Pre GE2025 Je, chini ya utawala wa Rais Samia ndio imevunjwa rekodi ya kukamatwa wapinzani wengi wa kisiasa zaidi ya 500 kwa siku moja?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Sasa hivi kuanzia serikali za mitaa,bunge na serikali kuu mko wenyewe tu jee mumefanya nii la maana tofauti na walipokuwepo wapinzani? Au kuongeza deni la njee toka T60 hadi T91 kwa kipindi hiki mko wenyewe tu?
 
Mkapa aliwashughulikia Wapemba wakaenda uhamishoni Shimoni Mombasa Kenya

Kwenye Kitabu chake Ben ametubu Dhambi zake kwa baba Mtakatifu Papa Francisco anayeketi kitini pake Mtume Petro na kwa Mungu wa mbinguni

Ulale Unono 😃
Kwa hiyo Mama analipa kisasi awabonde Watanganyika hadi wakimbilie Burundi siyo?
 
Huyo kibwengo hana akili ya kuyajibu maswali haya
 
ila tumshukuru tu Lisu hakuwa mnafiki alisema kabisa mwanzoni kwamba huyu chief hangaya ni mapema sana kumchekea hanatofauti na mwenda zake tuone namna ya ku-deal naye
 
yule hanatofauti na yezebeli
 
Maendeleo,mnashindwa na nchi ndigo kama Rwanda.

Nchi imejaa viongoz vichwa maji miaka nenda rudi.

Tangu lini mpinzani akakwamisha maendeleo nyie mazumbukuku.

Mpinzani anapitisha bajeti ipi kwa mfano.
Nchi hii,ndo Nchi ambayo darasa la Saba,anahoji utendaji wa kitaalamu wa msomi mwenye PhD.
Viongozi wote wa chama mtawaliwa kuwa hopless
 
Tuna wapinzani ambao kukamatwa na polisi wanaona ni sifa kwao na kuona ndio kuiva kisiasa kwa kupitia misukosuko, na tuna jeshi la polisi ambalo linapenda kuonyesha mabavu yake kwa kushughlika na wapinzani. Jeshi la polisi limekuwa linawapa umaarufu viongozi wa upinzani kwa kamata kamata ambazo hazina ulazima wowote.

Mwisho wa siku hakuna cha maana kwa wananchi katika hiyo michezo ya polisi na upinzani.
 
tunapolisi wa hovyo ambao wanaona ni sifa kwao kwa serikali kuwakamata na kuwapiga wapinzani
 
