Je dawa za kupunguza unene zinaweza kusababisha matatizo ya uzazi?

Nilimsikia Dk flani anaitwa Kweka simjui Kwa sura ana kipindi kila Jumatatu kuanzia nazani saa moja na nusu au mbili kasoro asubuhi redio Magic fm nazani aliongea Kwa mzigo kuhusu waTZ tunavyotakiwa kubadili mitindo yetu ya maisha! Akasema Siku hizi madaktari hawastuki kuona wagonjwa wa HIV Labda wenyewe waamue kuto kunywa Dawa , lakini madokta wengi concern Yao wengi Siku hizi hustushwa na magonjwa yasiyoambukiza ambayo yanaepukika na kutibika Kama mgonjwa aliwahi kwenda hospital , kisukari na BP
 
Je ukikata kata matango na limao ukaweka kwenye maji (jagi) halaf na tangawizi ukata,ukaweka huo mchanganyiko ukauweka 24 ,ukawa ynakunywa inasaidia nini,na unaitwaje huo mchanganyiko
 
Binafsi huwa namshangaa Mtu anayefanya kazi za kukaa Kwenye computer kutwa nzima halafu anakula milo mitatu ya nguvu Kama mkulima, fundi ujenzi, wanaotumia misuli na kutoka jasho, hiyo nasema Mimi binafsi baada ya kuanza kujitambua Kwa kusoma vitabu na Google , halafu kuna mambo mengi muhimu madokta wa bongo huwa hawayasemi kabisa au Kama kuna wachache wanaya sema lakini waTZ wanayapuuzia!
 
Je ukikata kata matango na limao ukaweka kwenye maji (jagi) halaf na tangawizi ukata,ukaweka huo mchanganyiko ukauweka 24 ,ukawa ynakunywa inasaidia nini,na unaitwaje huo mchanganyiko

Hiyo ni nzuri sana Ila usiweke sukari, juisi za diet zote haziwekwi sukari, chumvi , sukari na mafuta havifai Kwa anaetaka kupungua uzito! Hiyo ni nzuri lakini utakosa nyuzinyuzi fibers ambazo zinahitajika ktk kusaga Chakula mwilini ili kupata choo kikubwa ambapo ni mojawapo ya kuondoa sumu mwilini ikiwemo kuondoa lehemu
 
Huwa siweki sukari,,lakin yanakuwa na ladha mbaya[emoji23]
 
Tuweke basi hapa mkuuu
 

Unakula hivi kwa muda gani
 
Unakula hivi kwa muda gani

Inategemea Kati ya Mtu na Mtu Kwa sababu tunatofautiana lakini ukiweka nia na akili yako ukaiambilia shabaha yako lazima utapungua! Ushuhuda nilio nao wa Mtu wa karibu aliwahi kutumia tango nusu, carrot nusu, hoho nusu, na nyanya Maji nusu , asubuhi unakula hivyo, mchana hivyo na usiku hivyo, ukiweza kufanya hivyo Kwa uaminifu kabisa bila kula kitu kingine isipokuwa Maji ya kunywa Kwa wiki moja tu lazima lazima uta kupungua huyo Mtu alikuwa na kitambi cha wastani chote kwisha kazi! Toka wakati huo yuko Kama Mchina au Mzungu yaani ni English figure na yuko makini ktk kuona anakula nini na Kwa wakati gani! Imepita miaka miwili mitatu ndo na Mimi nikaamua kufanya maamuzi magumu ya kujikondesha! Ila ikitokea umekinai basi Mara moja moja kula Samaki au Kuku na kipande cha ndizi mbivu!
 
Huo mchanganyiko usiweke chumvi kabisa, chumvi inaongeza uzito Kwa njia ya fluid mwilini! Nashangaa Siku hizi hadi mahindi ya kuchoma eti Watu wanakula na chumvi [emoji87][emoji87][emoji87] mazoea mabaya sana! Siyo kila kitu lazima kukila, hata Kwenye bufee ya Chakula huwa nawashangaa ambao kuanzia Chakula Kwa kwanza hadi cha mwisho lazima achukue hadi sahani inamwelemea, ile maana Yake chagua kitakapo kufaa au kukipenda zaidi siyo kwamba uchukue vyote! Epuka kwenda mahali ambapo kunaliwa vyakula mwanzoni ingawa kadri unavyozoea na kujielewa hautaweza kukubali ushawishi wa marafiki na Watu wengine!
 
