Je, asili ya Washirazi ni Persia?

Je, asili ya Washirazi ni Persia?

Ila pia wapo wanyamwezi waliochanganyika kuoana na kuzaa na washirazi ambapo kizazi chao wanajiita waafro shirazi.
Hapa ngoja nikueleweshe kidogo.

Mzanzibar akija bara imeshazoeleka kuonekana kama hana kabila, lakini ukweli ni kuwa wengi wa wazanzibari ni wahadimu na wengine ni waafro shirazi kwa maana ni mulato (Afrika na shirazi) na wengine makabila yao yamestik kuwa vile vile kwakuwa hawakuwa na muingiliano wa mahusiano ya moja kwa moja na washirazi.

Moja ya makabila hayo ni yale ambayo walikuwa wakichukuliwa bara na kupelekwa visiwani kama watumwa enzi za biashara hiyo (Kamsome Tip-Tippu) na wengine ni wale ambao walitoroka bara kuepuka kuchukuliwa watumwa na kukimbilia visiwani kwa wakati huo.

Washirazi waizaa sana na wahadimu kuliko haya makabila yaliopelekwa visiwani enzi za utumwa na ndio maana wengi wa waafro shirazi sio kutoka katika haya makabila mengine.
Inaelekea wewe aidha hujui historia ya zanzibar na unazungumzia aidha kimasikhara. Hebu nenda kwenye historia ya zanzibar [tafuta vitabu au google utapata tu] ila achakuzungumzia kinadhararia wakati ukweli upo.
 
Inaelekea wewe aidha hujui historia ya zanzibar na unazungumzia aidha kimasikhara . Hebu nenda kwenye historia ya zanzibar [tafuta vitabu au google utapata tu] ila achakuzungumzia kinadhararia wakati ukweli upo.
Kumbe unaongelea kitu ambacho hukifahamu vizuri, hivi umafahamu maana ya neno Zenji bar?

Ukilipata utajua namaanisha nini kusema afro shirazi, hapo haimaanishi chama kama unavymaanisha kwenye afro shirazi party.
Hivo hakuna Afr America?
 
Tunapoongelea afro shirazi party = sawa sawa na muunganiko wa vyama viwili yaani African party na Shirazi party. Sawa. Lakini unapoongelea watu kuna
Washirazi = Shirazi
Waafrika(Waafro) = Wabantu
Sasa je kizazi kilichozaliwa kwa muunganiko huu (mulato) unakiitaje? Bila kuweka neno party linalomaanisha chama.
Na je wazanzibar ni wepi? Kwa maana ya tafsiri ya Neno lenyewe Zenji bar?
Ndugu yangu historia naijua vizuri sana kuliko unavyoielewa wewe. Nijibu ukirefer Afro american, wote ni wamarekani.
Nakusikitikia sana ila kama sikutaka malumbano humu lete utafiti. mimi ninapenda kuuliza,kudadisi hasa wazee wahusika, kusoma na ndiyo maana nilitaka wataalamu wengine humu ndani nao watoe maeleze yaliyo yakini. Tafadhali hebu japo google kidogo halafu utuambie.

Unajuwa watu wa aina yenu huwa vigumu kuukubali ukweli na ndiyo maana wengi wetu tunadhani kuwa Kiswahili ni Tanzania na tukiwaambieni kuwa siyo hivyo mtaanza mijadala ya kisiasa. SOMENI/FANYENI UTAFITI NDUGU ZANGU KWANI SIKU HIZI ELIMU YOTE IPO KIGANJANI
 
Nakusikitikia sana ila kama sikutaka malumbano humu lete utafiti. mimi ninapenda kuuliza,kudadisi hasa wazee wahusika, kusoma na ndiyo maana nilitaka wataalamu wengine humu ndani nao watoe maeleze yaliyo yakini. Tafadhali hebu japo google kidogo halafu utuambie. Unajuwa watu wa aina yenu huwa vigumu kuukubali ukweli na ndiyo maana wengi wetu tunadhani kuwa Kiswahili ni Tanzania na tukiwaambieni kuwa siyo hivyo mtaanza mijadala ya kisiasa. SOMENI/FANYENI UTAFITI NDUGU ZANGU KWANI SIKU HIZI ELIMU YOTE IPO KIGANJANI
Kule juu uliwahi kuongelea kuwa washirazi maeneo kama Bumbwini bado wapo unakumbuka? Maeneo kama Bumbwini hakuna washirazi zaidi ya Waarab wa kipemba. Sasa basi kama ulikuwa huelewi washirazi wenyewe sio kama wale unaosema wewe.

Washirazi wapo kama waarabu lakini sio weupe sana kama waarabu, vile vile mchanganyiko uliopo Zanzibar unawawia watu vigumu kuweza kuwatofautisha kwani mbali na Washirazi lakini pia kuna Wahindi, Washihiri, Waarab, wamanga, Bulushi. Je unalijua hilo.

Vp umepata jibu kuhusu kizazi cha wamarekani ambao ni Afro america?

Na vipi Wazanzibari ambao ni Afro shirazi?
 