Unaweza kuonesha namna gani Tamasha la vijana duniani na maadhimisho yake kwa CHADEMA kufanyika Mbeya kulikua na misingi halisi ya propaganda? labda kama hujui propaganda maana yake hasa ni nini! Nadhani kama unajua nini maana halisi ya propaganda ni vyema ungehusianisha na kilichoendelea Zanzibar kwamba uvccm WALIWEZA kuadhimisha siku ya vijana huku wakiwa na ulinzi wa vyote vya usalama kana kwamba wao ni sehemu bora zaidi ndani ya JMT inayojinasibisha kuwa ni nchi ya demokrasia inayoheshimu kanuni za demokrasia pamoja na haki za binadamu ambazo pia zimeelezwa katika ahadi za mwanaCCM kuwa binadamu wote ni sawa, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni na haki ya kusikilizwa ikiwa tu havunji sheria za nchi, hali kadhalika kila mtu ana haki ya kujiunga na chama chochote cha kisiasa na uhuru wa kukusanyika na kupata habari. Hivyo basi kama CCCM waliweza kufanya hivyo naamini ilikua ni haki kwa CHADEMA kama walivyofanya ACT wazalendo lakini haki hiyo imepokwa kihuni, kwani hata kuachiwa wameachiwa kihuni bila hata kupewa mashtaka ya jinai au mahakamani, kwani Masauni na Msajili wamekua washtaki na polisi wamehukumu. Hii inaondoa dhana ya utawala bora.
Ni kweli Magufuli alitaka kuua upinzani akafa yeye. Kwa imani yangu dhambi ni kukiuka makubaliano ya pande mbili. Kama taifa tulikubaliana kwamba nchi hii iwe ya mfumo wa vyama vingi vya siasa, na ili kuendana na hilo tukakubaliana kutunga sheria ya vyama vya siasa sambamba na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa. Na swala hili tukaliweka katika Katiba yetu kuonesha ni makubaliano yetu sisi watanzania. Hivyo basi jambo liliowekwa kimakubaliano mtu mmoja kwa mapenzi yake, tamaa zake na ubinafsi wake hawezi kuliondoa au kulikatza. Kimaadili tunasema huko ni kupotoka un-ethical na ni dhambi, na kama tunavyojua mshahara wa dhambi ni mauti basi mauti ilimfika kwa kutoheshimu makubaliano, ambacho angefanya ni kuomba ridhaa ya wananchi kufanya mabadiliko ya katiba ya kufuta vyama vingi na katiba kusema hivyo. Alichokifanya ni kujihusisha na uhalifu kama huu ambao uligharimu maisha ya watu akiwemo Akwilina aliyepigwa risasi na polisi lakini hatimaye Mungu hakumuacha atamalaki katika kuinyima haki. Anachokifanya Samia ni hicho hicho na mikono yake inaaza kushika damu na hakika damu isiyohatia itamlilia yeye na anawaotumia. Usidanganywe na majukwaa watu wana majuto sana binafsi huko mioyoni kwa kushiriki kupora haki na kumwaga damu zisizo hatia. Kusema kwamba CHADEMA na shughuli zao za kisiasa zinakwamisha maendeleo huo ni ujinga wa kiwango cha SGR kwa sababu hakuna siku CHADEMA wameshikilia account za serikali na hivyo serikali kushindwa kupeleka fedha za maendeleo au fedha za huduma za kijamii, Hakuna wakati ambao chadema tumewaona wakienda kuwatoa watumishi wa umma maofisini na kuwahamsisha kuacha kuwatumikia wananchi kama wafanyavyo CCM. Hakuna siku au wakati wowote chadema waliwahi kushika fedha za umma na wakatakiwa kuzilipa nao wakagoma na hivyo maendeleo kukoma. Ni aibu sana kufanya makosa halafu badala ya kuwajibika kwa makosa husika unakimbilia kusingizia wengine.
Nikionacho kuhusu kuzuiwa kwa tamasha na kukamatwa kwa viongozi wakuu wa chama ni kwamba:
1. Mtu anayedhani ana ushawishi katka eneo hilo ni kiongozi wa mhimili mmojawapo wa serikali (Bunge) na mara kadhaa tumeona akiwa na mamlaka juu ya vyombo vya dola. Mtu huyu pia ni mjumbe wa kamati kuu ya ccm kwa nafsi yake ya Uspika, Hali kadhalika hivi karibuni ameona kwamba amefanya maamuzi ya hovyo kwa kumfukuza Bungeni mtu aliyekua anatetea maslahi ya taifa kuhusu swala la Sukari ambalo linahusishwa kwa kiasi kikubwa na ofisi ya Rais na utafutaji wa fedha za kampeni. Maswala haya yalionekana lazima yangezungumzwa na viongozi wakuu wa chama na kwamba hatma ya vijana katika ajira na huduma bora za kijamii ikiwemo afya elimu na maji zipo kwenye hatma ya wanasiasa wachache ambao wameamua kufisidi fedha za umma ambazo zingetumika kufanya uwekezaji wa kisekta na kupanua wigo wa ajira na huduma. Ni dhahiri kwamba utitiri wa bajaji zinazotolewa na Mkuu huyo ili kuwapumbaza vijana ili wasahau kuhusu hatma yao baada ya kukosa nguvu za kuziendesha huku yeye akiwa amejikusanyia mamilioni na kustaafu kwa starehe yangejadiliwa na kumpotezea credibility.