Unaweza ukaamka asubuhi kunywa Maji lita moja Kabla ya mswaki, Kisha piga mswaki, oga! Breakfast mwingine anakula ndizi mbivu 2 tu hadi mchana anakula tango au mbogamboga na kijisamaki jioni Mayai mawili tu ya kuchemsha, vingine utajiongeza mwenyewe!
 
Kabla ya kuanza hakikisha umepima uzito wako, Kisha kula hivyo hapo Juu halafu nenda kapime uzito baada wiki moja Kama umeanza Jumamosi inayofuata kapime uone, na uwe mwaminifu kabisa bila kujidanganya mwenyewe! Hapo hata Pombe usithubutu kunywa hata tone!
 
ule tango na karoti nusu siku ya nne si utazimia jamani? tuweni realistic jamani mimi nikila mambogamboga siku ya tatu naishiwa nguvu kabisa inabidi nitafute wali
 
Kama huna dozi yoyote ya Dawa ya kunywa ya hospital basi nashauri pendelea kutokula usiku kabisa ukishakula mchana hiyo light lunch basi hiyo ndo ntolee hadi Kesho tena na kuendelea! Ukiweza kutokula usiku au ukala tango au glasi ya juisi isiyo na added suger nakwambia tarajia kuona matokeo makubwa sasa (BRN) !
 
ahhaaaa sasa hivi nimeamua kuacha sukari na chumvi nataka nione week hii kama nitapungua
 
Na Kwa muda mrefu ile endelevu la sivyo ukianza kula Kama kawaida uzito inajirudia palepale, ndo maana mwingine anafunga hali kabisa hata Siku arobaini lakini anapomaliza kufunga akarudia ulaji wake wa kawaida anajikuta anarudia uzito wake uleule
 
ule tango na karoti nusu siku ya nne si utazimia jamani? tuweni realistic jamani mimi nikila mambogamboga siku ya tatu naishiwa nguvu kabisa inabidi nitafute wali

Hauwezi kuzimia @ dada! Ndo maana nakwambia hadi moyo na akili yako na mwili wako uvitiishe lakini Kama hutailazimisha akili yako kukubaliana na shabaha yako basi utazimia Kweli ! Halafu usijisikilizie kuwa kawaida tu fanya shughuli zako Kama ilivyo desturi yako !
 
Kwanza jichunguze unene wako unasababishwa na nini 1) chakula 2) wa asili) 3) au wa kuridhika na maisha

Kama ni 2 na 3 chakula hakitakuwa na impact sana hata ukiacha kula ingawa bado utatakiwa usile sana
Kama ni wa no. 3 bas utapungua hasa endapo utaenda kinyume yaani ukiacha kuridhika na maisha.
Kama ni unene wa chakula basi unahitaji kufanya diet kwa sana na mazoezi, Unahitaji afya ya akili ili diet na mazoezi vilete matokeo, namaanisha unatakiwa kuwa relaxed no stress or worries, sahau kama we ni mnene na uweke nguvu kwenye mazoezi na diet, usifanye mazoezi asubuhi jioni unajiangalia kwenye kioo et kama umekonda. Ukiwa relaxed itasaidia mmeng'enyo wa chakula kufanya kazi ipasavyo kuliko ukiwa uko worried au stressed, pia usingizi, kulala kwa wakati na kwa masaa sahihi inasaidia mfumo wa mmengen'yo wa chakula kufanya kazi vizuri, na hasa ukiwa relaxed utalala vizuri na mwili utafanya kazi vizuri, na itakuwa rahisi kupungua, maji mengi yanasaidia pia
 
Mimi ilinitokea najisikia homa na baridi kali nikaenda hospital Pima kila kitu sina tatizo wakaniuliza umekula nini kikawambia mchana nilikula ndizi mbivu mbili sasa hapo ilikuwa usiku wa saa 4 wakasema Huyu ni Njaa mtafutieni Chakula nikarudi home nikala kijisamaki nikalala asubuhi nikaendelea Kama kawaida hadi leo no more turning back! Kusudia kukonda siyo kupungua uzito
 
Halafu Kwa wanawake nashauri wakachaki homoni Kama zimewiana vema, mathalani Kama dada unatumia Dawa za uzazi wa mpango hiyo tu yaweza kuwa sababu ya ongezeko la uzito na kutokupungua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…