Akilinjema
JF-Expert Member
- Aug 9, 2016
- 11,430
- 11,813
Je ukikata kata matango na limao ukaweka kwenye maji (jagi) halaf na tangawizi ukata,ukaweka huo mchanganyiko ukauweka 24 ,ukawa ynakunywa inasaidia nini,na unaitwaje huo mchanganyikoNEW DIET IN TOWN!
Jaribu hii diet haikunyimi sana...
1.Diet hii kwa siku za mwanzo zile 17 huruhusiwi kula wanga wa aina yoyote.Ugali,wali,ndizi,viazi,chips,pilau,biriani,chapati,maandazi,mikate,mihogo,bitumbua n.k hata kula kimoyomoyo hairuhusiwi.
2.Huruhusiwi sukari ya aina yoyote wala vinywaji vyenye sukari.Soda ni marufuku,juice za mabox hata ukitengeneza mwenyewe huruhusiwi.Pombe hairuhusiwi bia sijui wine or whisky vyote haviruhusiwi.
3.Mafuta hayaruhusiwi mafuta yanayoruhusiwa ni olive oil pekee mafuta ya mzaituni.
4.Hairuhusiwi kula late baada ya saa mbili usiku.Saa mbili ikukute unakula or umemaliza kula.
5.Huruhusiwi kushinda njaa.
6.Hii ni diet inayoruhusu vyakula vya protine na mboga mboga,matunda maalum sio kila tunda.
7.Mayai kwa ajili ya kifungua kinywa asubuhi mawili.Kwa kuchemsha au kukaanga.Ruksa kula ule ute kuliko kiini.Iwapo utakula viini visizidi vinne kwa wiki.Maana mayai yanacolestral ndio maana yana limit.
8.Samaki na kuku iwe kuchoma au kuchemshwa ndio anaruhusiwa kama mlo wa mchana au usiku.
9.Ukitaka kusnack kwenye saa tano au saa kumi tunakula yogurt tena ile ya asas ambayo ni low fat na sio tamu haina sukari ni plain.
10.Kusnack pia unakula matunda kama vile aple,chungwa,matunda jamii ya zabibu,jamii ya baries na mapeasi.Matunda haya yamechaguliwa mwanzoni kwani yanasaidia sana kuboost metabolism ili chakula kuyeyushwe haraka tumboni.Pia yana kiwango kidogo cha sukari.
11..Alfajiri ukiamka unakunywa kikombe cha maji ya moto yenye limao.Yanasaisia kurahisisha mmeng'enyo aa chakula kwa siku hiyo.
12.Kila baada ya mlo utakuwa green tea haya ni majani ya chai yale ya kijani sio meusi.Inamaana kwa siku vikombe vitatu asubuhi,mchana na usiku.
13.Hakikisha unakunywa maji sio chini ya lita 2 kwa siku maji yanasaidia sana kupunguza weight na pia husikii njaaa ukiyanywa ipasavyo.
MANUNUZI
1.green tea
2.yogurt zile za asas plain ambazo hazina sukari na ni low fat.
3.Matunda machungwa,peasi,zabibu,grape fruit,barries zile za aina zote.
4.Mafuta ya kupikia ya olive oil
5.Mayai
6.Samaki
7.Kuku mimi hununua vile vidari ambavyo vishawekwa kwenye kipakti kimoja zinakaa 6.
8.Mboga za majani aina zooote unazozijua wewe.