2. Ukweli mchungu ni kwamba hivi karibuni kumefanyika Uchaguzi wa Chama cha Wanasheria cha Tanganyika na kumpa Bwana Kajunjumele ushindi licha ya kumpiga ngwara au mitama ya kutosha. Ikumbukwe kwamba Kajunjumele amekua akizungumzia mambo kadhaa yanayohusu rasimali za nchi pamoja na haki za watu ambapo Mheshimiwa huyu amekua akilazimishwa yapitishwe katika kikao cha chama chini ya mwamvuli wa Bunge. Tumeona kusikia kuhusu swala la bandari ambalo bado halijapoa, lakini pia swala la Maasai Ngorongoro na jinsi haki zao zinavyohujumiwa. Ikumbukwe kwamba Bi. Tulia alizunguka mbeya yote akisema yeye ni mwalimu wa wanasheria na anajua kila kitu na kuwaita wanaohoji kuhusu mkataba wa bandari ni wapumbavu. Kwa bahati nzuri Mungu hakumuacha mpaka aone yule mpumbavu ambaye ni kkaka yake amekuja kuwa boss wake kwenye chama ambacho yeye ni mwanachama kwa lazima. Hivyo basi hofu kubwa ilikua ni kwamba kajunjumele lazima angewahutubia vijana wa Taifa kupitia vijana wa Mbeya kuwakumbusha kwamba umaskini wao, kukosa kwao ajira, kuuzwa rasimali za nchi, kuporwa kwa haki, kuongezeka kwa umskini wa kipato na matabaka kumesababishwa na chama ambacho Dada yao ni mwananchama na mtu wa juu kwenye ngazi za maamuzi ya hatma ya nchi. Hakika hotuba yake ingesisimua na kuamsha ari ya vijana kuwaadhibu katika kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa.

3. Kilichofanyika hakikua cha bahati mbaya bali ni makubaliano ndani ya kamati kuu ya chama cha mapinduzi na kuspine kwa kumuagiza katibu mkuu atoe agizo baada ya madhila kufanyika. Kama wamefanya jinai sheria zipo. Kumbuka akiongea Rais ameongea Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo vya usalama na ulizni, Raisi ni Mwenyekiti wa chama, hakuna mahali anavua kofia moja na kubaki na moja, ndio mana hata vikao vyake anafanyia ikulu. Polisi hawezi kutofautisha hapa anaongea Mwenyekiti wa chama au Rais, vivyo viongozi walioko chini yake hawawezi kutofautisha kuwa hapa anaongea kama nani , Rais au Mwenyekiti. Katiba tuliyo nayo ni mbovu na haifai.
 
tunapolisi wa hovyo ambao wanaona ni sifa kwao kwa serikali kuwakamata na kuwapiga wapinzani
Si polisi tu hata hao wapinzani wanaamini kuwa mwanasiasa wa upinzani bila kuwahi kukamatwa na kulala polisi basi bado haujawa mwanasiasa wa upinzani hodari.
 
Kabisa, Magufuli hakuendekeza hizi sarakasi.
Eti mtu anasemekana yupo mahututi ila anapata muda wa kuandika mtandaoni
 
Sio kukamata wapinzani tu Bali amevunja record ya Raisi ambaye hapendwi Tz
 
Si polisi tu hata hao wapinzani wanaamini kuwa mwanasiasa wa upinzani bila kuwahi kukamatwa na kulala polisi basi bado haujawa mwanasiasa wa upinzani hodari.
polisi wanaona wasipowakamata na kuwapiga wapinzani ccm watawaona hawatoshi kwa nafazi hizo kwahiyo
 
Si polisi tu hata hao wapinzani wanaamini kuwa mwanasiasa wa upinzani bila kuwahi kukamatwa na kulala polisi basi bado haujawa mwanasiasa wa upinzani hodari.
polisi wanaona wasipowakamata na kuwapiga wapinzani ccm watawaona hawatoshi kwa nafazi hizo kwahiyo lazma waonyeshe bidii kuwashugulikia wapinzania ili nao wapnde madaraja
 
Huyu mama kavunja rekodi toka tupate uhuru
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…