unaweza ukaona ni kwa jinsi gani wengi wetu tulivyo masikini wa (ki)mawazo halafu tunajiita GREAT THINKERS..!
 
Now you are talking......why do you think KUNUNUA AMERICA IS IMPOSSIBLE........???? unanikatisha tamaa au........????
 
Now you are talking......why do you think KUNUNUA AMERICA IS IMPOSSIBLE........???? unanikatisha tamaa au........????

Rejea post ya mwanzo na uisome kwa makini utapata jibu why it is IMPOSSIBLE.
 
Unabore ile mbaya,dreams zipo na zina stage zake,Ndege fine,lakini anza kwanza na makazi yanaofanana na kuwa na denge,tupishe walalahoi kimara ambao dreams zetu kwanza ni maradhi tu na kausafiri ka kawaida.
 


Hebu tufafanulie basi, labda ulikuwa unamaanisha..?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…