9.Limao au ndimu
Je ukikata kata matango na limao ukaweka kwenye maji (jagi) halaf na tangawizi ukata,ukaweka huo mchanganyiko ukauweka 24 ,ukawa ynakunywa inasaidia nini,na unaitwaje huo mchanganyiko
Huwa siweki sukari,,lakin yanakuwa na ladha mbaya[emoji23]Hiyo ni nzuri sana Ila usiweke sukari, juisi za diet zote haziwekwi sukari, chumvi , sukari na mafuta havifai Kwa anaetaka kupungua uzito! Hiyo ni nzuri lakini utakosa nyuzinyuzi fibers ambazo zinahitajika ktk kusaga Chakula mwilini ili kupata choo kikubwa ambapo ni mojawapo ya kuondoa sumu mwilini ikiwemo kuondoa lehemu
Tuweke basi hapa mkuuuMimi nikupe ushuhuda wangu miezi miwili ilopita nilikuwa Na uzito wa wastani wa 70 - 75 kg lakini leo nimepita 56 kg lakini shughuli Yake si ya kitoto, Na bado napambana haswa ! Yani baada ya muda itabidi nifanye shopping ya Nguo zote ! Nakutia moyo inawezekana kupungua ukiweka nia! Lakini mwenzio shuhuli yangu ni kula Matango tena nikikupa formula utashangaa
Iko hivi asubuhi tango moja , au nusu tango, nusu carrot na nusu nyanya , mchana vivyo hivyo na jioni, ukichoka kuvila kati ya mlo wowote unaweza kula ndizi mbivu moja au mbili, au Mayai 2 ya kuchemsha, au pakti ya mtindi moja tu au Samaki in any form! Hizo au au ni alternative to! Au unakula mboga za majani nyingi kidogo basi hasa Kwa jioni huo unakuwa ndo mlo wako wa usiku! Matango yasikosekane Kwenye friji wakati wote! Epuka kula mlo kati ya mlo!
Unakula hivi kwa muda gani
[emoji2] [emoji2] [emoji2]Jaribu kukopa mkopo mkubwa ambao hutaweza kuulipa, stress zake ni zaidi ya dawa.
ule tango na karoti nusu siku ya nne si utazimia jamani? tuweni realistic jamani mimi nikila mambogamboga siku ya tatu naishiwa nguvu kabisa inabidi nitafute waliInategemea Kati ya Mtu na Mtu Kwa sababu tunatofautiana lakini ukiweka nia na akili yako ukaiambilia shabaha yako lazima utapungua! Ushuhuda nilio nao wa Mtu wa karibu aliwahi kutumia tango nusu, carrot nusu, hoho nusu, na nyanya Maji nusu , asubuhi unakula hivyo, mchana hivyo na usiku hivyo, ukiweza kufanya hivyo Kwa uaminifu kabisa bila kula kitu kingine isipokuwa Maji ya kunywa Kwa wiki moja tu lazima lazima uta kupungua huyo Mtu alikuwa na kitambi cha wastani chote kwisha kazi! Toka wakati huo yuko Kama Mchina au Mzungu yaani ni English figure na yuko makini ktk kuona anakula nini na Kwa wakati gani! Imepita miaka miwili mitatu ndo na Mimi nikaamua kufanya maamuzi magumu ya kujikondesha! Ila ikitokea umekinai basi Mara moja moja kula Samaki au Kuku na kipande cha ndizi mbivu!
ahhaaaa sasa hivi nimeamua kuacha sukari na chumvi nataka nione week hii kama nitapunguaHuo mchanganyiko usiweke chumvi kabisa, chumvi inaongeza uzito Kwa njia ya fluid mwilini! Nashangaa Siku hizi hadi mahindi ya kuchoma eti Watu wanakula na chumvi [emoji87][emoji87][emoji87] mazoea mabaya sana! Siyo kila kitu lazima kukila, hata Kwenye bufee ya Chakula huwa nawashangaa ambao kuanzia Chakula Kwa kwanza hadi cha mwisho lazima achukue hadi sahani inamwelemea, ile maana Yake chagua kitakapo kufaa au kukipenda zaidi siyo kwamba uchukue vyote! Epuka kwenda mahali ambapo kunaliwa vyakula mwanzoni ingawa kadri unavyozoea na kujielewa hautaweza kukubali ushawishi wa marafiki na Watu wengine!
ule tango na karoti nusu siku ya nne si utazimia jamani? tuweni realistic jamani mimi nikila mambogamboga siku ya tatu naishiwa nguvu kabisa inabidi nitafute wali