Kwenye hii mada yako mi naona umenikumbusha kwenda kuzuru kaburi la babu yangu, Al-markhum Sheikh Thabit Kombo Jecha Al Shirazy. Ahsante kwa kunikumbusha[emoji106]
 
Kule juu uliwahi kuongelea kuwa washirazi maeneo kama Bumbwini bado wapo unakumbuka? Maeneo kama Bumbwini hakuna washirazi zaidi ya Waarab wa kipemba. Sasa basi kama ulikuwa huelewi washirazi wenyewe sio kama wale unaosema wewe. Washirazi wapo kama waarabu lakini sio weupe sana kama waarabu, vile vile mchanganyiko uliopo Zanzibar unawawia watu vigumu kuweza kuwatofautisha kwani mbali na Washirazi lakini pia kuna Wahindi, Washihiri, Waarab, wamanga, Bulushi. Je unalijua hilo.

Vp umepata jibu kuhusu kizazi cha wamarekani ambao ni Afro america?

Na vipi Wazanzibari ambao ni Afro shirazi?
Sijawahi kusema kuwa washirazi ni weupe kama waarabu. Hata hivyo siyo waarabu wote ni weupe kwani hata mimi nimeshawahi kuwaona waarabu wa aina hiyo na nilidhani kuwa ni mchanganyiko wa waarabu na wanubi lakini nikaambiwa kuwa siyo hivyo bali kuna waarabu wengi wa asili ambao siyo weupe hivyo basi kwangu mimi uarabu siyo lazima awe mweupe.
 
Kwenye hii mada yako mi naona umenikumbusha kwenda kuzuru kaburi la babu yangu, Al-markhum Sheikh Thabit Kombo Jecha Al Shirazy. Ahsante kwa kunikumbusha[emoji106]
Huyo babu yako alikuwa na hazina kubwa sana kuhusu haya tunayoyazungumza na ninaamini kabisa hata vitabu alikuwa na navyo kwani. MUNGU AMUWEKE MAHALA PEMA PEPONI.
 
Washirazi walipotoka zao maeneeo ya kwao (sasa Iran, hadhramut Yemen) walipitia na kuacha vizazi vyao maeneo ya pwani ya Afrika mashariki kuanzia Kenya, bagamoyo na visiwa vya Zanzibar
Kama nilivyosema hapo awali kuwa washiraz walikuwa excellent craftsmen,iptraders,artists,sailors etc etc na ndiyo maana kila walipohamia walipewa hadhi na aidha wafalme au viongozi wa sehemu hizo. Ukiangalia majengo ya kale Mombasa,Lamu,Kilwa,Mafia, Zanzibar yameathiriwa sana na utaalam wao.

Hivi leo kuna milango na madirisha almaarufu milango ya Zanzibar. Milango hii ilikuwa sehemu zote za ukanda wa pwani na leo hii wengi wanadhani kuwa ni ya waarabu lakini ukweli ni kwamba waarabu hawakuwa wajenzi na wanakshikaji wa nyumba. Lakini kwa vile majengo haya yalijengwa wakati wa himaya ya waarabu ndiyo maana yanaitwa hivyo.
 
Kuna wakati nilikuwa zbar. Nilichojifunza wengi wao pale hawajui historia ya nchi yao hiyo na hata historia ya asili ya jamii zao zilizopita au wanajitoa ufahamu.
 
"Persia" au "Peres" kama lilivyo lina tafsiri ya "Uajemi"historia inawaeleza washiraz kama jamii ya watu waliokimbia mtafaruku mkubwa wa kidini na wa kisiasa huko uajemi lakini hasa waliokimbia kuja pwani ya Afrika mashariki na Zenjbar walikuwa watu wa Jamii ya Kifalme na matajiri wakubwa kutoka katika milki na koo za kifalme ambao walikuwa wameweka makazi yao Oman.Jamii hiyo katika kukimbia na kuhama kwao walikuja na makundi ya watu wengi ambapo wengine waliamua kukaa katika upwa wa pembe ya Afrika kuelekea kusini mwa somalia,kenya,zanzibar,Tanganyika na Msumbiji urithi wa historia ya maisha yao unapatika kila pahala katika upwa wa maeneo yote waliokaa.
 
Wataalamu wa historia waliofanya utafiti asili ya Washirazi wanakubaliana hawatoki Uajemi=Iran. Kuna uwezekano ya kwamba watu wachache kutoka Uajemi walifika pwani la Uswahilini na kuoa hapa. Lakini kwa jumla ilikuwa zaidi fesheni kwa watu wa miji ya Waswahili kujipatia asili katika nchi za Waislamu. (Hii ni kweli pia kwa sehemu ya hao waliojiita "Waarabu", kama walikuwepo kabla ya kuhamia kwa Sultani ya Omani kuja Unguja). Hali halisi hakuna desturi za Kiajemi katika Afrika ya Mashariki.

Hata sikukuu ya "Nairuzi" (zaidi inaitwa Mwaka kogwa au Siku ya Mwaka) inatumia jina tu la Kiajemi lakini menginevyo haina uhusiano na Noruzi ya Iran (ambayo sharti inasheherekewa 20/22 Machi, yaani sikusare ya Machi).

Unaweza kusoma kwa undani hapa kwa google books katika kitabu cha De Vere Allen, Swahili Origins: Swahili Culture & the Shungwaya Phenomenon
 
Safi sana, ila kuna mdau kasema, wengi toka Unguja na Pemba hawajuwi haya yaliyosemwa humu, wangepata darasa kwa kweli.
Ila tunarudi pale pale, vile visiwa asili yao ni toka Bara, ila wamechanganyika na walowezi.
Bado ndugu zetu.
 
ngoja nivutr kiti niendelee kula nondo za kuijua asili yng...ila nnachokijua hata sie maniga tuliozaliwa zenji kwenye vyeti vyetu vya kuzaliwa,sehemu ya kabila tunaandikiwa Shirazi...au mtu akidakwa na askari akiambiwa ataje kabila lake anasema Mshirazi.

Simply,90% ya wazenji ni Washirazi...sasa cjui tunajinasibu na hao washirazi kimakosa au vipi..maana nikiangalia ukoo wangu simuonk hata mtu mmoja mwenye dalili za huo uarabu wa iran (persia) wote ni Afro safi...baada ya kusoma hiyo asili ya washirazi hapa..ndo najiuliza hivi wamatemwe,wamakunduchi, mtende, jambiani, kidoti nk huo ushirazi wameutoa wapi?

Kwa wale wenye asili ya uarabu kidogo ambao asilimia kubwa ni wapemba, hawa wanajinasibisha sana na wa oman ambao kimsingi sio washirazi! napata ukakasi kama kweli washirazi kwa maana ya washirazi bado wanaexist zenji coz mostly wanaonekana ni afro related people.

Pia najiuliza Mapinduzi ya znz yalikuwa ni dhidi ya mwarabu wa Oman tu, kwanini waarabu wa kipersia (shirazi) waungane na waafrika kuwaondoa waasia wenzao!
 
ngoja nivutr kiti niendelee kula nondo za kuijua asili yng...ila nnachokijua hata sie maniga tuliozaliwa zenji kwenye vyeti vyetu vya kuzaliwa,sehemu ya kabila tunaandikiwa Shirazi...au mtu akidakwa na askari akiambiwa ataje kabila lake anasema Mshirazi.

Simply,90% ya wazenji ni Washirazi...sasa cjui tunajinasibu na hao washirazi kimakosa au vipi..maana nikiangalia ukoo wangu simuonk hata mtu mmoja mwenye dalili za huo uarabu wa iran (persia) wote ni Afro safi...baada ya kusoma hiyo asili ya washirazi hapa..ndo najiuliza hivi wamatemwe,wamakunduchi,mtende,jambiani,kidoti nk huo ushirazi wameutoa wapi?

Kwa wale wenye asili ya uarabu kidogo ambao asilimia kubwa ni wapemba,hawa wanajinasibisha sana na wa oman ambao kimsingi sio washirazi! napata ukakasi kama kweli washirazi kwa maana ya washirazi bado wanaexist zenji coz mostly wanaonekana ni afro related people...

Pia najiuliza Mapinduzi ya znz yalikuwa ni dhidi ya mwarabu wa Oman tu, kwanini waarabu wa kipersia (shirazi) waungane na waafrika kuwaondoa waasia wenzao!
طيب
Mapinduzi ya zanzibar ni kweli kabisa yalilenga kuwaondoa waarab wa Oman. Washirazi walipotoka zao kwao Persia/Yemen kuingia katika mwambao wa Afrika mashariki pamoja na visiwani wao hawakutawala, bali walijichanganya na wenyeji na kuishi kama vile wenyeji walivyokuwa wakiishi pamoja na kuzaliana na wenyeji.

Hivyo basi nao wakawa ni watu wa kawaida kabisa, na vile vile waliwafunza wenyeji sanaa mbali mbali za usanifu majengo, milango na kadhalika. Ila waarab toka Oman wao walipofika ndio walitawala maeneo hayo na kuweka makazi yao pamoja na kuvifanya visiwa hivyo kuwa Makao makuu ya Utawala wao. Hivyo kutokana na udhalimu waliokuwa wakiufanya waarab hao na Waafrika kuchoshwa nao ndipo yalipofanyika mapinduzi.

Mapinduzi ambayo lengo likiwa ni kuteketeza kizazi cha waOman na vibaraka wao kutoka miongoni mwa waafrika. Na Kiukweli katika waarab hao wanaume wengi/wote waliuawa na wengine kutoroka isipokuwa wanawake ndio waliobaki. Leo hii ukiangalia kizazi cha kizanzibar na kuona baadhi yao kuna waarab basi elewa wengi wao asili yao ni wale mabibi zao ambao walisalia baada ya mapinduzi na kuolewa na wangazija, waafrika, pamoja na hao washirazi.
 
Mm ni mshirazi
Sawa. Je asili yako ni wapi?
Ingia kwenye [emoji116][emoji116][emoji116]huu uzi

Sent from my Infinix X573 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom